Nilifadhaika sana kupata watoto wa kike tu

Nilifadhaika sana kupata watoto wa kike tu

Kwanini ufadhaike kwa kuwa na watoto wa kike? Kumbuka bila mama yako labda usingekuwepo duniani na bila mkeo usingeitwa Baba. Tuache tabia ya kudharau watoto wa kike nao wana mchango wao mkubwa na wa maana sana katika jamii zetu.
Hali hii hutokea katika ndoa nyingi. Mke anazaa watoto wa jinsia moja tu mfululizo, ama wa kike au wa kiume tu. Wazazi wengi huwa wanapenda wapate watoto wa jinsia zote. Kwa sababu hiyo inapotokea wanapata watoto wa kiume tu au wa kike tu huanza kutafuta njia ya kutatua 'tatizo' hilo. Wengine huenda kwa madaktari kutafuta ushauri wa kisayansi na kufanikiwa kupata mtoto wanayemtaka; lakini wengine ushauri wa kisayansi bado hauwasaidii kupata mtoto wa kiume au wa kike.

Wazazi wanapofikia hali hiyo wengine huenda kwa waganga wa kienyeji na huko huishia kuchanganyikiwa tu kutokana na masharti magumu wanayoambiwa na mganga. Jaribu kuwaza mtu anaambiwa apeleke kwa mganga kinyesi "fresh" cha tembo ndio apate dawa!

Nakumbuka mme fulani alisababisha mgogoro katika ndoa yake baada ya kumgombeza mke wake kwanini anazaa watoto wa kike tu. Na waume wengine huamua kuwaacha wake zao au kuoa mke wa pili ili wajaribu kama watapata watoto wanaowataka kwa njia hiyo. Njia zote hizo zinaposhindikana hubaki na huzuni isiyokoma.

Mimi pia nimepitia hali hiyo. Mara ya kwanza mke wangu alipata mtoto wa kike. Mara ya pili akajifungua tena mtoto wa kike. Tulikuwa tunajitahidi angalau tupate mtoto kila baada ya miaka miwili. Mara ya tatu mke wangu akazaa tena mtoto wa kike. Hee nikaanza kufadhaika, maana nilitamani na mimi niwe na mtoto wa kiume. Sikumlaumu wala kumgombeza mke wangu kwanini anazaa watoto wa kike tu kwa sababu najua kisayansi mwanaume ndiye anayehusika zaidi kufanya mtoto wa jinsia ipi azaliwe.

Katika kutafakari nifanyeje nikakumbuka yale maneno ya Mungu yasemayo "Ombeni nanyi mtapewa" Nikakumbuka pia habari za mama mmoja katika Biblia aliyekuwa hapati kabisa watoto lakini baada ya kumwomba Mungu akapata.

Kwa sababu hiyo na mimi nikaanza kumwomba Mungu kwa juhudi kwamba mke wangu atakapojifungua mtoto wa nne, awe wa kiume. Ndugu zangu, Mungu hana upendeleo, alisikia maombi yangu na kutupatia mtoto wa kiume. Kinachotakiwa tu ni kuhakikisha mahusiano yetu na Mungu ni mazuri na kuomba kwa imani, pasipo shaka. Yote yawezekana kwake aaminiye(Mk 9:23).
 
Umemaliza..my lil bro ana 30 bt anafuliwa nguo bado na maza😱! Akichelewa kwenye mipombe yake wazaz wake hawakai..unawakuta wamesimama getini wanaangalia kila mtu nawaambiaga mna kazi..na yy anajua hawa wananipenda bas anakanyagia hapo hapo
Hongera kwa nyumbani kwenu kuwa na geti,swahiba wangu Shadeeya na wewe kwenu kuna geti?
 
Kwanini ufadhaike kwa kuwa na watoto wa kike? Kumbuka bila mama yako labda usingekuwepo duniani na bila mkeo usingeitwa Baba. Tuache tabia ya kudharau watoto wa kike nao wana mchango wao mkubwa na wa maana sana katika jamii zetu.
Mkuu umemaliza kila kitu,mtoto ni mtoto tu
 
Nadhani kikubwa kinachozingatiwa kwa wazazi wa kiume sio uwezo wa specific gender.
Bali ni transference of identity
 
Hali hii hutokea katika ndoa nyingi. Mke anazaa watoto wa jinsia moja tu mfululizo, ama wa kike au wa kiume tu. Wazazi wengi huwa wanapenda wapate watoto wa jinsia zote. Kwa sababu hiyo inapotokea wanapata watoto wa kiume tu au wa kike tu huanza kutafuta njia ya kutatua 'tatizo' hilo. Wengine huenda kwa madaktari kutafuta ushauri wa kisayansi na kufanikiwa kupata mtoto wanayemtaka; lakini wengine ushauri wa kisayansi bado hauwasaidii kupata mtoto wa kiume au wa kike.

Wazazi wanapofikia hali hiyo wengine huenda kwa waganga wa kienyeji na huko huishia kuchanganyikiwa tu kutokana na masharti magumu wanayoambiwa na mganga. Jaribu kuwaza mtu anaambiwa apeleke kwa mganga kinyesi "fresh" cha tembo ndio apate dawa!

Nakumbuka mme fulani alisababisha mgogoro katika ndoa yake baada ya kumgombeza mke wake kwanini anazaa watoto wa kike tu. Na waume wengine huamua kuwaacha wake zao au kuoa mke wa pili ili wajaribu kama watapata watoto wanaowataka kwa njia hiyo. Njia zote hizo zinaposhindikana hubaki na huzuni isiyokoma.

Mimi pia nimepitia hali hiyo. Mara ya kwanza mke wangu alipata mtoto wa kike. Mara ya pili akajifungua tena mtoto wa kike. Tulikuwa tunajitahidi angalau tupate mtoto kila baada ya miaka miwili. Mara ya tatu mke wangu akazaa tena mtoto wa kike. Hee nikaanza kufadhaika, maana nilitamani na mimi niwe na mtoto wa kiume. Sikumlaumu wala kumgombeza mke wangu kwanini anazaa watoto wa kike tu kwa sababu najua kisayansi mwanaume ndiye anayehusika zaidi kufanya mtoto wa jinsia ipi azaliwe.

Katika kutafakari nifanyeje nikakumbuka yale maneno ya Mungu yasemayo "Ombeni nanyi mtapewa" Nikakumbuka pia habari za mama mmoja katika Biblia aliyekuwa hapati kabisa watoto lakini baada ya kumwomba Mungu akapata.

Kwa sababu hiyo na mimi nikaanza kumwomba Mungu kwa juhudi kwamba mke wangu atakapojifungua mtoto wa nne, awe wa kiume. Ndugu zangu, Mungu hana upendeleo, alisikia maombi yangu na kutupatia mtoto wa kiume. Kinachotakiwa tu ni kuhakikisha mahusiano yetu na Mungu ni mazuri na kuomba kwa imani, pasipo shaka. Yote yawezekana kwake aaminiye(Mk 9:23).
Usikute huyo wa kiume sio wako ni kazi ya dereva bodaboda
 
Back
Top Bottom