Nilikuwa sijui: Asilimia zaidi ya 40 ya barabara za US ziko katika hali mbaya

Kuna kipindi mzee wangu alikuja kwenye mkutano New York City.

Akaja kunitembelea kwangu, akawa anasema "Hawa Wamarekani wabishi, walalamishi sana. Yani wanaweza kutumia saa nzima kubishana comma ikae wapi kwenye sentensi".

Huwajui figisu zao hawa.

Yani mtu anaweza kuwa na barabara nzuri tu, akalalamika sana barabara zangu mbovu kabisa, kwa figisu za kisiasa tu apewe hela afanye mambo yake anayoyataka.

Wewe Mtanzania ukisoma mitandaoni kama hujafika Washington DC utajua dooh, barabara zao mbaya sana hawa.

US kuna corruption na matatizo mengi, barabara za DC zina matatizo yake, lakini muktadha ni muhimu.

Marekani hapo DC mtu akisema "barabara mbaya" anamaanisha kitu tofauti kabisa na kusema hivyo Tanzania.
 
Ni sahihi, labda kama ni siasa au ujanjaujanja, maana mimi nimeisoma hii habari kwenye social media ya US (reddit) nikashangaa sana.

Nchi nzima yenye Square kilometer karibu milioni 10 kuwa na 40% ya ubovu wa barabara nchi nzima sio kitu kidogo kulinganisha na kwetu square km laki 9. Hata mwandishi aliandika kwa lengo la kutushangaza sisi tunaoamini US kule kumenyooka.

Ila ubaya huo hatuwezi kuulinganisha na kwetu.

Nimekupata sana aisee
 
Marekani wana mambo ya ajabu sana.

Wanachukua matunda. Halafu wanachagua yale ambayo mazuri kabisa, yenye smooth surface, halafu wanayapiga brashi fulani hivi yang'ae.

Yani tunda si tu linatakiwa liwe zuri kwa kuwa na virutubisho, linatakiwa ling'ae pia.

Matunda ambayo hayana smooth surface, yana madoa doa kidogo kwa nje, yamebonyea bonyea kidogo kwa nje, wanayatupa, wanasema haya si mazuri.

Na hayo matunda yanayotupwa inawezekana asiruhusiwe mtu kuyala kwa sababu hayajafikisha viwango, yametupwa.

Halafu, hapo hapo, kuna watu wengine wanakosa matunda, wanaishi kwa kula junk food. Wanasumbuliwa na obesity.

Sasa, ukiisoma hii habari ya watu wanaokosa matunda na kuwa na obesity, unaweza kuishia kusema Marekani kuna ukosefu wa matunda.

Kumbe ni bad policies za ubepari tu na roho mbaya za watu zinasababisha hivyo.

Sasa kwenye barabara pia, wewe unaweza kuona wenzako wameiita barabara mbovu, ukafikiri ni mbovu ina mashimo, kumbe wenzako wameiita mbovu kwa sababu haijang'aa, imekosa guardrails, imekosa kuta za kuzuia sauti za magari zisifike kwenye nyumba za watu zilizo karibu na barabara hiyo, imekosa alama za barabarani zinazo reflect mwanga sehemu fulani.

Wamarekani wamezoea kuendesha gari unajisikia kama upo katika ndege, wakikutana na vi pothole vidogo tu ambavyo kibongo hata hatu vi notice, wao wanaita barabara mbaya. Yani barabara isipokuwa almost 100% smooth kwao ni mbaya.

Ndiyo maana mtu ambaye nishaendesha barabara mbaya za Tanzania nikisikia wanasema barabara za DC mbaya, naweza kuelewa, kwa muktadha, kwao ni mbaya kwa sababu wanalinganisha na nzuri zao.

Lakini ukizileta barabara zao kwetu, mbaya zao ndiyo nzuri zetu.
 
Hilo Taifa lina laana. Hata hiyo misaada yao siyo ya kuishobokea kabisa.

Wako radhi kutengeneza migogoro duniani, ili tu wauze silaha! Wako radhi wakupe mamilioni ya dola kama msaada ili nchi yako iruhusu ushoga na usagaji! Hovyo kabisa. Taifa la uovu hilo.
 
Niliwaelewa vizuri kwenye ishu ya Savimbi. Waliopamua vita iishe Angola waliimaliza
 
Ukitaka kujuwa uovu wao ingia mitandaoni, soma ya kina Nkrumah, Toure, ya Zaire, hata ya Afrika Kusini tu walivyong'ang'ania ubaguzi usiishe! Yako mengi, Vietnam, ya Wahindi Wekundu! Wazungu wa USA ni mashetani, waovu, makatili!
Kuhusu barabara, kweli labda zipo mbaya ila ukilinganisha na za kwetu basi umepotea! Zilizo mbaya kwao kwetu tambarare, walete Kimara, Mbezi beach ndanj ndani, Bunju ndanj ndani, Mabwe...
Hatuna barabara siye tuna vichochoro!
 
Sasa híi si uswahilini Yao Kabisa hii!? Angalia wembamba WA Barbara !?
 
Marekani ameacha jenga barabara miaka ya 80 kwa ufupi Marekani haijengi barabara tena
Hii mbona ni uongo mkuu.
Nimefuatilia hapa naona kuna project kubwa ya ujenzi wa barabara iliyoanza 2014 na inatarajiwa kuisha 2030. North Carolina huko. Ni project ya Dola bil 1.7
Multi Lane roads.
 
Taifa la kishenzi sana hilo ,drug addicts ,homeless everywhere,huduma za jamii hovyo , crumbling infrastructure na bado washenzi democrats wanatumia billions of dollars kusambaza vita ,
Serikali ya kishenzi
Bora Trump arudi whitehouse

Sent from my Nokia 6.2 using JamiiForums mobile app
 
Serikali ya Democrats ni corrupt Hamna mfano ,
Military industrial complex lobbyists ( wamiliki wa viwanda vya silaha na wapigania maslahi yao ) ndio wanufaikaji wa ushenzi wa kusambaza vita duniani maana wanahonga sana kwenye congress na senate kupata wabunge wa kupigania maslahi yao na kuyalinda (lobbying) , wanafyonza pesa toka federal government kama military contracts na hapo hapo wanapata punguzo la kodi , hiyo yote ni maumivu kwa mwananchi kuongezewa kodi + uchakavu wa miundombinu + ukosefu wa huduma za kijamii + kuongezeka kwa umasikini


Sent from my Nokia 6.2 using JamiiForums mobile app
 
Usisahau mtumba wake ambao wao wanaona haufai kabisa na reject huku ndio grade one super

Barabara yake anayoona mbovu hata haifai kuvushia mifugo wewe ndio inayoelekea Ikulu😂

Na yote kwa yote , lile ni bara aisee sishangai kwa asilimia hizo na kwa ukubwa wa Marekani ukioanisha na Bongo ni sawa na kuilinganisha tabora na mjini magharibi

Wenzetu wapo mbali sana, sema wao barabara ikiwa na kipengele kidogo tu inaonekana haifai ilhali kwetu ndio mkazuzu
 
Hapa umepiga ya utosi.
 
😁
 
Hivi ni sahihi kweli kuilinganisha Marekani na Tanzania? Kumbuka ukubwa wa Marekani ni kama nusu ya bara la Afrika.
 
Wako busy kujenga Meli kubwa za kivita za kubebea ndege za kivita na projects nyingine za kivita.
Hakuna nchi ya kihuni duniani kama Marekani amini hivyo.
Wana matatizo ya hapa na pale kama sisi tuu japo siyo kiwango chetu ila wanapenda sana vita hawa jamaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…