Ni zipi mbinu za kudhibiti wizi kwenye duka la jumla?

Ni zipi mbinu za kudhibiti wizi kwenye duka la jumla?

Hello JF,

Moja kwa moja kwenye bandiko

Mimi ni mmoja wa wamiliki wa Duka la Jumla kiukweli hi biashara inalipa sana hasa inalipa faida ya milion 1.5 kwa mwezi kabla ya kutoa malipo ya wafanyakazi na Kodi ya pango nabaki na 600k au 700k Kama faida, kwa Duka moja.

Hivyo kutokana na biashara kukua nimefungua zaidi ya maduka 4 ya jumla katika mikoa ya Tanga Arusha Mwanza

Dar ndio mean Office ilipo

Biashara ambazo nazi-manege

Tomato, pemepers biscuits, kalamu, Super Grue, madaftari, pipi Big G, nk.

Changamoto ipo kwenye kulinda wafanyakazi wasiibie sana hadi kupelekea biashara kufa

Je, ni mifumo gani ya ulinzi niiweke ili kulinda Mahesabu pamoja na store?

Fsnya investment badala ya business au nenda pale Mlimani ity uone wanvyofanya tumia barcode
 
Mkuu usiombee!

Nilikuwa nafanya kazi na dogo mmoja nauza spare na oils,sasa siku moja akaja jamaa nilikumbuka kumuona sana akija kufanya manunuzi pale dukani so nikawa nimekariri bidhaa anazopenda kuchukua mara kwa mara ila siku hiyo akaja akataka bidhaa tofauti na alizozoea,(kwangu halikuwa tatizo)tatizo ni bidhaa aliyoagiza mbona carton yake ikaonekana nzito sana isivyo kawaida?

Normally,carton ya oil zile litre moja moja uzito wake hauzidi Kg10/12 but nikashangaa mbona hili boksi alilotoa huyu dogo linaonekana zito ameinua hadi mishipa ya shingo imemtoka na amelifunga kamba katikati?siyo kawaida kabisa box jepesi kufungwa kamba(ukweli sikuelewa na ilikuwa ni bahati yangu tu kama ningekuwa bize ningeshaisha)nikamwambia weka hilo box chini,akashtuka ohh bro unajua jamaa ana haraka sana nikamuuliza ana haraka mbona unamsemea wewe yeye hajasema mwenyewe?kuinua macho namuona jamaa yule mteja anavuka mtaa anakimbia na hela yake kaacha,nikajiuliza inakuwaje hapa?sijakaa sawa yule dogo akatoka mle ndani speed alikoswa koswa kugongwa na pikipiki.

Kwa ufupi,alikuwa amejaza spare battery terminals zile za gari kubwa zenye thamani ya Tsh 680,000/= kwenye boksi ya oil yenye thamani ya Tsh 56,000/= ambayo ndo nilikuwa nimelipwa mkononi!!utauwa mtu!!!mimi sasa hivi kama sipo office haifunguliwi acha nipate hasara ya siku kuliko kuamini tena mtu.
Ushauri huu mzuri.. thanks mkuu
 
P
Hapo Kwenye kupata store keeper mwaminifu ndo changamoto ilipo ......Maisha ya sahv kila mtu anataka kutoka .( Kuwa na maisha mazur) hii tamaa ndo inafanya watu wanakua sio waaminifu ... Wanaweza wakawa hawamuibii jamaa ..ila wanakuja na vitu vyao wanauza ... Ili na wao wanufaikie ...Hii michezo ipo sana
POINT ya mwaka
 
Boss hakuna njia ya kuzui kuibiwa ila kuna njia za kupunguza kuibida yaaani wizi ufanyike kwa uchache

1) tenganisha duka na stooo weka kumbuku kumbu ya mali inayoingia stoo

2) funga kamera mlangoni stoo kisha kila mali inayotoka stoo kwenda dukani/ kuuzwa lazima iandikwe

3)kazi yako kubwa iwe kuangalia ni mali kiasi gani inatoka/tafuta kijana wa stoo atakuwa anatoa mzigo

Mfumo huu unapinguza wizi wanatumia sana watu wa moshi mfano kwa MARENGA pale au Kwa LASWAI
 
Naona mpaka Sasa....jamaa hajapata mbinu sahihi...,....wapo waliosema mifumo,wengine camera.....zote zinamapungufu......kifupi binadamu ameshindikana.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Sijaona aliyeshauri bado kuhusu kutafuta watu ambao ni waaminifu na uaminifu wao utakuja pale umewalipa vizuri,unaweza ukafunga CCTV camera even ukakaa na kijana dukani still ukapigwa.

Nina experience na haya mambo,vijana huwa wanachonga deal na wateja wazoefu wa duka lako au wajanja wajanja walio nje mfano hapo umesema unauza biscuits, siujui bado utofauti wa bei kati ya carton ya biskut na tomato ipi kubwa ila wanachofanya huchana boksi la tomato na kuzitoa na kulijaza biscuits (ni mf kama kimoja wapo kitakuwa na bei kubwa zaidi) na kulifunga vizuri kisha anampanga mtu “bwana njoo dukani toa order ya tomato” mimi mteja nikija nakulipa wewe boss pesa ya thamani ya tomato let's say 30,000/= wewe utaagiza kamtolee tomato akiingia store anatoa lile box alilojaza biskut zenye thamani mf 70,000/= na box inapita mbele yako ukijua ni tomato kumbe sivyo.

Ni changamoto sana,may be kama alivyoshauri mdau hapo juu uwe na software utakayotumia kulinda mali zako nayo pia ni gharama nahisi but bora kuwa nayo.
Hii nimeichukua
 
Mkuu usiombee!

Nilikuwa nafanya kazi na dogo mmoja nauza spare na oils,sasa siku moja akaja jamaa nilikumbuka kumuona sana akija kufanya manunuzi pale dukani so nikawa nimekariri bidhaa anazopenda kuchukua mara kwa mara ila siku hiyo akaja akataka bidhaa tofauti na alizozoea,(kwangu halikuwa tatizo)tatizo ni bidhaa aliyoagiza mbona carton yake ikaonekana nzito sana isivyo kawaida?

Normally,carton ya oil zile litre moja moja uzito wake hauzidi Kg10/12 but nikashangaa mbona hili boksi alilotoa huyu dogo linaonekana zito ameinua hadi mishipa ya shingo imemtoka na amelifunga kamba katikati?siyo kawaida kabisa box jepesi kufungwa kamba(ukweli sikuelewa na ilikuwa ni bahati yangu tu kama ningekuwa bize ningeshaisha)nikamwambia weka hilo box chini,akashtuka ohh bro unajua jamaa ana haraka sana nikamuuliza ana haraka mbona unamsemea wewe yeye hajasema mwenyewe?kuinua macho namuona jamaa yule mteja anavuka mtaa anakimbia na hela yake kaacha,nikajiuliza inakuwaje hapa?sijakaa sawa yule dogo akatoka mle ndani speed alikoswa koswa kugongwa na pikipiki.

Kwa ufupi,alikuwa amejaza spare battery terminals zile za gari kubwa zenye thamani ya Tsh 680,000/= kwenye boksi ya oil yenye thamani ya Tsh 56,000/= ambayo ndo nilikuwa nimelipwa mkononi!!utauwa mtu!!!mimi sasa hivi kama sipo office haifunguliwi acha nipate hasara ya siku kuliko kuamini tena mtu.
Duuh aisee pole na hongera kwa machale. Napata wazo jipya pia hapa kwa kusoma hili
 
Ngoja ni-nene nliyojifunza hapa kwa faida ya wengine sharing is caring.

1. Dukani pawe na software nzuri yenye maingizo/mauzo/stock kifupi moments zote za dukani ziwe systematically.

2. Tenga muda, au weka mkakati au utaratibu wa kufungua box uangalie kilichomo ndani (Fanya randomly) na ukague mara kwa mara hata mpigaji onamjengea kuwa boss anakagua uchakachuzi. Beba box kadha wa kadha kupima uzito unafanana au unatofautiana.

NB kifupi uwe na utaratibu fulani wa kuwa Fanya waone boss yupo serious.

3. Kama utaweza ukatengeneza sole tape fulani unique yenye logo ya duka ukaimiliki only you mwenye duka. Ukapiga tape maeneo ya kufungua box Ili ukiona sign ya ujanja ujanja inakua rahisi kugundua ubadhilofu.

4. Camera muhimu kama walivyosema wadau wengine. Mdau mmoja akasema stoo na duka vitengane. Changamoto wkt mwingine zikiwa mbali mbali Kuna room ya manoeuvre ila ni kupambana TU.

5. Panga utaratibu wa kupita na stock na mauzo uone je mauzo na vilivyobaki vinaongea lugha moja au la! Wasikukariri kwamba Kila ijumaa boss anapita, Fanya mambo ya ghafla itawajengea vijana kujua wapo kwenye kikaango wkt wowote.

6. Kwa kweli nawashukuru nyote mliotoa nondo za kueleweka. Mmenipa new experience ikiwa nipo mbioni kufanya biashara hii. Mmbarikiwe na hayo hapo juu ni ambayo nimeona kama ni mkakati fulani wa kupunguza kupigwa.
 
Back
Top Bottom