#COVID19 Ni sahihi Humphrey Polepole kuonesha Msimamo wake wa kutochanjwa?

#COVID19 Ni sahihi Humphrey Polepole kuonesha Msimamo wake wa kutochanjwa?

Na huo unafiki wao tuliusema wakati ule, na hata sasa tumeendelea kuwaambia kuwa kumpokea Lowassa ilikuwa ni upuuzi kama upuuzi mwingine.
Kumbe unajua kwamba wanasiasa wote ndio walivyo ni wanafki.
 
Hivi waliopururwa na hili gonjwa walikuwa na matatizo ya lishe? Kwamba lile jiwe kumbe halikuwa jiwe?

View attachment 1884876

Pana wodi pale mwananyamala SSH alitimua mbio. Anaonaje pole pole akiwa anakwenda hata kuwasalimia salimia wale wagonjwa na kuwapa ndogo ndogo za mambo ya lishe?
Hizo ni Propaganda boss
 
Ni hiari, sasa kuonyesha msimamo wake kuna shida gani? Tumeona wengi wakionyesha misimamo yao ya kuchanja, na ni sahihi kwa maamuzi yao.
Msimamo akaonyeshe kwa familia yake.
 
Mkuu, Kama vile ninyi mnavyopambana ku advocate Chanjo, muache Polepole nae atumie Uhuru wake kwa kutoa maoni.
Ofcourse ni hatari kuhimiza wananchi wote kuchoma Chanjo ambayo ndio kwanza ipo kwenye Clinical trial. In fact tumeruhusu kuwa Taifa la majaribio. Hata Sasa tunachoma Chanjo ambayo hatuna uhakika wa protection yake dhidi ya new strains like Delta na Lambda. Chanjo hii haijulikani duration of protection; so hakuna anayejua baada ya kuchoma Sasa atatakiwa kupata booster dose lini. Ni Chanjo ambayo long term effects zake hazijulikani. Yaan hata wanaokataa kuwa inasababisha Erectile dysfunction hawana uhakika.
As a MD, nimechagua kuwa Kama Polepole.
 
Hii ni timu ya mwenda zake , ambao kwa sasa hawana tena jipya zaidi ya kujikosha ...
Ni muda wa nape kurudia kiti chake

sent from HUAWEI
 
Huo wizi unaofahamika ndio unaofanya ccm iwe madarakani kipindi chote hiki halafu wewe unaona ni kitu kidogo et ni wizi unaofahamika, sasa kama hilo umeweza kulikubali na kuliona dogo sasa hilo kubwa unalolishangaa hapa lipi wakati hata iweje ccm ilikuwa lazima tu iendelee kukaa madarakani kivyovyote vile.
Wizi upo kila mahali, lakini sio kwa ushenzi ule.
 
Mbona kipindi cha yule mtawala muovu hakujitokeza useme aache iwe hiyari, au ulikuwa unaona ni sawa yeye kushurutisha msimamo wake? Huyo Polepole kwakuwa ni mnafiki, majizi menzake ya kura yamkamate kwa nguvu na kumchoma sindano ya sumu.

Sasahivi kapewa hiyari shida iko wp?! Mbona una maswali ya kijinga sana!?
 
Hivi yule huwa ni Mzee au kijana? Aweke msimamo hata ikija ya yale maradhi yake
 
Huo uchaguzi unaolilia utafikiri huko nyuma kulikuwa na uchaguzi wa haki, wengine tulishaacha masuala ya uchaguzi bongo kabla hata ya huo uchaguzi unaouongelea ila mwenzetu sijui huo uchaguzi ndio mara yako ya kwanza kushiriki uchaguzi bongo.
Wajumbe hawakumuacha salama. Ha ha haaa!
 
Wizi upo kila mahali, lakini sio kwa ushenzi ule.
Hoja ya msingi ni kwamba ccm ilikuwa lazima iendelee kubaki madarakani kama kawaida yake iwe kwa wizi mdogo uliyouzoea au wizi mkubwa unaoulalamikia hapa, iwe kwa kubalance kama ulivyozoea au kutobalance kama ilivyotokea.
 
Mh Polepole yuko sahihi sana tu. Ndani ya CCM kunatakiwa kipindi hiki, kutokana na haya makundi mawili ya walio na wasio chanja yanayozaliwa na uamuzi huu wa kuchanja chanjo ya corona tupate uongozi mbadala ndani ya CCM ulio katika kusubiria.

Ni ukweli usiopingika baada ya Hayati JPM kuchukua nchi na upinzani kuwa na yale maaumuzi ya kubadili gia angani na uundwaji wa genge la ukawa, nchi hii upinzani umegeuka kuwa maiti iliyovalishwa suti nazifu tu.

Wakati umefika kwa wanaCCM wenyewe kuwa na uongozi mbadala kwa faida pana ya Taifa hili.
 
Hoja ya msingi ni kwamba ccm ilikuwa lazima iendelee kubaki madarakani kama kawaida yake iwe kwa wizi mdogo uliyouzoea au wizi mkubwa unaoulalamikia hapa, iwe kwa kubalance kama ulivyozoea au kutobalance kama ilivyotokea.

Sasa unataabika nini nikoweka wazi huo ushenzi, au mimi kuanika wazi uhuni ni jambo geni kwako?
 
Sasa unataabika nini nikoweka wazi huo ushenzi, au mimi kuanika wazi uhuni ni jambo geni kwako?
Kelele zako ni kama kwamba huko nyuma hali ilikuwa shwari kumbe walikuwa wana balance tu ila juu chini ccm lazima iendelee kuwa madarakani na ndio maana wengine tulishaacha ujinga wa kupiga kura maana toka mwanzo uchaguzi wa Tz ni usanii mtupu tu, sasa safari hii hawaja balance ndio kunakufanya wewe upige kelele.
 
Kelele zako ni kama kwamba huko nyuma hali ilikuwa shwari kumbe walikuwa wana balance tu ila juu chini ccm lazima iendelee kuwa madarakani na ndio maana wengine tulishaacha ujinga wa kupiga kura maana toka mwanzo uchaguzi wa Tz ni usanii mtupu tu, sasa safari hii hawaja balance ndio kunakufanya wewe upige kelele.

Kelele za wizi zipo miaka yote, na wala walikuwa hawabalance bali walikuwa wanazidiwa, kwani rate ya wapinzani ili inazidi kupanda, huku idadi ya ccm ikizidi kushuka. Ila uchaguzi uliopita dhalimu aliigiza ushenzi ambao haujapata kutokea. Tunamshukuru Mungu kwa kutuondolea yule mtu muovu bila damu kumwagika.
 
Ni ukweli usiopingika kuwa hatua za mwanzo za kupambana magonjwa ni kula vyakula Bora Kama wanavyohamasisha wataalaam wetu wa afya.

Hapa tutapata kingi ya miili yetu,lakini wakati wa magonjwa ya milipuko Kama ilivyo kipindi hiki,ni busara watu wakachanja chanjo ya Uviko-19.

Kwa sababu wengi wetu hatuna mazoea ya kufanya medical check kujua Hali zetu za afya .Lakini ni muhimu wizara ya afya na viongozi wa serikali wakati wanapohamisisha chanjo ya uviko-19 Basi wasisitize na ulaji wa vyakula vinavyo ongeza Kinga mwilini,mara kwa Mara
 
Kelele za wizi zipo miaka yote, na wala walikuwa hawabalance bali walikuwa wanazidiwa, kwani rate ya wapinzani ili inazidi kupanda, huku idadi ya ccm ikizidi kushuka. Ila uchaguzi uliopita dhalimu aliigiza ushenzi ambao haujapata kutokea. Tunamshukuru Mungu kwa kutuondolea yule mtu muovu bila damu kumwagika.
Kama kuzidiwa nadhani wangekuwa washaachia nchi mpaka sasa hivi maana toka enzi za Cuf huko, we kubali tu walikuwa wana balance kitu ambacho safari hii hakikufanyika wenyewe mlikuliwa msharidhika kule kubalance.
 
Back
Top Bottom