Nifanye nini kufuta kumbukumbu za matukio mabaya kwa watoto wangu?

Nifanye nini kufuta kumbukumbu za matukio mabaya kwa watoto wangu?

Kwahiyo asingekufukuza ungeendelea kuvumilia kipigo!![emoji848][emoji848][emoji848][emoji848]

Bahati mbaya hiyo haitokaa ifutike kamwee, ni kama kuchora tatoo. Hiyo ni kumbukumbu ya kudumu kwenye maisha yao. Wewe cha msingi sasa ni kuanza kuzungumza nao kuhusu na kuwaonyesha upendo. Waonyeshe madhara ya ulichopitia na kama ni wa kiume wasije kuwa kama baba yao na kama ni wa kike wasijevumilia kipigo.
 
.... pole Sana,ila naamini kuna reasons behind kwa nini alikuwa anakupiga. Mojawapo ni kuchepuka (labda ulianza mahusiano na huyu mumeo wa sasa wakati ukiwa na baba yao). Kwa kuwa tumesikia upande mmoja hatuna jinsi kupokea kama lilivyo. Too bad kwamba watoto wame-experience hilo.
kasome uzi wa Mwasapile

akivurugwa na mchepuko hasira anaenda kumalizia kwa mke na watoto

sasa hapo sijui na mke wa mwasapile alikuwa anachepuka
 
Kwa nini unawafundisha watoto kuwa baba anayempiga mama ni baba mzuri,,acha kuwafundisha hivyo wao wameona na wanajua kuwa siyo vizuri.Ila watasahau wakikua
 
Hivi nyie hamkuwa watoto? Baba yako anampiga mama yako anavimba uso ukiwa na miaka 5,6,7, 8... halafu usahau? Kama una akili ya kawaida ya binadamu, hauwezi kusahau. Unaweza kupotezea tu lakini siyo kusahau. Wapo pia wasioweza kupotezea. Wanakuwa maadui mpaka kifo.
Kwa nini unawafundisha watoto kuwa baba anayempiga mama ni baba mzuri,,acha kuwafundisha hivyo wao wameona na wanajua kuwa siyo vizuri.Ila watasahau wakikua
 
Salaam wakuu

Miaka michache iliyopita nilipitia mambo mengi kwenye ndoa ambayo nikiri kuwa hayakuwa mazuri kwa ukuaji wa watoto wetu kisaikolojia.

Watoto walishuhudia nikipigwa mara nyingi sana, nikitukanwa au kusemwa vibaya. Na hata kuna wakati ugomvi ukitokea chumbani walikuwa wanakuja kusikiliza mlangoni kwetu na kujua ndani kuna ugomvi au kusikia kilio na milio ya makofi na mangumi. Na pia walikuwa wanaona nikiwa nimevimba uso macho au michubuko iliyotokana na vipigo. Na mara kadhaa kama mlango haukufungwa walikuwa wakiingia chumbani kunitetea ili nisiumizwe zaidi.

Hawana umri mkubwa wote watatu bado wako shule za msingi. Mara nyingi walikuwa wakiona baba yao akifika tu na upepo wa ndani unabadilika kama sio wao kupigwa basi ni mama maana alikuwa mkali sana kwa watoto na kwangu.

Nilianza kuhisi tatizo kwao kipindi ambacho bado tupo pamoja hatujaachana. Siku moja mwanangu aliniuliza swali, MAMA KWANINI TUSIENDE KWA BIBI ILI BABA ASIKUUE? ( Kauli kubwa wakati akinipiga alikuwa anasema IPO SIKU NITAKUUA) na watoto walikuwa wanasikia hivyo kuoata hofu ya mimi kuuawa siku moja. Nikaamua kuongea na baba yao kuhusu swala hilo kuwa watoto wanahofu aache kunipiga ila akajibu nimewajaza sumu kuwa baba yao mbaya nk ioa sijawahi fanya hivyo na ukatokea ugomvi akanipiga na kunifukiza kabisa ili nisimwqribie watoto wake.

Japo baadaye niliwapata watoto na kuanza kuishi nao maana tangu hapo tuliachana moja kwa moja na sasa naishi maisha mengine. Ila tatizo limebaki owa watoto kioa mara wanaomhelea jinsi nilivyopigwa na yote.

Mnaweza kuwa mmekaa unaona mtu anasema mama bora tulivyokuja huku hata hupigwi tena, au wala sisi hatupigwi tena nk najaribu kuwaambia baba yenu anawapemda, ni mtu mzuri nk ila hawaeleqi na wananibishia na kumfananisha na monster wa kwenye movie. Binafsi siongelei chochote kibaya kwao ioa wao hawasahau katu. Na hata akipiga simu kutaka kuwasalimia hawakubali hadi nakata siki, nikimwambia hawataki ananilaumu kuwa wqnajaza sumu kitu ambacho sifanyi.

Naandika haya nikiwa nimeshajitahidi kufanya mambo kadhaa ikiwa ni pamoja kuwaamisha kwamba baba yao ni mtu mwema, na anawapenda ila hawakubali.

Binafsi nilishaolewa, sasa wanampenda baba yao mpya na wanasemq ndio baba yao na si yule mwingine( huwa wanamwambia wao wakiwa wanapiga naye stori, wanamwambia shule waitwe fulani bin jina la baba mpya) hataki kusikia kuhusu baba yao kabisa.

Je, hii inaweza saidika kifuta hizi kumbukumbh au niwaache tu walivyo?
Pole sana kwa hayo ila kwakuwa watoto walikuwa wanashuhudia hayo yote, ni vigumu sana kuwaaminisha kitu kingine mbali na uhalisia.

Haujachelewa hao wanao acha waamini kile wanachoamini mpaka utakapoona sasa ni watu wazima au tayari wanajielewa zaidi, wakumbushe uhalisia wote ila waeleze after all ni baba yao so wamsamehe na kuendelea na mambo mengine.

Stop stop kuwaaminisha kisicho unaweza sababisha tatizo lingine.

Ushauri tu

TEKERI.
 
Salaam wakuu

Miaka michache iliyopita nilipitia mambo mengi kwenye ndoa ambayo nikiri kuwa hayakuwa mazuri kwa ukuaji wa watoto wetu kisaikolojia.

Watoto walishuhudia nikipigwa mara nyingi sana, nikitukanwa au kusemwa vibaya. Na hata kuna wakati ugomvi ukitokea chumbani walikuwa wanakuja kusikiliza mlangoni kwetu na kujua ndani kuna ugomvi au kusikia kilio na milio ya makofi na mangumi. Na pia walikuwa wanaona nikiwa nimevimba uso macho au michubuko iliyotokana na vipigo. Na mara kadhaa kama mlango haukufungwa walikuwa wakiingia chumbani kunitetea ili nisiumizwe zaidi.

Hawana umri mkubwa wote watatu bado wako shule za msingi. Mara nyingi walikuwa wakiona baba yao akifika tu na upepo wa ndani unabadilika kama sio wao kupigwa basi ni mama maana alikuwa mkali sana kwa watoto na kwangu.

Nilianza kuhisi tatizo kwao kipindi ambacho bado tupo pamoja hatujaachana. Siku moja mwanangu aliniuliza swali, MAMA KWANINI TUSIENDE KWA BIBI ILI BABA ASIKUUE? ( Kauli kubwa wakati akinipiga alikuwa anasema IPO SIKU NITAKUUA) na watoto walikuwa wanasikia hivyo kuoata hofu ya mimi kuuawa siku moja. Nikaamua kuongea na baba yao kuhusu swala hilo kuwa watoto wanahofu aache kunipiga ila akajibu nimewajaza sumu kuwa baba yao mbaya nk ioa sijawahi fanya hivyo na ukatokea ugomvi akanipiga na kunifukiza kabisa ili nisimwqribie watoto wake.

Japo baadaye niliwapata watoto na kuanza kuishi nao maana tangu hapo tuliachana moja kwa moja na sasa naishi maisha mengine. Ila tatizo limebaki owa watoto kioa mara wanaomhelea jinsi nilivyopigwa na yote.

Mnaweza kuwa mmekaa unaona mtu anasema mama bora tulivyokuja huku hata hupigwi tena, au wala sisi hatupigwi tena nk najaribu kuwaambia baba yenu anawapemda, ni mtu mzuri nk ila hawaeleqi na wananibishia na kumfananisha na monster wa kwenye movie. Binafsi siongelei chochote kibaya kwao ioa wao hawasahau katu. Na hata akipiga simu kutaka kuwasalimia hawakubali hadi nakata siki, nikimwambia hawataki ananilaumu kuwa wqnajaza sumu kitu ambacho sifanyi.

Naandika haya nikiwa nimeshajitahidi kufanya mambo kadhaa ikiwa ni pamoja kuwaamisha kwamba baba yao ni mtu mwema, na anawapenda ila hawakubali.

Binafsi nilishaolewa, sasa wanampenda baba yao mpya na wanasemq ndio baba yao na si yule mwingine( huwa wanamwambia wao wakiwa wanapiga naye stori, wanamwambia shule waitwe fulani bin jina la baba mpya) hataki kusikia kuhusu baba yao kabisa.

Je, hii inaweza saidika kifuta hizi kumbukumbh au niwaache tu walivyo?
Pole.Ila siungi mkono watoto kuitwa jina la baba mpya mana wa kwanza hajawakataa.Kukubali hilo manake watoto ndiyo umetaka wakuongoze ktk maamuzi kitu ambacho kitaleta mtafaruku badaye mana hujawaasili kisheri(kurasimisha kwa baba mpya).Kingine ulipaswa kuchukuwa hatua za kisaikolojia kwa watoto.
 
Ni kweli kuna sababu. Sababu ni kuwa alikuwa ana mwanamke mwingine ambaye alikuwa anataka kuishi naye hivyo alikuwa ananifukuza niondoke aishi na huyo mwanamke.

Mwanaume ninayeishi naye sikuwa naye kipindi cha ndoa nilimpata baada ya kuachika.

Soma nyuzi za nyuma utakuja kukutana na kioamde kinachomuhusu.

Asante.
Sasa huyo mwanamke mwingine amemuoa?
 
Kwani umeambiwa mtoa mada anataka kuwapa jina la baba wa kambo? Kasome tena...
Pole.Ila siungi mkono watoto kuitwa jina la baba mpya mana wa kwanza hajawakataa.Kukubali hilo manake watoto ndiyo umetaka wakuongoze ktk maamuzi kitu ambacho kitaleta mtafaruku badaye mana hujawaasili kisheri(kurasimisha kwa baba mpya).Kingine ulipaswa kuchukuwa hatua za kisaikolojia kwa watoto.
 
Mm mwenyew nilishi maisha Kama ya hao wanao HV mzee wangu r.i.p alikuwa mtata San yaani nilimuona Mara kibao mzee wangu akimpiga maza na matuzi juu kwa juu .nilishaingilia kati lkn wapi tuliishiwa kupigwa wote mm na dad angu na mdg wetu tunabaki tunalia tu na mam pia mzee alipiga aise siyo utani kiliniumiza sna Kuna wakt nilianza kuvuta bangi ili niweze kupamabana na ukatili wa mzee wangu lkn wapi nilipigwa Zaid na ukatili ulizid wa mzee

Nilisha muona mam angu akikunnja nguo tayari kwenda kwao duh tulilia sna tukaenda kumuomba mzew mtu mzima aje amzuie mam asiondoke Hapo mzee Alisha sema aondoke ataki kumuona hapa

Mzee wetu alikuja kupunguza ukorofi around 2006 HV tayari kak zangu wako vyio vikuu na sis Yuko secondary

Automatically mzee alikuja San kurejesha upendo kwetu na kutuambia kuwa tuungane na tupendane San na kumjali mam yetu
Sijui pepo la ukorofi alilipata wapi mnk mama anasema hi tabia hajawia kuona

Mama alisema alichelewa San kupata watot alikaa miaka 6 Bila kuwa na watot na mzee alimvumilia sna bila kumnyanyaza Wala kutak kuoa Tena pmj na kushinikizwa na bb kuwa aoe mke mwingine sas anashanga mbna kabadili katikat hapo tulishangilia sna na kushangazwa kwa ukorofi wa mzee wetu wa gafla

Mpk mzee wetu anakuja kufariki aise alikuwa na upendo mkubwa sna kwetu ss na kutuasa kupendana na kumjali mama na ss pia tulimpenda Sana Bab yetu mno kwa jins alivyokuwa anatumbambania

Pole sana kwako huwenda Bab yule atabadilika sikutegemea mzee wangu kuja kubadilika na kurudisha upendo kwetu ss na kutupa kila kitu na elimu pia
 
Waache wakikua kila mtu na akili zake kichwani, huwezi futa hizo kumbukumbu kichwani mwao kilichobaki ni kika mtu atahukumu anavyoona sahihi.
 
Sasa na wewe unataka kuharibu kwa kusema uongo! Hao usione ni watoto ni binadamu nao na wana akili na hisia, kama waliona baba yao akikupiga na kutishia kukuua kwanini uwaambie baba yao ni mtu mzuri na anawapenda? Kwahiyo unawafundisha watoto kuwa mtu mzuri huwa anapiga watu na kutaka kuwaua.

Nadhani kwa kuwa umeshaondoka huko wewe usiongee kuwa baba yao ni mtu mzuri na anawapenda, kama hutaki kuongea ubaya wa baba yao basi kaaga kimya tu na uwaache wao waongee ili wayatoe mioyoni mwao. Usitetee ujinga wa baba yao utawavuruga zaidi!

Watasahau tu, hao ni watoto wanavyozidi kukua watayasahau yote hayo ila waache waongee na usitetee unyama wa baba yao
Big up Sana.. nimependa ulivyo mjibu.. congratulations for such wisert you have in case of giving someone's counseling.
 
Hivi nyie hamkuwa watoto? Baba yako anampiga mama yako anavimba uso ukiwa na miaka 5,6,7, 8... halafu usahau? Kama una akili ya kawaida ya binadamu, hauwezi kusahau. Unaweza kupotezea tu lakini siyo kusahau. Wapo pia wasioweza kupozea. Wanakuwa maadui mpaka kifo.
Maana ya kusahau hapa siyo kupoteza kumbukumbu ni ile waswahili wanasema "Yaliyopita sii ndwele tugange yajayo"
 
Ni ngumu hao watoto kusahau my dear..kikubwa wewe walee tu kwenye misingi mizuri mengine muachie Mungu..nilipita huko sijawahi sahau hata moja.
 
Hivi kuna mwanaume mwenye akili timamu anaweza kumpiga mkewe bila sababu yeyote!?, yaani unafika tu nyumbani unaanza kumpiga mke wako?!,labda mwanaume huyo awe na matatizo ya akili lkn kinyume na hapo Hapana,wanawake huwa wanajifanya innocent sana lakini ndio chanzo cha matatizo yote
 
Hivi kuna mwanaume mwenye akili timamu anaweza kumpiga mkewe bila sababu yeyote!?, yaani unafika tu nyumbani unaanza kumpiga mke wako?!,labda mwanaume huyo awe na matatizo ya akili lkn kinyume na hapo Hapana,wanawake huwa wanajifanya innocent sana lakini ndio chanzo cha matatizo yote
Kiukweli wanaume sijui tuwaelimishe mpaka lini ili muelewe kuwa ikiwa mwanamke ni chanzo cha matatizo suluhisho lake si kupigwa. Kuna wanawake ni vimeo tena vimeo kweli kweli sitaki hata kuwatetea, ila unachotakiwa kufahamu ni implications unazozizalisha katika kumpiga, kumbuka huyo mwanamke ambaye ni kimeo ni MAMA wa mtu mwingine, unapompiga madhara hayabaki kwake tu yanaenda hadi kwa wale wote wanaomuhusu, (watoto wake, ndugu zake, marafiki zake etc).

Sasa turudi kwako mr. muadabishaji kama una mama utajisikiaje kumuona anapigwa na baba yako kwa kile kinachoitwa chanzo cha matatizo? Tujaribu kutokuongea lugha ya ubinafsi katika hili. Usiongee as if duniani uko pekeako na hauhusiani na mtu yeyote!
 
Back
Top Bottom