Ni ushamba sana kutoka semina umebebelea kopo la maji uliyopewa kwenye semina, warsha nk

Ni ushamba sana kutoka semina umebebelea kopo la maji uliyopewa kwenye semina, warsha nk

Kuna binadamu mna roho mbaya sasa unataka maji yake amuachie nani kama hajayamaliza?

Mtoa post Acha makasiriko.
 
Huyo ni mimi kabsaaaa

iwe nimetoka kwenye semina au la, kama sina begi kubwa, lazma nitashikilia chupa ya maji mkononi kama bado nipo kwenye mizunguko yangu na sijali 📌📌
 
Hivi vitoto vya JF vinaleta thread kama hii ijadiliwe kweli??? huyu ndio great thinker???
nashangaa sana kuna kamoja juzi kalisema ati mtu kuongea kilugha chake ni ushamba . sijui mtu mshamba ni yupi?
mtu anatoka semina saa 10 jua limezama na anakwenda mbali... aache kubeba maji ili mvaa vinjunga na vi hereni asimuone mshamba?
 
Tunafanya maisha kuwa magumu kwa kupenda kufatilia na kutilia maanani vtu vidogo vidogo, Sasa mkuu niache maji halafu nikifika hapo mbele tu kidogo nikisikia kiu nianze tena kutafuta yanakouzwa ninunue?

Wengine muda wote tunatembea na maji iwe mkononi au kwenye begi.
 
Peace be upon you all,

Aise waTanzania ni watu washamba sana sana kabisa. Mwanzo nilidhani ni watumishi pekee wenye huu ushamba ila nimebaini ni watu wengi wa sekta zote.

Yani unakuta watu wamekwenda semina fulani alafu muda wa kutoka wamebebelea vimaji vya mia tano hako kakopo atakabeba njia nzima. Unajiuliza huyu ameshindwa kuyamaliza hayo maji na mara nyingi semina na warsha wanagawa vimaji vya 600 ml. (Vile vimaji vya 500 Tsh).

Wanamake sasa aise hawa ndugu ni washamba haswa, unakuta mmama na heshima zake semina imekwisha anaenda anaomba maji yaliyobaki chupa mbili tatu huyo anabebelea mpaka nyumbani, kwamba nyumbani kwake hakuna maji ya kunywa?

Na wenye ulimbukeni huu ni watu "wasomi" aise hopeless uncivilised graduates. Alafu wakiwa wamebebelea ukiwatazama hua wanaona fahari kweli kweli kutembea na maji waliyogaiwa kwenye semina, warsha nk
sasa maji yamebaki unataka yarudishwe dukani?
 
Peace be upon you all,

Aise waTanzania ni watu washamba sana sana kabisa. Mwanzo nilidhani ni watumishi pekee wenye huu ushamba ila nimebaini ni watu wengi wa sekta zote.

Yani unakuta watu wamekwenda semina fulani alafu muda wa kutoka wamebebelea vimaji vya mia tano hako kakopo atakabeba njia nzima. Unajiuliza huyu ameshindwa kuyamaliza hayo maji na mara nyingi semina na warsha wanagawa vimaji vya 600 ml. (Vile vimaji vya 500 Tsh).

Wanamake sasa aise hawa ndugu ni washamba haswa, unakuta mmama na heshima zake semina imekwisha anaenda anaomba maji yaliyobaki chupa mbili tatu huyo anabebelea mpaka nyumbani, kwamba nyumbani kwake hakuna maji ya kunywa?

Na wenye ulimbukeni huu ni watu "wasomi" aise hopeless uncivilised graduates. Alafu wakiwa wamebebelea ukiwatazama hua wanaona fahari kweli kweli kutembea na maji waliyogaiwa kwenye semina, warsha nk
wewe ndio Mshamba sana, nakuambia acha ushamba mkuu au ndio semina yako ya kwanza
 
Aise umenikumbusha wengine wanabeba pilau minofu ya nyama kwenye mikoba, jamani huko nyumbani hakuna chakula.

Unakuta dada mzuri anatembea nzia nzima ananukia pilau, kumbe kwenye mkoba kafungasha pilau la semina.
Watoto watajuaje kama mama alienda sehemu ina mnuso asipobeba 😅😅
 
hivi nn maana ya TAKE WAY????alaf mleta mada mwenyewe kakimbia angija mniite chap
 
Mi sioni hata tatizo liko wapi ikiwa maji aliyobeba ni share yake.
 
anataka na vipapatio, vidari, sambusa vikatupwe kwenye dustbin na maji yarudishwe dukani
 
Hebu tueleze kwanza..

Kubeba maji ya jero mpaka home.
Ina athari gani?
 
Wewe mwenyewe hukunywa ukabeba ndo mana ukawaona ungekua umekunywa hapo hapo ungebanwa na mkojo ungekua busy kukojoa
 
Back
Top Bottom