Nilisafiri kwa pikipiki Dar mpaka Tabora

Nilisafiri kwa pikipiki Dar mpaka Tabora

Uzuri mwingine wa boxer haina mitetemo so haichoshi kivile ukienda nayo umbali mrefu.
Next time usitembee usiku bora uweke malengo ya sehemu ya kulala, lala utapokua umefika at 6 PM.

Hongera sana mtoa mada.
Asante kwa ushauri ila mazingira yalinilazimisha lazima nitembee muda ule, ila mtu asikwambie boxer imetulia sana barabarani kuliko pikipiki nyingi halafu barabara ya vumbi mashine inachanja mbuga balaa nadhani kuna baadhi ya vijiji watakuwa walikuwa wanadhani labda imeibiwa sehemu.
 
Kila kitu kinawezekena sema sisi watanzania ni woga sana..
Mmi nimesafiri mara nne kwa pikipiki kutoka mbeya -bukoba via tabora na kwakuwa barabara ya sikonge ni mbovu majuzi nmenyookea singida-dom-iringa. chombo kikiwa ni pikipiki ya kichina aina ya SINORAY 150.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hongera sana mkuu hiyo safari ni klm ngapi makadirio?
 
Ata mm nmeona..yaani katumia saa Saba dar to Dom sawa na shabiby au kimbinyiko au ata private cars
Na sio hapo kumbuka hata ule muda ambao nilifika Tabora nilifika sawa na mabasi yanayotoka Dar lengo halikuwa kushindana na muda mwenyewe katika safari yangu nilikuwa na target zangu hasa kwenye mwendo na usalama wangu mwenyewe ukizingatia usafiri niliokuwa nautumia , halafu kuna hali ya bara bara dar to dom magari ni mengi barabarani kuliko ukitoka pale dom kuelekea singida kidogo kule gari zinapungua barabarani
 
Back
Top Bottom