Nilitapeliwa mpaka nahisi Dar es Salaam kila mtu ni tapeli

Nilitapeliwa mpaka nahisi Dar es Salaam kila mtu ni tapeli

πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Kuna mkuu alishawahi kuniPM akaniambia katika kundi ambalo sitakiwi kuligusa humu ni single mamaz...hii ilikuwa baada ya mimi siku moja kutema cheche kuhusu single mamaz

Nilimuelewa

Kwa hiyo najizuia sana kutaja hilo kundi kwasababu sitaki vita na mwisho wa siku mimi pia nitakuja kuwa mama siku moja na sijui mwisho wangu πŸ˜ƒ

CHAPUTA hao si wanaweza kuchukua 99% 🀣

Kataa ndoa hao sio wa kuwazingatia,mtu anapinga ndoa huku yupo ndani ya ndoa
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ kundi zito kuliko lote ni Kataa Ndoa,
Ila vita ya single mother, ni nzito mwaya.
 
Ujue katika mapambano ya kutafuta maisha hasa kwetu vijana huwa tunajitahidi kupita maeneo mbalimbali kurisk ili mambo yetu yatuendee vema.

Katika harakati zangu za kutafuta maisha nilishawahi pita maeneo tofauti tofauti na kote huko nilipata experience mbalimbali zilizonikomaza kifikra na kiupambanaji

Nakumbuka kuna kipindi ilinibidi niingie makao makuu kupambana ambako nilienda baada ya kusikia serikali imehamia huko hivo niliona kama ni fursa nikazamia huko kujaribu bahati yangu.

Hakika nilionja joto ya jiwe Dodoma ni ya moto kweli kweli ukifanya masikhara unaweza kufa kwa njaa nakumbuka mapambano yangu ya mwanzo nikiwa sina mtaji wowote zaidi ya nauli ya kunifikisha kule ilibidi nijiingize kwenye biashara ya kuuza ukwaju na kwa kipindi kile ilikuwa inalipa kweli kweli japo muziki wake wa kutembea na lile begi kwenye jua kali biashara ile ilinipa weusi wa Iddi amin dada.


Baada ya kuona nimesave kiasi kadhaa kutokana na kuifanya kwa muda mrefu niliweza kuwa na akiba kama ya laki saba hivi kwenye akaunti yangu ya Equity nikajisemea hii pesa nitaifanyia makubwa.

Hapo ndipo watu wa Dar wakashika hatamu, Nakumbuka nilipigiwa simu na rafiki yangu tuliyesoma nae shule ya msingi ambae tulikuwa tunawasiliana na alikuwa anazielewa hustling zangu, Yeye alikuwa akiishi Dar na alikuwa mnadhifu kweli kweli mara moja moja nikiwa na bando basi nilikuwa nikiona akijitupia mtandaoni akiwa kapendezea sana na vazi la suti wakati huo mimi hata kujipost nilikuwa naogopa maana sura yangu na kiboko vilikuwa vyafanana kwa kiasi.

Nakumbuka aliponipigia simu akanambia ananionea sana huruma kwa jinsi navoteseka na mapambano yangu ya ukwaju ili hali kuna fursa ambazo naweza fanikiwa kwa kutumia nguvu kidogo tu.

Akanambia nifunge safari niende dar akanipe fursa ambayo itanisahaulisha mateso yangu yote na kwa kuwa nilikuwa natamani sana kufanikiwa kwa mara ya kwanza nilinyofoa elfu hamsini katika akiba yangu ambayo nilikuwa nimeiweka kwenye kadi yangu ya benki na kuamua kwenda dar es salaam kwa usafiri wa shabiby

Ilikuwa safari yangu ya kwanza kwenda dar hvo muda wote nilikuwa nawasiliana na rafiki yangu mpaka ninafika dar es salaam ambapo nilikuja kupokelewa huku nikishangaa shangaa mabasi ya mwendokasi na mighorofa ambayo niliitazama hadi shingo ikauma.

Nilipofika geto kwa rafiki yangu asee niliona mwenzangu kajipata maana alikuwa na tv kubwa, sound music ya nguvu na vtu vingine kama fridge ndogo na sofa bed kali sana ilikuwa ni master room nikapatiwa maji nioge akaplace order tukaletewa chips kuku na yeye akamimina mvinyo kidogo kutoka jokofuni mwake mimi nikaomba kupatiwa soda ya coca cola!!

Kisha akanambia kesho yake ndio siku atanipeleka kwenye fursa ambayo imembadilisha maisha yake kwani akanambia yeye hata chuo hakumaliza aliiacha na alitumia hela ya ada kujiunga na hiyo fursa ila hajutii kabisa, Hapo alinitia hasira sana nikasema hapa ndio penyewe plus nina akiba ya kama laki sita na hamsini hivi basi hamna ninachohofia utajiri huu hapa.

Kesho yake ilikuwa ni siku ya jumamosi akaniazima shati lake la mikono mirefu na suruali ya mtelezo ili twende kwa hao maboss ambao ndio wenye fursa wenyewe, basi bhana tukaondoka hadi kwenye jengo moja la orofa refu sana nje kulikuwa na magari ya kifahari na ya kuvutia nikajisemea hapa kutoboa lazima

Tukaingia mpaka ndani waliponiona naingia wakaanza kunipigia makofi i hope rafiki yangu aliwaambia atawaletea mgeni kisha wakanambia you are the next millionaire hapo kichwa kilikuwa kikubwa balaa na rafiki yangu akanitambulisha kuwa namleta huyu naye awe miongoni mwa ma millionaire wenzetu.


Basi pale lecture ikaanza ambapo walikuwa wanaelekeza kwa michoro na product zao pia connection walizonazo nchi mbalimbali huku wakifanya zoom meeting na wazungu wa huko singapore na kuelezea manufaa utayopata baada ya connection utayotengeneza wakataja na package zao na faida utayopata kutokana na kifurushi utachokichagua.

Na wakaniuliza nichague package zao wapo walionyoosha mikono kuchagua package hadi za milioni mbili , rafiki yangu akasema atachukua package ya milioni tano nilishtuka sana walipofika kwangu nikaona kuna package ya laki tano nikasema naombeni hii.


Bila kuchelewesha wakaniletea mezani kwangu na kunipa utaratibu wa kuilipia nikatoka nje kulikuwa na atm nikawithdraw nikawapa laki tano rafiki yangu akitabasamu na kunipa mkono kwa maamuzi niliyoyafanya huku akinambia hutojutia.

Nikapokea kale ka mkoba ambako ndani kalikuwa na kahawa na baadhi ya madawa madawa ya asili ambayo walisema nikiyauza tu nitapata faida mara mbili ila connection ya watu nitaowashawishi wajiunge na ile kampuni itanipa hela nyingi sana.


Nikapata moto akilini nikajisemea hapa nikiingia dodoma moja kwa moja ni kwenda udom huko nitawaunganisha wengi sana.

Kesho yake nikaingia dodoma nilivofika gheto ndio kama akili zikanirudia nikaanza kujiuuliza maswali ya msingi kuwa hivi ni rahisi hivo, nikasema ngoja niingie site aseeeee.....ile kazi ngumu kila ninayemshawishi ajiunge ananambia nyie matapeli nikijaribu walau niuze product zao wanasema bei kubwa kichwa kikaanza kuwaka moto.


Nikajikuta vile vikahawa ambavyo walisema hamna hamna unaweza kuuza hadi elfu hamsini navikoroga na kunywa mwenyewe gheto huku nikiwaza sana na kumchukia yule rafiki kuwa kaniuza mwanae

Nilisota na kutembea hadi soli za viatu zikaisha na sikupata mtu nikaamua nirudi kwnye harakati zangu za ice cream na zile kahawa nilikunywa zote na yale madawa nikayauza kwa hasara nikarudisha kama laki na thelathini tu.

Tukio lile limenifanya nihisi dar kila mtu tapeli🎯
Pyramid scheme hizo kama Qnet na one coin hizo ziko nchi nzima sio dar tu
 
Asante hili jiji kila mtu mwongo mwongo hadi vibibi kizee


Kuna chumba nilikilipia kwa bibi mmoja kumbe kapokea kodi kwa watu wawili siku naenda kuhamia nakuta kuna mtu tayari kahamia

Afu akanambia tu mwenzako kashakuwahi na hela yako nishaitumia kirahisi tu hivo


Asee nilizungushwa sana kuipata pesa yangu na sikupata yote

Nikisema Dar kila mtu tapeli namaanisha.
Huyo dawa nikumvizia siku unapata chumba kwake ukishamlipa zile za mwanzo fresh zikiisha mpaka akuitie balozi na wew unatakiwa kumzungusha
 
Mimi waliniita lakini Mungu alikuwa upande wangu πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜… niliwasikiliza halafu nikawaambia sitaki πŸ˜…πŸ˜….

Nimefika pale wakamwita dada mmoja anajifanya alikuwa mwanachuo na sasa anamiliki gari kali baada ya kuuza madawa yao πŸ˜œπŸ˜…πŸ˜….

Nikamchunguza nikaona kama ni kikoti cha mtumba kavaa halafu kimenyooshwa sana πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜… sikuishia hapo nikashuka kwenye kiskuna weee cha kuokoteza Mwenge. Nikawaambia asante. Nikaishia 😜
TISS hawakuoni kuwa umekamilika kila idara..? ebu wakufanyie mpango wa kazi πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ€£
 
Tathmini ya haraka isiyo rasmi ya wanaJF

30% wamewahi kutapeliwa
30% ni wasukuma
20% waalimu
10% wanaishi Goba/Mbezi
10% bado naendelea kufuatilia, lakini ni either waArusha au wachagga...hapa sijajua lakini wanaweza kugawana
Niko nyuma yako na magwanda yangu kukulinda maana najua watakuvamia vibaya hovyo
 
Q net huwa nakumbuka nacheka walivochemka kwangu ,kwanza walikula maswali mengi mengi mfulizo af ujuaji mwingi plus usela na elimu af na IQ ya moto balaa hyo ni MWENGE DARU SALAAM ,RAMADA hapo kifupi walichoka mana matapeli wakataka kutapeliwa mpaka wakahisi wako na tundu lissu..mwishon nawaambia boss anipe buku 5 nfate hzo hela mageto nije nwape. daaah hawajaaamini hadi muda huo ndo mara ya kwanza kufika dar. yaaan
 
Aisee umenikumbusha kipindi kuna manzi nilikiwa namlia timing namuona kabisa huyu anaigia kwenye mtego mwisho wa siku ananiambia tukutane sijui kwenye mkutano halafu mwisho wa siku tukaingia ukumbini naambiwa Good morning mchana wa jua kali nikaona huu msala🐼
1000018341.gif
 
Ujue katika mapambano ya kutafuta maisha hasa kwetu vijana huwa tunajitahidi kupita maeneo mbalimbali kurisk ili mambo yetu yatuendee vema.

Katika harakati zangu za kutafuta maisha nilishawahi pita maeneo tofauti tofauti na kote huko nilipata experience mbalimbali zilizonikomaza kifikra na kiupambanaji

Nakumbuka kuna kipindi ilinibidi niingie makao makuu kupambana ambako nilienda baada ya kusikia serikali imehamia huko hivo niliona kama ni fursa nikazamia huko kujaribu bahati yangu.

Hakika nilionja joto ya jiwe Dodoma ni ya moto kweli kweli ukifanya masikhara unaweza kufa kwa njaa nakumbuka mapambano yangu ya mwanzo nikiwa sina mtaji wowote zaidi ya nauli ya kunifikisha kule ilibidi nijiingize kwenye biashara ya kuuza ukwaju na kwa kipindi kile ilikuwa inalipa kweli kweli japo muziki wake wa kutembea na lile begi kwenye jua kali biashara ile ilinipa weusi wa Iddi amin dada.


Baada ya kuona nimesave kiasi kadhaa kutokana na kuifanya kwa muda mrefu niliweza kuwa na akiba kama ya laki saba hivi kwenye akaunti yangu ya Equity nikajisemea hii pesa nitaifanyia makubwa.

Hapo ndipo watu wa Dar wakashika hatamu, Nakumbuka nilipigiwa simu na rafiki yangu tuliyesoma nae shule ya msingi ambae tulikuwa tunawasiliana na alikuwa anazielewa hustling zangu, Yeye alikuwa akiishi Dar na alikuwa mnadhifu kweli kweli mara moja moja nikiwa na bando basi nilikuwa nikiona akijitupia mtandaoni akiwa kapendezea sana na vazi la suti wakati huo mimi hata kujipost nilikuwa naogopa maana sura yangu na kiboko vilikuwa vyafanana kwa kiasi.

Nakumbuka aliponipigia simu akanambia ananionea sana huruma kwa jinsi navoteseka na mapambano yangu ya ukwaju ili hali kuna fursa ambazo naweza fanikiwa kwa kutumia nguvu kidogo tu.

Akanambia nifunge safari niende dar akanipe fursa ambayo itanisahaulisha mateso yangu yote na kwa kuwa nilikuwa natamani sana kufanikiwa kwa mara ya kwanza nilinyofoa elfu hamsini katika akiba yangu ambayo nilikuwa nimeiweka kwenye kadi yangu ya benki na kuamua kwenda dar es salaam kwa usafiri wa shabiby

Ilikuwa safari yangu ya kwanza kwenda dar hvo muda wote nilikuwa nawasiliana na rafiki yangu mpaka ninafika dar es salaam ambapo nilikuja kupokelewa huku nikishangaa shangaa mabasi ya mwendokasi na mighorofa ambayo niliitazama hadi shingo ikauma.

Nilipofika geto kwa rafiki yangu asee niliona mwenzangu kajipata maana alikuwa na tv kubwa, sound music ya nguvu na vtu vingine kama fridge ndogo na sofa bed kali sana ilikuwa ni master room nikapatiwa maji nioge akaplace order tukaletewa chips kuku na yeye akamimina mvinyo kidogo kutoka jokofuni mwake mimi nikaomba kupatiwa soda ya coca cola!!

Kisha akanambia kesho yake ndio siku atanipeleka kwenye fursa ambayo imembadilisha maisha yake kwani akanambia yeye hata chuo hakumaliza aliiacha na alitumia hela ya ada kujiunga na hiyo fursa ila hajutii kabisa, Hapo alinitia hasira sana nikasema hapa ndio penyewe plus nina akiba ya kama laki sita na hamsini hivi basi hamna ninachohofia utajiri huu hapa.

Kesho yake ilikuwa ni siku ya jumamosi akaniazima shati lake la mikono mirefu na suruali ya mtelezo ili twende kwa hao maboss ambao ndio wenye fursa wenyewe, basi bhana tukaondoka hadi kwenye jengo moja la orofa refu sana nje kulikuwa na magari ya kifahari na ya kuvutia nikajisemea hapa kutoboa lazima

Tukaingia mpaka ndani waliponiona naingia wakaanza kunipigia makofi i hope rafiki yangu aliwaambia atawaletea mgeni kisha wakanambia you are the next millionaire hapo kichwa kilikuwa kikubwa balaa na rafiki yangu akanitambulisha kuwa namleta huyu naye awe miongoni mwa ma millionaire wenzetu.


Basi pale lecture ikaanza ambapo walikuwa wanaelekeza kwa michoro na product zao pia connection walizonazo nchi mbalimbali huku wakifanya zoom meeting na wazungu wa huko singapore na kuelezea manufaa utayopata baada ya connection utayotengeneza wakataja na package zao na faida utayopata kutokana na kifurushi utachokichagua.

Na wakaniuliza nichague package zao wapo walionyoosha mikono kuchagua package hadi za milioni mbili , rafiki yangu akasema atachukua package ya milioni tano nilishtuka sana walipofika kwangu nikaona kuna package ya laki tano nikasema naombeni hii.


Bila kuchelewesha wakaniletea mezani kwangu na kunipa utaratibu wa kuilipia nikatoka nje kulikuwa na atm nikawithdraw nikawapa laki tano rafiki yangu akitabasamu na kunipa mkono kwa maamuzi niliyoyafanya huku akinambia hutojutia.

Nikapokea kale ka mkoba ambako ndani kalikuwa na kahawa na baadhi ya madawa madawa ya asili ambayo walisema nikiyauza tu nitapata faida mara mbili ila connection ya watu nitaowashawishi wajiunge na ile kampuni itanipa hela nyingi sana.


Nikapata moto akilini nikajisemea hapa nikiingia dodoma moja kwa moja ni kwenda udom huko nitawaunganisha wengi sana.

Kesho yake nikaingia dodoma nilivofika gheto ndio kama akili zikanirudia nikaanza kujiuuliza maswali ya msingi kuwa hivi ni rahisi hivo, nikasema ngoja niingie site aseeeee.....ile kazi ngumu kila ninayemshawishi ajiunge ananambia nyie matapeli nikijaribu walau niuze product zao wanasema bei kubwa kichwa kikaanza kuwaka moto.


Nikajikuta vile vikahawa ambavyo walisema hamna hamna unaweza kuuza hadi elfu hamsini navikoroga na kunywa mwenyewe gheto huku nikiwaza sana na kumchukia yule rafiki kuwa kaniuza mwanae

Nilisota na kutembea hadi soli za viatu zikaisha na sikupata mtu nikaamua nirudi kwnye harakati zangu za ice cream na zile kahawa nilikunywa zote na yale madawa nikayauza kwa hasara nikarudisha kama laki na thelathini tu.

Tukio lile limenifanya nihisi dar kila mtu tapeli🎯
Bila shaka ni QNET hiyo.
 
Back
Top Bottom