Nilitahadharisha hapa kuwa 'Kesi' imemkalia vibaya 'Mwamba' na hachomoki kirahisi nikaishia Kushambuliwa

Nilitahadharisha hapa kuwa 'Kesi' imemkalia vibaya 'Mwamba' na hachomoki kirahisi nikaishia Kushambuliwa

Acha kwenda jela, hata apigwe risasi hapo kwa Mkapa mchana kweupe, hakuna jipya kwenye hilo, yote ni marudio tu, na hakuna mtu anahitaji maana wako man.
Acha kunichosha kwa Maelezo yako mengi yaliyojaa tu Upuuzi na Unafiki mtupu. Nasisitiza tena kuwa mmeshachelewa na 'Mwamba' lazima Jela akakae angalau hata kwa miaka kadhaa.

Leo mbona hamnitukani Makamanda?
 
Mandela alikaa jela miaka 27 ANC ilikufa???wanajisumbua
Logically what exactly are you trying to Justify? Are you sure that the Late Nelson Mandela spent those 27 years behind Bars because he was a Terrorist like the Swahili Chagga you support?
 
Haki haijawahi kushindwa dhidi ya uovu ni suala la muda tu. Hapa tatizo ni katiba mpya kitu ambacho watawala hawataki kusikia Wana wa Israel walitembea kwa miaka arobaini kufika kwenye nchi ya ahadi licha ya changamoto na vikwazo walivyopitia ndivyo vivyohivyo kwa watanzania
Halafu 'Makamanda' leo mbona mnachangia 'Kihuruma' sana tofauti na mlivyokuwa mkichangia kwa 'Kunitukana' katika zile 'Threads' zangu Mbili nilizomuanzishia huyu 'Mwamba' wenu ili Kuwatahadharisha?

Yaani kabisa Philosopher King GENTAMYCINE nihisi Jambo au nionye kuhusu Jambo fulani halafu lisije kutokea? Thubutu....!!

Kitu pekee ambacho nawashauri ni Kumpambania tu Mtu wenu 'Mwamba' asifungwe miaka mingi kama ambavyo dalili zinaonyesha ili angalau hata afungwe tu kati ya miaka Mitatu au Minne.

'Makamanda' leo mbona hamnitukani?
 
sio kesi imekalia vibaya, sema RAIS SAMIA AMEMKALIA VIBAYA>>>NA ALIONGEA MAJIBU YA KESI MAPEMA BBC AKISEMA WENZAKE WALISHA HUKUMIWA>>>>NDIYO JAJI ANAENDELEA NA KESI AKAMPA CHEO CHA UJAJI KIONGOZI>>>>HUU UJINGA KILA MWENYE AKILI ALIUTAMBUA>>>>BOGUS KABISA>>>>KUJIDAI WACHA MUNGU>>>>OVYO PLUS>>>>HAKUNA MTU HAPO
'Makamanda' leo mbona hamnitukani?
 
Huyo Sabaya angepelekwa mahakamani au asipelekwe, matendo yake tuliyaona, na ushahidi wa unyama wake uko. Na sio yeye tu, viongozi wengi walifanya unyama chini ya utawala wa Magufuli na ushahidi upo. Kwa hiyo usidhani hukumu ya Sabaya ilitufanya tuone mahakama ziko huru, zaidi ya kushangaa mahakama imewazaje kumfunga kiongozi aliyekuwa anatekeleza amri za kiongozi muovu.

Halafu ni mtu mjinga tu mnaweza kumpoteza maboya kwa kutolea mfano hukumu ya Sabaya, na haya maamuzi ya leo ya mahakama dhidi ya kesi ya Mbowe. Na hata mahakama yenyewe inajiaabisha kwa kutoa maamuzi kwa lengo la kutaka kubalance mitazamo ya kisiasa. Ukweli tunaujua, na wala hatutegemei kuupata ukweli huo mahakamani, maana mahakama ni sehemu ya taasisi za umma zilizoharibiwa na mfumo mbovu wa utawala uliopo. Madai yetu ya katiba mpya yanazidi kupata nguvu kwa mambo ya aina hii.
Leo utasema maneno yote ila 'Mwamba' wenu ( wako ) Jela Kwake Wala haikwepeki na ni Suala la muda tu.

'Makamanda' leo mbona hamnitukani?
 
Majaji wangapi wameikimbia unaposema kila jaji? Jaji wa kwanza mlimkataa, mkaletewa huyu wa Sasa, huyu wa Sasa kapanda Cheo hivyo majukumu yameongezeka, naye nafsi yake imemsuta ameona Kwa majukumu aliyonayo Sasa atachelewesha kesi, Bora aachane nayo! Au mlikuwa mnataka jaji aendelee na kesi na awe anapiga kalenda kila siku kesi iende miaka 2? Haya si ndiyo tumekuwa tunayapinga kila siku, full exaggeration
Mkuu ni matumaini yangu umeshajiandaa kwa 'Matusi' yao kwani hicho ndicho wanakiweza ila siyo kutumia Akili vizuri Kufikiri kama ulivyofanya hapa.

Na sijui kwanini leo hawanitukani tena.
 
Logically what exactly are you trying to Justify? Are you sure that the Late Nelson Mandela spent those 27 years behind Bars because he was a Terrorist like the Swahili Chagga you support?
Nachukua nafasi hii kutangaza KUKUDHARAU MOJA KWA MOJA KATIKA KIPINDI CHAKO CHOTE KIFUPI ulichobakiwa nacho hapa duniani .
 
Hakuna Mahakama huru nchi hii.

Hii kesi ilistahili kufuwa siku nyingi tu.

Lengo ni kumuweka ndani wakiamini chama kitayumba na hii ni kwasababu akil zao ni fupi.
Sabaya kafungwa lakini na hizi hizi so hata mbowe akigungwa mahakama bado ni huru
 
Hakuna kesi pale, itaisha ni swala la muda tuu na Mbowe atatoka bila matatizo, na atakuwa maarufu kuliko sasa, acha wajionyeshe walivyo watupu, yule wa Zambia kishafungwa mara kibao na katoka kawa Raisi, Raila kafungwa mara kibao lakini ndio aliongoza Kenya kufanikiwa kuwa na katiba mpya, wataalam wameshajua siku za CCM zinahesabika ndio maana unaona vikesi kesi uchwara, mara kuzima internet nchi nzima, kujipendekeza na vipesa vya madawati etc vinaongezeka kila siku, CCM mjiandae kuwa chama cha upinzani lakini msiwe na wasiwasi mtakuwa katika mazingira mazuri ya haki na usalama
Yaani kwa Upuuzi wako huu naamini kuna 'Majuha' kadhaa hapa watakuamini na kujipa Moto.

Endelea tu Kuwadanganya na Kujidanganya ila wenye Akili tumejua 'Mwamba' yameshamkuta.
 
Ukitulia kabisa na kama tokea mwanzoni umeangalia Kesi ilivyoanza na inavyoenda huhitaji Akili Kubwa sana kujua kuwa ni Kesi ya 'Kimkakati' zaidi na lazima lililopangwa litokee.

Kwa nia njema tu nikaja na Threads zangu Mbili ( ambazo hata hivyo mpaka leo sijui kwanini ziliunganishwa au kufutwa ) kwa Makusudi kabisa nikitaka Mjadala wa 'Kihoja' uanze ili angalau Mawakili Wasomi wanaompambania waokote okote Mawili Matatu ya Kisheria waongezee na yao waliyonayo ili Mhusika anasurike na 'Kesi Mkakati' inayomkabili GENTAMYCINE nikaishia Kutukanwa, Kushambuliwa na Kudhihakiwa.

Haya baada ya Kilichotokea kwa hatua hii tu ya awali kile nilichokisema na Kukitahadharisha ukiwa na Akili Timamu na Kusoma pia Mazingira na Mtiririko wake mnadhani Mhusika haendi Kuozea Jela na labda ni suala la muda tu?

ANGALIZO

Sijamtaja Mtu katika Uzi wangu huu bali nimeelezea tu hivyo sitaki Kuulizwa namuongelea nani na mtakayemhisi huyo mmemuhusi nyie ila siyo Mimi Mleta Mada.

Taratibu sasa tutaanza Kuelewana JF!!!!
Hukushambuliwa, bali ulielezwa ukweli...

Kwamba, kesi hii Jaji au hakimu yeyote hahitaji kuwa amebobea kisheria kujua kuwa ni ya kutunga, ni baseless kisheria...

Mpaka sasa ukweli unabaki kuwa huu hata kama watampeleka jela...

Kwani kesi hii ina tofauti gani na ile ya Yesu Kristo miaka 2021 iliyopita...?

Honestly, haina tofauti kwa sababu zote ni za kutunga kwa kutumia ushahidi wa uongo...

Kwa kuwa walidhamiria kuwa iwe kwa jua au kwa mvua, Yesu Kristo lazima ahukumiwe kifo. Na kweli ilikawa vile. Lakini haikuondoa ukweli kuwa Yesu alishitakiwa kwa uongo na kwa hiyo hata hukumu yake ikawa ni ya kukomoa tu, haikuwa ya haki...

Vivyo kwa huyu jamaa (Mbowe) mfanano wa kesi take umejengwa ktk msingi wa uongo. Likely, watamhumkumu kifungo jela. Lakini watakuwa wamehukumu mtu asiye na hatia...
 
Akikutwa na hatia, hukumu ya Ugaidi akipona sana ni Life sentence au Kunyongwa hadi kufa kisheria. CHADEMA walichukulia hii case kiutani utani, sasa wanaona mtu karibia anaelekezwa kibra.
Hivi Mandela alishitakiwa kwa kesi ipi?
 
Ukiona rais anahonga cheo ili jamuhuri ishinde , ni wazi kuwa hii ni kesi ya kubumba [emoji23][emoji23][emoji23]
Ndiyo mnalijua leo? Na nilivyowatahadharisha kule nyuma kupitia zile 'Threads' zangu Mbili mlikuwa hamjalitambua hili?

Mmeyataka wenyewe acheni anyooshwe.
 
Tulikuwaga tunawashauri humu mawakili waulize maswali ya msingi na wakili wao msomi mzee wa PGO wakzarau wanaluliza walikamata mtuhumiwa akila supu au anatembea Hilo nalo swali? Hamna wakili hapo ni msanii tu kibatala na ndiye anayemuweka mbowe ndani muda mrefu kwa maoingamizi yasiyo na mashiko
Hawashauriki Mkuu hivyo acha tu yawakute ili Siku zingine Watu 'Neutral' kwa Mawazo na Fikra kama Sisi tukiwa tunawashauri kwa Kuwapenda wawe wanatuelewa na siyo kukimbilia Kututukana Kazi ambayo ndiyo wanaiweza na wamebarikiwa nayo.
 
Ujinga mtupu ..japo sipendelei akili za kushikiwa lkn sio kwa maamuzi ya jaji kutupa shauri kwa kutumia maelezo badala ya vifungu vya sheria...wewe Gentanin ningekuona wa maana km ungeleta facts za kisheria zaidi ya porojo tu....
 
Wakimfunga atakuwa Mandela..
Lets wait and see!!
Hukumu ya Mandela nayo ilikuwa ni ya Kimkakati na 'Political Oriented' kama ya huyu 'Mwamba' wenu?

Endeleeni tu kujipa Moyo ila hachomoki.
 
Hii kesi ukiiangalia kwa jicho la kimkakati, mshindi ni Mbowe, akifungwa ni mshindi na akiachiwa ni mshindi.
Yaani uende Kuozea Jela halafu uwe Mshindi? Sishangai kwani hata Mawakili wenu nao wana Uwezo huu huu mdogo wa kufanya Logical and Critical Arguments ndani ya Courtroom aliko 'Mwamba' wenu na hatimaye sasa dalili zote za Yeye kuyaanza Maisha mapya Segerea zimeanza Kujitokeza na ni Suala la muda tu ila sioni kama kwa Kesi ilivyo na 'Mkakati' uliopo atachomoka.
 
Wala hata hiyo post yako sikuiona, itakuwa kutukanwa? Kwahiyo leo hutakanwi kwa sababu unaonekana una msaada ama? Ni kwamba umejiona una influence sana kwenye hii kesi ya kubumba ama, mbona kama sikuelewi? Yaani ww huna impact yoyote kwenye hii kesi, na wala hutakaa uwe nayo zaidi ya kupiga debe kama sisi tu.
'Makamanda' leo mbona hamnitukani?
 
Acha kwenda jela, hata apigwe risasi hapo kwa Mkapa mchana kweupe, hakuna jipya kwenye hilo, yote ni marudio tu, na hakuna mtu anahitaji maana wako man.
Kamanda leo unaandika Kihuruma na Kilokole sana Kulikoni? Leo Matusi yako ( yenu ) hayako Viganjani Kwenu ili muendelee Kunitukana kama mlivyonifanyia huko nyuma?
 
Back
Top Bottom