Ni wakati wa Watanzania Bara kuanza kuteuliwa Zanzibar

Ni wakati wa Watanzania Bara kuanza kuteuliwa Zanzibar

Katiba mpya ya serikali 3 ndio mshumaa wa nchi hizi mbili ikiwa kama kweli tunataka muungano Zanzibar kuna mambo makubwa sana wanayakosa kwa JINI MUUNGANO lilovaa koti la Tanzania ni Tanganyikaaaa. G55 imekufa wapi ilikuwa inadai Tanganyika yenu.
 
Tatizo limeanzia kwa viongozi wetu.
Tanganyika ina viongozi wezi na mafisadi yasiyojali chochote.
Ni waigizaji tu kwa wananchi.
Zanzibar ina watu million 1 inaweza kutoa Rais wa Tanzania, huku Tanganyika ina wananchi million 57 haina uwezo hata wa kumweka mwenyekiti wa mtaa huko Zanzibar.
Watanganyika ni wapumbavu
Samahani kwa lugha niliyoitumia.
Mfufue Mzanaki umpe haya makavu maana ni yeye aliye lazimisha huu muungano.
 
Mkuu si kulaumu kwa kuwa hujui asili ya muungano wetu na nani alipendekeza na kwanini hayo mapendekezo ya mtindo huo yakubaliwe...! Ukitafuta utajua mkuu pengine ukaelewa busara za mzee wetu Nyerere wakati huo.
Kwa nini usiziweke hapa tukapata faida wote?.
 
Mnachanganya na kushindwa kutofautisha Kati ya "Serikali", "Taifa", "nchi" na "dola"(state)

Mwaka 1964 kilichounganishwa ni siyo nchi, Serikali wala Taifa, bali ziliungana dola mbili, Tanganyika na Zanzibar na kuzaliwa Tanzania.

Kimsingi, raia ni wa "dola" ndiyo yenye raia na siyo Taifa, wala Serikali (japo kwa kiswahili, tunatamka "nchi" kimaanisha "dola").

Kisheria, dola ziitwazo Tanganyika na Zanzibar zilifikia kikomo za kuzikwa mwaka 1964,kwa hiyo hazipo tena.

Hakuna ubishi kwamba Tanganyika haupo. Je, dola ya Zanzibar ipo? Ili kitu kiitwe dola kinakuwaje?

Ni, dola huundwa na 1.Serikali, 2.Mipaka, 3. Watu na 4. Uhuru (Uhuru wa ndani na nje).

Zanzibar, ina Serikali, mipaka na watu, ila inakosa kipengele kimoja tu cha uhuru ili iwe dola kamili.

Kwa hiyo dola ya Zanzibar haipo, na kwa kuwa haipo,basi hakuna raia wa Zanzibar, bali tuna raia wa Tanzania wenye asili ya Zanzibar, na moja wapo ni Rais Samia, S.H.

Zanzibar haina uhuru kamili wa kujiamulia mambo yake kitaifa na kimataifa. Hiki kigezo kingekuwepo, basi Zanzibar ingekuwa dola kamili, na Wazanzibar wangekuwa raia wa kigeni.
 
Muungano wa kizaman sana, kuajiriwa SMZ ukiwa mbara ni ngumu sana ila mzanzibar kuajiriwa Bara ni kawaida sana
Except Mapolisi na Wanajeshi.....!!!

Maza anadai katatua Kero. Hiyo sijui hajaisoma? Ama Kero ni zile tu zinazowahusu Wazanzibar....!!
 
Mnachanganya na kushindwa kutofautisha Kati ya "Serikali", "Taifa", "nchi" na "dola"(state)

Mwaka 1964 kilichounganishwa ni siyo nchi, Serikali wala Taifa, bali ziliungana dola mbili, Tanganyika na Zanzibar na kuzaliwa Tanzania.

Kimsingi, raia ni wa "dola" ndiyo yenye raia na siyo Taifa, wala Serikali (japo kwa kiswahili, tunatamka "nchi" kimaanisha "dola").

Kisheria, dola ziitwazo Tanganyika na Zanzibar zilifikia kikomo za kuzikwa mwaka 1964,kwa hiyo hazipo tena.

Hakuna ubishi kwamba Tanganyika haupo. Je, dola ya Zanzibar ipo? Ili kitu kiitwe dola kinakuwaje?

Ni, dola huundwa na 1.Serikali, 2.Mipaka, 3. Watu na 4. Uhuru (Uhuru wa ndani na nje).

Zanzibar, ina Serikali, mipaka na watu, ila inakosa kipengele kimoja tu cha uhuru ili iwe dola kamili.

Kwa hiyo dola ya Zanzibar haipo, na kwa kuwa haipo,basi hakuna raia wa Zanzibar, bali tuna raia wa Tanzania wenye asili ya Zanzibar, na moja wapo ni Rais Samia, S.H.

Zanzibar haina uhuru kamili wa kujiamulia mambo yake kitaifa na kimataifa. Hiki kigezo kingekuwepo, basi Zanzibar ingekuwa dola kamili, na Wazanzibar wangekuwa raia wa kigeni.
Kiufupi wao wamekosa uhuru kamili wa nchi ambao unawakilishwa na Tanzania kwenye maswala ya kupokea mikopo, masula ya kitaifa, n.k

Ila linapokuja swala la mambo ya ndani kiukweli tunapigwa mnoooo!!! sio kidogo ni sana tu!! yani sisi kwenye mambo yao ya ndani kama ajira na uongozi hatuhusiki ila wao wapo eligible na wanapewa kipaumbele sana wakija huku. Mnaweza kwenda pamoja kwenye interview una vyeti vyenye ufaulu mkubwa uliotukuka na umesomea udsm ila mzenji mwenye chetu chenye gpa ndogo kasomea chuo hata hakijulikani anakupiga kanzu kwa sababu tu ili kuweka uwiano katika ajira.
 
Kinachotakiwa kufanyika ni zanzibar kupewa hadhi ya mkoa, maana kwa population yake nafikiri inaweza kulingana na baadhi ya wilaya huku bara......vinginevyo katiba itamke waziwazi kabisa kwamba rais wa Tanzania asiwe mzanzibar ili ku maintain maslahi ya eneo kubwa la nchi......
Suala la rais kutokuwa Mzanzibari ndo suluhisho. Kama ilivyo UK ni vigumu mtu wa Scotland au Ireland kuwa PM wa UK. Hapa kwetu tunajidai eti tuna muungano wa kipekee, wakati kuna watu wanaumia na wengine wanakula raha na kudeka. Zbar wanadeka.
 
Except Mapolisi na Wanajeshi.....!!!

Maza anadai katatua Kero. Hiyo sijui hajaisoma? Ama Kero ni zile tu zinazowahusu Wazanzibar....!!
Mbona wanajeshi na polisi wanaajiriwa..
Polisi na wanajeshi wapi unaongelea?
JKT tulikuwa nao wakutosha
 
Except Mapolisi na Wanajeshi.....!!!

Maza anadai katatua Kero. Hiyo sijui hajaisoma? Ama Kero ni zile tu zinazowahusu Wazanzibar....!!
Wapo wazanzibari wa kutosha hizo idara, na wanaingia kirahisi mno
 
Haiingii akilini keki ya Zanzibar ni kwajili ya wazanzibari pekee ila keki ya huku bara wazazibar nao wana ila, yani chao ni chao peke yao ila chetu ni chao.

Yani huko zanzibar uongozi kuanzia uraisi, mahakamu wa raisi, wakurugenzi wa mashirika, teuzi, n.k ni wao tu ila ukija huku si ajabu kumkuta mzanzibar ni wazirri, mkurugenzi au mkuu wa shirika flani, n.k

Hata kwenye ajira za kawaida hizi za udaktari, uhandisi, uhasibu, ualimu, n.k huko kwao hizi ajira ni kwajili yao ila ukija huku wapo kibao kwene idara tofauti.

Sijui ni nini hiki,

Mwalimu nae alikuwa ni mtu tu kama wengine na sio kila kitu alichofanya kiwe kama msaafu, kiukweli kuna vitu ni lazima vibadilike.
Mungu ibariki Jamhuri ya watu wa ZanzIbar
 
Kinachotakiwa kufanyika ni zanzibar kupewa hadhi ya mkoa, maana kwa population yake nafikiri inaweza kulingana na baadhi ya wilaya huku bara......vinginevyo katiba itamke waziwazi kabisa kwamba rais wa Tanzania asiwe mzanzibar ili ku maintain maslahi ya eneo kubwa la nchi......
Ndio. Hawa waZanzibar waishie kutawala huko huko kwao na sio pande lote hili la huku Bara. Umakamu unawatosha.
 
Haiingii akilini keki ya Zanzibar ni kwajili ya wazanzibari pekee ila keki ya huku bara Wazanzibari nao wana hila, yani chao ni chao peke yao ila chetu ni chao.

Yani huko Zanzibar uongozi kuanzia uraisi, mahakamu wa rais, wakurugenzi wa mashirika, teuzi, n.k ni wao tu ila ukija huku si ajabu kumkuta mzanzibar ni wazirri, mkurugenzi au mkuu wa shirika flani, n.k

Hata kwenye ajira za kawaida hizi za udaktari, uhandisi, uhasibu, ualimu, n.k huko kwao hizi ajira ni kwajili yao ila ukija huku wapo kibao kwene idara tofauti.

Sijui ni nini hiki.

Mwalimu nae alikuwa ni mtu tu kama wengine na sio kila kitu alichofanya kiwe kama msaafu, kiukweli kuna vitu ni lazima vibadilike.
Mkuu unataka cheo gani pale Zanzibar "tukupe" ?
 
Yaani inakuwaje mzanzibari anaweza kuwa DC huku bara wakati Zanzibar hakuna mbara hata mmoja ni Dc.
Dc wa Iringa mjini ni mzanzibari
 
Kama Ambavyo Wafanyakazi kutoka sehemu mbalimbali hapa Tanzania walichanganywa kwa kupelekwa maeneo yasiyo na asili yao ili kuleta umoja, vivyo hivyo ilipaswa iwe kwa hizi sehemu mbili, tokea miaka ya sitini ingekuwa mtu wa mara anapangiwa kazi zenji na wa zenji yupo Songea na kadhalika kwa kada zote hakika tungekuwa nchi moja toka muda mrefu sana
 
Haiingii akilini keki ya Zanzibar ni kwajili ya wazanzibari pekee ila keki ya huku bara Wazanzibari nao wana hila, yani chao ni chao peke yao ila chetu ni chao.

Yani huko Zanzibar uongozi kuanzia uraisi, mahakamu wa rais, wakurugenzi wa mashirika, teuzi, n.k ni wao tu ila ukija huku si ajabu kumkuta mzanzibar ni wazirri, mkurugenzi au mkuu wa shirika flani, n.k

Hata kwenye ajira za kawaida hizi za udaktari, uhandisi, uhasibu, ualimu, n.k huko kwao hizi ajira ni kwajili yao ila ukija huku wapo kibao kwene idara tofauti.

Sijui ni nini hiki.

Mwalimu nae alikuwa ni mtu tu kama wengine na sio kila kitu alichofanya kiwe kama msaafu, kiukweli kuna vitu ni lazima vibadilike.
Kuwa na rais wawili wazanzibari sio sahihi. Tunataka katiba mpya iondoe huu ujinga
 
Ndio. Hawa waZanzibar waishie kutawala huko huko kwao na sio pande lote hili la huku Bara. Umakamu unawatosha.
Na kwa katiba hii iliyopo hata umakamu hauwafai maana matokeo yake ndiyo haya ya chifu hangaya
 
Back
Top Bottom