Umeshawahi kuwa baunsa na hujawahi hata kwenda gym kwa bahati mbaya?
Ni ile siku nimekunywa Konyagi,bwana kuna hali flani nilikua najiona kama
yule jamaa kwenye bapa la konyagi,Mimi ndio nataka kusikilizwa tu,tunarudi hostel
nafikishwa nnje hostel ilikua imezungushiwa senyenge,kupita ni lazima uiname uingie
kwani Baunsa mimi nataka kuinama sasa,yani naiambia senyenge inipishe mi nataka kupita
Buraza hiyo siku Ni yule mpenzi nliekua nae tu ndie alietumia akili nikajikuta kitandani,ila unafkiri
iliishia hapo? nilitapika nadhani bado kidogo nitapike utumbo,maana macho yalinitoka si kawaida..Kampani mbaya asee...