Nikiwa mdogo niliwahi kucheza draft na Jakaya Kikwete pale Magomeni bila kujua kuwa ni Waziri wa Fedha:Viongozi kuweni wanyenyekevu

Nikiwa mdogo niliwahi kucheza draft na Jakaya Kikwete pale Magomeni bila kujua kuwa ni Waziri wa Fedha:Viongozi kuweni wanyenyekevu

mdukuzi

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2014
Posts
20,925
Reaction score
51,688
Sikumbuki mwaka ila nakumbuka nilikuwa mdogo ,tulitoka na mzee wangu mitaa ya kariakoo tukaelekea mitaa ya Magomeni Mapipa mtaa sikumbuki ila ni karibu na Shibam.

Kufika pale kulikuwa na vijana watoto wamjini hakuna aliyezidi miaka 50,walikuwawakicheza draft,bao,zumna na kunywa kahawa

Vijana wa makamo wawili walikuwa wakicheza draft mmoja akamfunga mwenzake,akamtania kuwa hajui kitu bora acheze na mimi,hapo nikaachiwa nicheze na yule mwingine,yule mwenzake akaenda kusikiliza ushabuki wa mpira,walikuwa wamemzunguka mtu mmoja mnene mfupi ba sauti ya kukwaruza.

Miaka michache baadae nikagundua kumbe yule mtu niliyecheza nae draft ni Mh Waziri wa fedha Jakaya Mrisho Kikwete.

Na yule mtu mfupi mwenye sautiya kukwaruza alikuwa Jamhuri Kihwelu Tantalila,mchezaji wa zamani wa Simba.

Nilikuja tena kuonana na Mh Kikwete akiwa kwenye foleni ya ATM,CRDB Bank Holland House,Ohio Street,kipindi hicho akiwa waziri wa mambo ya nje miaka zaidi ya kumi tangu tukio la Magomeni.

Baada ya hapo niliishia kimuona kwenye luninga na magazetini

Kama mtakumbuka kipindi akiwa Rais alikuwa akitokea mara kadhaa kwenye media akishiriki mazishi ya watu ambao hata hawajulikani nchini,watu hao ni marafiki zake wa hali ya chini kabisa wakiwemo wa magomeni na Saigon Club na Hugo House Kinondoni alikokuwa akienda kunywa Supu

Kuna Mheshimiwa mmoja ajifanya kuigiza kuwa ni mtu wa matabaka yote ila technolojia ikamuumbua,muuza kahawa ni afisa wa TISS,mwingine akamuuzia muhindi wa kuchoma na bastola kiunoni kumbe ni maigizo tu .uungwana hauji kwa maigizo bali huzaliwa nao.

Kwa viongozi wa sasa sidhani kama kuna wazori wa fedha anayeweza kukaa kijiweni jioni,au waziri wa mambo ya nje anayeweza kukaa kwenye foleni ya ATM

Viongozi mmekuwa miungu watu mpaka mnatwambia tukimbilie Burundi.

Jifunzeni kujishusha kama Mh.Jakaya Kikwete nanyi mtakwezwa
 
The one and only JK Rais anayezeeka na Nyota yake ,Mwanasiasa aliyepikwa akaiva akafanya Siasa njema na kuishia kupendwa zaidi nje ya Madaraka.

Mwanasiasa ambaye Jiwe na Genge lake walitumia miaka yao yote sita kumtukana hadharani na kumzima mafichoni bila mafanikio wakaishia kuzimika wao.

Much respect brother,Longlive.
 
The one and only JK Rais anayezeeka na Nyota yake ,Mwanasiasa aliyepikwa akaiva akafanya Siasa njema na kuishia kupendwa zaidi nje ya Madaraka.

Mwanasiasa ambaye Jiwe na Genge lake walitumia miaka yao yote sita kumtukana hadharani na kumzima mafichoni bila mafanikio wakaishia kuzimika wao.

Much respect brother,Longlive.
Mungu ampe maisha marefu
 
Sikumbuki mwaka ila nakumbuka nilikuwa mdogo ,tulitoka na mzee wangu mitaa ya kariakoo tukaelekea mitaa ya Magomeni Mapipa mtaa sikumbuki ila ni karibu na Shibam.

Kufika pale kulikuwa na vijana watoto wamjini hakuna aliyezidi miaka 50,walikuwawakicheza draft,bao,zumna na kunywa kahawa

Vijana wa makamo wawili walikuwa wakicheza draft mmoja akamfunga mwenzake,akamtania kuwa hajui kitu bora acheze na mimi,hapo nikaachiwa nicheze na yule mwingine,yule mwenzake akaenda kusikiliza ushabuki wa mpira,walikuwa wamemzunguka mtu mmoja mnene mfupi ba sauti ya kukwaruza.

Miaka michache baadae nikagundua kumbe yule mtu niliyecheza nae draft ni Mh Waziri wa fedha Jakaya Mrisho Kikwete.

Na yule mtu mfupi mwenye sautiya kukwaruza alikuwa Jamhuri Kihwelu Tantalila,mchezaji wa zamani wa Simba.

Nilikuja tena kuonana na Mh Kikwete akiwa kwenye foleni ya ATM,CRDB Bank Holland House,Ohio Street,kipindi hicho akiwa waziri wa mambo ya nje miaka zaidi ya kumi tangu tukio la Magomeni.

Baada ya hapo niliishia kimuona kwenye luninga na magazetini

Kama mtakumbuka kipindi akiwa Rais alikuwa akitokea mara kadhaa kwenye media akishiriki mazishi ya watu ambao hata hawajulikani nchini,watu hao ni marafiki zake wa hali ya chini kabisa wakiwemo wa magomeni na Saigon Club na Hugo House Kinondoni alikokuwa akienda kunywa Supu

Kuna Mheshimiwa mmoja ajifanya kuigiza kuwa ni mtu wa matabaka yote ila technolojia ikamuumbua,muuza kahawa ni afisa wa TISS,mwingine akamuuzia muhindi wa kuchoma na bastola kiunoni kumbe ni maigizo tu .uungwana hauji kwa maigizo bali huzaliwa nao.

Kwa viongozi wa sasa sidhani kama kuna wazori wa fedha anayeweza kukaa kijiweni jioni,au waziri wa mambo ya nje anayeweza kukaa kwenye foleni ya ATM

Viongozi mmekuwa miungu watu mpaka mnatwambia tukimbilie Burundi.

Jifunzeni kujishusha kama Mh.Jakaya Kikwete nanyi mtakwezwa
Hiyo ni hobby ya wstoto wa mjini hawajivungi..We unashangaa kucheza draft akiwa waziri wa fedha wakati hii hobby aliendelea nayo hadi kwenye uraisi,,kuna mwaka fulani nafika kijijini kwetu Kibindu mkoani Pwani nakuta story nyumban kwamba Jana yake Kikwete alikuwa hapa na wamekula nae Ugali..

mimi binafsi nakumbuka mwaka juzi tulishiriki nae A to Z kwenye msiba wa jamaa yetu Bantu pale Morogoro shughuli zote kashiriki ikiwemo kula ubwabwa na kurusha michanga kaburini
 
Hiyo ni hobby ya wstoto wa mjini hawajivungi..We unashangaa kucheza draft akiwa waziri wa fedha wakati hii hobby aliendelea nayo hadi kwenye uraisi,,kuna mwaka fulani nafika kijijini kwetu Kibindu mkoani Pwani nakuta story nyumban kwamba Jana yake Kikwete alikuwa hapa na wamekula nae Ugali..

mimi binafsi nakumbuka mwaka juzi tulishiriki nae A to Z kwenye msiba wa jamaa yetu Bantu pale Morogoro shughuli zote kashiriki ikiwemo kula ubwabwa na kurusha michanga kaburini
Kitu ambacho hata wewe usingeweza labda ahaaa
 
Kuelekea sikukuu ya kumbukizi ya Mwendazake umeamua kumpa spana za Moto Moto hakika huyu SHETANI mmempania.
 
Kwa leo hii ni vigumu kwa Waziri au kiongozi wa hadhi ya juu kuishi hivyo kwa maana Upendo wa Wengi umepoa Sana...Waovu wameongezeka na Ukichangia na kukua kwa Teknolojia utashangaa kila mtu anachukua Smartphone anataka kuselfie,

mwingine anakupiga picha mgongoni...yaani ustaarabu umepotea kila mtu anakung'ang'ania ili tu auze sura mtandaoni kwamba alikuwa na wewe..

Yaani ustaarabu umepotea kabisa... Kwa hiyo kiongozi hata kama anatamani kiasi gani kujichanganya na watu anakuta anakosa ujasiri anaishia kujichimbia kwenye gari na Vyumba vya mahotelini..

Kama sikosei mwaka Juzi Bosi wa TISS kwa wakati huo Diwani Msuya alienda kwao Same kula sikukuu akapaki gari akaenda kusalimia majirani, Tayari Mtu ameshapiga gari picha na kuanza kuzisambaza Mitandaoni na Kejeli kibao.... Anashindwa kujua kwamba na yeye ni binadamu anahitaji Faraja na ushirika na Wananchi wenzake...

Yaani mtu akipata Fursa ya Kuongea na waziri hata kwa Dakika Mbili basi anaichukulia hiyo kama Fursa ya kumchongea Bosi wake kazini yaani anafukua Matatizo au changamoto ambazo pengine zingetatulika kwa Mazungumzo ya kawaida ofisini basi anaikuza inakuwa Kubwa.....

Mtu akipata namba ya kiongozi na kufanikiwa Kuchat naye kidogo basi ndiyo atawatishia wafanyakazi wenzake mpaka wakome Kitu kidogo tu anaanza vitisho, utasikia "Nampigia waziri nimueleze" alimradi tu utishie wenzako...

Katika Jambo ambalo tunatakiwa kujifunza ni Namna ya kuishi na viongozi....la sivyo Tutabaki kuwasikia Redioni na kuwatizama kwenye TV..
.
 
Sikumbuki mwaka ila nakumbuka nilikuwa mdogo ,tulitoka na mzee wangu mitaa ya kariakoo tukaelekea mitaa ya Magomeni Mapipa mtaa sikumbuki ila ni karibu na Shibam.

Kufika pale kulikuwa na vijana watoto wamjini hakuna aliyezidi miaka 50,walikuwawakicheza draft,bao,zumna na kunywa kahawa

Vijana wa makamo wawili walikuwa wakicheza draft mmoja akamfunga mwenzake,akamtania kuwa hajui kitu bora acheze na mimi,hapo nikaachiwa nicheze na yule mwingine,yule mwenzake akaenda kusikiliza ushabuki wa mpira,walikuwa wamemzunguka mtu mmoja mnene mfupi ba sauti ya kukwaruza.

Miaka michache baadae nikagundua kumbe yule mtu niliyecheza nae draft ni Mh Waziri wa fedha Jakaya Mrisho Kikwete.

Na yule mtu mfupi mwenye sautiya kukwaruza alikuwa Jamhuri Kihwelu Tantalila,mchezaji wa zamani wa Simba.

Nilikuja tena kuonana na Mh Kikwete akiwa kwenye foleni ya ATM,CRDB Bank Holland House,Ohio Street,kipindi hicho akiwa waziri wa mambo ya nje miaka zaidi ya kumi tangu tukio la Magomeni.

Baada ya hapo niliishia kimuona kwenye luninga na magazetini

Kama mtakumbuka kipindi akiwa Rais alikuwa akitokea mara kadhaa kwenye media akishiriki mazishi ya watu ambao hata hawajulikani nchini,watu hao ni marafiki zake wa hali ya chini kabisa wakiwemo wa magomeni na Saigon Club na Hugo House Kinondoni alikokuwa akienda kunywa Supu

Kuna Mheshimiwa mmoja ajifanya kuigiza kuwa ni mtu wa matabaka yote ila technolojia ikamuumbua,muuza kahawa ni afisa wa TISS,mwingine akamuuzia muhindi wa kuchoma na bastola kiunoni kumbe ni maigizo tu .uungwana hauji kwa maigizo bali huzaliwa nao.

Kwa viongozi wa sasa sidhani kama kuna wazori wa fedha anayeweza kukaa kijiweni jioni,au waziri wa mambo ya nje anayeweza kukaa kwenye foleni ya ATM

Viongozi mmekuwa miungu watu mpaka mnatwambia tukimbilie Burundi.

Jifunzeni kujishusha kama Mh.Jakaya Kikwete nanyi mtakwezwa
Kikwete drafti analijua?
Natamani nicheze naye nimpige supa
 
Back
Top Bottom