Nilibahatika sikupitia njia hii ila najua ni njia inayowaumiza sana watoto kisaikolojia na kuwaacha na chuki kwa wazazi

Na kama amekutusi mbele ya watoto? Hii inakuaje mkuu. Ukizingatia unafundisha watoto kutotumia lugha ya matusi
 
Ila wazazi tujitahidi sana kulea watoto maana hata wanaume wengi wanaopiga wake zao ukichunguza utagundua ni athari zilizotokana na malezi. Child abuse ni mbaya sana.
 
kabla sijaoa niliwaona wanaume wote waliooa ambao wanawapiga wake zao hawana akili na wala hawana upendo kwa wake zao, nilipoingia kwenye ndoa nikagundua walikuwa na akili na mapenzi ya dhati, ila za kuambiwa changanya na zakwako
Mkuu...lakini hoja ni kupiga mbele ya watoto..Haijazungumzia maswala ya kutopiga kabisaa..Yaani unampiga mkeo huku watoto wanashuhudia..
 
Na kama amekutusi mbele ya watoto? Hii inakuaje mkuu. Ukizingatia unafundisha watoto kutotumia lugha ya matusi
Huwezi kuzuia kosa kwa kufanya kosa jingine mkuu. Mwanamke kukutukana tu ni kosa achilia mbali kukutukana mbele ya watoto, lakin njia ya kumzuia asikutukane tena sio kumpiga mbele za watoto ukifanya hivyo utakua unatengeneza mfumo wa jino kwa jino kati yenu. Kama umeona kuwa hana busara basi wewe tumia busara.
 
Mkuu pole kwa unachopitia. Mara Fulani wanaume pia wanafanyiwa vitu vibaya na wanawake kiasi Cha kuchukia rohoni. Inawezekana kabisa mama yako alifanya usaliti uliomfanya baba yako awe na wasiwasi na uhalali wa kizazi chake. Hapo ndio shida inapoanza kwa mwanaume. Mtoto anakuwa muhanga wa kukosa kupata upendo na malezi kutokana na huo wasi wasi na hasa anapokosa kufanana na baba.
 
Ndio maana tunatumia fake ID mkuu..halafu huu so umbea, ni mijadala ya kujifunza...Karibu na endelea kufurahia umbea mkuu.
Sasa wewe unadhani ni jina au ID inayo-matter hapa au content ya kuwa unatoa siri za watu. Unajuaje kama jamaa yupo humu unadhani atakuchukulia wewe ni rafiki wa namna gani?

Mtu hamjaonana miaka leo mnaonana anakupa siri za familia yake unazimwaga mitandaoni. Hivi unadhani humu hakuna tuliosoma nao au waliokuwa wanaishi nao mtaa au jamii moja. Unadhani watu hawawezi kuonganisha dots kwa namna moja au nyingine. unadhani hiyo siri ya kutomjali mzee wake unajua wewe tu?

Haya umeyatapika kuwa mama yake alikuwa anadundwa. Unadhani jamaa anakuchukulia vipi?
kifupi wewe ni rafiki mpuuzi
 
Samahani mkuu ila mara nyingine mama zetu huwa wanakua na siri sana na nyingine huwa zinabomoa familia. Hizi mambo mtu unaoa halafu unasikia kwa watu kuwa mtoto wenu wa pili sio wako huwa zinachanganya kweli kweli. Hivi umewahi kujiuliza kwa nini baba alikutenga? Au kuna vitu ulifanya haujatueleza humu mkuu?
 
Ningependa nifunguke ya kwangu na mzee wangu lakn nafsi inasita Sana

Niseme tu tujutahid kuwashurikisha watoto wetu kwa kila Jambo unaloona liatawajenga kwa baade

Watoto hukua kulingana na wanachoona nyumbani hasa matendo ya wazazi na wakigundua Kuna Jambo unalificha wakikua utapata tabu Sana hata Kama utakuwa na kipato cha kueleweka uzeeni lakn ile faraja ya watoto utahiitaji tuu

Mm nimepitia hayo mazingira na nilipogundua mzee anamapungufu nishamshauri lakn DHARAU niliyooneshewa na mzee wangu ndio hii inanifanya niwe WABARIDII JUU YAKE

Leo anakumbuka lakn ameshachelewa kwa kweli nilifedheheshwa mbele ya familia na kila mwanafamilia alinidharau lakn leo hii kila mtu ukwel ameujua bahat mbaya na mm Nina mji wangu pia naangalia ya kwangu imewachukua miaka 15 kuujua ukweli

Wazazi tuwashirikishe watoto wetu na si marafiki ndio wawe wapanga mipango yenu ilihali watoto wengine washafka 20yrs unawaona wadogo
 
Mimi mzee wangu namuombea amekosea vitu kibao maishani mwake sasa asikosee kwenye kustaafu. Ukinipanga mimi na pombe hapa ukamwambia mzee achague bila unafiki atachagua pombe, na wala hajawahi lewa. Ni kwa sababu gharama zake kwangu hazijawahi zidi 500k kwa thamani ya TZS ya sasa. Pombe na starehe binafsi kwa mwezi ni kama najua hapungui 300k. Kwanza kwake nishapasahau
 
Nakubali kabisa kuna makosa akina mama hufanya ambayo hupelekea utengano au kupandikiza chuki toka kwa baba kwenda kwa mama na mama kumlisha sumu mtoto baba.

Kama nilivyosema mama japo alinieleza mabaya ya mzee ila hakuniambia mambo mengi kiviile ila nilipoenda kwake kwa muda mfupi niliona namna alivyokuwa akini-treat.

So hakuna kosa ambalo mimi nililifanya kustahili hiyo adhabu.
 
Nimekupa like mkuu
 
Uko sahihi kabisa mkuu, cha kufanya ni hivii..kama kweli baba una mapenzi na watoto wako utavumilia kila aina ya kioja ili tu watoto wapate kukua katika malezi ya pande zote mbili,. Ni hivyo tuu vinginevyo tutakuwa tunatengeneza jamii iliyojaa chuki.
 

SIMULIZI ZA NAMNA HII ZIKO NYINGI SANA:

NYAKATI ZETU HIZI NI VIZURI KUFIKIRI VIZURI, KUFIKIRIA PANDE ZOTE MBILI NA SIO KUTEGEMEA SIMULIZI TU:
1. HAO WANAWAKE WA MIAKA HIYO AU YA SASA,WAO SIO WATAKATIFU KWENYE NDOA.
2. MWANAUME KUPIGA MKE NI MATOKEO YA MWANAUME KUPIGWA HISIA ZAKE
3. HASIRA NI MATOKEO (REACTION); SIO DHAMIRA/NIA. kiasi eti uchague sehemu ya kwenda kupigia mkeo?. Ni kama chafya!!
4. HIVI KWANINI YEYE MWANAMKE ANAJENGA MAZINGIRA YA KUPIGWA MBELE ZA WATOTO?
5. JE UNAJUA UMUHIMU WA UWEPO WA BABA KWENYE FAMILIA? KWA NINI TUNAMWANGALIA KWENYE MABAYA YAKE TU?
 
Ndio maana mimi huwa nasema hivi, wanawake wanaovumilia mateso kwenye ndoa ukimuuliza kwanini huoendoki anakwambia eti kisa watoto, huwa hawajitambui, kuvumilia mateso huku watoto wanaona ni kuwatesa kisaikolojia, na watoto wengine waliokuwa kwenye mazingira hayo huwa either wanakuwa na tabia za ajabu au kama ni wakike basi anakuwa na chuki na wanaume au anaishia na yeye kuolewa na mwanaume design ya baba ake na kuishia kuteswa kama mama ake
 
Nimekuwa nikishuhudia mama anadundwa vilivyo na mshua kiukweli ilikuwa inaniuma sana pia, hata mimi nilimchukia sana mzee sema ndo nilikuwa namtegemea kwa kila kitu

Shule anilipie ada yeye, Mavazi yeye Chakula kiufilupi kila kitu yaani, hata mama mwenyewe pia alikuwa ni mama wa nyumbani tu, kuna siku mzee alimchalaza mama tena mbele ya washikaji kabisa wamekuja home kunitembelea iliniuma sana, ikawa wimbo school watu wote wakaelewa nilimchukia sana mzee japo sikuacha kumuomba mahitaji

Siku zote mama alikuwa anadundwa bila sisi (watoto) kuijua sababu ya ugomvi wao, na wakati huo watoto wote tulijikuta upendo upo kwa mama, alikuwa akudundwa tunamfariji sana, ilitokea siku moja nimeenda home kusalimia nikakuta ugomvi pia

Nimeshakuwa sasa simtegemei tena mshua, nikaona isiwe tabu ngoja leo niwakalishe wazee, nikamshika mzee nikamuomba akae tuongee nikamuita mama pia niliongea nao kama vile mimi ndo mzazi vile kiukweli nashukuru hawakuniona nimewakosea heshima baada ya mazungumzo nikaelewa mpaka leo sina kinyongo tena na mshua aiseee kwanza ana roho ngumu sana,

Ipo hivi kulikuwa kesi kama tatu hivii, kwanza mama kaenda kuvuna mazao shamba kauzia huko huko gunia nne za mpunga bila mzee kujua, pale home kuna dogo wa kike yupo kidato cha nne ni mwanakwaya sana (mtu wa dini) sasa mzee hakutaka aimbe alimruhu kusali ila sio kuimba kwaya maana alikuwa anapoteza sana mda badala ya huo mda kuutumia kusoma mama alipoona dogo anazuiwa kuimba wakashauriana na dogo, dogo akahamia kwa mchungaji wao tena bila hata mshua kujua

Mpaka mda huu mzee ndo anahudumia kila kitu home, ila mama kachukua madogo wawili wa kanisani kawaleta home wanaishi tu na mzee hakujulishwa pia

Aiseee washa mshua atie adabu watu wake, yaani mama anamzingua mzee anamnyima nyapu harafu mzee akitumia madaraka yake nijifanye kumchukia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…