Nilichojifunza kwenye Uchaguzi wa South Africa

Nilichojifunza kwenye Uchaguzi wa South Africa

econonist

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
20,189
Reaction score
29,663
Nilichojifunza kuhusu Africa Kusini kwenye uchaguzi wao , ni yafuatayo:

1. Kwenye uchaguzi wao wameaangalia sera zaidi, sio vyama vya siasa au utumbuizaji wa wasanii kwenye majukwaa ya kampeni. Kwa mfano chama Cha Julius Malema kimeshindwa kuungwa mkono kwa pale alipoleta sera ya kufungua mipaka (Open Border Policy) wasouth wakaachana naye. Sasa hivi chama chake kimeporomoka mpaka nafasi ya nne kwa kujikusanyia asilimia 9 ya kura.

2. Uchaguzi upo wazi. Waandishi wa habari wanaruhusiwa kuhudhuria tukio la kuhesabu kura. Hili limetia moyo Sana. Hata kituo Chao kikuu Cha kujumuisha kura Kiko friendly hakuna mapolisi Wala Usalama kuzuia watu. Matokeo yote yatapatikana kwenye dashboard na kila wakala mkuu wa chama anakuwa na eneo lake la kupokea matokeo kutoka kwa mawakala wake na anaweza kuthibitisha ukweli wake kwa kuangalia matokeo kwenye dashboard.

3. Utendaji wa serikali ndio utategemea mafanikio ya uchaguzi unaofuata. Chama tawala kinapofanya madudu ndio jinsi kinavyojipunguzia uwezekano wa kuendelea kukaa madarakani. Kwenye huu muhula ulioisha ANC imefanya vibaya sana kiutawala, Ajira imekuwa changamoto, umeme, maji na pia Hali ya kiuchumi sio nzuri. Hivyo waafrica Kusini wameamua kupima utendaji wa ANC kwa kura walizoipa.

4. Wasouth wameanza kujifikiria kukipa nafasi chama cha DA ambacho kina chimbuko la wazunguWasouth wanadhani DA inaweza kuirudisha Afrika Kusini kwenye mstari. Maana weusi wenzao akina Zuma ni rushwa tu na Gupta's wake, huku Ramaphosa akifukia mabilioni ya Fedha kwenye mashimo nyumbani kwake mpaka kupeleka wafanyakazi wake wa nyumbani kuanza kufukua na kudokoa hizo pesa.

5. Pia nimejifunza ya kwamba kuwa chama Cha ukombozi sio ticket ya kufanya ufisadi na ujinga mwingine.
ANC walitumia kadi ya kuwa chama Cha ukombozi kufanya madudu na kutojihusisha na mambo ya wananchi, Leo hiyo kadi haifanyi kazi kabisa. Wapiga kura hawajali Nini Wala Nini.

6. Mwisho, uchaguzi wa South Africa umejikita kwenye uchumi zaidi. Ni chama gani kitatoa ahueni ya uchumi ndicho kinasikilizwa na sio vinginevyo.

Ni hayo tu kwa Sasa,

By the Econonist.
 
1. Kwenye uchaguzi wao wameaangalia sera zaidi, sio vyama vya siasa au utumbuizaji wa wasanii kwenye majukwaa ya kampeni. Kwa mfano chama Cha Julius Malema kimeshindwa kuungwa mkono kwa pale alipoleta sera ya kufungua mipaka (Open Border Policy) wasouth wakaachana naye. Sasa hivi chama chake kimeporomoka mpaka nafasi ya nne kwa kujikusanyia asilimia 9 ya kura.
Malema alikuwa anapinga Xenophobia ndio maana amekimbiwa na wapigakura wengi lakini kwangu namuona ndio amekomaa Kisiasa na ni PanAfricanist.

Kumbuka South Africa kuna wahamiaji wengi kutoka Ulaya Mashariki lakini Xenophobia inawaathiri zaidi wahamiaji kutoka Nchi za Kiafrika.
 
Nilichojifunza kuhusu Africa Kusini kwenye uchaguzi wao , ni yafuatayo:

1. Kwenye uchaguzi wao wameaangalia sera zaidi, sio vyama vya siasa au utumbuizaji wa wasanii kwenye majukwaa ya kampeni. Kwa mfano chama Cha Julius Malema kimeshindwa kuungwa mkono kwa pale alipoleta sera ya kufungua

By the Econonist.
Boss ahsante kwa uchambuzi wako murua kabisaa.Heko kwako!!🙏🏿
Paragraph yako hii imenifanya mimi ambae sikufuatilia kabisa kinachoendelea South Africa kupata habari nzima ya uchaguzi huo.Ahsante sana
 
Vyama Vya Tanzania havinaga Sera ndio sababu 2020 Shujaa Magufuli alijipangia safu yake ya Wabunge hadi wa Upinzani
Kama havina sera wananchi waachwe waamue wenyewe sio kuwaamulia wchague nani. Pia Kwa Tanzania hakuna voter confidence, Yani wapiga kura hawaamini Tume ya uchaguzi, wanaona kura zao zitapotea.
 
Vyama Vya Tanzania havinaga Sera ndio sababu 2020 Shujaa Magufuli alijipangia safu yake ya Wabunge hadi wa Upinzani
Hakuna hiyo. Zaidi ya ANC na Da, hakuna chama kinacho we za kumlinganisha na CDM kwa mfano. Huku kwetu CCM wamemonopolize mno kila kitu wanacontrol wao. Tatizo ni kuwa ANC hawana uwezo wa kumanipulate uchaguzi kama CCM au ZANU PF.

Tatizo la ANC ni kuwa uchaguzi kule ni free and fair... Hivyo wameadhibiwa na hasira ya Wapiga kura. MK wamepata kura za kikabila kutokana na hasira zao kwa ANC kwa jinsi wanavyomtreat Zuma.

Vilevile matatizo ya ajira, maji na umeme yamewafanya watu wapoteze confidence na ANC. Hiyo ndiyo sababu ya kuanguka kwenye National votes.
 
Nilichojifunza kuhusu Africa Kusini kwenye uchaguzi wao , ni yafuatayo:

1. Kwenye uchaguzi wao wameaangalia sera zaidi, sio vyama vya siasa au utumbuizaji wa wasanii kwenye majukwaa ya kampeni. Kwa mfano chama Cha Julius Malema kimeshindwa kuungwa mkono kwa pale alipoleta sera ya kufungua mipaka (Open Border Policy) wasouth wakaachana naye. Sasa hivi chama chake kimeporomoka mpaka nafasi ya nne kwa kujikusanyia asilimia 9 ya kura.

2. Uchaguzi upo wazi. Waandishi wa habari wanaruhusiwa kuhudhuria tukio la kuhesabu kura. Hili limetia moyo Sana. Hata kituo Chao kikuu Cha kujumuisha kura Kiko friendly hakuna mapolisi Wala Usalama kuzuia watu. Matokeo yote yatapatikana kwenye dashboard na kila wakala mkuu wa chama anakuwa na eneo lake la kupokea matokeo kutoka kwa mawakala wake na anaweza kuthibitisha ukweli wake kwa kuangalia matokeo kwenye dashboard.

3. Utendaji wa serikali ndio utategemea mafanikio ya uchaguzi unaofuata. Chama tawala kinapofanya madudu ndio jinsi kinavyojipunguzia uwezekano wa kuendelea kukaa madarakani. Kwenye huu muhula ulioisha ANC imefanya vibaya sana kiutawala, Ajira imekuwa changamoto, umeme, maji na pia Hali ya kiuchumi sio nzuri. Hivyo waafrica Kusini wameamua kupima utendaji wa ANC kwa kura walizoipa.

4. Wasouth wameanza kujifikiria kukipa nafasi chama cha DA ambacho kina chimbuko la wazunguWasouth wanadhani DA inaweza kuirudisha Afrika Kusini kwenye mstari. Maana weusi wenzao akina Zuma ni rushwa tu na Gupta's wake, huku Ramaphosa akifukia mabilioni ya Fedha kwenye mashimo nyumbani kwake mpaka kupeleka wafanyakazi wake wa nyumbani kuanza kufukua na kudokoa hizo pesa.

5. Pia nimejifunza ya kwamba kuwa chama Cha ukombozi sio ticket ya kufanya ufisadi na ujinga mwingine.
ANC walitumia kadi ya kuwa chama Cha ukombozi kufanya madudu na kutojihusisha na mambo ya wananchi, Leo hiyo kadi haifanyi kazi kabisa. Wapiga kura hawajali Nini Wala Nini.

6. Mwisho, uchaguzi wa South Africa umejikita kwenye uchumi zaidi. Ni chama gani kitatoa ahueni ya uchumi ndicho kinasikilizwa na sio vinginevyo.

Ni hayo tu kwa Sasa ,

By the Econonist.
Kwenye point yako ya kwanza naomba nikupinge. Kwazulu Natal hawajachagua chama Cha Zuma Kwa sababu ya sera. Zuma alikua Raisi wa nchi Kwa miaka karibia kumi. What can he do different that now as an old man of 82 years old that he couldn't do when he was in power?
They voted along tribal line.
As for ANC they need to purge itself from corruption within it's ranks. The crime level, inequality is quite high. For people who are in the rulling party it is easy to get money and lucrative government tenders. Also the electricity problem is bringing the economy to it's knee. They need to at least eat their ego and form a coalition with DA party. They have shown how to rule by the way they have run Western Cape and Cape Town itself. Professionalism and not the badge that his or her mother fought the Apartheid should be the qualification. Also the youth should be taught how to work in order to get a good life. Nothing came easy, hardworking and determination is the key.
 
Hakuna hiyo. Zaidi ya ANC na Da, hakuna chama kinacho we za kumlinganisha na CDM kwa mfano. Huku kwetu CCM wamemonopolize mno kila kitu wanacontrol wao. Tatizo ni kuwa ANC hawana uwezo wa kumanipulate uchaguzi kama CCM au ZANU PF.

Tatizo la ANC ni kuwa uchaguzi kule ni free and fair... Hivyo wameadhibiwa na hasira ya Wapiga kura. MK wamepata kura za kikabila kutokana na hasira zao kwa ANC kwa jinsi wanavyomtreat Zuma.

Vilevile matatizo ya ajira, maji na umeme yamewafanya watu wapoteze confidence na ANC. Hiyo ndiyo sababu ya kuanguka kwenye National votes.
Kweli kabisa.
 
Sera za kutaifisha Migodi hazina tija na haziwezi kutatua tatizo la Ajira watakaofaidika ni Makada na Wanasiasa kama walivyoiua Tanzania.
Nadhani hiyo sera ilitolewa kisiasa Zaidi. Kwa mfano kwenye manifesto ya MK wanadai watataifisha Ardhi bila fidia. Kwa Dunia ya Leo Hilo haiwezekani. Tena kwa South Africa
 
Pia nimejifunza ya kwamba kuwa chama Cha ukombozi sio ticket ya kufanya ufisadi na ujinga mwingine.
ANC walitumia kadi ya kuwa chama Cha ukombozi kufanya madudu na kutojihusisha na mambo ya wananchi, Leo hiyo kadi haifanyi kazi kabisa. Wapiga kura hawajali Nini Wala Nini.

6. Mwisho, uchaguzi wa South Africa uuchafuzi.mejikita kwenye uchumi zaidi. Ni chama gani kitatoa ahueni ya uchumi ndicho kinasikilizwa na sio vinginevyo
Kuna lichama Fulani hata haijali kuhusu kunyimwa kura maana haitegemei kura kubakia madarakani.
 
Back
Top Bottom