Nilichekwa sana Style yangu ya malezi ila leo hii watu wanatamani kuniiga

Nilichekwa sana Style yangu ya malezi ila leo hii watu wanatamani kuniiga

INaonyesha unakaa eneo la low class kwa Walala hoi ila wewe una kanafuu kidogo ni kama wewe ni katajiri fulani katikati ya maskini kwa ulivyojieleza lakini ungekuwa unakaa high class areas hicho ulichoandika chote ni hopeless mfano hakuna mtoto high class anatembea dakika 25 kwenda shule
Mkuu hivi high class ya watu wengine inaweza kukufanya na wewe uwe tajili?
 
Mkuu hivi high class ya watu wengine inaweza kukufanya na wewe uwe tajili?
Ukiishi eneo la high class ambao kila mtoto anapelekwa shule na school bus au na gari ya wazazi wa kwako ukimtembeza kwa miguu kwenda shule atajiskia kunyanyasika na kuona mzazi hampendi wala kumjali atajisikia vibaya mno lakini kama yako uswahilini low class ambao asilimia kubwa wanaenda kwa mguu shule ataona sawa tu
 
Ukiishi eneo la high class ambao kila mtoto anapelekwa shule na school bus au na gari ya wazazi wa kwako ukimtembeza kwa muhimu kwenda shule atajiskia kunyanyasika na kuona mzazi hampendi wala kumjali atajisikia vibaya mno lakini kama yako uswahilini low class ambao asilimia kubwa wanaenda kwa mguu shule ataona sawa tu
Hayo ni mawazo yako mzazi; mtoto anahitaji kueleweshwa akielewa hawezi kuwa hivyo!
Ujue shida kubwa ya wazazi huwa hatujibu majibu ya watoto kwa ufasaha! Hivyo watoto wengi hubaki na majibu yao kichwani yasiyo chakatuliwa
 
Nimesoma kwa umakini huu uzi, hongera mkuu, ila hapo bado hujamaliza kila age inachangamoto zake kwa malez ya watoto. Usijipe bigup sanaaa. Ila bravo.
 
Kijijini huko anaenda maana mkoa ninao fanya kazi ndio bibi yake alipo na ni umbali wa kama dakika 45 tu, nilikuwa nampeleka nikienda kwa bibi ila cha kushangaza watu hawakosi cha kusema.

Wengi nilikuwa nawasgangaa wanasema ni mambo yaliyopitwa na wakati mi nikawa nacheka tu kwamba eti atafundishwa vitu vibaya na watoto wa kijijini, atarogwa, atazama mtoni, atapigwa jiwe anapowinda, n.k. Yes ni hatari zinazoweza kutokea lakini thia is life, haya ndio maisha ya mwafrika.

Kwa ufupi kuna kioindi flani nlikuwa naenda sana huko kwenye vikao flani vya huko nikifika namwacha kwa bibi,

nachokumbuka kwa sana wenzake wa kule huwa wanajipikiaga chakula kwa hio nae ndo akajifunzaga huko kujisongea ugali,

Tuliozaliwa kijijini na Kisha kuja mjini ukubwani aloo tunayajua maisha kinoma.

Utotoni Kwanza full kucheza porini michezo ya kujificha, kombolela, rede, kuruka kamba, kuwinda ndege, kuwinda nyani, kuchoma misitu Moto (utukutu), kutafuta uyoga, kugema ulimbo wankutegea ndege, kutega kware na tetere kwa mitego.

Kuchonga PIA, kuchonga ngorogojo (sijui Ni kkswahili sahihi??) Kuchonga magari ya udongo na magunzi.

Kuchunga mbuzi porini masafa ya mbaaaaali huko milimani na mabondeni mnakutana kundi kubwa na wachungaji mnafurahi pamoja. Kuogelea mtoni na mabwawani, kuvua samaki kwa ndoano mtoni.

Kwenda kuvua samaki kwa nyavu mnakaa porini huko wiki nzima. Kufanya vibarua vya kulima maporini hukoo mnakuwa mnalala huko kama wiki nzima. Kuwinda nyani, sungura, swala n.k kwa mbwa!!


Daaah let me go to the village next year!!!!!!
 
Umefanya sahihi kasoro kumruhusu aende nyumba za watu..
Anaweza kuwa abused huko sexually usijue..
Na mtoto mwenzie au watoto wakubwa wanaokuja nyumba hiyo hata houseboy au housegirl..

Siku hizi kuna shule za serikali English medium...naona kama Better kuliko private English medium

Tuko pamoja
 
Tuliozaliwa kijijini na Kisha kuja mjini ukubwani aloo tunayajua maisha kinoma.

Utotoni Kwanza full kucheza porini michezo ya kujificha, kombolela, rede, kuruka kamba, kuwinda ndege, kuwinda nyani, kuchoma misitu Moto (utukutu), kutafuta uyoga, kugema ulimbo wankutegea ndege, kutega kware na tetere kwa mitego.

Kuchonga PIA, kuchonga ngorogojo (sijui Ni kkswahili sahihi??) Kuchonga magari ya udongo na magunzi.

Kuchunga mbuzi porini masafa ya mbaaaaali huko milimani na mabondeni mnakutana kundi kubwa na wachungaji mnafurahi pamoja. Kuogelea mtoni na mabwawani, kuvua samaki kwa ndoano mtoni.

Kwenda kuvua samaki kwa nyavu mnakaa porini huko wiki nzima. Kufanya vibarua vya kulima maporini hukoo mnakuwa mnalala huko kama wiki nzima. Kuwinda nyani, sungura, swala n.k kwa mbwa!!


Daaah let me go to the village next year!!!!!!
Matunda pori Sasa daah,

makusu
matunda damu
zambarau
mashindwi,
 
Umefanya vema,umebakiza kimoja tu,
Mruhusu likizo akale matunda pori kijijini.
Kuna fulu,sada na majina mengine kutegemea na mkoa atakaoenda.
Mruhusu akawinde,ndege,senene,panya na vingine kutegemeana na mkoa,
Mruhusu akafundishwe kutega mitego ya kware,njiwa na ngedere na kutafuta uyoga, inategemea namkoa atakao enda.
Ukifanikiwa kumpeleka likizo zote
Huta kuwa na haja ya kumpeleka jkt kwa mujibu wa seria.
Sasa hivi fulu si ndo zinatoa maua eeh😀😀
 
Umefanya sahihi kasoro kumruhusu aende nyumba za watu.

Anaweza kuwa abused huko sexually usijue.

Na mtoto mwenzie au watoto wakubwa wanaokuja nyumba hiyo hata houseboy au housegirl.

Siku hizi kuna shule za serikali English medium. Naona kama Better kuliko private English medium.
Nafikiri hapo bora kumpa elimu
Kuwa akatae katu anything to do with kushikana mwili sehemu za siri ama kukaa sehemu asiyo na amani nayo.,na awe free kueleza yatakayomsibu mapema

mana ndo ashaanza kukua hivyo no turning back
 
Malezi si kitu cha mchezo ukilala waweza kuza toto zembe zembe. Likizo peleka bushi akafundishwe kutengeneza na manati kuvua samaki etc.
 
Umefanya sahihi kasoro kumruhusu aende nyumba za watu.

Anaweza kuwa abused huko sexually usijue.

Na mtoto mwenzie au watoto wakubwa wanaokuja nyumba hiyo hata houseboy au housegirl.

Siku hizi kuna shule za serikali English medium. Naona kama Better kuliko private English medium.
Naomba kuzijua hizo shule za serikali ambazo ni English medium. Mimi niko Arusha.
 
Safi kabisa, sisi kuna ps 4 hapa home.mdg wetu kamaliza diploma ya ualimu ila jamani akijifungia humo chumbani anaweza akaanza game saa 12 asbh anatoka jion yaan hata kula hali.hana socialize tionkabisaaaa
 
Umefanya vema, umebakiza kimoja tu

Mruhusu likizo akale matunda pori kijijini.

Kuna fulu,sada na majina mengine kutegemea na mkoa atakaoenda.

Mruhusu akawinde,ndege,senene,panya na vingine kutegemeana na mkoa.

Mruhusu akafundishwe kutega mitego ya kware,njiwa na ngedere na kutafuta uyoga, inategemea namkoa atakao enda.

Ukifanikiwa kumpeleka likizo zote

Huta kuwa na haja ya kumpeleka jkt kwa mujibu wa seria.
aisee mafulusad saf sana.sis na mengine yanaitws sasati chachu flan hiv.na mengine yanaitws matogo au matogho mlenda mlenda hiv likichanganya tam balaa na kuchezea minyaaa na mazambarau kula sana panda sana miti hio.watoto wa siku hiz kwa kwel lazima aende mkoa akale
 
Back
Top Bottom