Ni wakinga wachache tupo kwenye mambo ya Siasa, Siasa ni kazi ya ziada kwa wakinga

Ni wakinga wachache tupo kwenye mambo ya Siasa, Siasa ni kazi ya ziada kwa wakinga

Kuhusu Saving au akiba

Huwezi kuwa na nidhamu ya akiba kama huna lengo

Kwa wakinga linaanza kwanza neno Lengo baadae inafuata akiba

Ukiweka akiba bila lengo lazima utaitumia hiyo akiba yako

Mfano:Mwaka 2023 nataka niwe na Vanguard new Model hii ndio lengo langu kuu

Natafuta bei ya Vanguard sokoni kwa sasa ni kiasi gani?

Nagawa Bei ya Vanguard na idadi ya miezi au week ili nijue yanipasa kuweka kiasi gani?

Kama nikiona hata nikijibana bado bei ya Vanguard sitaifikia naweza badili aina ya gari kabisa?

Nikiona lengo hilo halifai naachana nalo kabisa

Kuweka lengo ni kazi kuliko akiba, Wengi wana pesa wanayoita ndogo lakini hawajui wafanye kitu gani

Tatizo sio akiba, Tatizo kubwa ni malengo

Lengo moja ukiona haiwezekani weka lengo jingine hii ndio principal yetu sisi wakinga

Nakupa mfano wangu binafsi ambao nimemuambia mtoto wangu juzi anayetaka kuoa

Nimemuuliza una lengo gani mwakani akaniambia anataka kuoa, Nikamuuliza Pesa utatoa wapi zako au za kuchangiwa akanijibu za kwake

Alianza kuweka laki Saba tangu January mwaka huu Kwa ajili ya harusi mpaka sasa muda huu ana Milioni sita na laki tatu 6,300,000. kufika mwakani mpaka mwezi anataka kuoa atakuwa na Milioni zaidi ya tisa za kwake binafsi sio za kuchangiwa
Mkuu nimekuelewa sana,mimi nimekaa sana Makambako so naelewa wakinga walivyo na nidhamu ya pesa ila leo umenifungua namna wanavyofanya.

Ofcoz wakinga mnaushirikiano sana aisee,dogo anaweza toka bulongwa akaja mjini kwenye duka la kaka,akifanya kazi akapata uzoefu kaka anammegea dogo hata M30 (kulingana na ukubwa wa biashara) dogo nae anaenda kuanzisha himaya yake anamvuta dogo mwingine toka bush,kwa hilo hongereni sana.

Ukienda makambako sahivi wakinga wamenunua subaru forester kwa kasi balaa,wanaigana kwa mambo ya maendeleo.

Sent from my SM-J260F using JamiiForums mobile app
 
Mpumbavu pekee ndo atachukia mada kama hizi. Kitu muhimu ni kuona kuwa mtoa mada analenga nini, lugha anayotumia n.k. Mtu hatukani kabila lingine, hatukani dini ya mtu, hana lugha yoyote mbaya ya kutweza ama kubagua wengine just anaridhisha nafsi yake na wale wanaokubali mada yake shida ipo wapi?

Aidha, umelazimishwa na nani kusoma? Si uneona kichwa cha mada? Si uishiti tu? Kwani, humu JF unasoma kila uzi? Mbona kuna uzi mamia unapotezea,inakuwaje unase hapa? Si kwamba una tatizo binafsi?

Acha bullying za kipumbavu na heshimu mawazo ya wengine.
Sahihi kabisa mkuu. Huyu jamaa wa ajabu sana. Hapa wengine tunajifunza kupitia huu uzi. Mleta mada ameuweka kiungwana sana.

Wakati mwingine tukapata mbinu za ujasiliamali kutokana na hoja kama hizi.

Abdul Mganyizi
 
Zile kafara za watoto huwa zinawaongezea utajiri au ni uongoo...!
Wakati mwingine jaribu kujiongeza. Ukibaki na mawazo mgando kama hayo, hutasogea mkuu. Hizo imani za kwamba kabila fulani liko hivi au vile, ni imani za watu wasio na mawazo. Bado na wewe unawaza kijima hivyo!?
 
Wakati mwingine jaribu kujiongeza. Ukibaki na mawazo mgando kama hayo, hutasogea mkuu. Hizo imani za kwamba kabila fulani liko hivi au vile, ni imani za watu wasio na mawazo. Bado na wewe unawaza kijima hivyo!?
Nimekaa Njombe, najua ni kweli.
 
Mkuu, Ni kweli ule ni ushamba tu wa wazee wetu wa zamani

Kizazi cha wakinga kama Fred Vunja Bei ni kizazi kipya kilichoenda shule na kuwa na exposure

Nenda Leo pale Kariakoo vijana wa Kikinga wapo smart sana na wanakula pamba vizuri

Kama nilivyosema hapo awali wazazi wetu hawakwenda shule, Shule inasaidia pia mtu kuwa mstaarabu sana

Leo hii kuna mabadiliko makubwa sana kwa sisi wakinga
Unamfahamu Kasisi wa Paradise Hotel pale Soweto Mbeya. Mbona anaishi kwenye nyumba ya matofali haina umeme
 
Zile kafara za watoto huwa zinawaongezea utajiri au ni uongoo...!
Ni elimu ya afya tu haikuwepo muda mrefu huko Makete

Mtu akiwa na mtoto akaumwa kwashakoo utaambiwa uchawi

Mtoto hakupata chanjo udogoni akipata tatizo utasikia kafara

Fuatilia Leo kama utasikia hayo mambo

Ingekuwa kweli basi hapo kariakoo kila siku wakinga wangehudhuria msiba badala ya kazi
 
Kwanini waitwe wachawi wao tu? inamaana wakinga wanamaendeleo sn kiasi kwamba tunawaonea wivu? hakuna lolote

Wachaga wanaitwa wezi, wakinga wanaitwa wachawi, waha wanaitwa wachawi trust me hayo makabila ndio kwangu naona ni wapambanaji kweli kweli na hawana longolongo na ndio maana wataendelea kua juu Mkinga anaduka dogo kijijini kwao, chakula wanachokula nyumbani mchana ndio anapelekewa na yeye pia, wewe kijijini hapo hapo unakanyaga supu lini utasave pesa
 
Naomba tujuze kidogo, hivi inakuwaje Mkinga anakuja hapa Dar yuko hoi kiuchumi, atauza kahawa na kashata kwa mwezi tu, mwezi unaofuatia anakuwa na frames kadhaa Kariakoo, inawezekanaje hili?

Sio kweli hili unalosema, ukiona mkinga kaja Dar sio kwamba kaanzia kupambania Dar utakuta kaanzia mbeya huko, au tunduma au Zambia au njombe, sasa kwenye kuusoma mchezo ndio anajitahidi kufanya kitu cha kawaida kabisa lakini anamtaji wake, au ana binamu au kaka yake ambae anamfundisha kazi hivo pamoja na mtaji wake huku akisubiri kuongezewa na kupewa njia hana budi kukaa pale kwenye duka la kaka au binamu awe kama mfanyakazi ili ajifunze kazi ikoje.
 
Naomba tujuze kidogo, hivi inakuwaje Mkinga anakuja hapa Dar yuko hoi kiuchumi, atauza kahawa na kashata kwa mwezi tu, mwezi unaofuatia anakuwa na frames kadhaa Kariakoo, inawezekanaje hili?
Hata mimi wakati nakuja Dar kwa mara ya kwanza nilikuja na nguo moja tu ambazo ndio nilikuwa nimezivaa, Sio kwamba wazazi hawakuwa na pesa au Mimi sikuwa na pesa ni njia za kusoma mazingira tu

Nikiwa na umri wa miaka 10 nilikuwa ninajua aina za misumeno ya kupasulia mbao na aina za mbao na jinsi ya kufunga mzigo na kuusafirisha Dar kwa wazazi

Nilifahamu hata tani kwa kuona tu idadi ya mbao

Na wazazi wameishi hapo Dar kitambo wakiuza mbao maeneo ya Buguruni na Mwenge enzi hizo

Unapoenda kufunga mzigo kijijini wa viazi au maharage ukivaa kiheshima utapigwa sana bei, Kila Mkinga anajua hilo bora uonekane fara

Kuuza chai hata Mimi nilifanya ili Kuzoea mazingira na vichochoro vya kariakoo

Usipozunguka utajifunza muda gani, Unapouza kashata unapata story watu wanaishi vipi, wanakaa vipi

Sio kweli ukiona Mkinga anafanya umachinga ukafikiria hana pesa

Mkinga anaweza akajifanya machinga wa vyombo huku anazaidi ya mtaji wa Milioni 100.Ni kusoma mazingira na Kujifunza kuna siku ukianguka utapambana vipi

Ishu ni lengo. Anauza kashata ili afikie lengo,
 
Bado suala la kafara za binadamu kwenye utajiri wa wakinga ni kubwa sana, bado wakinga wana safari ndefu ya kupata utajiri wa kutumia akili na sio ndagu. Wachagga wapo mbele sana kwa hilo.
Wachaga wote wamekimbia biashara kariakoo wamebaki kidogo

Tatizo la wachaga wanauza vitu vya kizamani Halafu wanakomaa bei kubwa

Wachaga na wakinga wanapishana kweny Bei

Wakinga ni watu wa kumuheshimu mteja na wana negotiate bei

Wachaga hawana Customer Care mkuu

Anaomba mteja bei ipungue, mchaga anagoma. Mkinga anaangalia margin tu hata kidogo anauza ili mzigo utoke

Hakuna kafara
 
Mkinga akifa na mali zinakufa

Hii issue ni makabila mengi Afrika, kwa sababu kwenye kuhustle unakuta kila step unafanya mwenyewe na hauna uwazi kwenye biashara yako tofauti na watu weupe wahindi au wazungu ambao kwanza wana formal way ya kufanya shughuli zao, ndio maana hawayumbi Mzee ASAS kafa lakini hata kelele huwezi kusikia na kampuni inasonga, Mzee Mengi alivokufa hadi leo wako mahakamani wanagombea urithi.
 
Hii issue ni makabila mengi Afrika, kwa sababu kwenye kuhustle unakuta kila step unafanya mwenyewe na hauna uwazi kwenye biashara yako tofauti na watu weupe wahindi au wazungu ambao kwanza wana formal way ya kufanya shughuli zao, ndio maana hawayumbi Mzee ASAS kafa lakini hata kelele huwezi kusikia na kampuni inasonga, Mzee Mengi alivokufa hadi leo wako mahakamani wanagombea urithi.
Ni kweli lakini Kumbuka sisi wakinga huwa tunaoana sisi kwa sisi

Mwanamke wa Kikinga ni tofauti sana ukimuoa, Wanakomaa na Biashara sana,

Anafahamu malengo yenu, Na hakuna utani kwenye ishu za pesa
 
Ila wakinga noma sana.
Kumtoa hela mkinga hata kwa faida yake mwenyewe ni kama kukamua jiwe upate juisi.
Ni wagumu kinoma.
Wako tayari hata kunyongwa lakini pesa isitoke, watu wanawasema wapare ni mabahili, hawajawaona wakinga.
Siri ya utajiri ya mkinga ipo hapo
 
Yuko mmoja mfanyabiashara enzi hizo, mbinu za mdani za kuweka akiba ya savings alizotumia ni kuwa na selifukonteni ya choo cha shimo, kulala kwenye kitanda cha kamba na mkeka, kuvaa suti na kandambili. Vyumba vyao wanavyochimbia fedha ni marufuku kwa mwanafamilia mwengine kuchungulia humo.
 
Siasa inataka akili na Wakinga hawana akili
Akili zipi zinatakiwa, Mimi ni mwana ccm

Na Nipo ndani ya CCM nakula maisha, Nimesomesha watoto nikiwa ccm kwa pesa za Serikali

Utabaki na vyeti vyako huku watoto wako wakikosa pesa kwa mawazo ya Akili

Huku kwenye siasa hapa Tanzania unasoma upepo na kuchukua hatua

Endelea kukaa na akili zako, Bungeni unatakiwa ujue kusoma na kuandika tu
 
Back
Top Bottom