Ni wakinga wachache tupo kwenye mambo ya Siasa, Siasa ni kazi ya ziada kwa wakinga

Ni wakinga wachache tupo kwenye mambo ya Siasa, Siasa ni kazi ya ziada kwa wakinga

Hata mimi wakati nakuja Dar kwa mara ya kwanza nilikuja na nguo moja tu ambazo ndio nilikuwa nimezivaa, Sio kwamba wazazi hawakuwa na pesa au Mimi sikuwa na pesa ni njia za kusoma mazingira tu

Nikiwa na umri wa miaka 10 nilikuwa ninajua aina za misumeno ya kupasulia mbao na aina za mbao na jinsi ya kufunga mzigo na kuusafirisha Dar kwa wazazi

Nilifahamu hata tani kwa kuona tu idadi ya mbao

Na wazazi wameishi hapo Dar kitambo wakiuza mbao maeneo ya Buguruni na Mwenge enzi hizo

Unapoenda kufunga mzigo kijijini wa viazi au maharage ukivaa kiheshima utapigwa sana bei, Kila Mkinga anajua hilo bora uonekane fara

Kuuza chai hata Mimi nilifanya ili Kuzoea mazingira na vichochoro vya kariakoo

Usipozunguka utajifunza muda gani, Unapouza kashata unapata story watu wanaishi vipi, wanakaa vipi

Sio kweli ukiona Mkinga anafanya umachinga ukafikiria hana pesa

Mkinga anaweza akajifanya machinga wa vyombo huku anazaidi ya mtaji wa Milioni 100.Ni kusoma mazingira na Kujifunza kuna siku ukianguka utapambana vipi

Ishu ni lengo. Anauza kashata ili afikie lengo,
Ahsante kwa ufafanuzi huu, una dada single ila asiwe na mtoto uniunganishie?
 
Ni kweli lakini Kumbuka sisi wakinga huwa tunaoana sisi kwa sisi

Mwanamke wa Kikinga ni tofauti sana ukimuoa, Wanakomaa na Biashara sana,

Anafahamu malengo yenu, Na hakuna utani kwenye ishu za pesa
Na ufugaji mandondocha vipi, wanakomaa kuwalisha ili biashara iendelee ikiwa wewe mumewe mfugaji umekufa?
 
Na ufugaji mandondocha vipi, wanakomaa kuwalisha ili biashara iendelee ikiwa wewe mumewe mfugaji umekufa?
Nimecheka sana
Hizi story za Ndondocha kila mkoa nazisikia. Kila kabila hapa Tanzania kuna story mara vibwengu

Ukiishi Arusha utasikia wachaga wana ndondocha

Ukiishi Mbeya hivyo hivyo utasikia yule Bibi wa kinyakyusa ana Ndondocha

Nyumba kukiwa na mtu mwenye tatizo la akili utasikia amefanya Msukule, Haya mambo ni kila sehemu

Elimu inahitajika sana kwa watanzania kuhusu magonjwa ya Akili, Kila mgonjwa wa akili kwenye nyumba anaitwa Ndondocha au amefanywa msukule
 
Nimecheka sana
Hizi story za Ndondocha kila mkoa nazisikia. Kila kabila hapa Tanzania kuna story mara vibwengu

Ukiishi Arusha utasikia wachaga wana ndondocha

Ukiishi Mbeya hivyo hivyo utasikia yule Bibi wa kinyakyusa ana Ndondocha

Nyumba kukiwa na mtu mwenye tatizo la akili utasikia amefanya Msukule, Haya mambo ni kila sehemu

Elimu inahitajika sana kwa watanzania kuhusu magonjwa ya Akili, Kila mgonjwa wa akili kwenye nyumba anaitwa Ndondocha au amefanywa msukule
Lakini kwa Wapemba, Wakinga, Wapare, Wachagga ni jambo la kawaida sana kwao kufuga aliens (ndondocha), sijawahi amini hawa watu hata siku moja.
 
Unamfahamu Mwakipande au humfahamu?

Unafahamu Leonard au humfahamu?

Mimi nimefika kwa Mwakipande the Leonard

Nilipada gari toka Njombe mpaka Ikonda, Baada ya kufika Ikonda nikakodi boda boda kuna milima balaa mpaka kwa Mwakipande, Simu network mpaka upande mlimani

Nimelala hapo Kwa Mwakipande na kaburi hilo la mleta mada nalifahamu

Na nimefika huko mambo yangu yamenyooka

Anachoongea mleta mada kina maana sana

Wewe hujui biashara wala hufahamu kitu

Mleta mada Nakubaliana nae asilimia 100% ni mzaliwa wa huko na ana undugu na hao watu

Mleta mada hapa JF alikuwa mwana ccm na mtetezi wa JPM, Ameleta mada nyingi sana sio kama wewe

Wewe unamjua Leonard Mwakipande, Hebu elezea kama unamjua kwa kueleza umri wake ni Mzee au kijana na ana wake wangapi?

Aliyefika huko anafahamu ana wake wangapi na anafahamu umri wake kwani lazima aseme anapoagua

Ongea ana mke au wake wangapi?
Rafiki ukiona mimi ninajibu swali gani utagundua kuwa jibu langu linasahihisha kuwa Mangula siyo Mkinga ni Mbena! Maneno yote hayo ya nini!?
 
Rafiki ukiona mimi ninajibu swali gani utagundua kuwa jibu langu linasahihisha kuwa Mangula siyo Mkinga ni Mbena! Maneno yote hayo ya nini!?
Sio kila mtu anayeitwa Sanga ni mkinga

Sio kila mtu anayeitwa Abdallah ni muislam

Sio kila mtu anayeitwa John ni mkristo

Sio kila mtu anayeitwa Nyoni, Ngonyani, Mapunda au Nyati ni mngoni au ana uhusiano na Songea Ruvuma

Mangula anaishi Njombe, Ninakubali
Kuthibitisha Mangula ni mbena au Mpangwa ni kazi ngumu sana

Mimi nimeishi huko kaskazini, Watu wanajua mimi ni wa huko. Hata nikikutana na watu kwenye channel za Deal wanajua mimi wa huko, Ni ngumu sana Kuthibitisha kabila la mtu au mahusiano ya dini na jina lake mpaka mtu mwenyewe athibitishe

Mfano:Zakaria kakobe tunamfaham vizuri sana kama mchungaji na mtanzania, Aliombwa athibitishe Uraia wake kama yeye ni mtanzania kwa kuonyesha makaburi ya Babu mzaaa Babu aliyezaa Babu wa mzaa Babu. Kakobe alishindwa

Mfano:Jeneral Ulimwengu amewahi kuwa Mkuu wa wilaya Tanzania, Wakati wa Mkapa Aliombwa athibitishe Uraia wake na kabila akashindwa

Hivyo usimsemee Mangula kuwa ni Mbena ingawa nakubali Manguli anaishi Njombe

Achana na mambo ambayo huna Hakika

Achana na mambo ya kusikia, Ishi maisha yako ya kweli
 
Sio kila mtu anayeitwa Sanga ni mkinga

Sio kila mtu anayeitwa Abdallah ni muislam

Sio kila mtu anayeitwa John ni mkristo

Sio kila mtu anayeitwa Nyoni, Ngonyani, Mapunda au Nyati ni mngoni au ana uhusiano na Songea Ruvuma

Mangula anaishi Njombe, Ninakubali
Kuthibitisha Mangula ni mbena au Mpangwa ni kazi ngumu sana

Mimi nimeishi huko kaskazini, Watu wanajua mimi ni wa huko. Hata nikikutana na watu kwenye channel za Deal wanajua mimi wa huko, Ni ngumu sana Kuthibitisha kabila la mtu au mahusiano ya dini na jina lake mpaka mtu mwenyewe athibitishe

Mfano:Zakaria kakobe tunamfaham vizuri sana kama mchungaji na mtanzania, Aliombwa athibitishe Uraia wake kama yeye ni mtanzania kwa kuonyesha makaburi ya Babu mzaaa Babu aliyezaa Babu wa mzaa Babu. Kakobe alishindwa

Mfano:Jeneral Ulimwengu amewahi kuwa Mkuu wa wilaya Tanzania, Wakati wa Mkapa Aliombwa athibitishe Uraia wake na kabila akashindwa

Hivyo usimsemee Mangula kuwa ni Mbena ingawa nakubali Manguli anaishi Njombe

Achana na mambo ambayo huna Hakika

Achana na mambo ya kusikia, Ishi maisha yako ya kweli
Kwa akili hii, hata Mangula mwenyewe angekataa kuwa siyo Mkinga ungebisha!!
 
Wewe ni muongo na story zako za vijiweni hebu tuambie ni nani unae mfahamu na umemuona kamuweka mzazi kwenye chumba cha siri.

Hilo la ubahili ndilo linafanya wakinga hata wakitajirika wasiishi maisha ya anasa ndicho nimejifunza kwao kwa kweli ni mabahili kwelikweli tena hasaa, hata kununua nguo tu huwa anaona anapunguza pesa kwenye mzunguko wa biashara yake.
Sasa huo si ni ujinga?
 
Sio kweli hili unalosema, ukiona mkinga kaja Dar sio kwamba kaanzia kupambania Dar utakuta kaanzia mbeya huko, au tunduma au Zambia au njombe, sasa kwenye kuusoma mchezo ndio anajitahidi kufanya kitu cha kawaida kabisa lakini anamtaji wake, au ana binamu au kaka yake ambae anamfundisha kazi hivo pamoja na mtaji wake huku akisubiri kuongezewa na kupewa njia hana budi kukaa pale kwenye duka la kaka au binamu awe kama mfanyakazi ili ajifunze kazi ikoje.
Alichoeleza mtoa somo leo kuhusu Wakinga ni kweli kabisa. Yaani jamaa wanajituma ni balaa. Utakuta Mkinga ni Mkurugenzi wa Shirika fulani lakini bado ana biashara za mbao, viazi na maduka. Halafu kwa miaka ya kuanzia 90 Wakinga wamesomesha sana watoto wao ili waje wasimamie biashara zao. Binafsi nina rafiki zangu ambao walipeleka watoto wao kusoma Nairobi - Kenya, Afrika ya Kusini na hata Uingereza, leo ndio wasimamizi wa biashara za wazazi wao. Hiki ndio chanzo cha Kariakoo kutekwa na Wakinga.
 
Umenikumbusha mfanyibiashara mmoja wa mabasi Njombe aliyekuwa anaitwa Widambe.Naye alikuwa na chumba ambacho ndugu walikuwa hawaingii.Alifia Mnazi Mmoja kwa kukanyagwa na gari.Nasikia alivunja masharti ya kutoacha mlango wazi, mkewe akaingia akaona vimbwanga vilivyokuwemo.Naambiwa alikufa saa ile ile mkewe aliyofungua mlango.
Widambe alikuwa ni Mbena sio Mkinga!
 
Yale maghorofa Kariakoo ni ya wakinga

Onyesha ya kwenu
Usipanic mkuu Mimi sijazungumza kuhusu kabila,nisome vizuri hakuna sehemu ata moja nimetaja kabila, Mimi napinga na kuunga hoja Tu!!

Uhalisia usipojidhihirisha kwenye Jambo lolote ujue kuna lililofichwa ndani yake
 
Anafikiri akipata milioni 100 basi kuimaintain iendelee kubaki au kuzalisha ni rahisi rahisi tu.Tujifunze kwa wale waliokuwa wanashiriki Big brother Africa walikuwa wanapata mamilioni lakini yanaisha yote.Kutunza hela na kuzalisha nyingine sio kazi ndogo
Kutaka kumantain mtaji wa ml.100 kwa kuuza kahawa na kashata,Kula kwa mama ntilie ni kanuni ambayo haina uhalisia kwangu, ninukuu "kwangu" sijakulazimisha huo ndio MSIMAMO wangu.
 
Mada nzuri. Nakubali kwamba Wakinga wapo vizuri kwenye biashara hasa kizazi chao kipya hiki cha sasa. Lakini mimi nakataa vitu viwili kwenye hii mada:
1. Kuamini kwamba ubahili kupita kiasi unaweza kuwa chanzo cha kutajirika
2. Kuaminisha watu kuwa wakinga ni washirikina ndio maana wanafanikiwa kibiashara.
Mimi nakataa dhana zote mbili.
Tukubali kwamba mafanikio ya kibiashara ni umadhubuti wa kutumia akili(mental smartness) na ubunifu.
Mimi nafanyia kazi zangu nyingi katika Kanda ya Nyanda za Juu kusini ambayo kimsingi ni mikoa ambayo imeshikwa na wakinga kiuchumi sana.
Sijaona mkinga aliyefanikiwa anayevaa vibaya, ambaye hana gari, asiyewatoa washikaji zake bia, nyama choma.
Kuanzia wanaochimba dhahabu Chunya, Wafabiashara wa vitenge na vipodozi Tunduma, wamiliki wa hotel Mbeya mjini, wamiliki wa bar Mbeya, wamiliki wa maduka Makambako na maeneo yote.
Sijawahi kurealize hizo tabia zinazosemwa.
Ninachoona kwa wakinga ni umadhubuti wa kutumia akili.
Kufanya economics of scale na kutake risk.
Lakini pia kuwa tayari kusubiri payback period ya mradi wake.
@Kinuju , Super Sub Steve huo ndio uhalisia watu tunataka tujifunze ili tuwe matajiri. Sio kunambia mtu anaingia mjini na ml.100 anausoma mji kwa kuuza kahawa na kashata, kula kwa mama ntilie ndio aweze kumantain kuja kuwa tajiri ,

brazaz iyo ni risk unaweza poteza pesa yako kwa kujiuguza ,afya hulindwa na pesa kwa Kula vizuri,kulala pazuri, kuvaa nadhifu.

Kama utatafuta pesa adi kupata mtaji wa ml.100 alafu uje Dar ufanye biashara ya kahawa na kashata, ule mama ntilie,ulale chumba cha elfu 40 jangwani kumantain mtaji wako usipungue, Mimi siwakatalii kila mtu na mtazamo wake.( Narudia tena kwa mtazamo wangu mtu huyo ni mlozi ao akili haipo Sawa)

Uhalisia ni kama ameacha shamba lake la miti kaja mjini na kauza kahawa miaka mitatu ,mti umekomaa kauza kapata ml. 100 obviously atabadili biashara.
 
Thubutu!

Wachagga wengi wanafuga mandondocha majumbani mwao!
Mimi ni shuhuda wa tukio la ROMBO/ Leto kuna mfanyabiashara ambaye tulizika mdogo wake baada ya miezi miwili marehemu akatolewa dukani kwa Kaka yake.

Kaburi lilifukuliwa wakafanya matambiko ya kuchinja kondoo kaburini .

Jamaa Catholic wamemtenga, kanisa katoliki Leto.

Na zaidi ya yote ni eneo lenye mazezeta wakutosha ,watu wapo mijini wanachuma mali Tu.
 
Ni swali la ukweli nimekuuliza kwa sababu namfahamu Mkinga mmoja aliyekuwa muuza kahawa na kashata na sasa (toka mwaka juzi) ana maduka pale Kariakoo, akiulizwa na washikaji anasema ni biashara yake ya kahawa na kashata ndiyo iliyomfikisha pale. Pia kuna tetesi zinasema, kila mwaka yeye lazima akafanye sadaka kwao na akirudi anafungua frame ingine.
Hakuna uhalisia iyo mali ina makando mengi,

Aseme aliacha shamba la miti wakati anasubiri ikomae akaja mjini kuuza kahawa,akavuna na kwa kuwa kapata mtaji na watu anaoshinda nao mazingira yake ya kahawa na kashata ni wafanyabiashara basi wakamsaidia mawazo kulingana na mtaji wake iyo haina makandokando inaeleweka.

Hesabu rahisi tu kwa wastani duka frame+bidhaa =Ml.100

Kahawa ameuza miaka mitano
Siku165 × miaka5= siku 1,825

Sh.100,000,000 ÷ siku1,825= Sh. 54,794.5

Ni muujiza yaani auze kahawa na kashatakwa siku atunze Sh.54,794.5 kwa muda wa miaka mitano ndio atafungua frame moja.

Swali: je biashara ya kahawa inaweza kumpa mtu akiba ya 54,000 kwa siku?
 
Hakuna uhalisia iyo mali ina makando mengi,

Aseme aliacha shamba la miti wakati anasubiri ikomae akaja mjini kuuza kahawa,akavuna na kwa kuwa kapata mtaji na watu anaoshinda nao mazingira yake ya kahawa na kashata ni wafanyabiashara basi wakamsaidia mawazo kulingana na mtaji wake iyo haina makandokando inaeleweka.

Hesabu rahisi tu kwa wastani duka frame+bidhaa =Ml.100

Kahawa ameuza miaka mitano
Siku165 × miaka5= siku 1,825

Sh.100,000,000 ÷ siku1,825= Sh. 54,794.5

Ni muujiza yaani auze kahawa na kashatakwa siku atunze Sh.54,794.5 kwa muda wa miaka mitano ndio atafungua frame moja.

Swali: je biashara ya kahawa inaweza kumpa mtu akiba ya 54,000 kwa siku?
No, kahawa na kashata inakupa change ya shillingi 3,000 mpaka 10,000 kwa siku na inategemea
 
Back
Top Bottom