Nilidhani ukiingia mbuga ya wanyama Unaona wanyama kirahisi kumbe napo tabu tupu

Nilidhani ukiingia mbuga ya wanyama Unaona wanyama kirahisi kumbe napo tabu tupu

Hivi majuzi nilibahatika kufika Ngorongoro National Park eneo la Crater; nikitarajia kuona wanyama wakubwa kwa ufasaha kama inavyosimuliwa kwenye movie mbalimbali za wanyama.

Niseme kwa dhati kabisa baada ya kuzungushwa mda mrefu niliambulia kuona nyati, kiboko, digidigi, punda na ndege flamingo. Lakini Tembo nilioneshwa miguu tu walipokanyaga sikuwaona, simba nao nilioneshwa kwa mbaali sana tena wawili tu wadogo kama mbwa, nikaoneshwa kichaka cha Faru wanamopenda kukaa lakini sikuona!

Kiufupi roho yangu haikuridhika kabisa bora ningeangalia movie tu!

Matarajio yangu nilizani nitaona Faru, chui, twiga, Tembo na wanyama wengine kirahisi kumbe sio kazi rahisi kama nilivyotarajia.

Nifanyeje Next time ili niwaone wanyama kiufasaha kama tusimiliwavyo?
Halafu acha kupotosha watoto na watu wa aina yao. Ngorongoro SIYO National Park. Usiniulize ni nini, fukunyua uelewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu,utalii uko hivi! Kwanza uwe na muda wa kutosha,pili pochi angalau iwe nene kiasi,mambo ni hivi,unamwambia guide unapenda kuona mnyama yupi,yeye anajua muda na mahali sahihi wanapopatikana(japo wakati mwingine wanaweza wasiwepo)ila bado guide ana second option! Muda ni jambo muhimu sana kwa utalii! Mfano mimi napenda kuingia hifadhini mapema sana kabla ya magari mengine hayajaingia,advantage yake ni kuwa tutaanza kuwaona wanyama adimu kuanzia karibu tu kabla hata hatujaingia huko ndani ndani maana kabla magari hayajaanza kuvuruga pori wanyama wengi huwa wanapenda kuja barabarani au karibu na barabara,sasa ikiwa umeingia hifadhini saa sita na ukatembezwa mbio kama Mwenge hutaona raha ya utalii,na pia kama mlienda na magari kama ya shule au wafanyakazi(in large group)na kibali chenu kinaisha saa kumi na mbili,ukute na guide anayewaongoza ameshawasoma na kujua hii kazi nnayoifanya haina Tip lazima awakimbize kama Mwenge ili akatege mingo za maana!!! Mzungu aje kutoka ulaya kuja kumuona Twiga live halafu arudi kwao hajamwona? Jipange mkuu! Ikiwa hujashinda Bingo haina maana kuwa Bingo hainaga mshindi! Hukucheza vya kutosha!!
Mkuu umeeleweka kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
nilikaaa Arusha miaka mi3 na nikafanya safari za Ngorongoro crater 4! SIMBA niliwaona mara moja tu wakiwa kikundi Ktk safari moja tu! Chui sikuwaona hata safari moja! Niliwaona na wamasai wengi
 
nilikaaa Arusha miaka mi3 na nikafanya safari za Ngorongoro crater 4! SIMBA niliwaona mara moja tu wakiwa kikundi Ktk safari moja tu! Chui sikuwaona hata safari moja! Niliwaona na wamasai wengi
ndo vile
 
Hivi majuzi nilibahatika kufika Ngorongoro National Park eneo la Crater; nikitarajia kuona wanyama wakubwa kwa ufasaha kama inavyosimuliwa kwenye movie mbalimbali za wanyama.

Niseme kwa dhati kabisa baada ya kuzungushwa mda mrefu niliambulia kuona nyati, kiboko, digidigi, punda na ndege flamingo. Lakini Tembo nilioneshwa miguu tu walipokanyaga sikuwaona, simba nao nilioneshwa kwa mbaali sana tena wawili tu wadogo kama mbwa, nikaoneshwa kichaka cha Faru wanamopenda kukaa lakini sikuona!

Kiufupi roho yangu haikuridhika kabisa bora ningeangalia movie tu!

Matarajio yangu nilizani nitaona Faru, chui, twiga, Tembo na wanyama wengine kirahisi kumbe sio kazi rahisi kama nilivyotarajia.

Nifanyeje Next time ili niwaone wanyama kiufasaha kama tusimiliwavyo?
Nenda serengeti national park utaona kila kitu hata ukitaka kushika sharubu za simba utazishika tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi majuzi nilibahatika kufika Ngorongoro National Park eneo la Crater; nikitarajia kuona wanyama wakubwa kwa ufasaha kama inavyosimuliwa kwenye movie mbalimbali za wanyama.

Niseme kwa dhati kabisa baada ya kuzungushwa mda mrefu niliambulia kuona nyati, kiboko, digidigi, punda na ndege flamingo. Lakini Tembo nilioneshwa miguu tu walipokanyaga sikuwaona, simba nao nilioneshwa kwa mbaali sana tena wawili tu wadogo kama mbwa, nikaoneshwa kichaka cha Faru wanamopenda kukaa lakini sikuona!

Kiufupi roho yangu haikuridhika kabisa bora ningeangalia movie tu!

Matarajio yangu nilizani nitaona Faru, chui, twiga, Tembo na wanyama wengine kirahisi kumbe sio kazi rahisi kama nilivyotarajia.

Nifanyeje Next time ili niwaone wanyama kiufasaha kama tusimiliwavyo?
mbuga ambayo unaweza kuwaona wanyama live hadi ukawashika na kuongea nao ni la chaz sinza, the great park tbt, maeneo mbali mbali ya buguruni, magomeni na sinza yete...ushuhuda hata jana nilipita kwenye kati mbuga moja niliyotjaja hapo na wanyama wako wengi kweli kweli....
 
mbuga ambayo unaweza kuwaona wanyama live hadi ukawashika na kuongea nao ni la chaz sinza, the great park tbt, maeneo mbali mbali ya buguruni, magomeni na sinza yete...ushuhuda hata jana nilipita kwenye kati mbuga moja niliyotjaja hapo na wanyama wako wengi kweli kweli....
wakuchora au?
 
Mnawaua kwa ujangili mnategemea nini? Kinachofuata sasa ni kufunga safari hadi ulaya kwenda kuwaangalia kwenye zoo za wazungu.
 
Kabisa Bro, mwaka jana mwezi wa saba nilikwenda serengeti pia. Alinifariji Twiga tu akivuka barabara mbele yetu ule mwendo wake sita sahau, anavutia sana. Nilitegemea kuwaona simba na tembo kwa wingi nasikitika haikua bahati yangu.

Nilijiuliza inakuaje kwa Wageni kutoka mataifa ya mbali wanapotembelea mbuga zetu na wasione walichotarajia, huwa wanajiskiaje?!
Ulienda Serengeti kutalii hususani ama kupita tu barabarani ukiendelea na Safari zako? Haiwezekani uende Serengeti ukomee kuona twiga madaha pekee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pita barabara ya Morogoro to Iringa, pale Mikumi utajionea freely hususani kipindi hiki hadi simba utawaona pembezoni mwa barabara tu
yaaps , nakumbuka mwaka jana mwezi wa saba hivi wakat naenda ifakara nilipita pale mida ya saa moja kasoro tukawaona, watu wakasema n km bahati maana ni adimu sana kuwaona maeneo ya wazi mida km ile, sana sana usikuu,
 
Wazungu hua wakiingia huko hawakai siku moja .wanaweka camp kabisa la week hata sasa wew umepita siku moja uwaone wote hao kwan walikua na miadi na ww...afu usikute hata darubin hukua nayo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali sijui imeferi wapi kwa sasa zamani kwenye baadhi ya mikoa kulikuwa na zoo mfano mwanza ple pasiasi ulikuwa ukienda unaona wanyama takribani wote wakiwa wamefungiwa kwenye mabanda, pale Tabora kulikuwa na zoo napo ulikuwa hivyo hivyo siku za sikuu au week end wazazi walitembelea na familia zao kwenda jionea wanyama na ndege wa aina mbali mbali

Kuna kipindi nilienda dar zoo nikiwa na picha ile ile ya zile zoo nilizokuwa nikiziona udogoni mwangu ila nilipofika uko hakuna lolote niliona simba tu

Wito wangu wizara husika ebu fanyeni kitu watoto wapate kukifunza kwa kuona siyo lazima sote twende bugani ona mdau analalamika hapa kafika mbugani hakuna kitu

Tatizo waziri mwenye dhamana kageuka mwandishi wa story za Instagram sijui nje ya box baada kudeal na vitu vya msingi vilivyofanya tumjue yupo kutuadithia hadithia tu akitaka tuamini kakulia kwenye shida yeye ni mpambanaji tunasubilia ajichanganye tufukue makaburi
Sisi watetezi wa wanyama tunapinga enslqvement ya wanyama pori.
Huyo kuku tu ukimfanyia ndivyo sivyo tunaku mind pia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila hifadhi inasifa zake na wanyama ambao waweza kuwaona kirahisi hivyo ni vyema ukafanya tafiti kabla ya kuamua ni hifadhi gani unataka kwenda kutembelea.

Kwa mfano kama unataka kuona jua likizama na makundi makubwa ya nyumbu nenda Serengeti na kama unataka kuona Tembo kwa wingi na wakubwa zaidi basi usisite kwenda Tarangire.
Akitaka kuwaona simba kwa ukaribu zaidi aende Ruaha au akitaka kuona simba na kukaribia kuliwa apige misele kwa boda boda au piki poki ameneo ya rufiji hasa karibu ya selous

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kifupi kwenye TV unawaona vizuri kuliko mbugani,hata uende mara hamsini au mara mia haitatokea uone aina zote za wale wanyama "pendwa" kwa safari moja.
Trip nyingine hata ukiishia kuona punda tu usishangae.
Hivi majuzi nilibahatika kufika Ngorongoro National Park eneo la Crater; nikitarajia kuona wanyama wakubwa kwa ufasaha kama inavyosimuliwa kwenye movie mbalimbali za wanyama.

Niseme kwa dhati kabisa baada ya kuzungushwa mda mrefu niliambulia kuona nyati, kiboko, digidigi, punda na ndege flamingo. Lakini Tembo nilioneshwa miguu tu walipokanyaga sikuwaona, simba nao nilioneshwa kwa mbaali sana tena wawili tu wadogo kama mbwa, nikaoneshwa kichaka cha Faru wanamopenda kukaa lakini sikuona!

Kiufupi roho yangu haikuridhika kabisa bora ningeangalia movie tu!

Matarajio yangu nilizani nitaona Faru, chui, twiga, Tembo na wanyama wengine kirahisi kumbe sio kazi rahisi kama nilivyotarajia.

Nifanyeje Next time ili niwaone wanyama kiufasaha kama tusimiliwavyo?
 
Back
Top Bottom