Nilikuwa sijui: Asilimia zaidi ya 40 ya barabara za US ziko katika hali mbaya

Kilichoongelewa sio direct imelinganishwa ila usome uzi vizuri, haihitaji akili nyinyi kujua nini kinaongelewa.

Mleta mada anaongelea ubovu wa barabara za USA, sasa huwezi kumsema mtu wakati kwako hakuko sawa.
Nilikuwa sijui kama US superpower wa dunia kuna mabarabara mabovu zaidi ya 40% na tena kwa muda mrefu. Tena hadi wananchi wanalalamika mashimo yanawaletea ajali.

Ni hilo tu
 

Itakuwa California mashambani wanakolima maparachichi, karanga, machungwa n.k
 
Huko kwenu ni asilimia ngapi?
 
Mkuu sisi kinachotumaliza kiakili na kiubunifu ni CCM
 
Define "mbaya sana" kwa muktadha wa Marekani na "mbaya sana" unayoielewa wewe, kwa muktadha wa Tanzania.
 
Define "mbaya sana" kwa muktadha wa Marekani na "mbaya sana" unayoielewa wewe, kwa muktadha wa Tanzania.
Ni mbaya kiasi cha kulalamikiwa kusababisha ajali.

Hii ni sehemu ya nukuu kuhusu hali ya barabara Washington DC kwa Mujibu wa ASCE

American Society of Civil Engineering (ASCE) gave Washington D.C.’s roads a D+rating. The annual infrastructure report found that less than half of D.C.’s roads were in “good” condition, while 25% were in “poor” or “worse” condition. According to the report, D.C. is one of the most congested cities in the country, averaging 82 hours of delay per driver each year
 
Bado huja define mbaya ni nini kwa muktadha wao na wetu. Hata barabara nzuri ikiwa na dereva asiye makini ajali inaweza kutokea.

Mimi nimeendesha gari barabara za Tanzania na hizo barabara za Washington DC. Sizijui kwa kusoma mitandaoni, nimeendesha gari kote huko.

Hawa watu inawezekana wakawa na kishimo kimoja kwa kilomita tano wakaiita barabara mbaya.

Hawa hata kukiwa na foleni tu wanasema barabara mbaya, kwa maana ya kwamba planning ya barabara ni mbaya, barabara haitakiwi kuwa na foleni.

Halafu wewe ukisikia wanaiita barabara mbaya unafikiria ni sawa na barabara mbaya ya Bongo ambayo ina mashimo kama sehemu iliyopigwa mabomu huko vitani Vietnam.
 
Tanzania sio mbaya tu bali sehemu kubwa ambapo barabara zipotakiwa kuwepo hazipo kabisa.
Barabara nyingi haziko katika kiwango.

Nilikuwa sijui kama nchi makini kama US yenye kugawa pesa hovyo, mfano mfano tangu 1947 imeshaipa israel msaaada zaidi ya Trillioni 900 wakati wanabarabara zinazoua raia, mashimo mengi.

Bila muktadha kama unabarabara zinazoua raia kwa miuktadha pote ni tatizo bila kujali idadi.

Kama US wanamalalamiko ya barabara zinazoua Raia kwa sababu ya ubovu basi hazifai kama ambavyo zetu hazifai kwa kuua wengi zaidi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…