Ni nini kazi ya Katibu Mkuu Kiongozi?

Ni nini kazi ya Katibu Mkuu Kiongozi?

Mfano kama mtu wa karibu wa rais akifa kwa korona hali ya afya ya rais inakuaje?
Kama ni mfuatiliaji wa mambo unaweza kuona kuwa hata jana Raisi akiingia kumuaga Kijazi kuna umbali uliwekwa kati yake na wasaidizi wake.Kujibu swali lako ni kuwa maisha ya Raisi yanakuwa hatarini kwa kuwa karibu na mtu ambaye anaweza kumuambukiza ugonjwa wa hatari.
Rais ni kiongozi Mkubwa sana kiasi ambacho afya yake ikitetereka hata uchumi unaweza kuanguka.
Sidhani kwa hali ilivyo JPM anaweza tena kutoka na kuchanganyika na watu wa mtaa wa Congo na akifanya hivyo ina maana idara yetu ya kumlinda imeshindwa kutumia mamlaka yake.
Tumewahi Barack Obama akiingia mtaani na hata kula mkahawani lakini ukiangalia kwa makini tayari eneo lipo chini ya ulinzi mkali.
 
Ndiye administrator mkuu wa ikulu anayesimamia mambo ya kiutawala kwa wafanyakazi wote wa Ikulu pamoja na wale walioteuliwa na rais. Kwa marekani anaitwa Chief of Staff.
Hapana umekosea. Katibu mkuu wa Ikulu yupo na ana majukumu kama ya makatibu wakuu wengine wa wizara.

Katibu mkuu kiongozi siyo Chief of Staff bali ni Chief Secretary na ndiye mwenyekiti wa makatibu wakuu wengine wa wizara. Yeye ni mkuu wa watumishi wa umma wote yakiwemo mashirika na taasisi za serikali. Yeye ndiye katibu wa Baraza la mawaziri ambalo mwenyekiti wake ni Rais.
 
Kikatiba ni mtumishi wa umma lakini kiutendaji ni mtu wa karibu mno na kiongozi wa nchi .Ni mkono wa kulia wa Rais.Yeye ndiye mkuu wa watumishi wa umma,ndiye kiongozi wa makatibu wakuu wote,NI KATIBU WA BARAZA LA MAWAZIRI (Baraza la mawaziri ndiyo serikali yenyewe).Kwa ujumla baada ya Rais ndiye mtu wapili kujua mambo actually karibu yote ya serikali.
SI MTU MDOGO HATA KIDOGO!!
 
Kwa mnao mlinganisha chief secretary na chief of staff Wa marekani mnakosea. Mamlaka ya chief of staff Wa marekani yanaanza Na kuishia west wing. Hakuna chief of staff Mwenye mamlaka kwenye wizara yeyote marekani. Kwetu chief secretary ni Mkubwa Wa makatibu wakuu wote. Kwenye utumishi wa uma usiokua Na siasa hakuna Mkubwa kumzidi. Yeye ni mkuu Wa utumishi Wa umma maana yake ndo mtumishi Wa umma namba moja. Pia ni katibu Wa baraza la mawaziri. Ni mjumbe asiyekua na kura kwenye baraza la mawaziri. Huandaa ratiba Na mihutasari ya yatokanayo na vikao hivo. Yeye ndiye mshauri namba moja Wa raisi kuhusu mambo ya utendaji Wa serikali. Ndo kiungo kati ya siasa Na utendaji.
 
4(3)(d) ni Mamlaka ya Nidhamu kwa watumishi wa Umma wanaoteuliwa na Rais.

Kwenye hiyo sehemu hapo juu. Anaweza wajibisha mawaziri? Au hayo mamlaka yake yanaishia wapi?
Mawaziri sio watumishi wa umma. Viongozi watumishi wa umma wanaoteliwa na Rais ni kama makatibu wakuu na wasaidizi wao. Wakurugenzi wa halmashauri,makatibu tawala mikoa, wakuu wa taasisi za umma n.k.
 
Kikatiba ni mtumishi wa umma lakini kiutendaji ni mtu wa karibu mno na kiongozi wa nchi .Ni mkono wa kulia wa Rais.Yeye ndiye mkuu wa watumishi wa umma,ndiye kiongozi wa makatibu wakuu wote,NI KATIBU WA BARAZA LA MAWAZIRI (Baraza la mawaziri ndiyo serikali yenyewe).Kwa ujumla baada ya Rais ndiye mtu wapili kujua mambo actually karibu yote ya serikali.
SI MTU MDOGO HATA KIDOGO!!
Hapa napata swali lingine...
Mbona kama hakuwa na ulinzi wa kumlinda kivileee.. maana kwa maelezo yako.. yeye ni mtu mwenye siri nyingi sana za nchi
 
Hii article (c) ndo hua inanichanganya. Nashindwa kumtofautisha na prime minister as all we know prime minister has mandate of give directions and instructions to any institution in the country the same applies to chief secretary.
PM ni kiongozi wa shughuli za serikali pale Bungeni, nje ya hapo hana mamlaka labda apewe na Rais, hukumbuki sakata la Koroshow aliambiwaje? Rais hata akitaka kuteuwa mtu anaweza akamuuliza kwanza Chief Secretary na hata ahitaji ushauri wa Makamu Rais au PM, hata watumishi wote ukitaka jambo lako lifike haraka kwa Rais basi mtumie Chief Secretary maana wao na Presidaa wanakutana karibia kila siku.
 
Kikatiba ni mtumishi wa umma lakini kiutendaji ni mtu wa karibu mno na kiongozi wa nchi .Ni mkono wa kulia wa Rais.Yeye ndiye mkuu wa watumishi wa umma,ndiye kiongozi wa makatibu wakuu wote,NI KATIBU WA BARAZA LA MAWAZIRI (Baraza la mawaziri ndiyo serikali yenyewe).Kwa ujumla baada ya Rais ndiye mtu wapili kujua mambo actually karibu yote ya serikali.
SI MTU MDOGO HATA KIDOGO!!
Pia ni kiongozi wa mabalozi wote wa Tanzania
 
Hapa napata swali lingine...
Mbona kama hakuwa na ulinzi wa kumlinda kivileee.. maana kwa maelezo yako.. yeye ni mtu mwenye siri nyingi sana za nchi
Unataka awe na ulinzi kama wa Makonda?Gari anayotumia sio STK bali CS (chief secretary).Naamini alikuwa analindwa vizuri na ni mtu aliyekuwa very busy.
Anyway awamu hii kuna matumizi mabaya ya ving'ora na misafara kwani hiyo ni haki yako kuona kama alikuwa halindwi sana (relative to other state officials)
 
Yaani ni kama Mungu na mwanae wa pekee, Yesu Kristo, ukaribu wa Mkuu wa nchi na Katibu Mkuu kiongozi. Sijui umeelewa? Maana tukikupa vifungu vya sheria ujue wajibu wa CS, hutajua vema. Umeelewa au bado umelewa?
Sijaelewa mkuy. Kwasababu hivi vyeo ni vya kipuuzi havina maana vinaelemea tu walipa kodi na vyoo vya ikulu kujaajaa hovyo kila mara
 
Kikatiba ni mtumishi wa umma lakini kiutendaji ni mtu wa karibu mno na kiongozi wa nchi .Ni mkono wa kulia wa Rais.Yeye ndiye mkuu wa watumishi wa umma,ndiye kiongozi wa makatibu wakuu wote,NI KATIBU WA BARAZA LA MAWAZIRI (Baraza la mawaziri ndiyo serikali yenyewe).Kwa ujumla baada ya Rais ndiye mtu wapili kujua mambo actually karibu yote ya serikali.
SI MTU MDOGO HATA KIDOGO!!
Kweli unaelewa
 
Kikatiba ni mtumishi wa umma lakini kiutendaji ni mtu wa karibu mno na kiongozi wa nchi .Ni mkono wa kulia wa Rais.Yeye ndiye mkuu wa watumishi wa umma,ndiye kiongozi wa makatibu wakuu wote,NI KATIBU WA BARAZA LA MAWAZIRI (Baraza la mawaziri ndiyo serikali yenyewe).Kwa ujumla baada ya Rais ndiye mtu wapili kujua mambo actually karibu yote ya serikali.
SI MTU MDOGO HATA KIDOGO!!
Mara baada ya raisi makamu,mara baaada ya raisi waziri mkuu mara baada ya raisi spika wa bunge,yaani vyeo kibao alafu kazi zile zile
 
Ninadhani kwa lugha rahisi Katibu Mkuu Kiongozi ni Mtendaji Mkuu wa Serikali (Chief Executive Officer), kuanzia kwenye utendaji kazi wa kila Siku wa Baraza la Mawaziri(Cabinet), uchumi, kusimamia utumishi wa umma, Ku-head Makatibu Wakuu, n.k.
 
Back
Top Bottom