Mwenye Jina la soundtrack au wimbo wwnyewe wa filamu ya uzalo inayorushwa na kituo pendwa cha zaman ITV.....Tafadhari nitumie au nijuze jina lake niutafute
 
Niliomba waimbo wa Ngoni Tribe uitwao Manungayembe,lakini kimya,kama kuna mtu anao autupie jukwaani humu
 
Tuunashuhudia kuagana na ndugu yetu..
Mweenzeetuuu,ndugu yeetuuu(mwalimuu),mwaalimu nyereereee.
MWENYE NAYO JAMANI
 
Kuna jamaa alifanya kama kuurudia wimbi wa KIBIBI.

akaimba:

Kibibii mambo poaa
Kibibi tutaoana

Na kuna sehem akaimba.

MAX na ZEMBWELA waje kutuchekesha.

Wanakwetu mwenye huo wimbo atuwekee tuenjoy. Ilikuwa kwenye miaka ya 2004 hadi na 2006 hivi kama skosei.

SUKAH
 
Kuna nyimbo nadhani inaitwa jasmini
wanaimba hivi
"jamsin toto la kishua, nimekuzimia
naja kwako nipokeee,jasmin mim masikini wa hali duni......"alaf kuna sehem wanaimba "wenye maneno usiwaskilize matajiri hawana mapenz jasmin....."
Nimeitafuta toka mwaka 2009
 
Mmh chief hii nyimbo nimewahi isikia nafikiri kwenye tamthilia flan ya kibongo ....kupata official track itakuwa kipengele
 
Kuna wimbo sijui kaimba nani

" Maisha mbona unanihangaisha
Ipo siku nami nitayapatia"
Baadhi ya mistar yke
" Bos wangu ni mdogo,mimi ni mkubwa namweshimu kwa sababu ya maisha".
Mwenye nao please naomba
 
Bandugu Nisaidieni Hizi Nyimbo Sijui Nani Kaimba Ila Mmoja una Mashairi Yafuatayo...
..Uwezo Sina ningekujengea Nyumba...
Uwezo Sina ningekununulia Gari...
Uwezo Sina Ningekununulia Mtumbwi Ukavue Samaki... Bali matatizo madogo madogo hayatonishinda... Sababu Jungu kuu Halikosi Ukoko..... Akiba Yangu Ya Mapenzi Nakupa wewe....
Wimbo Mwingine Ni Huu..... Ukimuona Huko aliko Mwambieni Kweli nateseka eee Thamani yake bado Ipo Moyoni Mwangu....
Naombeni Sana Mniambie Hata majina na Bendi nijue pa Kuanzia kutafuta
 
Kuna wimbo sijui kaimba nani

" Maisha mbona unanihangaisha
Ipo siku nami nitayapatia"
Baadhi ya mistar yke
" Bos wangu ni mdogo,mimi ni mkubwa namweshimu kwa sababu ya maisha".
Mwenye nao please naomba
Upo katika miondoko ya reggae siyo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…