Ni vituko gani ulishawahi kufanyiwa na mwenye nyumba wako hadi ukatamani uhame uache Kodi?

Ni vituko gani ulishawahi kufanyiwa na mwenye nyumba wako hadi ukatamani uhame uache Kodi?

Dah sio powa mwanangu ile nyumba ni nzuri sana ila🙌.

Niliishi Kwa miaka miwili bila shida yoyote ghafla tu mwaka wa tatu nikiwa pale shida zikaanza. Kuna matukio matatu yanilitokea
1.Usiku nimezima taa nilale ghafla naona mtu anapita kwenye Kona ya kitanda anaelekea konani nikajua wenge la usingizi nikapotezea,night nipo kwenye usingizi nasikia sufuria zangu zinafunuliwa mezani ukiwasha tochi au taa hausikii kitu ukizima harakati zinaendelea.
2.Niliamka saa 10 usiku kuoga ili niwahi lindo ile natoka nje nakutana na watu wawili wamekaa katikati ya uwanja tunaangaliana mwili ulisisimka kinoma
3.Nilikuta vitu ambavyo sivielewi vimemwagwa mlangoni kwangu yani kitu kama damu/dawa za kienyeji.
Hili tukio la tatu ndio lilinifanya nisepe kabisa pale na hii ni baada ya kuongea vizuri na wazee wa mtaani na kunipa historia kamili ya ile nyumba Kwa undani.
Na kila mpangaji alikua alikutana na vituko vya aina tofauti tofauti Kuna dada mmoja alikua anakuta kinyesi Cha binadamu katikati ya kitanda.
Hali hii imenifundisha kutafuta taarifa muhimu ya sehemu unayotaka kuamia kabla ya kulipa kodi na kuanza kuishi.
Hiyo picha inaonesha kitu nilichokuta kimemwagwa mlangoni
Ulipiga picha kabisa
 
Wenye nyumba wengi wachawi sana!! Kuna siku nimetoka kuoga nikawa napaka mafuta, ghafla nikaona mlango unafunguka wenyewe na nilifunga na funguo.!! Nikatulia nione nani anaingia, holaa hakuna mtu.
Siku nyingine nimelala nimevaa kipensi na tshirt, asubuhi nimejikuta niko kichele 🤣🤣🤣
Nikajua labda itakuwa nimejimix nikaanza kuitafuta ile pensi sijaiona, baada ya siku tatu naona mtoto wa mwenye nyumba ananiletea eti alianua kwenye kamba na nguo zao.!! Nikamwambia hiyo nguo una uhakika umeianua kwenye kamba?? Nikaona anaona km aibu, baada ya siku kadhaa akanisimulia story nzito.
Siku nyingine nimerudi nimechoka nimekaa naangalia tv, naona mkono wa skeleton unanifanyia massage dadeq 🤣🤣🤣🤣

Mwisho nilimtolea uvivu mwenye nyumba akanipa notisi.!! Ila baada ya kuomba mzigo nikamwambia ntamwambia mkeo.
Vipi ulipojitazama hapo kwenye hazina kuu ya taifa hukuona mabadiliko yoyote say uteute mweupe wenye kuteleza? Kama uliona hicho kitu ufanye maombi
 
Nna rafiki yangu akija anapiga simu kabisa tuwafungie mbwa 😂😂😂😂
Waliwahi kumsindikiza kutoka getini mpk ndani, hana hamu nao🤣

Mwenzio nishavuliwa sana mawig mpk siku niliyomzaba ndo alijua wig halitakiwi kutolewa kichwani 🤣🤣🤣
Ila naipenda mimbwa yangu ina uchizi flani naenjoy sana.!! Kuna mwanaume alikuwa anajifanya jeuri alikuja kwangu nikamsakizia acheze nao, mpaka leo ananimind 🤣🤣🤣
Siji kwako tutakutana Hyatt tu 🙌🙌
 
Nyumba nyingine nilihama sababu ya mtoto wa mwenye nyumba. Ni mdogo 13 years ananiambia uncle nakupenda nataka uwe my boyfriend. Si unajua hivi vitoto vya English Medium.

Nikaona hapa siku sio nyingi nitaitwa mbakaji. Katoto kuna siku kamekuja ghetto, kanajichekesha chekesha tu, nikakauliza Jacqueline how can I help you? Kakajibu nothing, just close the with a key, I want to sleep with you.

Aisee akili ikaniruka nikasema huyu Mzee wa Kichagga kamtuma mwanawe ili nitolewe kafara?

Kimbembe ikawa namna ya kukaondoa chumbani bila ya kukatimizia ndoto yake.

Nikakapa 10,000 nikakaambia kakalete soda baridi sana tuwe tunakunywa kabla hatujalala.

Kalipotoka, nikafunga mlango nikaondoka nikaanza kurudi usiku mkali,.Hadi nilipopata nyumba ya kuhamia
Ili shawai kunikuta kama ivi Ila kalikuwa na miaka 12 baba yake alikuwa mjeshi pale Ihumwa Dodoma. Nika msanua kwa baba yake. Baba yake kwa Asira akampeleka kwa bibi yake kijijini nikabaki salama
 
Kuna mzee mmoja wa kizaramu nilipanga kwake, Akiwa hana hela ya pombe anakuja kunisumbua alafu kibabe mara niwe nawai kurudi mara, oohh sitaki wauni kwangu mara sitaki kuona mwanamke kwangu. kuna siku alikamatwa na polisi kwenye ubanda wa gongo alikaa siku tatu kituoni Alivyo toka akaja kunizingua kwa nini sijaenda kumuangalia
kituoni. akarusha Kofi Nika kwepa Aisee nilimpa kichapo mpaka niliua. Kesi ilinisumbua Ila nashukuru imeisha vizuri.
 
Sina experience ya upangaji sana maana nimepanga miaka 3 tu kwa nyumb mbili tu ya tatu ni kwangu. By the way wenyenyumba yangu walikuwa watu poa sana, japo nyumba yangu ya kwanza nilipoenda kutaffa chumba alinipangisha mke wake coz nyumba niliokuwa naishi ni nyumba ya nje, na mwenye nyumba nyumba yake ni mbali kidogo, so mimi sikumjua faza house, bali maza hoyse tu, so nikawa napeleka kodi kwake kila ikiisha kumbe maza anaila bila kumpa mzee, sasa siku moja nashangaa anakuja bodaboda mmoja hom ananiambia anataka kunifaham nikamuuliza anifaham kama nani, akaniuliza naishije pale bila kulipa kodi nikabaki nashangaa kumbe ndie alikuwa faza house wangu. Ni jamaa ambae namuonaga mtaani na alishanipeleka chuoni kama bodaboda zaid ya mara 3 ila sikuwah kujua kama ndie faza house, Inasemekana dogo alikuwaga na pesa ila alifirisika akaamua kujiajili kama bodaboda japokuwa alikuwa na nyumba tayari.

Tukaleteana noma baadae tukayamaliza na kukubaliana kodi itakayofuata nimpe yeye sio mke wake, in short wote walikuwa warangi.

Hapo nilihama baada ya kuona chumba hakitosherezi uhitaji wangu kilikuwa kidogo nikahamia chumba na sebure baada ya kupata mtoto na wife na hapo ndipo niliishi hadi nikupomaliza nyumba yangu na kuhamia kwangu,

Saiz nasumbuana na wapangaji hadi nawaza kwann hawana busara kuna dogo hapa nimempangisha flem ya biashara ni mbishi halipi umeme kila sku napewa taarifa zake nampango nimkande siku moja na kumfukuza hana heshima kabisa
 
Nakumbuka miaka hiyo ndio nimepata kazi benki Fulani, nikapata nyumba Sinza ya mama mtu mzima kijana.

Akanikaribisha sana, hakuwa na noma, nilipokuja kununua flat TV enzi hizo plasma tv ndio zimetoka, hamna cha LCD na LED ni ndoto kabisa, yaani ndio kwanza watu wachache sana tumeamza kujikwamua kutoka kwenye machogo.

Basi yule mama akawa anataka muda wote aje ashinde ghetto kwangu, anavaa nguo very light.

Kuna siku jumamosi nimemaliza kufua, nikasema Leo nijilipie, nikachukua Konyagi kubwa, nikawa na Dodoma wine, kwenye oven kilo mbili za kitimoto zinaokwa taratibu. Mara ghafla mlango unagongwa huku mtu akiingia ndani bila kukaribishwa.

Nilikuwa Niko na boksa tu sikuwa natarajia mgeni, akaniudhi sana. Nikakimbilia taulo, akanifuata akanivua taulo. Nikasimama wima hasira Imenijaa.

Akaanza kujiliza ohh Mimi nakupenda siku zote, wewe unajidai huoni.

Nikamkaripia nikamwambia anikome. Baada ya hapo alianza chuki na visa, nilikaa miezi minne tu nikahama.
Aisee.
 
Mimi na wasela wenzangu enzi hizo tuko form six, katika kujiandaa tukaona ni vyema tupange chumba ili tuweke Kambi ya masomo.

Usiku mmoja nikashtuka usingizini, tukamuona baba mwenye nyumba na mkewe na watoto wako uchi wa mnyama wanaizunguka nyumba.

Nikawaamsha wenzangu. Chumbani kuna Giza hatujawasha taa hivyo tunawaona kwa uzuri sana.

Baada ya wiki tu tukahama. Walikuwa Wana roho nzuri sana utadhani watu kumbe ni mashetani
Aisee
 
Nakumbuka miaka hiyo ndio nimepata kazi benki Fulani, nikapata nyumba Sinza ya mama mtu mzima kijana.

Akanikaribisha sana, hakuwa na noma, nilipokuja kununua flat TV enzi hizo plasma tv ndio zimetoka, hamna cha LCD na LED ni ndoto kabisa, yaani ndio kwanza watu wachache sana tumeamza kujikwamua kutoka kwenye machogo.

Basi yule mama akawa anataka muda wote aje ashinde ghetto kwangu, anavaa nguo very light.

Kuna siku jumamosi nimemaliza kufua, nikasema Leo nijilipie, nikachukua Konyagi kubwa, nikawa na Dodoma wine, kwenye oven kilo mbili za kitimoto zinaokwa taratibu. Mara ghafla mlango unagongwa huku mtu akiingia ndani bila kukaribishwa.

Nilikuwa Niko na boksa tu sikuwa natarajia mgeni, akaniudhi sana. Nikakimbilia taulo, akanifuata akanivua taulo. Nikasimama wima hasira Imenijaa.

Akaanza kujiliza ohh Mimi nakupenda siku zote, wewe unajidai huoni.

Nikamkaripia nikamwambia anikome. Baada ya hapo alianza chuki na visa, nilikaa miezi minne tu nikahama.
Kwa hiyo ndiyo ukamchukia huyo "mama mtu mzima kijana"?
 
Back
Top Bottom