Ni vitu vipi vinaiangusha Tasnia ya Bongo Movie? Changia Mawazo

Ni vitu vipi vinaiangusha Tasnia ya Bongo Movie? Changia Mawazo

Tanzania hakuna Film Schools hivyo kutarajia wafanye ubora zaidi ya hapo ni miujiza tu...hizo nchi zote unazozitaja zina Film Schools za kutosha.

Ipo haja ya kuandaa kizazi kipya kuhusu suala zima la filamu.

Watoto wangali Wachanga Wanapaswa kufahamu umuhimu wa screen play na jinsi ya kuzitumia...kwa leo hii ukitaka uwalazimishe hawa waliopo sio kazi rahisi maana wameshakomaa na waliingia kwenye hii tasnia bila kujali sana mambo mengi yanayoijenga tasnia...shortcut ni nyingi na ukiwauliza watakwambia ni ufinyu wa bajeti.

Suala la kuatengeneza Filamu ni gumu tofauti kabisa na wengi tunavyochukulia.
uliwaifanya utafiti ukakuta hakuna film schools ? hii ni pumba
 
Kanumba ndo alikuwa anaibeba industry ya Bongo Movie,kwahyo kifo chake ndo kiliharibu kila kitu maana Hawa waliobaki Ni wababaishaji tu
sio kweli alivyoondoka STEPS ambaye alikuwa msambazaji na muwekezaji mkuu ndo soko liliyumba hata kanumba alikuwa anapewa hela na steps afanye movie hata angekuwepo nani angemuwezesha
 
Uwekezaji.
Hakuna aliye tayari kuwekeza vilivyo kwenye hii sekta kwasababu soko la filamu kwa hapa ndani (na Afrika Mashariki kwa ujumla) liko tricky sana, hakuna uhakika wa faida kama wenzetu wa wa Asia Ulaya na Marekani ambao wana masoko kwenye nchi na mabara mbalimbali kama China.

Sababu kubwa ya soko kukosa uhakika ni kwamba hakuna njia ya uhakika ya kuuza kazi za filamu na zikafikia watazamaji kwa asilimia angalau 50%, njia ya uhakika kidogo ni CD ambapo wizi wa kazi umeshamiri.

Pamoja na yote hayo, ukweli ambao haufurahishi ni kwamba "kifo cha Kanumba ni pigo kubwa katika safari ya maendeleo ya soko la filamu nchini"... kwanini? Enzi za uhai wake, Kanumba alianza kujaribu kutafuta mwanga kuhusu matatizo yaliyopo hapo juu.

1. Alianza kujaribu kutanua soko la filamu za Bongo kwa kushirikiana na Wanigeria.
2. Steve alikuwa akifanya uwekezaji mkubwa hasa wa fedha kwenye filamu zake.
3. Aliingia mikataba mbalimbali ya uuzaji wa filamu (nasikia).
Jamaa alikuwa masihi wa Bongo movie (my take).

Akitokea mtu akajaribu akaongoza njia katika kutatua angalau baadhi ya matatizo hayo matatu (investment, soko na udhibiti), kutakuwa na exponential efect kwa ukuaji wa Bongo movie.
KWANZA HATA YEYE STEVEN SIO YEYE ALIYEANZA KULETA USHIRIKIANO NA WANAIJA YEYE ALISHIKWA MKONO NA DIRECTOR MTITU GAME NA SUALA LA UWEKEZAJI STEPS NDO ALIKUWA MAIN SPONSOR WA WATENGENEZA FILM TZ HATA KANNUMBA MWENYEWE HAKUWA ANATOA PESA YAKE ALIKUWA ANAPEWA NA STEPS NDOMAANA MOVIE NYINGI ZINA NEMBO ZA STEPS
 
WaTz tunatakiwa tujiamini hasa inapotokea kuna waigizaji wa nje na igizo linahitaji kiingereza kutumika. Niliangalia inaitwa married to work kama sikosei, inapokuja sehemu ya MTz kuongea kwenye mkutano, na inategemewa atoe maelezo yaliyosimama, basi hicho kipande kinatolewa sauti, anaonelana akiinua mikono na modomo inacheza, hakuna sauti. Baada ya kipande hicho anaonelana kisifiea kwa jambo ambalo wasikilizaji na watazamaji hawakusikia akiongea. Tubadilike.
 
Back
Top Bottom