Nilichojifunza Uchaguzi wa Kenya: Tuwape nafasi Matajiri na Watafutaji

Nilichojifunza Uchaguzi wa Kenya: Tuwape nafasi Matajiri na Watafutaji

Siasa za Kenya sizitofautishi sana na siasa za Marekani! Wao wanaamini sana katika kumpa nafasi mtu anayeonesha ana uwezo wa kutafuta pesa na kupambana kupata pesa! Ndo mana inawezekana hata kiuchumi wako vizuri kuzidi sisi ingawa na sie tunajikongoja kuwafikia

Wakenya sio waumini sana wa ngonjera za sijui nichagueni mimi sio mwizi, mimi sio fisadi kwa sababu wanajua watu wanaopenda kujivika hizo sifa sio watu wenye akili za kimaendeleo na hawawezi kuhimiza vizuri maendeleo yao!

Kutoka kwa Jomo Kenyata mpaka kwa Daniel Arap Moi, kuja kwa Kibaki mpaka kwa Uhuru Kenyata na sasa naona Hustler William Ruto anaenda kubeba ndoo.

Wote ni watu wenye ukwasi ambao wako proud na ukwasi wao na wanatumia ukwasi wao kama njia ya ku motivate watu wengine kuwa na ukwasi.

Tanzania tujifunze hili kutoka Kenya mambo ya mtu kujisifia umaskini na kujiona ndo ticket k ya kuwa kiongozi tuachane nayo.

Kuanzia saivi tuanze kuangalia maisha ya mtu kama anajiweza kiuchumi vizuri, ana mali anazoziendesha vizuri, ana nyumba nzuri na ya kisasa na ana biashara nzuri ambayo ana imanage vizuri kama kigezo cha kumpa mtu uongozi.

Suala la kuteua sijui mtu hohehae asiye na mbele wala nyuma huku tukitegemea apandishe uchumi wetu liwe mwisho kuanzia leo.
Wale ni watafutaji? Watafutaji ni watu kama yule mmiliki wa The Royal Media Services, sio watu waliotumia nafasi zao kufanya ufisadi wa kutisha.
Huna pointi kabisa kama mifano yako ni wanasiasa wa Kenya.
 
Wale ni watafutaji? Watafutaji ni watu kama yule mmiliki wa The Royal Media Services, sio watu waliotumia nafasi zao kufanya ufisadi wa kutisha.
Huna pointi kabisa kama mifano yako ni wanasiasa wa Kenya.
Wewe una ushahidi wa ufisadi wao? Au akili za kimaskini zinakusumbua tu?
 
Wewe una ushahidi wa ufisadi wao? Au akili za kimaskini zinakusumbua tu?
Hivi kuna maskini anayemchukia tajiri? Hata hapa Tanzania, kuna mtu maskini anayemchukia tajiri? Wapiga kura wengi nchi hii ni watu wa hali gani?
Kuna tajiri anayependa kusimama kupigwa na jua ili ampigie mwanasiasa kura?
 
Msomi asiye na kitu akichaguliwa atakusaidia nini?

Mtu ambaye hana akili na utafutaji na maendeleo atakusaidia nini wewe? Ndo mana kila siku mnahangaika kutotendewa haki na tra na brela maana mtu anakuwa waziri wa fedha na hata hajawai kufanya biashara au hana hata biashara inayolipa kodi ili ajue kwa namna gani anatakiwa kuboresha mazingira ya wafanyabiashara
Ni afadhali Kiongozi maskini,msomi, mwenye AKILI ya uongozi kuliko Kiongozi TAJIRI Mwizi.

Sina tatizo na mtu kuwa TAJIRI, Bali Nina tatizo na TAJIRI alietajirika Kwa wizi.

Kama ni TAJIRI Kwa HAKI hamna shda. Bt ninyi waizi lazima TUWAFILISI kwanza, pesa ya Damu na laana haifai, pesa ya kuuza Ngada ndo aje awe kiongozi marufuku ktk Nchi yangu TANZANIA.

Ameeeen.
 
Wewe una ushahidi wa ufisadi wao? Au akili za kimaskini zinakusumbua tu?
Una matatizo ya akili? Wagombea wote wa Kenya walikua na kauli mbiu ya kupambana na ufisadi.

Kenya wao maadui zao
Umaskini
Maradhi na
Ufisadi
 
Una matatizo ya akili? Wagombea wote wa Kenya walikua na kauli mbiu ya kupambana na ufisadi.

Kenya wao maadui zao
Umaskini
Maradhi na
Ufisadi
Anayeongoza kwenye mchakato wa kura ametajwa kwenye kashfa ngapi za ufisadi? Kwa nini watu wamempa kura kwa wingi huu?
 
Huna pointbza kuwatetea ndio maana unaulizia ushahidi kama vile nimewashtaki Mlimani Law Courts.
Hao sio watafutaji. Kama sio mafisadi, ukatuonyeshe mabwawa yaliyochimbwa kwa Ksh. 21 B na team Ruto.

Wewe una ushahidi wa ufisadi wao? Au akili za kimaskini zinakusumbua tu?
 
Ni afadhali Kiongozi maskini mwenye AKILI ya uongozi kuliko Kiongozi TAJIRI Mwizi.

Sina tatizo na mtu kuwa TAJIRI, Bali Nina tatizo na TAJIRI alietajirika Kwa wizi.

Kama ni TAJIRI Kwa HAKI hamna shda. Bt ninyi waizi lazima TUWAFILISI kwanza, pesa ya Damu na laana haifai, pesa ya kuuza Ngada ndo aje awe kiongozi marufuku ktk Nchi yangu TANZANIA.

Ameeeen.
Maskini mwenye akili ndo yukoje?

Tajikistan mwizi kakuibia nini?
 
Anayeongoza kwenye mchakato wa kura ametajwa kwenye kashfa ngapi za ufisadi? Kwa nini watu wamempa kura kwa wingi huu?
Huenda hufatilii umerupuka tu. Vita kubwa hapo ni odinga anamtuhumu ruto kuwa ni fisadi na mwizi, Rito anamtuhumu Kenyatta na odinga kuwa ni wezi na mafisadi. Na ameapa aliwa raisi atawanyoosha.
 
Huna pointbza kuwatetea ndio maana unaulizia ushahidi kama vile nimewashtaki Mlimani Law Courts.
Hao sio watafutaji. Kama sio mafisadi, ukatuonyeshe mabwawa yaliyochimbwa kwa Ksh. 21 B na team Ruto.
Haijui Kenya na siasa zake. Huko rushwa na ufisadi ndio adui wa nchi Kama ilivyo huku kwetu kwenye umaskini, maradhi
 
Huenda hufatilii umerupuka tu. Vita kubwa hapo ni odinga anamtuhumu ruto kuwa ni fisadi na mwizi, Rito anamtuhumu Kenyatta na odinga kuwa ni wezi na mafisadi. Na ameapa aliwa raisi atawanyoosha.
Nimekuuliza Ruto anayetajwa kwa kashfa nyingi za ufisadi kwa nini anaongoza kwa kura?
 
Kuna tofauti kati ya kupambana ku-build wealth na kuiba, Matajiri wa Tanzania ni wezi, tajiri aliyepambana alikuwa Mengi tu, wengine wote wezi!
Wizi ni tafsiri uliyojiwekea kichwani kwako

Hao matajiri unaosema wezi wamekuibia nini?
 
Halafu inaonekana mleta mada hujui architecture ya siasa za Kenya. Siasa za Kenya ni za makundi sio za vyama vya siasa. Hakuna chama cha siasa cha kusema kimempitisha mgombea, ni mgombea na marafiki zake wanaanzisha chama, anajiita party leader then anakuwa mgombea moja kwa moja.
 
Maskini mwenye akili ndo yukoje?

Tajikistan mwizi kakuibia nini?
Tutaelewana tu.

Maskini mwenye akili ya uongozi ni yule alietoka ktk familia za kipato Cha chini aliyezaliwa na karama ya uongozi,

Wapo wengi wamemaliza vyuo hawana pesa mnazotaka wawahonge Ili wachaguliwe. Bt unakuta wanapendwa na wananchi.

Tanzania yetu MATAJIRI wengi ni WEZI, WAKWEPA Kodi, wauza Drugs, hao hawafai kutuongoza, hawana uchungu na Walio maskini.
 
Haijui Kenya na siasa zake. Huko rushwa na ufisadi ndio adui wa nchi Kama ilivyo huku kwetu kwenye umaskini, maradhi
Kati ya mimi na wewe nani anayejua siasa za Kenya?

Kati ya Ruto na Odinga nani mwenye kashfa nyingi za ufisadi jibu hilo na kwa nini Ruto anaongoza sasa?
 
Halafu inaonekana mleta mada hujui architecture ya siasa za Kenya. Siasa za Kenya ni za makundi sio za vyama vya siasa. Hakuna chama cha siasa cha kusema kimempitisha mgombea, ni mgombea na marafiki zake wanaanzisha chama, anajiita party leader then anakuwa mgombea moja kwa moja.
Hilo halihusiani na mada jikite kwenye mada
 
Bongo haina mwenye afadhali. Ukimuweka kapuku ndio wale akishashika madaraka akawa na mamlaka anafanya kujilimbikizia utajiri tu kwanza. Kazi inakuwa ndio hio maendeleo hakuna story na mambo ya kugandamizana tu kila siku.

Ukimpa madaraka tajiri ndio umemfungulia mlango wa kuendesha biashara zake bila kutoa kodi bandarini na kualika magenge ya wafanyabiashara wenzake. Kuanza kugawana rasilimali za nchi na kuuza wanyama yani nchi inageuza bidhaa.
Maendeleo yatakuja ila level ya ufisadi inakuwa deep sana.

Dawa ni kuwa na katiba strong na system nzuri ya check and balance. Mtu akizingua anakula shaba live kikatiba kabisa.
 
Tutaelewana tu.

Maskini mwenye akili ya uongozi ni yule alietoka ktk familia za kipato Cha chini aliyezaliwa na karama ya uongozi,

Wapo wengi wamemaliza vyuo hawana pesa mnazotaka wawahonge Ili wachaguliwe. Bt unakuta wanapendwa na wananchi.

Tanzania yetu MATAJIRI wengi ni WEZI, WAKWEPA Kodi, wauza Drugs, hao hawafai kutuongoza, hawana uchungu na Walio maskini.
Hilo la matajiri wa Tanzania ni wezi umelitoa wapi? lina uthibitisho gani?

Nani kakwambia kuzaliwa familia ya kimaskini ndo kuwa kiongozi bora? Kama huna akili ya kutafuta pesa na kuhangaika update pesa unawezaje kuweka na kusimamia sera ili nchi iwe tajiri?
 
Hilo halihusiani na mada jikite kwenye mada
Wewe utakuwa tu ni chawa wa watu wanaoimpress ufisadi hapa nchini.
Kuna mtu aliwahi kunyimwa kura humu nchini kwa sababu ya utajiri wake? (Tukirudi kwenye facts around this discussion).
Mo wa Simba alikuwa mbunge katika moja ya mikoa maskini kabisa nchi hii.
Turky alikuwa mbunge, Abood ni mbunge katikati ya maskini.
Wewe tupe ushahidi wa tajiri kunyimwa kura.
 
Back
Top Bottom