Ni shule gani ya sekondari ilijengwa na wakoloni Waarabu halafu Serikali ikaitaifisha baada ya uhuru 1961?

Ni shule gani ya sekondari ilijengwa na wakoloni Waarabu halafu Serikali ikaitaifisha baada ya uhuru 1961?

Waarabu hawajawahi kutawala Tanganyika

Mwanzoni mwa miaka ya 1700, Baada ya Kristo, Sultani wa nchi ya Kiarabu, ya Oman, aliteka Pemba na Kilwa.Na badae miji yote ya Pwani ya Afrika ya mashariki ikawa chini ya utawala wa Sultaani wa Oman. Mwaka wa 1840, Said bin Sultani alihamisha makao makuu ya himaya yake, kutoka Oman, akahamia Zanzibar. Sasa pwani yote ya Afrika Mashariki na Oman Uarabuni, ilikuwa chini ya serikali ya Zanzibar

Kilwa sio Tanganyika ?
 
Habari wadau.

Nasikia baada ya kupata uhuru mwaka 1961 Serikali ilitaifisha shule zilizojengwa na wakoloni. Mfano shule zilizojengwa na wakoloni wazungu kama Minaki, Ilboru, Pugu, Mazengo, forodhani, etc

Je, ni shule zipi zilitaifishwa ambazo zilijengwa na wakoloni Waarabu?

Maana waarabu walitangulia kuja Tanganyika na Zanzibar kwa kwa miaka zaidi ya 500 kabla wakoloni wazungu hawajaja.

Zanzibar pia waarabu walifika mapema sana maana msikiti wa Kazimkazi ulijengwa mwaka 1006 AD, waarabu walitawala kwa miaka mingi Zanzibar na walifika mapema sana, naomba mnitajie ni shule gani ya sekondari waarabu walijenga Zanzibar, na ilijengwa mwaka gani?
Hapo kuna vitu viwili niwasaidie wakati nyerere anataifisha shule taasisi nyingi za waarabu hazikuwepo ila zilikuwepo taasisi za dini ya kiislamu mfano mzuri ni agha khan and ect... ambazo baadhi zilikua zinaendeshwa na waarabu nazo mali zake pia zilitaifishwa!!!Mfano mzuri taasisi za washirazi na taasisi za Ismailiya zote hizi zilikua na shule za mafunzo either dini au elimu dunia!!!!Kumbukumbu zipo au wewe unataka kujua waarabu kama walijenga shule za elimu dunia????????Kusema kweli wakoloni wa kiarabu hapa tanganyika hasa upande wa zanzbar hawakujihusisha sana na elimu dunia masna ingewanufaisha tabaka la chini(Wabantu)!!!Hasa wakoloni wa kiarabu kutoka Oman!!!!!Sababu omani kwenyewe elimu dunia ilianza kuuingia pale Sultan Qaabos alipompindua baba yake na kufanya mageuzi ya kiutamaduni na kiuchumi
 
Mwanzoni mwa miaka ya 1700, Baada ya Kristo, Sultani wa nchi ya Kiarabu, ya Oman, aliteka Pemba na Kilwa.Na badae miji yote ya Pwani ya Afrika ya mashariki ikawa chini ya utawala wa Sultaani wa Oman. Mwaka wa 1840, Said bin Sultani alihamisha makao makuu ya himaya yake, kutoka Oman, akahamia Zanzibar. Sasa pwani yote ya Afrika Mashariki na Oman Uarabuni, ilikuwa chini ya serikali ya Zanzibar
Kabla ya hapo huko nyuma walikua wanakaa wafanyabiashara wa kiarabu na wabantu!!!Sultan Sayeed Alipokuja kuteka yeye akaanzisha utawala baadae akahamia kabisa!!!Kuna binti yake wa kike aliandika kitabu miaka hiyo na kuna page kawaponda sana watu wenye ngozi nyeusi(Wabantu)!!!!Kitafute kinaitwa Memory of Arabian Princess tafuta nakala ya kingereza!!
 
Waarabu walitawala mwaka gani? wale ni wafanyabiashara walikuwa na trade routes zao walipopita ndo waliacha tamaduni zao...
Walitawala Ukanda wa Pwan mikoa yote ya pwanii ilikuwa chini ya sultani wa Zanzibar
 
Wagalatia kwanini munateseka sana na Waarabu?
Watu wengi wa pwani waliokuwa chini ya utawala wa Sultani Mwarabu hulalamikia wazungu kuwa waliwanyima elimu kwenye kelele zao na maandishi yao

Wakati mzungu alikuja baadaye sana .Mwarabu ndie aliwahi na kutawala Zanzibar na Tanzania bara Ukanda wa Pwani

Badala ya kuwalakamikia waarabu waliowatawala miaka mingi kuwa hawakuwajengea shule za elimu dunia Kelele wanapekea wazungu waliokuja baadaye sana
 
Waarab wametawala Zanzibar na Pwani kwa miaka karibubl 1,000 na hata maili kumi za pwani Mjerumani aliuziwa na Sultan wa Zanzibar. Walishindwa kijenga shule au vyuo? Bado kuna pockets nyingi za nchi Waarabu walikuwepo kwa mida mrefu kama watawala kabla ya Wazungu kama vile Ujiji, Tabora, na central corridor karibu yote. Hawana cha kujitetea...
Lakini utakuta kutwa watu wa Pwani na Zanzibar hulaumu wazungu waliokaa muda mfupi kuliko waarabu wao

Kiongozi wa kuwapiga mawe wazungu kuwa waliwanyima waafrika wa Pwani na Zanzibar ni mtu mwenye asili ya kiarabu anaitwa Mzee Mohamed Said kaandika vitabu vingi vya kuponda wazungu ili kuficha aibu ya waarabu wenzie ambao kwa miaka elfu moja waliyotawala Zanzibar na ukanda wa pwani hawakuanzisha shule wala vyuo vikuu

Si kuwa havikuwepo nchi za kiarabu vilikuwepo lakini hawakuleta
 
Watu wengi wa pwani waliokuwa chini ya utawala wa Sultani Mwarabu hulalamikia wazungu kuwa waliwanyima elimu kwenye kelele zao na maandishi yao

Wakati mzungu alikuja baadaye sana .Mwarabu ndie aliwahi na kutawala Zanzibar na Tanzania bara Ukanda wa Pwani

Badala ya kuwalakamikia waarabu waliowatawala miaka mingi kuwa hawakuwajengea shule za elimu dunia Kelele wanapekea wazungu waliokuja baadaye sana

sasa mkuu waarabu watajengaje shule hio miaka unayoizungumza wakati hata wao wenyewe hawakuwa nazo? Hayo mambo ya shule ni program za kimagharibi na wazungu ndio waliozisambaza kwenye ulimwengu na ni moja ya silaha yao kubwa wanayoitumia katika kuutawala Ulimwengu. Waarabu walikua na njia zao za kitaalmu zakiasili kama ilivyo kwa waafrika.
Mzungu ndie aliekuja nayo hii elimu ya ki secular ambao ndio mfumo wa elimu wa kisasa na yeye ndie alichagua nani wakumpa. Na wakati waislamu walipoanza kuji organize katika kutengeneza mazingira ya wao kupata hiyo elimu ndipo Nyerere alipowakata miguu. kwanini munakuwa na shida kwenye kufahamu?
 
Waisilam wangejenga vipi nawao hawa kuwa watala wa nchi hii wazungu ndio waliokuwa watala kwa mgogo wa kanisa
Uislam upo Kilwa na Bagamoyo toka miaka ya 1200 huko kabla hata wazungu hawajaota kuja Huku.

Jibuni swali la mtoa mada acheni janjajanja
 
Waarabu Wana mifumo yao ya elimu huu mfumo wa shule ni mfumo wa wakoloni wa kizungu. Hata waafrika tulikuwa na mfumo wetu wa elimu. Waarabu walijikita Sana kueneza dini na utamaduni wao. Mfumo wao wa maisha ni elimu ya dini na biashara, thus hata sasa 80% ya matajiri nchini ni waislamu sababu ya asili yao. Hizi elimu za kukariri darasani KISHA ukaajiriwe serikalini ni ideology za Wakristo. Wafanyabiashara wengi ni waislamu, wamiliki wa malori, mabus, daladala, tax, maduka, magorofa, viwanda, masokoni wengi ni waislamu . Wakristo wapo kwenye ajira zaidi unajenga nyumba moja ya kuishi na moja ya kupanga maisha yameishia hapo unastaafu unasubiri kufa kwa cycle hio hio.
Sasa mbona wewe unapeleka watoto wako shule katika huo mfumo wa wazungu?
 
Waarabu walitawala mwaka gani? wale ni wafanyabiashara walikuwa na trade routes zao walipopita ndo waliacha tamaduni zao...
Uko Dunia Gani mkuu.?

Tangu Karne ya Kumi na mbili Kilwa inakaliwa na Waarabu na lilikua ni Jiji kubwa Afrika Mashariki na Kusini yote. Lilikua ni Jiji la maana sana lenye kila aina ya maisha ya Raha na likiwa na pesa yake .
Hujawahi kufika Kilwa mkuu. ?
Wamatumbi wenye asili ya Kiarabu hawskutokea Kwa bahati mbaya mkuu.

Elimu rasmi ya darasani ni Mali ya mzungu Hilo anayebisha anabisha TU kishabiki maandazi.

Waarabu wamekuja Tanganyika zamani sana kabla ya Kuvurumishwa na wareno na wajerumani na kusambaratika kabisa. Karne ya Saba Waarabu wanafanya biashara na Pwani ya Afrika Mashariki. Karne ya Kumi na mbili wakaanza makazi Kilwa na kuwa kama Wenyeji na kuunda himaya kubwa sana.

Hata Mkoloni Mjerumani alikaribishwa Tanganyika na Mwarabu ndio maana walikua wanapitia Zanzibar kujitambulisha na kupewa Kibali Cha kuingia Nchini.Walipewa maeneo ya kutembelea ya Bara mana watu wa bara walikua ni wakorofi na wengi hawakua na dini ya kiislam hivyo Waarabu waliamua kuwapa Wazungu maeneo hayo watembelee na kufanya uchunguzi wao na kuhubiri dini ya kikirsto. Baadae Wazungu wakatumia Dini na Shule kueneza ukoloni na kupata nguvu kubwa kuliko Waarabu waliotangulia Karne nyingi na kujikuta wote wanatawaliwa na wazungu.
 
Sasa una elimu ambayo ni ustaarabu wa kimagharibi hamna cha maana...Wao wanajielewa hawakopi ovyo kama nyie wana elimu zao Wana maisha Bomba hata maendeleo makubwa.

We Tanzania one unajiproud na nn ? Zaidi ya kuwa mjinga .

Dunia nzima Afrika ndo tunafuata elimu za wazungu coz bado hatujiwezi nenda Korea, China, Iran Wana mifumo yao tofauti na elimu zao hata kiteknolojia wako juu.
Waafrika Bado wanaakili za hovyohovyo Kwa sababu ya Imani za hovyohovyo.

Wakristo hasa wakatoliki wanajishikamanisha sana na Wazungu na kuwaona kama ndio miungu mpaka kuweka picha za kijana mzungu mwenye macho ya bluu eti ni picha ya Yesu. Wanaabudu sanamu ya mzungu wakiita yesu na picha ya mdada mzungu wanamwita bikira maria. Yesu alikua ni Myahudi anayefanana na mwafrika na hakuwa mzungu. Lakini Hilo hata haliwafungui macho kabisa wanazudi kujifanya Dunia ya Kiafrika kuwa chini ya wazungu kuanzia kwenye Imani mpaka maisha ya kijamii na kisiasa na kiuchumi.

Siku waafrika watakapo sema no kwenye dini na siasa na uchumi Afrika itakwenda mbele sana.
Kuna watu ndani ya mifumo ni mawakala wa Himaya ya Kirumi na wako tayari kufanya hujuma yoyote ili TU Wazungu wakanywe mvinyo Pale Vaticani. Ujinga mtupu. Kama Mungu ni Roho Kwa Nini awakilishwa na kakundi ka wajanja wanaojificha Vatican na kuitawala Dunia yenye wajinga wengi Kwa mgongo wa dini.?

Mbona tungeweza kuwa Wakristo lakini bila kuathiriwa na Mila za Kizungu nauzungu?
Kama Ukristo ulianzishwa na Yesu kwa Nini tusifuate taratibu zinazoendana na maisha ya alipoishi Yesu ambapo ni Afrika na Uarabuni au Mashariki ya Kati? Yesu alizaliwa Israel na kukulia misri ambapo ni Afrika wakati huo hakuna dini ya Kiislam ya Leo lakini palikua na dini inayofanana na ya Uislam lakini pia hapakua na dini ya Kikirsto ila palikua na upagani unaofanana na Ukristo wa Leo.

Kwa upande wa pili Bado Uislam ni tishio Kwa Afrika na Dunia nzima mana lengo la Waarabu ni kuitawala Dunia Kwa mgongo wa dini.
Wakiitawala Dunia wale wasio Waarabu watakua ni watumwa wao. Kwanza Waarabu walipokuja Afrika walizaana sana na kukaribia nusu ya Bara la Afrika Sasa ni Waarabu au Wana asili ya Kiarabu. Kizazi Cha mwafrika kimenusuriwa na Mzungu.

Sasa jambo la Ajabu mwafrika anaingia madarakani Kwa Lengo la kulinda maslahi ya Vaticani au Saudi Arabia.
Uhalifu wote ndani ya madraka na watawala unalenga kulinda maslahi ya Waziungu na Waarabu
 
Sasa ndugu mwandishi mbona ushazitaja hapo kwenye uzi tayari? Unataka tuongeze nyingine au conceptyako ilikiwa ni kujua tu kama zipo hizo shule? Ok, shule kongwe kabisa kuliko zote hapa Tz ni Tanga Technical, kuna Bagamoyo, Pugu, Tabora boys nk
 
Back
Top Bottom