Nilidhani ukiingia mbuga ya wanyama Unaona wanyama kirahisi kumbe napo tabu tupu

Mikumi miaka hiyo palipendeza Ila ni miaka ya 1990s. Wanyama wa aina zote kuanzia Simba, nyati, Tembo, Twiga, swala, pundamilia, nyani n.k. wakionekana ukiwa barabarani tuu. Ila sasa sionagi kitu

Sent using Jamii Forums mobile app
ujangili ulikithiri mkuu, kuna habari niliisoma eti 60% ya tembo wetu walipotezwa kwa kipindi kifupi sana chini ya miaka 10
 
ujangili ulikithiri mkuu, kuna habari niliisoma eti 60% ya tembo wetu walipotezwa kwa kipindi kifupi sana chini ya miaka 10
Ni kweli. Zamani ukipata haina haja ya kwenda Serengeti . Wanyama aina zote walikuwa wanaonekana
 
Mkuu Ngorongoro mbona ndio centa yenyewe ya chui. Kuna Chui milia, Chui madoa, na wale duma aise ni wengi huu ndio msimu wao ..njoo chap hata kesho utawakuta ..simba ndio usiseme wamezaliana kinoma, kuna hadi simba milia (tiger) wameanza kuletwa ili kuzoea mazingira ya Africa. Njo Serengeti ndio utashaaa ..hao swala wa kila aina, nyati sasa ndio balaa ..hao Punda milia ndio usiseme ..nyumbu ndio kwao kabisa kuna ndege wa kila aina Mkuu nashangaa wewe unasema ujawaona ..embu kunjua roho towa pesa uone wanyama ..ushawai kumuona live Chui Duma akimchomoa Swala ..hahha najua ujawahi kuona ..au kundi la simba likipambana na boonge la nyati ..nyati aliyoshiba haswa ..basi njo Tarangire aise utayenjoy sana.
 
Miaka ya 1998 nikiepo pale Tanzania advantist primary school - Arusha tulipelekwa Tarangire . Pale Tarangire nilifanikiwa kuona Tembo, Simba, twiga nk. Kwa kweli kama bado Tarangire ipo bado vile nikuhakikishie Ile itakuepo ndio mbuga nzuri Tanzania kuona wanyama kirahisi. Mikumi pale zamani ilikuepo ni rahisi kuobserve hao wanyama but not these days . Unaweza kupita mbuga nzima usiambulie kitu
 
Oooohhh
 
Ulitaka upige nao selfie
 
Mimi baada ya kutembelea mbuga kadhaa hapa, nime conclude siende tena mbungan. Nikitaka kuona wanyama na mishe zao vzur nachek national geographic(wild),hapo napata maelezo ya kunitosha
 
Ulitumia njia gani? ukitaka kuona wanyama mbugani lazima ujipange vilivyo kwa kutoa pesa nyingi tofauti na vile tunatangaziwa kwenye vyombo vya habari, tatizo ni serikali kuwaachia watu binafsi kuongoza watalii, miaka ya nyuma watumishi wa hifadhi ndio ilikuwa kazi yao kuu sasawamebaki kufanya kazi za ulinzi wa wanyama na kuchukua tozo tu hayo mengine hayawahusu. Unapoenda hifadhini utakuta karibu hifadhi nyingi zina nyumba za kufikia wageni ambazo hutoza kati ya TZS 20,000 hadi 25,000 tatizo linakuja kupata mtu wa kukupeleka kwenda kuwaona wanyama ambao wanaweza kuonekana kwa wingi mbali na hizo nyumba za kufikia wageni, mara nyingi wanyama huwa kwa wingi mbali kama vile km 50 na kuendelea kwenye mapori kwa hiyo hapo inabidi mukodi waongoza watalii binafsi ambao wana magari yao na hutoza kati ya TZS 400,000 kwa siku ,ili kupunguza gharama inabidi muwe angalau watu 4. Kwa wale wenye pesa huenda kwenye makampuni ambayo yamejenga makambi yao ndani ya mbunga sehemu ambazo wanyama hupita na sehemu hizo ziko ndani zaidi ukiwa kwenye hizo kambi huweza kuwaona wanyama kwa karibu zaidi ukiwa kwenye kambi hizo lakini tatizo ni kuwa unapolipia malazi pekee jua mambo ya usafiri hadi huko ndani ni juu yako na hapo ndio shughuli ipo. Kwa kifupi kwenda kuona wanyama wakubwa 5 ni kazi kubwa na inahitaji mkwanja mrefu, pia kuna wakati mnaweza zurura mbugani mkaishia kuwaona tembo, nyati lakini kwa farusi rahisi sababu wanalindwa na wapo wachache sana tena wa kuwa hesabu, twiga utawaona kwa wingi lakini hawa wa jamii ya paka kama vile simba,chui hawa inakuwa ni wa kubahatisha ila msimu wa mvua nyingi ni rahisi kuwaona sehemu za miinuko kwa kuwa hawapendi kukaa majini kwa muda mrefu kwani kucha zao huoza wakikaa kwa muda mrefu kwenye maji.
 
Saf
 
Mbona wamasai wanaishi nao na niwazima!
Wamasai ni specie tofauti na wamezoeana na simba n.k, we ulishasikia hata Simba amemla mtoto wa kimasai?

Hata kula tu ng'ombe wa mmasai ni ngumu...ila ni mara kadhaa simba wanaua na kudhuru binadamu wengine

Kuna dawa wanapaka wamasai Hata wakipita jirani na simba kwa mita 3 wanakuwa kero kwa simba na wanyama wengine

Kingine wamasai wamekuwa wakiua simba mara kadha wa kadha bila risasi na simba wanajua hilo
 
Hiyo dawa kama ipo basi inafaa wamasai wauze getini ili watalii tupake tunapoingia hii ni fursa kwa wamasai
 
Tena huko Crater ni rahisi zaidi kuwaona wanyama kwa kuwa wako ndani ya eneo ambalo hawaham
Although ana bahati hata kuwaona hao, maana amekwenda kipindi bado wanyama walio zubaa hawajaondoka kupanda juu kutafuta malisho.
 
Kwenye video ndio wanaonekana kirahisi mkuu,huko msituni ni kuviziana maana wanajificha kila mnyama anaogopa mbabe wake na wengine wanajificha Ili wawinde.
 
Zoo ya Tabora enzi zile(miaka ya sabini) kulikua na Sokwe Mtu akiitwa Sada. Kulikua na Simba ambaye akiunguruma kishindo cha sauti yake kilienea mji mzima
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…