Ni upi utaratibu wa kumrudisha mke asiye na nidhamu nyumbani kwa wazazi wake?

Mwisho wa mwaka huu mkuu nenda naye kwao ukifika wewe muache kwa wazazi waambie utawatumia nauli ili warudi maana hesabu zimekaaa vibaya tumia njia hyo mkuu.
 
Unampeleka kwa wazazi wake kufanya nini?! Kama mmeshindwana kila mtu akae kwake kama kuondoka hapo mnaweza kubaliana wa kuhama, kama ni nyumbani kwako yeye aende kwake kama mmepanga gawaneni vitu kila mtu kivyake.
Huyo ni mtu mzima kwanini umpeleke kwa watu wengine?
Grow up Man.
 
Kama umepanga ondoka kwenye nyumba.. nenda kapange sehemu nyingine muache akae humo Ndani mwenyewe.. au usitumie chochote chake Wala usimuongeleshe Wala Kulala nae chumba kimoja na Kama ikiwezekana mtengenezee fumanizi kabisa Kama ushahidi wa sababu ya kuachana.. maamuzi magumu yanahitaji watu wenye mioyo migumu
 
Huyo jamaa nae ni tahira utaombaje msamaha kwa kitu ambacho hujafanya?,na anaanzaje tena kuishi na Mwanamke anaye kusingizia uongo mkubwa namna hiyo mbele ya watu?
Huo ni utahira.
Hayo unajiongelea wewe. Wanaoishi wana mengi usiwaone wanatembea,
Kuna mmoja na alikuwa na uwezo mkubwa,kamshika ugoni mke wake analiwa nanmlinzi,tenanchumbani kwake. Kapiga eeeeh wote tembezea kichapo. Mlinzi si akasema na wanae ada wanalipiwa na hilo limama! Jamaa akaamua aende kwao. Alikuwa na mtoto kama wa miaka miwili. Baadae jama kawatafuta wazee waende kuyamaliza mke arudi. Walivyofika,walilukwa wakaonekana wajinga. Ikawa kwamba mwanaume alimtega mtu ili amfukuze kwa sababu hamtaki ameshakuwa na hela. Jama aliaibika mwenyewe,na akaomba yaishe yeye sasa.
 
Dah! Mkuu,kumbe na wewe!? Pole sana. Kwanza likitokea hilo,tambua huyo si mkeo.
Sasa unaposema majirani wasijue,kwa hali hiyo unadhani wanajua mangapi? Hata usiyoyafanya wanajua. Hapo utasubili kutangazwa kuwa umefumaniwa na binti wa kazi,tena chini ya miaka 18.
Hapo usipokua muangalifu,unaishia jera.
Nyumba kama umejenga,kubali hasara. Maana umejitakia mwenyewe. Ila kama mmepanga,si wewe unalipa kodi? Hama. Uanze maisha upya. Jibu utaliona. Hata wanaomtafuta si kwa sababu wanajua ana kwake? Aanze kuomba matumizi na kodi uone sasa kama wote hawatakimbia. Akikupa watoto wako,lea. Akiwachukua,muachie. Kikubwa tu kila baada ya mda furani,mahitani yao yazingatie
 
Mwisho wa mwaka huu mkuu nenda naye kwao ukifika wewe muache kwa wazazi waambie utawatumia nauli ili warudi maana hesabu zimekaaa vibaya tumia njia hyo mkuu.
Hili ni kwa wale mama wa nyumbani mzee. Na kuna mtu alisema,unaachana nae,anaolewa mlango wa pili hapo hapo mnapokaa.

Tatizo kubwa kwa watu wanaokaa wote,hawawezi kukwambia chanzo cha mgogoro. Hiyo siku zote ni siri ya wawili waliowahi kuwa wanalala na mavazi ya Adam na Hawa.
Sasa,ukute mama ana biashara zake,hata kama anakaanga dagaa,umwambie aende kwao? Utaambiwa tangulia ntakukuta. Utakuwa na la ziada?
 
Kila jamii ina utaratibu wake. Uliwezaje kuoa bila kujua tararatibu nyingine za ndoa? Rudi kwa hao hao waliokuozesha watakupa utaratibu.
 
Hata mama yako alikuwa mke kwa baba yako,dada yako ataenda kuwa mke na shangazi yako vile vile...kikubwa tujifunze kutumia hekima ya kimungu kipindi cha kutafuta mchumba atakae kuja kuwa mke....

Wanawake wengine sijui ni ufinyu wa uelewa! Sijui wanachelewa kupevuka akili!? Wengine wapo kwenye ndoa lakini ni kama mgeni anae tegemea kuondoka muda wowote......

Sura,maumbile ni nyongeza tu kwenye mahusiano...tabia ndo kila kitu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…