Niandae bajeti ya mafuta kiasi gani kwenda Singida?

Niandae bajeti ya mafuta kiasi gani kwenda Singida?

Acheni ubishi hiyo gari nimeinunua kwenye mnada wa pale TPA mwezi january mwaka huu.

Picha za mafano wake nimezituma hapo juu, daah kweli kuna watu wabishi sana utadhani wapo sayari ya mars
Minada TPA huwa ni lini
 
Mkubwa hii ishu ya RPM has a lot to do na idadi ya gears. Gari nyingi za Toyota automatics zina gear 4.

Ili ku cover speed yote ya kisahani lazma gia ziwe ndefu ndefu ila kikomo huwa ni 5,600-6,000 😂! Sasa gear 4 uzigawe kwenye 6K rpm sio mchezo ndio maana gari nyingi including yangu nikishazidi 120 tu rpm inakimbilia 3! Hamna jinsi utafanya, gari ina gear 4 na kumaliza speed lazma rpm zifike ukomo.

Ila Mark X yenye gia 6 unaweza laza mshale ikiwa hata haijafika 3500rpm. Engine kubwa haitumii nguvu sana ku acquire speed.

Same as BMW wao gari zao wanajaza gia nyingi so ni rahisi gari kufika speed kubwa ikiwa kwenye rpm ndogo. Unakuta gari ina gear 8 ila ukifika gear ya 4 tu tayari uko 150 rpm bado iko chini.
Sio kwel kwamba kumaliza speed kisahani rpm inakuwa mwisho

Just cross multiplication Kama mguu ukiwa light at 130kph rpm ikawa tatu may be hapo tunaongelea kina brevis na wenzake Basi 180 utaipata rpm ikiwa below 4500 ila Kama utakuwa unaitafuta 180 kwa speed Kali gari itapangua gia na kujikuta unafika hapo na gia ya tatu huku RPM ikiwa elf sita na,,, gari nyingi zinaeza kaa 180rpm ikiwa chini ya hapo



Kumbuka gia ya mwsho sio kwa ajili ya kutafuta top speed ni for cruising tu...range Rover 4.4l v8 inaeza fika top speed na gia ya sita tu gia ya 7 na 8 ni for cruising where 2800rpm 8th speed uko 240Kph
 
Brother nauwezo wa kyuingiza gia zote rpm isivuke 3 na nikaenda hata speed 180 rpm isivuke 3...

Automatica vehicle unaweza kuengage gia zote kama manual tu na ukaweza kucontrol rpm isivuke 3
😁😁 Hichi ndo nilikataa na haiwezekani hata waliopinga hawakujua namaanisha nini ...gia naweza panga zote na sivuki 3k rpm kila gia nikapanga gia zangu tano

Buuuut speed husika vs ratio ya gia husika at any rpm ita vary kulingana na speed ya gari yako


Mfano umepanga gia zako tano ukafika 3k rpm hapo speed ikawa 130kph kwa hio unataka sema utaendelea Hadi unafika 170 rpm imenata kwenye tatu😁

Em fanya hivi chukua gia mbili ziunge pamoja meno yake labda kwa chain ..gia A iwe na meno kumi , gia B iwe na meno 20

Gia A iwe driver, then gia B iwe driven, gia A ikizunguka Mara 20 gia B itazunguka Mara 10 Wala haiwezi badilika kamwe ..Sasa em nielekeze njia hapo ya kufanya gia A izunguke Mara 20 huku gia B ikizunguka zaidi ya Mara 10 ikiwa zipo connected together by a ratio of 2:1
 
Rpm kwa gia husika speed ni fixed haitabadilika kamwe

Hi maswala ya tembea na rpm flani.. unataka sema kwamba hata akiwa 140kph rpm anaweza amua iwe 2.5[emoji16][emoji848]

Gear ni fixed ratio hazibadiliki kama 4th gear rpm ikawa 3k na speed ikawa 120kph Basi huwezi fika 130 afu rpm imebaki pale pale utacross multiplication kujua RPM itakuwa ngap Kama utasogea Hadi 130 na kuendelea
Pia maswala ya RPM kila engine kwenye body husika zitakuwa tofauti kulingana na nguvu ya engine

Mfano pindi premio ikiwa na 4th gear 3k rpm speed ni 120 Basi engine kubwa zaidi inaeza kaa vizuri 120kph bila rpm kufika 3k au engine ndogo inaeza fika hio speed mfano Suzuki kei 0.7l ila haiwezi kaa RPM tatu Kama ilivokaa premio na magari mengine

3K rpm last gear kwa range Rover ya 2013 diesel 4.4L v8 speed hapo itakuwa 220kph

Premio, mark x, crown, brevis 3k rpm last gear speed huwa 120-135kph
Kirikuu 3k rpm speed ikizid sana ni 90

Toyo 3k speed 35 gia ya mwsho

Kwa hio ushauri atembee speed 80-90 mwendo mzuri wa wese rpm itakapokuwa hapo hapo ndo uwezo wa gari
Pia haya yote ulioyaandika yanategemea aina ya gearbox iliopo kwenye gari husika, kimfano gear box ya kawaida ya outo inakula zaidi mafuta kuliko gearbox ya outo ambayo ni c.v.t.
 
Minada TPA huwa ni lini
Hii unajisajili TRA kwa kupitia TIN yako hivyo nenda kwenye ofisi ya eneo lako waombe wakusajili online bider, utakuwa unaingia kwenye website yao kutazama kama kuna mnada.
 
Pia haya yote ulioyaandika yanategemea aina ya gearbox iliopo kwenye gari husika, kimfano gear box ya kawaida ya outo inakula zaidi mafuta kuliko gearbox ya outo ambayo ni c.v.t.
Yes CVT Kuna ka uhafadhali


Nishatoka na 5A safari kilometa 920.. speedometer haikuwa accurate dash ikisoma 70kph speed iko 103 kwa gps

Ila safari nzima hakuna saa nimecruise na 3k rpm muda wote nilikuwa 2- 2.8rpm

Means safari nzima hakuna saa nimegonga 130kph kwa rpm hizo
 
Hakikisha tu unafanya service, itapunguza sana fuel consumption, two, hakikisha uendeshaji wako ni mzuri, ukiweza kuchezea kwenye RPM ya 2-3.5 utasevu pakubwa saaaana, Mafuta ya 450,000 Hadi 550,000 "yanaweza" kuwatosha. Hakikisha unajaza full tank, usijaze Robo robo pia usijaze kwenye vituo vya kihuni.

Last month nilitoka Dar, nikaenda Kwa Msisi (Mkata-Tanga) then nikaendelea na safari ya Dodoma nikaenda Matumbulu, nikaenda Manyoni Hadi Itigi.

Niliondoka saa tisa usiku Dar, nikajaza Mafuta ya 220,000 pale Mlimani city, nikaenda safari zangu, nikaja kujaza Mafuta ya 40,000 Ihumwa wakati naingia Dodoma, Kesho nikaenda Matumbulu (25km) Kutoka Dodoma mjini Ile Iringa road then mchana nikaendelea na safari nikajaza pale Total kule four ways ya 50,000 nilipofika Manyoni nikajaza ya 50,000. Nikafika Itigi nikiwa na robo tank juu kidoogo Karibu na half.

Kwa wewe unayeenda Moja kwa Moja nadhani hata 250,000 Inawezekana ikakufikisha depending na aina Yako ya uendeshaji

Nilihakikisha sizidi 4rpm kwahio karibia 90% ya safari nilikua Chini ya hapo, sikua na ligi na mtu barabarani.
Gari ilikua ni BMW salon.
Kumwambia aendeshe rev kati ya 2 hadi 4 rpm humsaidii sana .
Ni kweli kabisa hizo rev range huwa zinatoa good fuel economy , lakini ni jinsigani unafika kwenye hizo rev ndio somo kuu.
Inatakiwa kukanyaga acc pedal kwa upole sana , assume kuna yai bichi kati ya mguu na pedal , na hutaki yai lipasuke wakati unakanyaga
 
Kumwambia aendeshe rev kati ya 2 hadi 4 rpm humsaidii sana .
Ni kweli kabisa hizo rev range huwa zinatoa good fuel economy , lakini ni jinsigani unafika kwenye hizo rev ndio somo kuu.
Inatakiwa kukanyaga acc pedal kwa upole sana , assume kuna yai bichi kati ya mguu na pedal , na hutaki lipasuke wakati unakanyaga
Hahahaha hapo anatakiwa sasa ajiongeze Mpwa, anatakiwa akanyage pedal like anabinya nyonyo kuangalia saratani
 
Acha ubishi wewe usijibu kitu kama haukijui.

Hii gari ni manual na ni 4wheel full time na mifumo yake yote ya suspension ni kama rav4.
Gari hizi zipo nyingi sana uganda na congo wanaziita land cruise.
Jamaa ana asili ya ubishi wa ajabu sana. Kuna siku alikuwa anabisha ukubwa wa engine hauhusiani na displacement nikajua hamna mtu hapo,halafu anaelimisha watu kuhusu magari, sometimes ni better kukaa kimya kutokuumiza kichwa.
 
Back
Top Bottom