Nilichowafanya hawa mabinti wa IFM hawatanisahau

Huwa inauma sana kugharamia mtu halafu usipate kitu!
 
Sasa umeandika nini unaleta mambo ya kisingeli kama ujajipanga na starehe acha kwani lazima? kulikuwa na sababu gani kuwatoa IFM hadi huko barakuda? Kwanini asiende viwanja vya masaki, kinndoni, sinza, goba mpaka awapeleke kinyerezi huo unabaki niushamba labda na wewe unateteni jamii hiyo hiyo yakpumbfu!
 
Ndio maana nimeongelea tatizo la jamaa kuwanyamazia...alipoona wamekuja wengi alipaswa amwite pembeni wajadiliane na kubadili location waende sehemu rahisi ili kuweza kuwa handle wote kuliko kuwakimbia.

Pili jamaa alijipanga kwa starehe ya wawili na sio kijiji
 
Eeeh bhana eeh!! Hii inanikumbusha mbali sana aisee, kuna manzi mmoja nilikuwa namfukuzia Muda Mwingi sana lakini sikuweza bahatika kukutana nae yaani outing kwan alikuwa anakataa kutoka!!

Mwamba sikukata tamaa niliendelea kumsumbua sana aisee, ikafika mwisho akakubali kutoka na Mimi hapo sina shida na Pesa kwani teyar Mwamba Mfuko unasoma na Boom la kutosha aisee kipindi icho tunatolea Pesa Pale Azikiwe Branch Posta!!

Muda ukafika kama saa Moja hiv jioni nikaita Uber nikamwambia aje karibia na Freemason area!! Eeh bhana eeh kuangalia yuko na Mtu 3 na yeye wa nne hiv!! Then kucheki nawaona wale wadada wa Kujirusha sana coz nawajua si unajua kichuochuo!!

Mwamba nikaona hii hali sio ya kawaida wakafika pale tukaingia kwa Uber sasa Akili ikanicheza sasa hapa tunaelekea wap kwa Hiki kikundi lakini mala ya kwanza Dereva nilimwambia anipeleke masaki coz mtoto ni mmoja najua !!

Mara paap masaki hiyo tukaenda sehem moja hilikuwa imechangamka sana na watoto wa kishua balaa tukafika pale!! Kila mtu anaagiza anajo Jua yaaani hapo akili haisomi kabisa najikuta kila kitu naitikia Yeah kwelii!!

Baada ya Muda nikamtumia message Yule manzi kwamba naomba nikatoe ela kwenye ATM si unajua sikujua kama unakuja na Ndugu zako!!

Faster mwamba nikatoka weeeeh! Nikaenda kwa Ndugu yangu Gongo la mboto na Simu nikazima!! Aisee siku nakutananae alinitukana sana
 
Kwenye hii sekta,nakuvukia kofia mkuu.

Hunaga ushauri mbovu. Mkuu wewe una asili ya Tanga nini Mana unaonyesha Ni mtaalamu Sana wa mapenzi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…