Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Habari za muda huu wana JF,

Nchi yetu ni kubwa na Ina miji na vijiji vingi lakini Kuna baadhi ya maeneo unaweza ukahisi sio sehemu ya nchi yetu mpaka ukajiuliza maswali kuwa Hawa watu waishio hapa walivutiwa na Nini mpaka wakaweka makazi ya kudumu maeneo haya

Mfano, Mimi niliwahi kutembelea Kijiji cha Baranga kata ya sirorisimba kupitia Kyagata. Nilistajabu na kujiuliza Hawa watu huku wanaishije?

Ukame ndo kwao, maji shida, Hali ya hewa mbovu, jua kali ndo kwao, vurugu Sasa ndo chimbuko lake. Siku moja tulikuwa na mechi ya kirafikina timu ya Kijiji jirani ile tupo kwenye gari tukashangaa tunaanza kurushiwa mawe barabarani.

Kwa kuwa sisi tulikuwa wageni tuliogopa sana lakini wenyeji wakatuambia msiogope hao wote tutakutana kwenye mnada. Siku nyingine tulikuwa Mnadani Sirorisimba siku hiyo kulikuwa na mgogoro wa mpaka wa shamba kati ya ukoo na uko huku polisi wakiwa na mitutu ya bunduki lakini ilivyo ajabu watu wa kule nilishudia wakibebana na kuhamasishana wabebe mishale waende wakaanzishe vurugu.

Wewe ulipita wapi na ulistaajabu nini?
Tabora Kuna sehem Moja Kuna njia panda ya kwenda mpanda na barabara lingine linaingia maporini......Picha linaanza mwenyeji alokuja kutupokea usiku mwenyewe alitupoteza, pili hatukua tukiona nyumba Wala chchte ni Giza tu......Tumesogea mbele tukashuka kweny gari kuangalia tuelekee usawa gani katokea bonge bonge ya joka tukakimbilia kweny gari tukaanza tena kuitafuta njia tukaipata

Tulivofika hapo msibani tukala tukala usiku nmelala nasikia kitu kikubwa kipo mgongoni kwangu kuwasha tochi nakutana na panya analinga a kichwa na Putin. Weeeh nlipiga kelele watu wote wakaamka nduki
Asubui nmeamka wakasema tuende tukapaone sehem alipozikwa ndugu yetu tukafika tukaanza kurudi nyumbani tukakutana tena na joka nlikua natetemeka hadi nikaingia period

Tukarudi nyumbani muda wote natembea sion nyumba za watu nkajiuliza Ina maan huku watu wanatokea wapi kumbe huko ndani ya msitu zaid

Siku tunarudi tukakutana barabarani na fisi mara na mbwa mwitu mara nyoka kakaa katikati ya barabara eeeh nyumba tukaona chache sana zenyewe ziko mbali mbali
Tulivofika center bwana weeeh nilijikuta nipo hospital maan nlikata moto gafla baada ya kusema tumbo linauma

Nilijiuliza watu huko wanaish vp, nyoka kila Kona, fisi mbwa mwitu,wanakunywa maji meupe kama maziwa, hospital ni mbali kias kwamba lazima uombe Pooh
 
Kijiji cha Gamboshi kilichopo wilayani Bariadi mkoani Simiyu.

Ntarudi.
Kutoka Bariadi mjini unapita kijiji cha Ngulyati kiasi cha kilometa 30 Mashariki ya Bariadi katika barabara itokayo Bariadi kwenda Magu, lakini hakuna kibao kinachotambulisha Kijiji cha Gamboshi mwanzoni mwa barabara ya vumbi inayoelekea Gamboshi kutoka Ngulyati.

Upande wa kaskazini kijiji hicho kinapakana na kijiji cha Kisesa kilichopo wilaya ya Busega, kusini kinapakana na Nyamswa, Magharibi kijiji cha Lulayu, kusini- Magharibi kijiji cha Ditima na Mashariki kijiji cha Miswaki.

Wananchi wa kijiji hicho ni wacheshi, wachapa kazi na wanajali wageni kwa kuwapa historia ya kijiji hicho huku wakitumia nafasi hiyo kuwaondolea dhana iliyojengeka kuwa ni kijiji cha wachawi.
 
Tabora Kuna sehem Moja Kuna njia panda ya kwenda mpanda na barabara lingine linaingia maporini......Picha linaanza mwenyeji alokuja kutupokea usiku mwenyewe alitupoteza, pili hatukua tukiona nyumba Wala chchte ni Giza tu......Tumesogea mbele tukashuka kweny gari kuangalia tuelekee usawa gani katokea bonge bonge ya joka tukakimbilia kweny gari tukaanza tena kuitafuta njia tukaipata

Tulivofika hapo msibani tukala tukala usiku nmelala nasikia kitu kikubwa kipo mgongoni kwangu kuwasha tochi nakutana na panya analinga a kichwa na Putin. Weeeh nlipiga kelele watu wote wakaamka nduki
Asubui nmeamka wakasema tuende tukapaone sehem alipozikwa ndugu yetu tukafika tukaanza kurudi nyumbani tukakutana tena na joka nlikua natetemeka hadi nikaingia period

Tukarudi nyumbani muda wote natembea sion nyumba za watu nkajiuliza Ina maan huku watu wanatokea wapi kumbe huko ndani ya msitu zaid

Siku tunarudi tukakutana barabarani na fisi mara na mbwa mwitu mara nyoka kakaa katikati ya barabara eeeh nyumba tukaona chache sana zenyewe ziko mbali mbali
Tulivofika center bwana weeeh nilijikuta nipo hospital maan nlikata moto gafla baada ya kusema tumbo linauma

Nilijiuliza watu huko wanaish vp, nyoka kila Kona, fisi mbwa mwitu,wanakunywa maji meupe kama maziwa, hospital ni mbali kias kwamba lazima uombe Pooh
Hizi period za mwendokasi zinatishia afya ya dada zetu
 
Dodoma ni hatari ,kuna vijiji vinapatikana shortcut (mpwapwa to Iringa road)
Imagine hadi wakiona gari wanakimbia,ilibidi tushuke kwanza tuwauulize maswali ya hapa na pale kuhusu maji,chakula maana Hamna mazao kabisa na vumbi linatimka muda wote ,Vitoto vimebuka hatari unahisi hata wakipiga maji hawatakati,kiswahili pia shida
Kuna kijiji huko dodoma walishambulia watafiti.
 
Tabora Kuna sehem Moja Kuna njia panda ya kwenda mpanda na barabara lingine linaingia maporini......Picha linaanza mwenyeji alokuja kutupokea usiku mwenyewe alitupoteza, pili hatukua tukiona nyumba Wala chchte ni Giza tu......Tumesogea mbele tukashuka kweny gari kuangalia tuelekee usawa gani katokea bonge bonge ya joka tukakimbilia kweny gari tukaanza tena kuitafuta njia tukaipata

Tulivofika hapo msibani tukala tukala usiku nmelala nasikia kitu kikubwa kipo mgongoni kwangu kuwasha tochi nakutana na panya analinga a kichwa na Putin. Weeeh nlipiga kelele watu wote wakaamka nduki
Asubui nmeamka wakasema tuende tukapaone sehem alipozikwa ndugu yetu tukafika tukaanza kurudi nyumbani tukakutana tena na joka nlikua natetemeka hadi nikaingia period

Tukarudi nyumbani muda wote natembea sion nyumba za watu nkajiuliza Ina maan huku watu wanatokea wapi kumbe huko ndani ya msitu zaid

Siku tunarudi tukakutana barabarani na fisi mara na mbwa mwitu mara nyoka kakaa katikati ya barabara eeeh nyumba tukaona chache sana zenyewe ziko mbali mbali
Tulivofika center bwana weeeh nilijikuta nipo hospital maan nlikata moto gafla baada ya kusema tumbo linauma

Nilijiuliza watu huko wanaish vp, nyoka kila Kona, fisi mbwa mwitu,wanakunywa maji meupe kama maziwa, hospital ni mbali kias kwamba lazima uombe Pooh
Poleeee 🤣🤣🤣
 
Dodoma ni hatari ,kuna vijiji vinapatikana shortcut (mpwapwa to Iringa road)
Imagine hadi wakiona gari wanakimbia,ilibidi tushuke kwanza tuwauulize maswali ya hapa na pale kuhusu maji,chakula maana Hamna mazao kabisa na vumbi linatimka muda wote ,Vitoto vimebuka hatari unahisi hata wakipiga maji hawatakati,kiswahili pia shida
Mpwapwa kwa ujumla tu sijawahi kabisa kupaelewa.
 
Ukitokea W .Mkalama ukipita daraja la sibiti kwenda kutokea Meatu Kuna Kijiji baada ya Daraja la sibiti ambalo limeshakamilika ujenzi asee wale watu is so special tulikuta ngoma pale asee vitoto umri around 16 /20 vinacheza chuchu hazarani ..hakika iyo siku mkuyenge ulipata tabu sana
 
Kwa mara ya kwanza kufika kijiji cha Bugamba kilichopo mwambao wa Ziwa Tanganyika Kigoma vijijini nilipigwa na mshangao baada ya kushuka kwenye boti kutokea Kibirizi Kigoma ! Pale boti zinapoegesha sikuona nyumba yoyote ! Mwenyeji wangu kaniambia tunaenda nyumbani yaani ananionyesha juu utafikiri tunaenda mwezini ! Kutoka hapo tunapanda huko juu nilitaka kulia maana chini Ziwa Tanganyika juu ndio kijijini, halooo kupanda ilibidi mpaka nishikwe mkono. Kufika huko juu ndoo nakuta kijiji na shule ya msingi ukitizama chini ziwa Tanganyika liko bondeni ! Kwa kweli inatisha kijiji hicho hakuna shamba la maana sehemu kubwa ni milima tu mihogo wanalima kwenye mitelemko ya milima na ukiteleza unaporomokea ziwani na ziwa lina kina kirefu ni hatari. Pale kijijini hakuna baiskeli maana mazingira hayaruhusu ! Shughuli za uchumi pale ni uvuvi. Ukitaka kwenda kijiji cha jirani cha Zashe au Mwamgongo lazima utumie boti kwa mguu haiwezekani.
Toka siku hiyo nikajua sababu ya waha wengi kukimbilia mikoa ya Jirani kama Mwanza, Geita, Tabora na Katavi maana mazingira ya maeneo hayo ni magumu sana. Kweli maeneo hayo ukifika mpaka unajiuliza kwamba hivi hawa watu huku walifuata nini.
Mkuu 😂😂😂
Mimi nina picha kabisa za hivyo vijiji nimefika huko yaani sehemu hata baskeli haifiki. Usafiri ni mitumbwi tu.
Niliwauliza hivi mnajua rais wa sasa hivi ni nani? Wakasema samia nikasema mmejuaje maana huku tv hamna wala network hashiki😂
Sema yale mazingira ya ziwani mazuri sana kama unataka kufanya retreat ya kujitenga na watu. Ukijani na ziwa + milima milima.
Yaani mtu anaamka asubuhi anaenda kupia mswaki ziwani maana ziwa lipo umbali kama wa mita mia.

Hiyo ya kulima milimani nilishagaa sana maana wakati wa kushukainabidi uwe makini kweli kweli unaweza kuteleza na kuanguka bondeni huko.

Baada ya kwenda hilo eneo niligundua kwanini Wasanii wakipanda kilimanjaro huishia njiai.
Mimi napenda nature, nimetembea mapori mengi humu TZ na kujionea mengi
 
Vijiji vingi vya wilaya ya Bariadi mkoa wa Simiyu utashangaa wasukuma Sijui walifata nini huko, unakuta kijiji hakina umeme Wala maji. Yaan Maji yao wanachimba mabwawa kipindi cha mvua Maji yanatuama humo basi ng’ombe na binadam wote ndo mnakunywa Maji hayo!! Maji Kama maziwa kuna wachawi huko sijapata ona!! Wanga wananza kuwanga saa moja jioni!! [emoji2][emoji2]
Huko unakuta msukuma ana ng’ombe 50-100 ila anakula ugali na dagaa wa mwanza wale gredi ya mwisho kabisa ambao huwa kwaajili ya vyakula vya Kuku!![emoji2][emoji2] huko ikifika saa 12 jioni tembo kutoka serengeti wanaingia kijiji kula miwa[emoji23][emoji23]

Sasa bosi hapo ni Bariadi... Ukiingia ndani kuna wilaya kama itilima nk. saa 11 fisi wanapiga misele.
 
Back
Top Bottom