Ni wakinga wachache tupo kwenye mambo ya Siasa, Siasa ni kazi ya ziada kwa wakinga

Ni wakinga wachache tupo kwenye mambo ya Siasa, Siasa ni kazi ya ziada kwa wakinga

Tetete wakinga wana mali gani na waha? wachaga sawa
Unajua mimi watu huwa nawaangalia tu hivi muha anamali gani ya kushangaza? Mi bora hata Wakinga kidogo! Kuna watu ni very calm lakini wanamaisha makubwa sana! Hata wakurya tu hawaonekani sana maana wako na wilaya moja ya tarime ila kwenye maisha ya biashara wako mbali!
 
Yuko mmoja mfanyabiashara enzi hizo, mbinu za mdani za kuweka akiba ya savings alizotumia ni kuwa na selifukonteni ya choo cha shimo, kulala kwenye kitanda cha kamba na mkeka, kuvaa suti na kandambili. Vyumba vyao wanavyochimbia fedha ni marufuku kwa mwanafamilia mwengine kuchungulia humo.
Umenikumbusha mfanyibiashara mmoja wa mabasi Njombe aliyekuwa anaitwa Widambe.Naye alikuwa na chumba ambacho ndugu walikuwa hawaingii.Alifia Mnazi Mmoja kwa kukanyagwa na gari.Nasikia alivunja masharti ya kutoacha mlango wazi, mkewe akaingia akaona vimbwanga vilivyokuwemo.Naambiwa alikufa saa ile ile mkewe aliyofungua mlango.
 
Kama ukuhusisha familia kwenye biashara zako ukifa lazima biashara zife, hili si la wakinga bali ni kwa Watanzania wote.

Bishara nyingi zinakufa kwa vile hawawezi kutoa siri za giza za mafanikio ya hizo biashara zao. Wewe ukamuambie mtoto biashara hii imefanikiwa kwasababu yuko ndugu yako kaka/dada/ mjomba/binamu/mjukuu nk tulimua kwa kumtoa kafara kwa sababu ya nyota yake. Ama yuko ndugu yako kwa maana iyohiyo hapo juu kwasababu ya nyota yake na kibali chake tumemuwangia ni kapuku zezeta ndio haya mafanikio tuliyonayo.

Kwa kweli haya mambo ni wazi sana kwenye baadhi ya wafanikiwa katika nyanja mbalimbali za maisha. Jaribu kufatilia kwa wahindi na waarabu yako mandondocha ya kutosha achilia mbali vifo vya kutatatanisha vya wafanyakazi wao na baadhi ya wanafamilia. Nilipita mahali pale Itetemia ndondocha linagawa mikate na kuvunja vifaa vya bakery kwa kwenda mbele. Watu wanagombania mikate inavyosambazwa. Jamaa mmoja mwenyeji na jirani wa hilo eneo akasema ndio zake linacharukwa akili kila majira flani ya mwaka.
 
Daaah!!! Hatimaye wakinga wanaanza kusikika kila Kona ya Tanzania, kwa biashara na kuzisaka hela mpo vizuri sana, lakini bado hamjanishawishi kwenye kuleta maendeleo kwenye wilaya yenu, bado watu wengi huko vijiji vya Igolwa, ipepo, masisiwe nk, wanaishi kwenye nyumba zisizoridhisha ilihali vijana wao mna hela na biashara kubwa mijini.

Hakikisheni wilaya yenu ya Makete inapendeza kwa majengo, masuala ya ninyi kurudi misibani na hafla mbalimbali msilale hata usiku mmoja kwa hofu ya mtalala nyumba gani muache, vilevile waboresheheni wazee wenu mambo yanayohusiana na kilimo maana wanachoka sana na migunda inayopatikana kilomita kadhaa kwa umbali.
 
Unajua mimi watu huwa nawaangalia tu hivi muha anamali gani ya kushangaza? Mi bora hata Wakinga kidogo! Kuna watu ni very calm lakini wanamaisha makubwa sana! Hata wakurya tu hawaonekani sana maana wako na wilaya moja ya tarime ila kwenye maisha ya biashara wako mbali!
Ni kelele tupu hawana lolote
 
Wewe ni muongo na story zako za vijiweni hebu tuambie ni nani unae mfahamu na umemuona kamuweka mzazi kwenye chumba cha siri.

Hilo la ubahili ndilo linafanya wakinga hata wakitajirika wasiishi maisha ya anasa ndicho nimejifunza kwao kwa kweli ni mabahili kwelikweli tena hasaa, hata kununua nguo tu huwa anaona anapunguza pesa kwenye mzunguko wa biashara yake.
Unaona ni sifa nzuri kuwa bahili? Kipato hakijifichi ukiweza kuficha kipato kama si mchawi basi akili yako haiko Sawa. Siwezi kumiliki asset ya Milioni 200+ ambayo ipo kwenye mzunguko alafu utegemee kukutana na Mimi kwa mama ntilie ao Karume nachagua mtumba
 
Kiongozi usiseme ubahiri, Sisi sio wabahiri tunakua na Malengo

Ukiwa na Lengo huwezi kula pesa hovyo hovyo
Una lengo la kujenga nyumba, Unaweza tumia 100,000 Bar? Ukigawa 100,000 kwa tofali la 1000 unapata tofali 100

Mtu akiomba laki 100,000 nitampa au nitanunua tofali.? Lazima ninunue tofali
Inategemea na kipato cha mtu, narudia tena NI uchawi ao ukosefu wa akili. Una asset ipo kwenye mzunguko kwa siku hukosi faida ya laki 1, alafu ushindwe kunywa BIA ya 100,000 Weekend kisa unajenga ?

Laki 1 per day- mavazi yako ni suruali 3,000 shati la 2,000 kiatu cha 6,000 kisa unajenga ? BADO NITATAKA UPIMWE AKILI.

Hela ni kipimo cha nguvu/power huwezi kuwa una hela utake kuvaa,Kula,kulala ,anasa sawa na mtu wa kipato cha chini (mfano,:mmiliki wa Duka la jumla Kariakoo anaagiza chakula anacho agiza machinga anayenunua bidhaa kwake na kuuza nje ya Duka lake) uyo ni mchawi ao akili haipo Sawa.
 
Ngoja tusubiri tuone hiki kizazi cha wakinga ambao baadhi mmeelimika.

Ila kwa kizazi kilochopita ushirikina ulikuwepo kwa kiasi cha kutisha.

Nina marafiki zangu wawili wakinga, kwao kuna wamama wanacheka cheka tu, siku nzima kuhesabu vidole.

Kuna mwengine nae nlishuhudia anamfuga mbuzi tangu nipo darasa la tano hadi naingia form 5, enzi hizo huyu mzee kila wiki mara 3 anaenda makete huko anazuga kabeba kuni kutoka makete kwenye surf yake kumbe watu tulishajua.

Pia mwengine hapa Mbeya ana gesti yake, nje kuna mbwa koko wengi hataki wafukuzwe.

Kiufupi nmeishi na wakinga, ni watu smart, ila linapokuja swala la ushirikina hapo ndio nawakwepa.

Wakinga wanapenda toyota surf aisee 😂😂😂😂
 
Hata mimi wakati nakuja Dar kwa mara ya kwanza nilikuja na nguo moja tu ambazo ndio nilikuwa nimezivaa, Sio kwamba wazazi hawakuwa na pesa au Mimi sikuwa na pesa ni njia za kusoma mazingira tu

Nikiwa na umri wa miaka 10 nilikuwa ninajua aina za misumeno ya kupasulia mbao na aina za mbao na jinsi ya kufunga mzigo na kuusafirisha Dar kwa wazazi

Nilifahamu hata tani kwa kuona tu idadi ya mbao

Na wazazi wameishi hapo Dar kitambo wakiuza mbao maeneo ya Buguruni na Mwenge enzi hizo

Unapoenda kufunga mzigo kijijini wa viazi au maharage ukivaa kiheshima utapigwa sana bei, Kila Mkinga anajua hilo bora uonekane fara

Kuuza chai hata Mimi nilifanya ili Kuzoea mazingira na vichochoro vya kariakoo

Usipozunguka utajifunza muda gani, Unapouza kashata unapata story watu wanaishi vipi, wanakaa vipi

Sio kweli ukiona Mkinga anafanya umachinga ukafikiria hana pesa

Mkinga anaweza akajifanya machinga wa vyombo huku anazaidi ya mtaji wa Milioni 100.Ni kusoma mazingira na Kujifunza kuna siku ukianguka utapambana vipi

Ishu ni lengo. Anauza kashata ili afikie lengo,
Kutembea na bidhaa mkooni Kariakoo huku una mtaji kiasi cha 100ml eti kuusoma mchezo!!!! Icho NI kipimo cha uchawi ao ukosefu wa akili.
 
Naomba tujuze kidogo, hivi inakuwaje Mkinga anakuja hapa Dar yuko hoi kiuchumi, atauza kahawa na kashata kwa mwezi tu, mwezi unaofuatia anakuwa na frames kadhaa Kariakoo, inawezekanaje hili?
Wengine wanakuja tayari wana mitaji yao, ile kuuza kahawa na kashata ama umachinga ni njia ya kusoma mji...

Huwezi kufungua biashara kubwa kwenye mji wowote bila kufanya uchunguzi wa kina.
 
Bado suala la kafara za binadamu kwenye utajiri wa wakinga ni kubwa sana, bado wakinga wana safari ndefu ya kupata utajiri wa kutumia akili na sio ndagu. Wachagga wapo mbele sana kwa hilo.
Uchawi hauna kabila wala Rangi...sijui unasemea wachaga gani mzee..
 
Back
Top Bottom