Niezeke bati la kiwanda gani kati ya Alaf na Sunshare?

Niezeke bati la kiwanda gani kati ya Alaf na Sunshare?

Usiezeke na bati kabisa. Kuna ujenzi aina mpya umeanzishwa Tanzania na mzee wa Madrassa, hauna haja ya bati na nafasi yote ya kuezeka bati unapata kuitumia.
Tupe elimu na ufafanuzi juu ya huu ujenzi ili nasi tunufaike mkuu.
 
Tupe elimu na ufafanuzi juu ya huu ujenzi ili nasi tunufaike mkuu.
Nakushaauri uwasiliane na mtaalam wa huo ujenzi, anajitangaza sana humu na ameweka namba za kuwasiliana nae kwa whats app, anaitwa Abdul Ghafur 0625249605
 
Kwa sababu umesema wewe sio injinia basi acha nikufundishe..

Kwanza hii hoja ya uzito wa paa kwamba msingi utashindwa himili ni hoja mfu na ya upotodhaji!

Hivi nikuulize uzito wa zege la spab, beam, colums plus tofali na uzito wa bati kipi kizito? Kama msingi unahimili uzito wa slab na beams utashinwa himili kauzito ka bati?

Jua kwamba kabla ujenzi haujaanza usanifu lazima ufanyike na injinia. Na katika hatua hii ndio ana take into account na huo uzito wa bati unao usemea... Na huwezi jenga kabla ya usanifu haujafanywa na kupitishwa!

Unless uwe umetumia makanjanja mtaani ila mpaka msingi unajengwa jua washajua una uwezo wa kuhimili uzito wa bati na slab na kila kitu!

So hiyo hoja ya bati kuwa zito futa maana haina mantiki!
Wewe ndio umeharibu kabisa? Kwahiyo kama uzito wa slabs na tofali waweza kuhimilika, ndio tuongezee mzigo mwingine bila ulazima wowote? Inaelekea hujui hesabu za kujumlisha na kutoa. Halafu unatuletea mambo ya mahesabu ya mainjinia kama vile hujui ujenzi wa watanzania walio wengi ulivyo. Kifupi jamaa kachambua kimantiki na kitaalamu kabisa. Ulichofanya wewe ni uvurugaji wa hoja.
 
Wewe ndio umeharibu kabisa? Kwahiyo kama uzito wa slabs na tofali waweza kuhimilika, ndio tuongezee mzigo mwingine bila ulazima wowote?

Mwisho wa siku utauliza "kwa hiyo kama uzito wa slab na tofali unaweza himilika ndio tuongeze uzito nondo?"...
 
Yaani mama sikunyengine nenda tu pale Sunshare moja Kwa moja patana mwenyewe unasubiria bati Zako unaondoka hakuna cha Alaf wala mnyama Simba.

Kikubwa nikuhakikisha bati umenunua kiwandani mwenyewe hapo Sunshare ni madhubuti mno fundi wala hajakundanganya nimeezeka Chanika Taliani mwaka wa 7 halijapauka mvua ikipiga ndo yanazidi kung'aa kama limepauliwa Leo Ila ndo ivo ushafanya maamuzi usibabaike na majina.
 
Tuelezee wewe jinsi unavyojua kutokana na maelezo yao tuyapime hapa. Haya mambo ya ku-refer naona kama ni ukanjanja tu.
Una haki ya kuona vyovyote uonavyo baada ya kufanya tafiti japo ndogo. Bila tafiti utabaki kuwa wewe kanjanja.

Wasilaiana nao, nimeweka namba zao juu hapo, na wamo humu JF. Kama huwezi, mimi siwezi kukusaidia zaidi ya kukupa mawasiliano nao. Tatizo nini?
 
Tuelezee wewe jinsi unavyojua kutokana na maelezo yao tuyapime hapa. Haya mambo ya ku-refer naona kama ni ukanjanja tu.
Hajafanya vibaya kukuelekeza kwetu. Tupo hapa JF na namba alizokupa ni zangu binafsi.

Nadhani Umewahi kusikia kuwa siku hizi Tanzania watu wanaezeka kwa mtindo ambao bati halionekani. Sisi tumeenda mbali na kisasa zaidi ya bati kutoonekana. Tunaunda (precast) vifaa maalum vya zege kwenye kiwanda chetu kidogo hapa Misugusugu, Kibaha. Pia tuna uwezo wa kuundà vifaa hivyo site ya mteja ili kupunguza gharama za usafirishaji vifaa.

Vifaa hivyo (slabs) vinakua mbadala wa bati na mbadala wa gypsum boards kwa pamoja.

Kwa vifaa hivyo Unapunguza gharama za kuezeka kwa bati, zinapunguza gharama za.mbao za bati, zinapunguza gharama za gypsum boards na mbao zake. Pia utapata nafasi juu ya kufanya chochote upendacho. Tuna supply vifaa na pia tuna mafundi wazoefu.

Programme yetu inaitwa Abraar Bricks Nyumba kwa wote. Ubora wa hali ya juu kwa gharama nafuu.

Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kwa whatsqpp 0625249605.

Pia tunaweza kukujibu hapa swali lolote ulilonalo.

Karibu sana.
 
Hajafanya vibaya kukuelekeza kwetu. Tupo hapa JF na namba alizokupa ni zangu binafsi.

Nadhani Umewahi kusikia kuwa siku hizi Tanzania watu wanaezeka kwa mtindo ambao bati halionekani. Sisi tumeenda mbali na kisasa zaidi ya bati kutoonekana. Tunaunda (precast) vifaa maalum vya zege kwenye kiwanda chetu kidogo hapa Misugusugu, Kibaha. Pia tuna uwezo wa kuundà vifaa hivyo site ya mteja ili kupunguza gharama za usafirishaji vifaa.

Vifaa hivyo (slabs) vinakua mbadala wa bati na mbadala wa gypsum boards kwa pamoja.

Kwa vifaa hivyo Unapunguza gharama za kuezeka kwa bati, zinapunguza gharama za.mbao za bati, zinapunguza gharama za gypsum boards na mbao zake. Pia utapata nafasi juu ya kufanya chochote upendacho. Tuna supply vifaa na pia tuna mafundi wazoefu.

Programme yetu inaitwa Abraar Bricks Nyumba kwa wote. Ubora wa hali ya juu kwa gharama nafuu.

Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kwa whatsqpp 0625249605.

Pia tunaweza kukujibu hapa swali lolote ulilonalo.

Karibu sana.
Ningeonapo kapicha ka nyumba iliyopauliwa kwa mtindo huo ningeweza kuhamasika zaidi,nina nyumba ya kupaua nakusanya nguvu
 
Kupauka kwa bati hakutegemei imetengenezwa wapi. Angalia specs . Omicron ni kipimo muhimu kwenye Kupauka kwa rangi. Kinacho wabeba ALAF ni brand na siyo ubora. Ando na Sunshare wana quality bora. Ask ALAF to give you a written guarantee ya hate miaka mitano. Kama hela ipo nenda Nabaki Decra.
 
Hajafanya vibaya kukuelekeza kwetu. Tupo hapa JF na namba alizokupa ni zangu binafsi.

Nadhani Umewahi kusikia kuwa siku hizi Tanzania watu wanaezeka kwa mtindo ambao bati halionekani. Sisi tumeenda mbali na kisasa zaidi ya bati kutoonekana. Tunaunda (precast) vifaa maalum vya zege kwenye kiwanda chetu kidogo hapa Misugusugu, Kibaha. Pia tuna uwezo wa kuundà vifaa hivyo site ya mteja ili kupunguza gharama za usafirishaji vifaa.

Vifaa hivyo (slabs) vinakua mbadala wa bati na mbadala wa gypsum boards kwa pamoja.

Kwa vifaa hivyo Unapunguza gharama za kuezeka kwa bati, zinapunguza gharama za.mbao za bati, zinapunguza gharama za gypsum boards na mbao zake. Pia utapata nafasi juu ya kufanya chochote upendacho. Tuna supply vifaa na pia tuna mafundi wazoefu.

Programme yetu inaitwa Abraar Bricks Nyumba kwa wote. Ubora wa hali ya juu kwa gharama nafuu.

Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kwa whatsqpp 0625249605.

Pia tunaweza kukujibu hapa swali lolote ulilonalo.

Karibu sana.
kapicha mzee Ghafur
 
Karibu
YVOM.jpg
 
Naomba nitoe mchango wangu kutokana na nilichojifunza kwa muda mfupi kwenye hii industry ya roofing.

Kwanza nisema watu wengi kila siku wanajenga au kufanya biashara hizi lakini kuna mahali wanafeli ku grasp taarifa sahihi za kitaalam.

Nitazungumzia viwanda nilivyotembelea Alaf, Sunshare, Bati Bomba na kingine pale Tabata..

Gauge za mabati hutofautiana kulingana na unene au thickness ya bati, G30 inakadiriwa kuwa na thickness ya 0.25mm na G28 ni 0.35mm. This is techinical diferences. Na pia kuna chemical diferences lakini karibu zote zinafanana maana zimeundwa na Aluminium na Zinc ktk ratio tofauti tofauti. Zinc na Aluminium ndio properties zinazozui bati kuota kutu kama ikiform zinc oxide au Aluminium Oxide.

Matumizi ya Gauge ktk nyumba.

Kama mleta mada alivyouliza nini tofauti ya matumizi ya bati G28 dhidi ya G30.

1. Hutegemea na mahitaji ya mjengaji, mfano serikali inayojenga majengo makubwa kama kiwanda, godauni, shule au hospitali hutumia bati zenye thickness kubwa kutokana na umuhimu wa jengo lenyewe tofauti na mtu binafsi anayejenga nyumba ya vyumba vitatu.

2. Uimara wa nyumba, msingi na teknolojia ya ujenzi. Hapa tunaona kuwa nyumba kubwa inahitaji mabati mengi zaidi. Lakini pia kama nyumba imejengwa na Fundi Maico yatarajiwa viwango vyake vya uimara( strength) ya msingi na ukuta vitakuwa si mujarabu hivyo kuezeka nyumba hii kwa G28 inaweza kupeleka uzito mkubwa unaoweza kuhatarisha maisha ya nyumba yako. Vile vile kama hali ya hewa ya udongo, maji kutwama, mmomonyoko n.k vyaweza kupelekea nyumba kutitia.

Hii ni muhimu kwa sababu Bando la bati 16 , G28 lina karibu uzito wa kilo 92 wakati bando la bati 16 G30 lina uzito wa takribani kilo 50. Kwahiyo nyumba kubwa kama shule, godauni, kanisa au hospitali utajenga kwa bando ngapi na huo msingi na ardhi vitahimili hizo tani za uzito wa paa??

3. Teknolojia ya uezekaji. Hii inaenda sambamba na ukubwa wa jengo. Nyumba zetu hizi kenchi hadi kenchi ni mita moja tu au chini ya hapo. Shule na kanisa au msikiti vipimo ni vikubwa zaidi so yafaa G28.


Kuhusu Bei za Mabati kutofautiana.


Katika uchunguzi wangu nilifikia hitimisho kuwa hakuna tofauti kubwa ktk bei na utofauti wa bei haumanishi yenye bei kubwa ni imara na bora zaidi. Fuatana nami:


Wauzaji wengi watakueleza kuhusu Gauge ya bati, rangi, na urefu na bei kamwe hawakwambii upana wa bati.

Mfano. Kiwanda cha tabata bati la G30. Migongo mipana( msauzi) urefu futi 10 linauzwa elfu 30. Bati hilo hilo Kiwanda cha Bati Bomba wanauza elfu 28,500. Lakini ni hivi upana kwa Tabata ni 750mm wakati BatiBomba ni 90mm. Vivyo hivyo Sunshare bati zao upana ni 870mm na wanauza elfu 34,500 kwa bati hilo hilo la urefu futi 10, G30 na rangi ile ile.

Kwa G28 Batibomba wanauza futi 10 migongo mipana kwa 34500 wakati ALAF wanauza takriban 55,500. Unaweza kudhani Alaf wanauza bei kubwa sana lakini ALAF bati zao upana ni 1220mm wakati Batibomba ni 900mm. Hapa utaona kuna tofauti kubwa sana. Uki converge hizi factors kwa pamoja utakuta wote bei karibu sawa.

Mfano huo huo unaenda kwa Sunshare na Tabata.
So utahitaji kununua mabati machache ALAF a utahitaji mabati mengi Sunshare.

Jambo lingine linaloweza kuchangia utofauti wa Bei( usihusishwe na ubora au uimara) ni miundo mbinu ya uzalishaji mali pamoja na rasilimali watu.

Mfano. ALAF wana majengo mazuri ya kisasa ya kibiashara full kiyoyozi na ukifika pale kama uko nyumbani au ofisi ya CAG Kichere. Wakati ukifika Tabata na Batibomba joto na vumbi mwendo mdundo wanazalisha kwenye magodown hapo hapo ndio wateja wanachukulia mizigo yao. Hawa watu hawawezi kuchaji bei sawa. Lazima bei za pango na mandhari mazuri uyalipie. Hivyo hivyo kwa Makampuni mengine.

Ushindani wa kibiashara: makampuni mengine nje ya ALAF ni mapya na mageni. Hivyo wanaunafuu kidogo kutokana na mahitaji ya kujitangaza na kujitanua. ALAF tayari ni mkongwe wajenzi wa viwanda na serikali inachukua mizigo mikubwa kwake. Hana shida na hizo milioni zako 2,3, 4, 5...


Kuhusu Malighafi

Wote wananunua kwa supplier wanaofanana. Aidha South afrika au China na india. Na wote mali zao huingizwa zikiwa tayari zimeshachanganywa materials na Rangi. Kazi yao hapa Dar ni kukata na kukunja muundo unaotaka IT4, IT5, Versatile, Romantile....etc.

NB: mimi sio Injinia wa ujenzi wala sina any formal profession kwenye industry hii. Hii ni kutokana na elimu ya hapa na pale niliyodanya mimi mwenyewe kwa kuona, kuuliza, kushika na kusikia viwandani.

Penye makosa/ mapungufu wataalam karubuni kurekebisha.
Ujengewe sanamu mkuu.
 
Back
Top Bottom