Soma hiyo injinia usitake kupotosha
Kufufuka Kwa Wafu
12 Basi kama tumehubiri ya kwamba Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu, inakuwaje baadhi yenu mnasema hakuna ufufuo wa wafu? 13 Lakini kama hakuna ufufuo wa wafu, basi Kristo hakufufuliwa. 14 Na ikiwa Kristo hakufufuliwa kutoka kwa wafu, mahubiri yetu ni bure na imani yenu ni bure. 15 Na zaidi ya hayo, tunaonekana kuwa tunamshuhudia Mungu uongo, kwa sababu tumeshuhudia kumhusu Mungu ya kuwa alimfufua Kristo kutoka kwa wafu. Na kumbe hakumfu fua, kama kweli wafu hawafufuliwi. 16 Kwa kuwa kama wafu hawa fufuliwi, basi hata Kristo hajafufuliwa. 17 Na ikiwa Kristo hajafufuliwa, imani yenu ni bure; nanyi bado mngali katika dhambi zenu. 18 Pia waamini wote waliokufa wakimwamini Yesu wamepotea. 19 Na kama imani yetu ndani ya Kristo ni kwa ajili ya maisha haya tu, basi sisi tunastahili kuhurumiwa kuliko watu wengine wo wote duniani. 20 Lakini ukweli ni kwamba Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, matunda ya kwanza ya wote waliolala. 21 Kwa maana kama vile kifo kilivyokuja kwa njia ya mtu mmoja, vivyo hivyo, ufufuo wa wafu umekuja kwa njia ya mtu mmoja. 22 Kwa kuwa katika Adamu watu wote hufa, vivyo hivyo katika Kristo wote wata fanywa kuwa hai. 23 Lakini kila mmoja kwa mpango: Kristo ni mat unda ya kwanza ya ufufuo; kisha wale walio wake wakati atakapo kuja watafufuliwa. 24 Ndipo mwisho utafika, wakati ambao ataka bidhi Ufalme kwa Mungu Baba, akiisha angamiza kila mamlaka na uwezo na nguvu. 25 Kwa maana Kristo atamiliki mpaka Mungu ataka powaweka adui zake chini ya miguu yake. 26 Adui wa mwisho kuan gamizwa ni kifo. 27 “Kwa maana Mungu ameweka kila kitu chini ya utawala wake, chini ya miguu yake.” Ni wazi kwamba maneno haya, “Kila kitu kimewekwa chini ya utawala wake,” hayamjumlishi na Mungu ambaye ameweka vitu vyote chini ya Kristo. 28 Vitu vyote vikishawekwa chini ya utawala wake, ndipo naye Mwana atakuwa chini ya Mungu ambaye ameviweka vitu vyote chini yake, ili Mungu awe yote katika yote.
29 Vinginevyo, kwa nini watu wanabatizwa kwa niaba ya wafu? Kama wafu hawafufuliwi kamwe, mbona watu wanabatizwa kwa niaba yao? 30 Na kwa upande wetu kwa nini tunajitia hatarini kila wakati? 31 Nakufa kila siku, nasema kweli ndugu zangu, kama ninavyojivuna kwa ajili yenu katika Kristo Yesu, Bwana wetu. 32 Kama nilipigana na wanyama wakali huko Efeso kwa sababu za kibinadamu, nimepata faida gani? Kama wafu hawafufuliwi, basi, “Tule na kunywa, kwa maana kesho tutakufa.” 33 Mtu asiwadanga nye, “Ushirika na watu wabaya huharibu tabia njema.” 34 Pateni tena fahamu, muache kutenda dhambi. Kwa maana baadhi yenu hawam jui Mungu; nasema mambo haya ili muone aibu.
Sent from my SM-J610F using
JamiiForums mobile app