Ni sababu ipi ya paka kumtesa panya kwa kumchezea badala ya kumuua haraka?

Ni sababu ipi ya paka kumtesa panya kwa kumchezea badala ya kumuua haraka?

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Kiukweli paka ni wanyama wakatili sana, kuna paka hapa nyumbani huwa akikamata panya huko store inakuwaga ni mateso makali sana kwa panya.

Anachofanya anambeba panya kwa mdomo anamleta uwanja wa wazi anamwachia, hapo panya akianza kukimbia paka anamrukia anampiga makucha panya, anambeba upya kwa mdomo anamleta katikati ya uwanja anamwachia huku akijifanya kama vile hana muda naye.

Pindi panya akidhani kasemehewa anaanza kukimbia haraka lakini paka hamwachi afike mbali anamrukia anampiga makucha anambeba, yani ni hivyo hivyo mpaka panya anaishiwa matumaini kabisa anatulia tu kakubali yaishe ndio analiwa.

Ni mateso makali mno kwa panya, badala ya kuuliwa haraka anauliwa taratibu sana kwa maumivu makali sana kisaikolojia.
 
Huwa anafanya hivyo pia akiwa anawafundisha wanae stadi za kazi na maisha ya kujitegemea manake paka wakiwa kwenye vijiwe vyao vya kahawa wanasemaga binadamu sio wa kumwamini, lazima wajifunze kutafuta kwa mikono yao.
 
yani ni hivyo hivyo mpaka panya anaishiwa matumaini kabisa anatulia tu kakubali yaishe ndio analiwa.
mouse-acting-dead-funny-animals.gif
 
Kama kuna kitu kitu huyo mnyama ananiudhi basi ni yale makelele yao ya kubembelezana kama binadamu. Yaani wanapenda kuharibu usingizi wa watu kwani wanapenda kubembelezana usiku mwingi hata ukiwafukuza muda mfupi wanarudi na kelele zaidi ya za mwanzo wakati mwingine nahisi ni kama wanafanya makusudi kuharibu usingizi wangu.
 
Paka ni CCTV ya [emoji89], usiulize sana, namaanisha, unaweza ukawa unamfuga paka ili akutunzie nyumba yako dhidi ya Panya na wadudu wengine, lakini paka ni kiumbe mmoja mwenye uwezo mkubwa sana kuliko binaadamu tumchukiliavyo, paka wana mawasiliano ya moja kwa moja na viumbe tofauti na Binaadamu paka wanamtumia kum trace binadamu.
 
Hapo paka anakuonyesha tu kuwa jinsi gani ?wakoloni walivyowatesa BABABU/MABIBI zetu na bado akili yako haitaki kuelewa tu WALITESWA zaidi ya huo mfano wa paka kwa panya MKUU.. ila usiwachukie
 
Kiukweli paka ni wanyama wakatili sana, kuna paka hapa nyumbani huwa akikamata panya huko store inakuwaga ni mateso makali sana kwa panya.

Anachofanya anambeba panya kwa mdomo anamleta uwanja wa wazi anamwachia, hapo panya akianza kukimbia paka anamrukia anampiga makucha panya, anambeba upya kwa mdomo anamleta katikati ya uwanja anamwachia huku akijifanya kama vile hana muda naye.

Pindi panya akidhani kasemehewa anaanza kukimbia haraka lakini paka hamwachi afike mbali anamrukia anampiga makucha anambeba, yani ni hivyo hivyo mpaka panya anaishiwa matumaini kabisa anatulia tu kakubali yaishe ndio analiwa.

Ni mateso makali mno kwa panya, badala ya kuuliwa haraka anauliwa taratibu sana kwa maumivu makali sana kisaikolojia.
ni sawa hana tofauti na policcm wa nchi hii kwa viongozi wa chadema
 
Back
Top Bottom