Nilikuwa mfuasi wa Trump Kwa Muda Mrefu sana Ila Kwa Hili la Kusitisha Misaada na Ruzuku upande wa Afya Sikubaliani nalo, amekosea sana

Kiongozi naona unaongelea issue tofauti. Takwimu zako niza mchango katika UN na tunachoongelea hapq ni Trump ku free mchango wa Marekani katika kutoa foreign aid ambapo Us inatoa takribani usd.68bilion a year, EU usd.38billion na China 4.5billion.
Ukiwa na mahaba na nchi za Magharibi hauwezi kuijua wala kuiona misaada ya China.

Ukizungumzia upande wa capital China inatoa msaada mkubwa kuliko US na EU zikijumuishwa pamoja.

Nikupe tu mfano wa mradi wa China wa BRI angalia hizo takwimu ikifananishwa na Marekani








Imefikia hatua Marekani mpaka imeanza kufunga baadhi ya programu zake za kutoa misaada kwa sababu ya tatizo la fund
 
Kumbe ndio maana Trump amekuwa na kasi ya kupunguza misaada
 
Shida iko kwako zaidi kuliko kwa Trump. Alizunguka USA kote kuomba kura ili aweze kutekeleza, na wamarekani wengi wakampa na sasa anatekeleza sera zake, wote mliomuunga mkono mnapaswa kumpigia makofi Trump kwa kutekeleza ilani.

Next time mtajifunza kuacha kushabikia vitu ovyo ovyo.
 
Point hii dah kweli kuna vichwa vimewekwa bench wakati kuna masifuri wameshika Nchi
 
Trump kaanza kuwanyoosha wagonjwa wa Ukimwi wenye TB na wajawazito ila hapa kwa wajawazito kasingiziwa
 
Madawa mtapewa,ila fedha za kununulia madawa hapana.
 

Hakuna njia rahisi kwenye maisha, hasa yahusuyo taifa bila KUJITAMBUA.

Tutambue tunahitaji kula kwa urefu wa kamba yetu pia kama Taifa/nchi. Kujibebisha kwa Wamarekani hakutupi haki ya msingi ya wananchi wetu kuhudumiwa na wao/Wamarekani.

Tujiulize:

Tanzania si mtoto wala mjukuu wa Marekani. Tulipata uhuru kama nchi, inabidi tujisimamie na tuwasimamie wananchi kama nchi huru ili tuwe na nafasi ya Uhuru huo, Haki na Wajibu kama nchi.

Hii itatupa nafasi ya kusimama na kusema hili sawa au hili hapana tunapoletewa na hao wadau wa maendeleo. Wakati Mmarekani akituhudumia kwa mtindo husika, je tumeweza kujikwamua kwa kiasi gani? Je ndo uhalisia?

1: Tumewekeza kiasi gani kama Taifa kwenye elimu, afya, sayansi na teknolojia wakati pesa ya Wamarekani imechukua jukumu hilo.

2: Tumewekeza kiasi gani kwenye upatikanaji wa chakula kwa jamii yetu?

3: Tumewekeza kiasi gani kwenye tafiti ili kuweza kukuza uwezo wetu wa kuzalisha mahitaji ya taifa na watu wake dawa?

4: Ni kiasi gani cha pesa tunazopata ndani kinaenda kutatua matatizo ya msingi ya wananchi?

5: Ni kiasi gani cha pesa tunachozalisha kinatumika kufanya uzalishaji zaidi, multiple effect?

6: Ni kiasi gani cha pesa zetu kimepelekwa kutatua upunguzaji wa magonjwa yasiyo ya kuambukiza na ya kuambukiza, matatizo ya lishe miongoni mwa jamii?

7: Au ni pesa kiasi gani inatumika kwa majukumu ya msingi dhidi ya yale ya ANASA, huku wananchi wanalelewa na JIRANI?
Akili ziturudie, tuwe na matumizi kadri tunavyopata. Nguo ya kuazima haiwezi kukuaitili.

8: Turudi kwenye MOTHER BOARD, tuchole NEW ROAD MAP, viongozi warudishwe kwenye DEFAULT SETTING. Tuulizane maswali magumu ili tuweze kutatua matatizo yetu na kutoka hapa na kila mmoja afurahie kuzaliwa au kuishi kwenye nchi yetu iliyojaliwa maliasaili kibao.

Tusionene haya, mficha uchi kifo humuumbua, tunaenda kuumbuka kwa kuwa taifa la kusifu na kuabudu.
 
Wewe ni Daktari usiejitambua.

Why Trump akujali wewe kwa kodi za wananchi wake?

Punguza matumizi hutaki, kuzalisha huwezi unakodisha bandari na vyanzo vilii vya mapato.
Sasa unaweza nini?
 
Ninachofahamu baada ya miaka 60 ya uhuru:
1. Bado tuna maeneo( hata ndani ya miji mikubwa) hayajapata maji safi na salama.
2. Bado kuna maeneo hayana huduma za afya.
3. Wanafunzi wengi hasa wa shule za msingi wanakaa chini.
4. Bado kuna maeneo hayafikiki kipindi chote cha mwaka kwasababu ya miundo mbinu mibovu ya barabara. ( ongezea zingine)
 
Kuna sauti nasikia masikioni mwangu "Tanzania ni nchi huru isiingiliwe kwenye maamuzi yake. Hatufundishwi cha kufanya". Kumbe ni kauli tu hatujiwezi.
 
China ni nchi ya pili kwa uchumi mkubwa duniani, anamfuatia Mmarekani. Marekani ilikuwa inatoa usd.bilioni 65 kwa mwaka katika kutoa misaada ikifuatiwa na EU bilioni 38, tulitarajia China izibe gap la Mmarekani katika kipindi hiki
China wako busy na mambo yao
 

Tatizo letu ni ngumu kuelimisha mtu wa kawaida ambaye anaona serikali ina nunua magari ya milioni 400 kwa gari moja halafu kwa upande mwingine ni lalama hizi za ukosefu wa pesa. Kwanini wasingeomba misaada ya magari na kuweka hizo pesa kwenye miradi ya kuokoa maisha. Tatizo ni ubinafsi. Huwezi kumlaumu Trump na kusema serikali inafanya vizuri. Ungetakiwa kulaumu wote hapo kidogo tungekielewa. Sisi wenyewe tumejisahau
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…