Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Ni sehemu gani ya nchi, mji au Kijiji ulifika mpaka ukajiuliza watu waishio huko walifuata nini?

Nimefanya kazi kama na kuishi huko. Nakushauri, nenda kapige mishe. Ni eneo zuri sana na watu wanalima sana. Kilimo kikubwa ni Mpunga na wanatoa kwenye bonde la Mwamapuli, Mamba, lake Rukwa na Kasansa. Kuna elimu za umwagiliaji za uhakika na Mpunga wanaolima hawatumii mbolea. Pana mzunguko mkubwa wa Pesa kwani wasukuma na Waha wengi wameinvest huko kwenye Kilimo, Biashara na ufugaji. Pia wanalima ufuta kama zao lingine la kibiashara. Pamechangamka sana na muda wataipata hadhi ya Mamlaka ya Mji mdogo Maji moto. Panapitika mwaka mzima kwa barabara za uhakika, unaweza kwenda Sumbawanga, Mpanda Mjini na Tabora pitia daraja la Kavuu. Nenda mkuu, ukiwa na akili unatoka kimaisha. Kunefunguka sana japo ni nilitoka huko 2014
asande sana mkuu.
 
Sasa panaweza kuwa Pazuri kwani ni kijiji na sasa ni kata ya Wawindaji. Nimeishi huko japo zamani. Barabara sasa nasikia ni ya uhakika na mawasiliano sasa nasikia yapo. Ni pazuri kwa kweli kwani jamaa wanalima sana japo zao kubwa ni Tumbaku. Kijiji hiki kuna misitu mingi ya asili ukiwa Majanja unapiga maisha oitia Mininga na Mikora. Pia kuna wanyama wengi ukiwa jangili utapiga pesa. Kijiji hiki kuna kijiji kingine jirani kipo Singida kama sikosei, kuna madini na watu wanapiga sana pesa. Ni pazuri bro, nenda kafanye Maisha japo nakushauri Majimoto is the best.
thanks alot bro, asande sana kwa maelezo yako,

ubarikiwe.
 
Sehemu nyingine ipo wilaya ya Mbalali mkoa ni Mbeya kule Blonde la Mpunga la Usangu. Kule kuna vijiji vingi Sana. Kuna Kijiji nilikaa pale Miezi nilishangaa Sana.

1. Sikuwahi kusikia Kuna kituo cha police au police . Kule bangi inavutwa kama sigara.

2. Kwa wale wala kitimoto kule inauzwa kama Dagaa.

3. Kwasababu kitimoto ni nyingi Sana na hawaoimi Kwa kilo wanaweka Kwa mafungo kama nyanya. Kitimoto ya 4,000 ukimaliza wewe ni shujaa.

4. Sikuwahi kuona limao, kitunguu , Ndizi za kuiva wala nyanya.

5. Hiyo kitimoto inapikwa Ila bila hivyo vitu hapo juu.


6. Usiku kuisikia Sauti ya wanyama wakali kama Simba na tembo ni kawaida.


7. Kuna Baridi usiku kama uko Yemen au Kwenye Vilima Vya magaidi wa Taliban kule Afghanistan.

8. Sikuwahi kuona kiwanja cha mpira hata kupiga danadana.


9. Kule mchele na wali unaweza Kula Hadi ufe hakuna Kijiji nimetembea tanzania nikakuta kina mchele kama kile.
 
Tabora Kuna sehem Moja Kuna njia panda ya kwenda mpanda na barabara lingine linaingia maporini......Picha linaanza mwenyeji alokuja kutupokea usiku mwenyewe alitupoteza, pili hatukua tukiona nyumba Wala chchte ni Giza tu......Tumesogea mbele tukashuka kweny gari kuangalia tuelekee usawa gani katokea bonge bonge ya joka tukakimbilia kweny gari tukaanza tena kuitafuta njia tukaipata

Tulivofika hapo msibani tukala tukala usiku nmelala nasikia kitu kikubwa kipo mgongoni kwangu kuwasha tochi nakutana na panya analinga a kichwa na Putin. Weeeh nlipiga kelele watu wote wakaamka nduki
Asubui nmeamka wakasema tuende tukapaone sehem alipozikwa ndugu yetu tukafika tukaanza kurudi nyumbani tukakutana tena na joka nlikua natetemeka hadi nikaingia period

Tukarudi nyumbani muda wote natembea sion nyumba za watu nkajiuliza Ina maan huku watu wanatokea wapi kumbe huko ndani ya msitu zaid

Siku tunarudi tukakutana barabarani na fisi mara na mbwa mwitu mara nyoka kakaa katikati ya barabara eeeh nyumba tukaona chache sana zenyewe ziko mbali mbali
Tulivofika center bwana weeeh nilijikuta nipo hospital maan nlikata moto gafla baada ya kusema tumbo linauma

Nilijiuliza watu huko wanaish vp, nyoka kila Kona, fisi mbwa mwitu,wanakunywa maji meupe kama maziwa, hospital ni mbali kias kwamba lazima uombe Pooh
Mwaka gani hii ilikuwa?
 
Kuna kijiji kipo Iringa ndanindani[emoji16][emoji16]

Asubuh nikaletewa maji ya kuoga nikaoga fresh sasa ilivyofika jioni nikasema ngoja niende na huyo dada nikachote mwenyew [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hicho kisima unachota maji pamoja na chura, unafanya kuwatoa chura kwenye ndoo ili upate maji aiseeh

Ikifika mida ya saa 12 jioni wanakijiji wote wanaenda kilabuni inshort kijiji kizima wanamwagilia moyo[emoji23]
 
Nimesafiri karibia mkoa mziam wa sumbawanga na katavi nilienda kijij kimoja kipo nkasi gerezani kule tulienda nikakuta kijij sijui ndio center watu Ni wakora kinyamaa wakta nacheki cheki Kama nitampata mwalifu tulio muendee nikaona ngoja nichungulie ndani Kuna kibanda kipo kipo naziona silaya nzito nzito ndani mle nikasema moyon muda wowote nitatandikwa risasi

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Siku moja niko na jamaa yangu tunatafuta mashamba ya kukodi ya alizeti tulikua na mwenyeji anatutembeza mashambani. Mchana tunataka kurudi mwenyeji akatuambia twende kwanza kwake tule ndio tuondoke. Tukaona si mbaya.
Tumefika tukaenda sebuleni Chakula kikaja nikasahau kabisa kama Chakula chao kikuu ni mlenda.
Bwana bwana ulikuja ugali mgumu na mlenda mimi nilikua sijawahi kula mlenda wala ugali wa mtama[emoji28]

Nilihangaika mwenye ananiambia mbona hauli au chakula kibaya? Mimi naguna guna tu[emoji23], nilishwindwa kula aisee ilibidi nikaupiga picha hii hapa chini.
Yaani utadhani unakula hina. Watu wanawakiwa na jua huko ndio maana miguu yao imekomaa halafu myembamba kama mianzi imechomekwa kwenye mapaja [emoji125][emoji125]View attachment 2379797
Mi pia nilishindwa kula huu mlen damwenzenuu Kaahh!!!
 
Narudia tena hakuna mkoa masikini kama Dodoma.

Mkoa ule ni hatari huko wilayani.

Nilienda huko Kijiji Cha Chimendeli wilaya ya Bahi, Kwanza hiki Kijiji ndio kinaongoza kutoa omba omba wengi Sana tanzania.

Familia zinashindana kuja mijini kuomba omba. Mzazi anaweza kumtuma mtoto wake aende mjini awe omba au mzazi anaweza kuja mjini na familia nzima waje kuwa omba omba!

Kwa ambao mko Dar Es Salaam kuanzia Leo jitahidi ukikutana na omba omba watoto au wazee wadadisi Kwa maswali halafu waulize wanatoka Kijiji gani. Halafu piga nao story hutakaa uamini !


Kama ulivyo kwenu vijana wanasoma Kwa jihadi zote waje kuwa Madaktari Ila kuna sehemu hii tanzania watu Wana ndoto za kuwa omba omba. Au kama hamuamini Ulizieni hata walimu WA Shule walioko hicho Kijiji. Watoto hawaendi shule.

Sehemu ni kame.


Lile eneo unaweza kudhan upo Pakistan au Kule Yemen.


Eneo lingini ni vijiji vya wilaya ya kongwa.


Acha niishie hapa.
Uko sahihi 100%nakukubalia nimepitia vijiji vingi vya Dodoma ,Kuna umaskini wa kutisha
 
Kuna kijiji nilifika kutafuta ndizi biashara miaka hiyo.
Aisee ni mbali katikati ya turiani na korogwe njia ya pori kwa pori.hamna magari ni kwenda kwa baskeli tu alafu unachepuka kwenda mlimani huko nikakuta kakijiji aisee vijumba kichekesho,alafu wana mfalme wao yaani chakula wanakula woote familia zoote pale kwa mfalme.
Kila kaya inaleta ilichopika pale.
Nilikula mboga mboga mpk nilikoma.
Siku nikalogwa nikanunua kuku 2 wameniuzia wao wenyewe kaya 1 niliokuwa nakaa nikawapa wapike nikajua ntakula japo nusu aaah wakapeleka kwa mfalme kule tunakokula nikaambulia kibawa,yaani mkulu ana nyofoa kinyama anampa mtu kushoto au kulia kwake kinatumwa mpk kikufikie kila mtu kakishika
Nilikasirika sana.
[emoji28][emoji28][emoji28]

#MaendeleoHayanaChama

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Kuna kijiji nilifika kutafuta ndizi biashara miaka hiyo.
Aisee ni mbali katikati ya turiani na korogwe njia ya pori kwa pori.hamna magari ni kwenda kwa baskeli tu alafu unachepuka kwenda mlimani huko nikakuta kakijiji aisee vijumba kichekesho,alafu wana mfalme wao yaani chakula wanakula woote familia zoote pale kwa mfalme.
Kila kaya inaleta ilichopika pale.
Nilikula mboga mboga mpk nilikoma.
Siku nikalogwa nikanunua kuku 2 wameniuzia wao wenyewe kaya 1 niliokuwa nakaa nikawapa wapike nikajua ntakula japo nusu aaah wakapeleka kwa mfalme kule tunakokula nikaambulia kibawa,yaani mkulu ana nyofoa kinyama anampa mtu kushoto au kulia kwake kinatumwa mpk kikufikie kila mtu kakishika
Nilikasirika sana.
[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]
 
Kuna kijiji kinaitwa lipalilo kule hakufai mwaka 2013 labda sahivi Kuna mabadiliko Ila mazingira ya wakinga magumu sana
Na Kuna Kijiji Cha utengule pembezoni mwa safu za milima ya Kipenge Mkoa wa Njombe Ni Kama Kisiwa wakinga wa kule wakitaka mahitaji wanakuja wilaya jirani ya Kyela sehemu hiyo inaitwa Ngyekye kupitia hiyo milima wakati huo nasoma Shule moja Matema Beach Sec Basi usiku unaona tochi hapo ujue ndo wanashuka Mnadani kufuata mahitaji hasa siku ya alhamisi. Utastaajabu mlima una urefu wa Mita 2600 lakini wanashuka madebe ya ngano kichwani au maharage ndipo auze halafu arudi na madebe ya mchele. Sisi tulipanda ule mlima tukiwa hatuna mizigo lakini tulichoka mpaka tulitoa jasho la njano. Jamaaniiiiiiii usimuliwe tu unakutana wamama mpaka wanavipara nywele zimenyonyoka ktokana na kubeba mizigo wakati huo anapanda mlima akiwa na andasket tu maziwa yote njenje Kama makilikili na hawashtuki. Duuuu Tanzania Ni Pana. Sijui walifuata nini Kule.
 
Habari za muda huu wana JF,

Nchi yetu ni kubwa na Ina miji na vijiji vingi lakini Kuna baadhi ya maeneo unaweza ukahisi sio sehemu ya nchi yetu mpaka ukajiuliza maswali kuwa Hawa watu waishio hapa walivutiwa na Nini mpaka wakaweka makazi ya kudumu maeneo haya

Mfano, Mimi niliwahi kutembelea Kijiji cha Baranga kata ya sirorisimba kupitia Kyagata. Nilistajabu na kujiuliza Hawa watu huku wanaishije?

Ukame ndo kwao, maji shida, Hali ya hewa mbovu, jua kali ndo kwao, vurugu Sasa ndo chimbuko lake. Siku moja tulikuwa na mechi ya kirafikina timu ya Kijiji jirani ile tupo kwenye gari tukashangaa tunaanza kurushiwa mawe barabarani.

Kwa kuwa sisi tulikuwa wageni tuliogopa sana lakini wenyeji wakatuambia msiogope hao wote tutakutana kwenye mnada. Siku nyingine tulikuwa Mnadani Sirorisimba siku hiyo kulikuwa na mgogoro wa mpaka wa shamba kati ya ukoo na uko huku polisi wakiwa na mitutu ya bunduki lakini ilivyo ajabu watu wa kule nilishudia wakibebana na kuhamasishana wabebe mishale waende wakaanzishe vurugu.

Wewe ulipita wapi na ulistaajabu nini?
Lindi
 
kuna mtu amewahi kufika kijiji kinaitwa “mbaa na vya mbele yake”? Ruvuma huko?2013 nilifika hakukuwa na mawasiliank yoyote ya simu ,ukihitaji mfanye mawasiliano hadi msogee kwenye baadhi ya miinuko mikubwa inayofahamika hivyo hapo utakuwa watu wengi kila mtu anafanya mawasiliano na usafiri gari zikifika kwenye milima mnashuka ipande yenyewe kwanza abiria ndio mfwate,gari ikipita wanaikimbilia na kuiimbia

Nilienjoy safari na mazingira ya beach sio mchanga ni mawe na fukwe zake unaweza kwenda umbali mrefu bila kuzama
Siku hizi huko network ipo powa sana.kijiji kinaitwa Mbaha,vingine ni Lundu ,Lituhi,Nkiri,Mango,nk asubuhi hakuna chai unapata mchemsho wa samaki au dagaa fresh na ugali wa unga wa mihogo
 
Ukitokea W .Mkalama ukipita daraja la sibiti kwenda kutokea Meatu Kuna Kijiji baada ya Daraja la sibiti ambalo limeshakamilika ujenzi asee wale watu is so special tulikuta ngoma pale asee vitoto umri around 16 /20 vinacheza chuchu hazarani ..hakika iyo siku mkuyenge ulipata tabu sana
Wanyantuzu hao na mila zao

Ukifumwa na binti kule ngwekwe inakuhusu ( faini ) na wanakususia mtoto wao sijui utafanyaje maana nyengine ni za kutegesha

Wengi hawajasoma na hawajui kiswahili mtoto akisoma mahari za ng'ombe zinapungua kuogapa matatizo na serikali ndio maana wanaambiwa wajifelishe
 
Siku hizi huko network ipo powa sana.kijiji kinaitwa Mbaha,vingine ni Lundu ,Lituhi,Nkiri,Mango,nk asubuhi hakuna chai unapata mchemsho wa samaki au dagaa fresh na ugali wa unga wa mihogo
Yes , mbaha na huko kwengine na wenyeji wakarimu sana maeneo yote hayo tuliyozunguka muda wote tuliikuwepo walionyesha ushirikiano nasi na hata chakula wakajitolea kwa Hiari yao ni samaki,kuku,mbuzi na unga wa muhogo

Tatizo lilikuwa kwenye network tu na ilikuwa inashika MTN na radio za Malawi ,kingine lugha kwa wakazi ya maeneo yale

Mpakani Tz - Malawi walizoea kupita kama nyumbani kwao,mambo ya taratibu na Sheria baadhi walikuwa hawajui + athari
 
Back
Top Bottom