Nilishangaa Waziri Mbarawa kutumia muda mwingi kuelezea mradi ambao watanzania hawautaki

Nilishangaa Waziri Mbarawa kutumia muda mwingi kuelezea mradi ambao watanzania hawautaki

Umetumwa na wamiliki wa Malori weye hivi mfano mizigo makontena 100 yavutwe na kichwa 1 Cha treni kutoka Dar Hadi labda Itigi Kisha Malori yapeleke huko wilayani huoni gharama kubwa inakuwa imeokolewa au Makonte yaende Hadi Mwanza hata mafuta yakisafurishwa Kwa Reli bei inapungua kuliko Kwa Njia ya barabara, duniani kote usafiri wa Reli ni WA nafuu zaidi
Sio kwa reli ya mjerumani
 
Sio kwa reli ya mjerumani
Fuatilia data utaona, na usiidharau Ile Reli bado inabeba mizigo hata Kwa miaka 100 ijayo tukiwa makini itaendelea kufanya kazi kama Ulaya bado steam engine zipo kwanini tudharau Reli ya Mjerumani?
 
SGR inapita katika mikoa 10. Kwa nini unaona haiwagusi watanzania wengi...!? Au bado unataka tubaki enzi za chukuchuku train......!!?
Mi nafikiri Katiba Mpya kama itakuja kiwepo kipengele cha kama mtu anaongea pumba, unaenda TRA unalipia kumchapa bakora moja, mbili hadi sita kwa mfano. Hoja za hovyo kama za mleta mada hii haziwezi kuonekana.
 
Uko sahihi kwa kiasi kikubwa sana
 
SGR itabeba mpka mchanga wa dhahabu... Bado pamba, Michele, kahawa, mawese, tumbaku, karanga, sunflower seeds etc.... Tuongeze tu uzalishaji. Reli Mwanza inasarve Kagera na Mara.... The biggest population ya nchi iko lake Victoria.
The biggest population ipo kweli kanda ya ziwa , ila the big producers wapo kusini , very far from Sgr, mbao bado itaenda mwanza kwa barabara na mahindi yatafika huko kwa barabara pia .
Halafu unapokuwa na project kubwa kama Sgr hutakiwi kufikiri vitu vidogo kama mafuta ya alizeti misigiri na kibaigwa ,
 
Fuatilia data utaona, na usiidharau Ile Reli bado inabeba mizigo hata Kwa miaka 100 ijayo tukiwa makini itaendelea kufanya kazi kama Ulaya bado steam engine zipo kwanini tudharau Reli ya Mjerumani?
Nilienda kuulizia nauli ya dar Morogoro ni kubwa kuliko nauli ya bus nilichoka
 
Na katika bajeti ya mwaka huu hakuna mradi mkubwa wa maji wala barabara moja ktk mikoa ya kusini [emoji26][emoji26]na PM yupo anajua anashindwa kubalance distribution ya national cake [emoji706][emoji706]
Hawa wanatuchukulia sisi wananchi km watu wajinga ila ipo siku tutawageukia ...Halafu kiongozi Anachukua Bilioni 70 na ushee anasimama jukwaani na Kusema Watu wa Arusha nimewapa Bilion 70 za maji...Arusha hawana shida na maji hata siku moja kuliko Lindi na Mtwara .....


Mimi siwezi kuipigia makofi SGR
WALA treni ya gesi ikiwa sipati maji Safi Wala barabara nzuri....
 
Mkuu, ukijadiliana na watu wanaotumia emotions utachoshwa! Kama mradi huu unakosa pesa zote ningepeleka SGR hadi Manyoni (kuondoa congestion Dodoma) na kisha nikatoa SGR Dodoma mpaka Tunduma. Kosa ninaloliona kwa SGR ni kuipeleka Mwanza badala ya kusini ambako kuna Malawi, Zambia na super-rich DRC. Otherwise SGR si upotevu wa pesa kama mradi unakamilika on time and budget!
Hakuna kosa lolote linalotakiwa tangu tumepata uhuru mikoa yote Tanganyika ingeunganishwa na SGR n mpaka sasa kuna haja ya kuunganisha mikoa yote kwa SGR huwezi kusafiri kwa bus kwa masaa 12. Ulaya safari zote ndefu unasafiri kwa treni sio bus. Wenye malori bahati mbaya viongozi wetu wengi wanafanya biashara hiyo ndio wanaua treni SGR na hata ile ya zamani chukuchuku
 
Umesahau kuwa kuna reli ya TAZARA ambayo ndio ilikuwa lengo lake hilo; kuhudumia mikoa Pwani, Morogoro, na ya kusini nyanda za juu pamoja na nchi jirani!! Sasa TAZARA na umuhimu wake wote tumeitekeleza badala ya kuiimalisha matokeo yake ndio hayo ya kuelekeza nguzu zote kwenye SGR mradi ifike MWANZA!!
Wabunge wa mikoa ya nyanda za juu kusini wanaomba kiwanja cha Ndege kipewe jina la TULIA badala ya kuomba na kuhimiza Serikali kuimalisha reli ya TAZARA!
Moja ya makosa ambayo Mimi Kama mwananchi ,,na siwezi kumsamehe mwalim Nyerere Ni pamoja na suala la kuondoa reli ya kusini ,,sijui alimshauri halafu ubaya Ni kwamba reli ilijengwa na wakoloni Sasa kwann mwalimu aitoe na alipeleka wap..nyanda za juu kusini pamoja na Lindi na Mtwara tumeonewa Sana....Kuna wilaya moja mkoani Mtwara likuwa na mashine kubwa ya Maji wakaja wanaCcm kuondoa kimagumashi inasemekana ipo Dodoma...Kusini tumedumazwa Sana....halafu nikimuona mtu anabana pua eti kusini nyie maskini nakereka Sana...


Rais Samia toka aingie Amekwenda Mwanza sio chini ya Mara tano.,Arusha sio chini ya Mara 4 Kilimanjaro sio chini ya Mara Tano...huku kusini hajawahi kanyaga hata Mara moja ...Nyie edeleeni kutupuuza watu was kusini tu
 
Mtoa mada anasikitisha Sana naona hajui faida ya Reli ukilinganisha na barabara, SoMo la form Two.
 
Jana wakati waziri wa ujenzi na uchukuzi anahitimisha hoja zake kimsing iangetueleza mpango wa kujenga barabara kuunganisha wilaya zetu na mikoa kuliko kuelezea mradi wa SGR. Huu mradi ni wazi watanzania wengi hawajaufurahia kwani hauwagusi watanzania wengi unapitia sehemu chache sana kulinganisha na ukubwa nchi yetu. Ushahidi ni kuwa ni km hakuna wabunge walioujadili, asilimia 96 walijadili barabara zilizo katika maeneo yao. Rais aliyejua mahitaji ya watanzania ni Jakaya Mrisho Kikwete. Mwaka 2010 alikuja na ajenda ya kuunganisha mikoa kupitia makao makuu ya mikoa. Vilevile aliunganisha nchi yetu na nchi za jirani kupitia mipaka yetu.

Kiukweli kwa mtazamo wangu matrilioni yaliyopelekwa kujenda SGR yangetumika kuunganisha wilaya zetu na kumalizia kuunganisha mikoa iliyobaki. Kwa mfano kwa mkoa wa Morogoro ijengwe barabara ya Ifakara-Kilombero-Mahenge-Malinyi-Mwaya na kuunganisha Morogoro - Songea na Njombe. Ijengwe Barabara ya Handeni-Kiteto-Kondoa. Same-Simanjiro-Arusha. Barabara ya Karatu-Mbulu-Haydom-Nduguti-Gumanga-Ibaga-Sibiti-Meatu-Lalago-Kolandoto na Lalago-Maswa. Barabara nyingine muhimu kama ya Karatu-Matala-Meatu. Barabara ya nafikiri Kilindi-Turiani-Dumila-Kilosa

Hii ni mifano michahe ninayoweza kuitoa. Hizi barabara zingegusa maisha ya watanzania moja kwa moja Tanzania yetu ingependeza sana. Matrilioni yanayotumika kujenga SGR yangeelekezwa ktk hizi na zingine zinazofanana na hizi.
Nikikuita NDEZI NI KOSA kisheri? Kisa mradi ulianzishwa na mtu msiyempenda basi mnachukia hata kama ni wa maslahi ya nchi. We tril.15 zinakuuma nini kwenye ujenzi wa miundombinu ya nchi wakati watu wanaiba mabilioni na trilion na hukemei hilo. Watanzania wasioutaka labda wewe na ukoo wako. Tuzo mnafurahia ila ujenzi mnauchukia eti uchumi wa vitu. Kama kwenu hakufikiki mtapanda treni na mikokoteni.
 
Ukweli usemwe hizi akili za kutaka kufanya Jambo kubwa wakati dogo bado Ni kipuuzi.......robo tatu ya barabara za Lindi na Mtwara zinazounganisha wilaya zake hazina lami...

Robo tatu au tuseme asilimia 98 ya wakazi wa Lindi na Mtwara hawana maji salama mpk leo wanamkamua chura mtoni ....hivi nyie vingozi mnajua kweli mahitaji was wananchi....

Halafu wewe unasimama kwa kubana pua eti mikoa nn....halafu kwny kampeni unakuja Tena kuomba kura .....



Halafu wewe utakuwa umekulia IKULU TU...
TARURA watashughulikia huko acha tudeal na maslahi mapana ya nchi. Yaani tusinunue meli ya mizigo kisa namtumbo hakuna baiskeli? 😁😁 tusiboreshe bandari ya kigoma kisa kivuko cha kigamboni hakiko sawa?
 
Sgr kupita kwenye mikoa mingi sio hoja , je hiyo mikoa iko kwenye production pipeline ya kulisha Sgr?
Dar mwannza sgr itarudi empty mana hakuna cha kubeba kuja Dar
Ulitaka ielekezwe wapi itakapoka na vitu? Kwa hyo malori yakitoka mwanza huwa yako empty? 😃😃 akili kisoda. Itabeba hata vyuma chakavu na mifugo 😐
 
Ulitaka ielekezwe wapi itakapoka na vitu? Kwa hyo malori yakitoka mwanza huwa yako empty? 😃😃 akili kisoda. Itabeba hata vyuma chakavu na mifugo 😐
Kusini pekee ndio ina flow ya vitu to and from!
Mwanza huduma anabeba cement wazo kwemda mwanza wakati wa kurudi huwa anabeba hari gari juu ya gari,yani maana yake hakuna return cargo halafu unajenga sgr ukitegemea itarudi na mizigo.
The elites are full of doubts while the fools are full of hope , Rwanda analeta gari empty dar es salaam all the way from kigali halafu unajenga sgr kwenda huko ukitegemea faida itapatikana vipi?
 
Ukichelewa kupata hela,utakutana na wajinga wengi sana!!
 
Jana wakati waziri wa ujenzi na uchukuzi anahitimisha hoja zake kimsing iangetueleza mpango wa kujenga barabara kuunganisha wilaya zetu na mikoa kuliko kuelezea mradi wa SGR. Huu mradi ni wazi watanzania wengi hawajaufurahia kwani hauwagusi watanzania wengi unapitia sehemu chache sana kulinganisha na ukubwa nchi yetu. Ushahidi ni kuwa ni km hakuna wabunge walioujadili, asilimia 96 walijadili barabara zilizo katika maeneo yao. Rais aliyejua mahitaji ya watanzania ni Jakaya Mrisho Kikwete. Mwaka 2010 alikuja na ajenda ya kuunganisha mikoa kupitia makao makuu ya mikoa. Vilevile aliunganisha nchi yetu na nchi za jirani kupitia mipaka yetu.

Kiukweli kwa mtazamo wangu matrilioni yaliyopelekwa kujenda SGR yangetumika kuunganisha wilaya zetu na kumalizia kuunganisha mikoa iliyobaki. Kwa mfano kwa mkoa wa Morogoro ijengwe barabara ya Ifakara-Kilombero-Mahenge-Malinyi-Mwaya na kuunganisha Morogoro - Songea na Njombe. Ijengwe Barabara ya Handeni-Kiteto-Kondoa. Same-Simanjiro-Arusha. Barabara ya Karatu-Mbulu-Haydom-Nduguti-Gumanga-Ibaga-Sibiti-Meatu-Lalago-Kolandoto na Lalago-Maswa. Barabara nyingine muhimu kama ya Karatu-Matala-Meatu. Barabara ya nafikiri Kilindi-Turiani-Dumila-Kilosa

Hii ni mifano michahe ninayoweza kuitoa. Hizi barabara zingegusa maisha ya watanzania moja kwa moja Tanzania yetu ingependeza sana. Matrilioni yanayotumika kujenga SGR yangeelekezwa ktk hizi na zingine zinazofanana na hizi.
Nilikuwa na mawazo hayo hayo.
Magufuli alitutoa nje ya reli kwa ubinafsi wa kufikiria miradi ya kuunganisha kwao tu.
 
Kusini pekee ndio ina flow ya vitu to and from!
Mwanza huduma anabeba cement wazo kwemda mwanza wakati wa kurudi huwa anabeba hari gari juu ya gari,yani maana yake hakuna return cargo halafu unajenga sgr ukitegemea itarudi na mizigo.
The elites are full of doubts while the fools are full of hope , Rwanda analeta gari empty dar es salaam all the way from kigali halafu unajenga sgr kwenda huko ukitegemea faida itapatikana vipi?
Kusini itabeba vitu gani? Mazao ama? Kumbe kilichokuuma ni kutofika kusini ila siyo kwamba huitaki, haya iliyokuwepo ilibeba vitu gani kutoka mwanza to dar? Hv hiyo sgr ni ya mizigo tu ama ipo na ya abiria?
 
Ukweli usemwe hizi akili za kutaka kufanya Jambo kubwa wakati dogo bado Ni kipuuzi.......robo tatu ya barabara za Lindi na Mtwara zinazounganisha wilaya zake hazina lami...

Robo tatu au tuseme asilimia 98 ya wakazi wa Lindi na Mtwara hawana maji salama mpk leo wanamkamua chura mtoni ....hivi nyie vingozi mnajua kweli mahitaji was wananchi....

Halafu wewe unasimama kwa kubana pua eti mikoa nn....halafu kwny kampeni unakuja Tena kuomba kura .....



Halafu wewe utakuwa umekulia IKULU TU...
Ambavyo hauko organized katika hoja zao inaonyesha huna uelewa wa mambo. Mambo ya maji hayana uhusiano na Wizara inyaohuiska na mambo ya uchukuzi na usafirishaji. Kuhusu kujenga SGR haina maana kuwa hawajengi barababara; mambo yanakwenda pamoja. Kama wewe hupendi mradi huo usiseme watanzania wengi hawautaki. Tabia ya kutaka kila mtu afurahishwe na mambo yanayofanwa na serikali ni upuuzi. Ukaisema umalize kujenga barabara zote, by the time unamaliza kujenga ile barabara ya mwisho, wale walipata barabara ya kwanza watakuwa wanalalamika kuwa birabara imeshabomoka. Utakuwa unauridia yale yale.
 
Back
Top Bottom