Ni zawadi gani nzuri, inayoweza kumfurahisha na kumuachia kumbukumbu ya furaha mkeo/mumeo aliyepitia changamoto kali kipindi cha nyuma?

Ni zawadi gani nzuri, inayoweza kumfurahisha na kumuachia kumbukumbu ya furaha mkeo/mumeo aliyepitia changamoto kali kipindi cha nyuma?

Mpe Charahani tu mwanamke Mengine yote upuuzi mtupu.
 
TOKENI KIDOGO SEHEMU MKALE MAISHA KWA UTULIVU... USIACHE WATOTO WENU... KAENI SEHEMU MKIWAANGALIA WATOTO WENU WAKIFURAHI WAKICHEZA... HUKU MKIZUNGUMZA NA KUNYWA NA KULA...

PITIENI SEHEMU KITUO CHA WATOTO YATIMA NA WATOTO WENU WACHEZE WOTE WAACHIENI CHOCHOTE... AU NENDENI MKATEMBELEE FAMILIA MASKINI MKAWASAIDIE CHAKULA HATA KILO KILO ZA MCHELE NA SUKARI NA MAFUTA... ILI AONE WAPO WENYE TABU NA SHIDA KULIKO YEYE... HIZO NI CHANGAMOTO TU KAPITIA AWE NA SUBRA...

HAYO YOTE MNAYAFANYA MKIWA VACATION MBALI NA NYUMBANI...
 
Nawaza zawadi ya kumpatia mke wangu kama 'surprise' tu, kutokana na changamoto alizopitia mwaka jana, mwezi kama huu, mpaka ikafikia hatua ya kukata tamaa ya kuishi.

Alifiwa na mzazi wake aliyempenda sana; aliyekuwa akimuuguza muda mrefu.

Kabla ya mzazi wake hajafariki, ndani ya wiki mbili hivi, 'wife' akafanyiwa upasuaji mkubwa, hajamaliza hata wiki, akatakiwa kufanyiwa tiba ya mionzi. Ile kuanza tu tiba ya mionzi, mzazi wake akafariki.

Ndani ya muda mfupi, vichwa vilikuwa vimevurugika sana; lakini tuliweza kuhimili ingawa changamoto zilikuwa nyingi.

Sasa nawaza, nimpe zawadi gani itakayomsababisha kutoa machozi ya furaha, iwe kama 'surprise'.

Kama gari, yeye siyo mpenzi sana, hata lililopo huwa halitumii; kama ni nyumba, anaweza asione kama zawadi, kwa sababu itakuwa kama sehemu ya familia (yeye na watoto).

Nawaza, zawadi ambayo yeye ataiona inamgusa yeye tu.

Karibuni kwa mawazo.
Hongera sana mkuu kwa kuona umuhimu wa kumpa mkeo zawadi kwa changamoto alizopitia

WANAUME WENGINE HAWAJUI,HAWAONI UMUHIMU WA KUTOA ZAWADI KWA WAKE ZAO WAPOWAPO TU jifunzeni kwa huyuuu

Mtoe mpeleke hata dubai akapumzike,
 
Tafuta eneo zuri ambalo limetulia hasa hotel zilizopo kwenye mbuga za wanyama huko au hoteli zilizo karibu na mwambao wa ziwa lolote kwenye Beach nzuri na tulivu, kaeni chini nunua chakula anachokipenda na kaa mkao wa kumwangalia kisha mwambie namna unampenda mwambie hata kama kutakuwa na changamoto ya zile zilizopita bado utaendelea kuwa nae tumia siku hata 3 na ikiwezekana zima hata simu tumia mda huo kuongea nae, kama ni mkristo nunua zawadi Bible mpe mwambie nakupa neno la uzima baki nalo duniani na mbinguni
Fuata ushauri wa huyu jamaa!.. ni ushauri Bora kabisa
 
Back
Top Bottom