Mwizukulu mgikuru
JF-Expert Member
- Oct 21, 2021
- 5,715
- 13,739
Usiongee kwa kufata mapenzi uliyonayo.....ongea kwa uhalisiaWe nae ndio umekosa cha kusema.mpanda watu wanaendesha dualis na harier watu wana hela za madin na ndege ipo dar. Mpanda labda ulifika ya karne ya 12.ila sio mpanda hii mzee
Kule ndio wenye hela wanajenga,kwa kishua kule,Nenda Morogoro shuka msamvu, chukua bodaboda akupeleke hadi shule ya msingi kikundi, nauli 1500.
Ukifika pale angalia mlimani kule watu wamejenga mlimani yaani. Sasa unajiuliza hawa watu hata mabati walipelekaje kule!
Asante ww ndo umeelekeza vzuri kabisa kabisaNadhani una maanisha njia panda ya Ipole, wilaya ya Sikonge, Tabora; ukiacha barabara ya kuelekea Mpanda, unayooka kushoto kwako kuelekea Rungwa. Hapo mlipokutana na bonge la joka hapo panaitwa Kitunda. Usipochukua tahadhari unaweza liwa na simba. Mbele kidogo kuna mji unaitwa Kitunda - watu wanachimba madini pale. Ukitoka Rungwa unaelekea Kambi Katoto (upande wa kusini), Chunya kisha unaelekea Mbeya. Unabidi uwe na roho ngumu kiasi ili uweze kuishi kule. Ukitoka Rungwa kuelekea Kaskazini utaingia Itigi, kisha barabara kuu kuelekea Singida au Manyoni.
Yani Mkuuu mim nikiona joka naweza Kata moto Ile siku sitasahau....... siku tatu nkaona mweziNadhani una maanisha njia panda ya Ipole, wilaya ya Sikonge, Tabora; ukiacha barabara ya kuelekea Mpanda, unayooka kushoto kwako kuelekea Rungwa. Hapo mlipokutana na bonge la joka hapo panaitwa Kitunda. Usipochukua tahadhari unaweza liwa na simba. Mbele kidogo kuna mji unaitwa Kitunda - watu wanachimba madini pale. Ukitoka Rungwa unaelekea Kambi Katoto (upande wa kusini), Chunya kisha unaelekea Mbeya. Unabidi uwe na roho ngumu kiasi ili uweze kuishi kule. Ukitoka Rungwa kuelekea Kaskazini utaingia Itigi, kisha barabara kuu kuelekea Singida au Manyoni.
Asante ☺️Poleeee 🤣🤣🤣
Wapo busy kununua V8 lakini kutenga million 500 kujenga barabara ya changarawe au kuchimba visima hawana muda na pesa hizoUzi mzuri sana, huko maporini inaonekana ndipo penye hela. I wish watu wa serikalini wangeona huu uzi labda wangeingiwa huruma kutafuta hivi vijiji na kupeleka services especially kuwachimbia visima vizuri vya maji na zahanati
Zanzibar INA ukubwa gani?Yah ni kweli ata Zanzibar kuna maendeleo kushinda Tanganyika, Nimeishi Zanzibar sikuwahi kuona Wamama wakipata shida ya maji na huduma za hospitali na usafiri, umeme upo kila sehemu, sehemu zote za Tanzania Zanzibar hawana shida za huduma za kijamii huduma zote zimewafikia wananchi, tembea Zanzibar kote huwezi kukuta mama kabeba ndoo ya maji kichwani , na uko vijiji huduma zote zipo, yani Zanzibar kuna vitu vingi vya elektroniki mpaki vijijini, Zanzibar mtu kukupa nyumba uishi au kukuazima gari lake uendeshe ni jambo la kawaida tena uko ni mashambani.
Kama huna hela kweli dar joto kali sanaDar es salaam joto kali hapakaliki.
Njombe si serikali inautaja wa tatu kwa maisha bora nchini...au kuna niombe nyingine [emoji23][emoji23]Mikoa hii vijiji vyake ni shida Dodoma, Njombe, Katavi, Kigoma, Tabora, Ruvuma, Manyara.
Ndio mkoa gani hukuKawe kapina -Heka kumi kwa elf 15 .Ukiwa na 50 na nyumba unajenga kabisa .Tanzania bado poriii.
Tabora .Ndio mkoa gani huku
Watu mna unafiki humu hivi mmeshindwa kutaja vijiji vya Singida kweli???
Watu wa singida vijijini ni watu wa ajabu sana. Imagine mtu ana kuku zaidi ya 50 lakini hachinji hata iweje...Ajabu ni kua hua wanauza kuku ili wapate hela ya kununua mlendawa kusagwa. Yaani huo mlenda unakua kama unakula ugali na hina zile za miti.
Mnyaturu akija kwako usimpikie kuku wala nyama pika mabamia wanapenda makamasi kamasi kwente chakula chao[emoji23][emoji125][emoji125]
Mwakaleli- Tukuyu Mbeya. Aisee baridi lilinushinda pale Mwax sec.
Wadau mnavisahau vijiji vya wilaya ya Chunya-Mbeya. Makongolosi, isangawana,sangambi, kuishi kule kwataka Moyo. Jua ndio kwao, maji Sasa Ni shida, Ardhi Ni mawe tu.
Chato
Najiuliza sana watu wa chato wanaishije.
Kama siyo uchizi lile wazo la kujenga ule uwanja lilitolewaje na fedha zikatengwa.
Sasa kuna mataahira bungeni wakaja na wazo chto iwe mkoa alafu Muleba iwe sehemu ya huo mkoa...
Yaani sisi wahaya tukawe ndani ya mkoa wa chato?
Hii nchi iliingiliwa kinyume na maambile aise
Watu wa serkali nani? Watu wapo busy kuipigania familia zao we endelea kubana pua watu wa serkaliUzi mzuri sana, huko maporini inaonekana ndipo penye hela. I wish watu wa serikalini wangeona huu uzi labda wangeingiwa huruma kutafuta hivi vijiji na kupeleka services especially kuwachimbia visima vizuri vya maji na zahanati
Mkuu hukuona sehemu tambarare ukitoa sehemu zenye milima?Kwa mara ya kwanza kufika kijiji cha Bugamba kilichopo mwambao wa Ziwa Tanganyika Kigoma vijijini nilipigwa na mshangao baada ya kushuka kwenye boti kutokea Kibirizi Kigoma ! Pale boti zinapoegesha sikuona nyumba yoyote ! Mwenyeji wangu kaniambia tunaenda nyumbani yaani ananionyesha juu utafikiri tunaenda mwezini ! Kutoka hapo tunapanda huko juu nilitaka kulia maana chini Ziwa Tanganyika juu ndio kijijini, halooo kupanda ilibidi mpaka nishikwe mkono. Kufika huko juu ndoo nakuta kijiji na shule ya msingi ukitizama chini ziwa Tanganyika liko bondeni ! Kwa kweli inatisha kijiji hicho hakuna shamba la maana sehemu kubwa ni milima tu mihogo wanalima kwenye mitelemko ya milima na ukiteleza unaporomokea ziwani na ziwa lina kina kirefu ni hatari. Pale kijijini hakuna baiskeli maana mazingira hayaruhusu ! Shughuli za uchumi pale ni uvuvi. Ukitaka kwenda kijiji cha jirani cha Zashe au Mwamgongo lazima utumie boti kwa mguu haiwezekani.
Toka siku hiyo nikajua sababu ya waha wengi kukimbilia mikoa ya Jirani kama Mwanza, Geita, Tabora na Katavi maana mazingira ya maeneo hayo ni magumu sana. Kweli maeneo hayo ukifika mpaka unajiuliza kwamba hivi hawa watu huku walifuata nini.
Nimecheka kwa kelele ha haaa.Kuna vijiji vipi Bumbuli daah wakuu acheni tu tulienda na gari njian watu wanatushangilia kma ni Raisi anapita tukafika mwisho wa barabara tukaanza kubeba jeneza hadi nyumbani tulichoka zaidi ya masaa6 kule tuwaachie nguruwe pori au wahamishiwe vijiji vya Kilimanjaro kuacha Mwanga.