Nilivunja Ndoa Zangu 3 Kulipiza Kisasi (Kisa Cha Kweli)

Nilivunja Ndoa Zangu 3 Kulipiza Kisasi (Kisa Cha Kweli)

Charlote, baada ya mume wake kujihusisha na mapenzi na msichana aitwaye Husna, Charlote anaamua kumtafuta mama wa Husna ili kumueleza juu ya swala hili akiamini kwamba ni mama mwenye busara ambaye anaweza kumuonya bintiye kuacha mahusiano na Jones, mumewe Charlote. Lakini kwa bahati mbaya anakutana na mama ama mke ambaye hana busara wala hekima na kumjibu Charlote majibu ambayo kwayo sasa anaamua kulipiza kisasi.

Tayari Charlote ameshaanza mahusiano ya mapenzi na mume wa mwanamke huyo yaani baba wa Husna, na mapenzi yao yamepamba moto , isipokuwa Charlote anafanya kwa siri sana ili isijulikane, sijui nini azma yake.

Je kisasi chake kitafanikiwa ama la?Endelea kujisomea katika sehemu hii ya Tano.
 
SEHEMU YA TANO: SHAMBULIO LA NAFSI
PART 1


Kwa Majidi nilipata mtihani kidogo mkubwa, sikujua nimuingilieje, na lengo langu ilikuwa kuvuruga na kuharibu haswa, niliamua kulipiza kisasi ambacho si mama yake Husna wala Husna ambao wataumia maishani mwao mwote,
Kitendo cha Mume wangu Joe kuwa na mahusiano na Husna kiliniuma sana, niliumia kwani nilikuwa msichana ambaye nilikuwa najitunza, nampenda na kumheshimu sana, lakini niliamini pendo lake la dhati kwangu.
Hiyo haitoshi , kiliniuma zaidi pale ambapoo nilipomuuliza alikataa na kunifanya mimi ni kama mtoto mdogo na asiyetambua jambo.
Hizi fikara ndizo ambazo zilikuwa zikizidisha chachu katika kisasi change, na hata pale akili zinaponirudia na kuona nakosea ninapokumbuka hayo, hasa maneno ya mama yake Husna eti, KAMTOSHELEZE MUMEO… haya yalinifanya nishikwe na hasira kama swira aliyepigwa jiwe likamkosa.
Kumtosheleza ndio nini? Alikuwa na uhakika gani kwamba simtoshelezi? Ohooo,, hivi kumbe mwanaume akitoshelezwa hatoki eeee.. sasa Jones kilichomtoa ndani ni nini na kumfuata Husna msichana ambaye kila nilipojaribu kuangalia na kufananisha namna tunavyoonekana mimi nay eye wala hakunifikia kwa lolote, si umbo, sura , elimu wala Tabia, nilijiuliza na kukosa jibu.
Kisha nikapata jibu kwamba kuna wakati wanaume wanapenda wanawake wabaya. Hili ndilo jibu nilipata.
Kwa uzuri niliokuwa nao, kwa heshima na utii kwa mume na urembo kamwe usingenifananisha na Husna.
Sura umbo wala tabia ya husna havikuwa vizuri, na wala hakuwa msichana mrembo. Nilipata jibu kwamba wanaume hupenda pia wasichana wa SURA MBAYA.
Nilishikwa na hasira kila mara nilipokuwa nikitafakari haya.
Lakini msaidizi wangu Balantine alikuwa pembeni akiniliwaza kila nilipokuwa ninapata mawazo.
Mapenzi ama mahusiano yangu na Mzee zuberi hayakuwa ya furaha wala sikuyafurahia hata kidogo, ni kwa vile nilikuwa nalipiza kisasi tu.
Jones kilimuuma sana kwa namna nilivyobadilika , alikuwa akijuta kwa nini nakunywa pombe kiasi kile, nilipenda pombe sana, niliifurahia, nilikunywa nililala na kuridhika kabisa.
Jones alianza kukonda na kuwa na mawazo mengi sana, sijui kwa nin…
Kuna wakati nilimueleza bila kumficha, Husna si yupo, go, nenda she is available.
Kila nilipomueleza hivyo alichukia sana na mimi kilinichekesha sana.
Muda ulipita,
Nikiwa nimekaa sebuleni nilipata wazo jipya, ilikuwa ni siku ya Jumatatu asbh nikiwa namalizia kunywa juice ili nielekee ofcn.
Nilifika ofcn, baada ya kufungua ofc na kuangalia kazi zangu za siku hiyo nilijiona nina nafasi.
Mara moja nilichukua simu ya ofcn na kupiga kwa Majidi.
Halooo.. upande wa pili ulipokea.
Haloo… nilijibu.
Kisha nikajitambulisha…. Kwamba mimi ni mteja nahitaji flat screen za sumsang kama pc 10 hivi kwa bei nzuri.
Majid alionekana kwenye simu kufurahi sana, alitaka kujua napatikana wapi,,
Nilimueleza kwamba anipatie kwanza bei , nilimpa aina ya screen na ukubwa.
Aliniambia zinauzwa milioni 1.2.
Nilimuambia nikichukua pc 10 atanifanyia punguzo la bei? Alikubali akasema ndio atafanya punguzo la bei.
Aliniomba sana tuonane ili tuweze kuzungumza kwani hana dukani kwa sasa ila ameziagiza na mzigo wake utafika Zanzibar bandarini muda si mrefu.
Nilimueleza niko na shunguli nyingi, isipokuwa nitamjulisha nitakapokuwa na nafasi
Alinihoji ni za matumizi gani,, nilimueleza ni mepata oder kwa mwenye hotel , anataka pc zaidi ya 30. Ila kwa kuanzia anahitaji pc 10 kwanza.
Majid ni kama aliingia uchizi, kwani nilimchizisha pia kwa kumwambia nitahitaji simu za mezani extentions, friji za vyumbani na mazulia.
Aliniambia hivi vyote ana uwezo wa kuvipata.
Nilikubaliana naye nionane naye siku inayofuata jioni. Na kumuomba sana hii deal asijaribu kuongea na mtu kwani sitaki kuipoteza, hivyo asishirikishe mtu ili tusije kosa pesa.
Aliniambia nisijali.
Nilikata simu na kuachia tabasamu kwani tayari nilishajua ndege kanasa kwenye mtego wangu, sina haja ya kikimbia pole pole namkuta kwenye mtego. Maskini Majid bwana harusi mtarajiwa.
Tulikubaliana kukutana kwenye hotel Fulani na baadae nilikata simu huku nikiwa na furaha sana.

Siku iliyofuata nilijua fika ninatakiwa kukutana na Majid, ninamfahamu kwa sura na muonekano wako. Ni kijana mdogo ambaye anaonekana kujiheshimu, kujipenda na kusaka pesa. Ni kijana mwenye asili ya Kiarabu, ni mwenyeji wa Tabora, hupendelea kumuita Majidi Muarabu wa Nzega… hivi ndivyo ilikuwa ukitaka kufika dukani kwake lazma utumie jina hili. Ni kijana ambaye anapenda maendeleo sana, anajishughulisha mno, mpenda dini yake sana . Na hata baada ya kuanza kuwa na mahusiano na Husna , husna naye alianza kuvalia vyema, kwa kujitanda na kujifunika sana, sio husna Yule niliyemuona amevaa leggings na dress top siku ile niliyopishana naye kwenye ngazi, lakini pia siku nilimkuta ofcn kwa mume wangu alikuwa kavalia kigauni kifupi sana kilichoacha paja zake wazi. Nilipokumbuka hili nilianza kupata tena hasira.
Ohooo, sasa nitafanya hivi, najua umbo langu ni zuri, linavutia, nitavalia vyema kama Salha, nilimkumbuka Salha, mwanachuo mwenzangu miaka hiyo iliyopita, alinifundisha kuvalia kama yeye mara kwa mara. Aliniambia nina umbo zuri sana sipaswi kuliachia ila kulihifadhi kwa ajili ya mume wangu. Mara zote aliponiambia hivyo tulicheka. Hivyo nilisema sasa nitavalia hivyo.
Nilikumbuka kwamba nina sketi nzuri ndani, nilikumbuka nina mtandio, nilipoamka ashb nilijiandaa.
Nilivalia vyema sketi ndefu, sendoz zilizoacha vidole vyangu vya miguu wazi, na blauzi ya mikono mirefu, kisha nikafunga kitambaa kichwani na kutupia ushungi, Manshalah,, ungeniona katu usingeniita Charlote, ungeniita pengine Hidaya jina alilonibatiza Mzee Zuberi.
Pole pole nilitoka ndani. Jones mume wangu alinitazama, akaniambia wewe… niligeuka akaniuliza umevaaje hivyo? Nilimtazama na kumwambia kwani nimevaaje?
Akasema unaenda wapi? Nikamwambia naenda ofcn.
Akaguna,,, kisha akasema subiri tuongozane. Sikukataa, nilimsubiri,
Geti lilifunguliwa kisha tukaondoka kuongozana.
Nilitangulia mbele akafuata nyuma.
Nilifika ofcn nikashuka, akaniaga na kuniambia siku njema, nilimwambia asante.
Niliona namna ambavyo Jones anaumia kwa kunikosea.
Lakini hata nilipojaribu kumhurumia nilikumbuka neno la mama yake Husna,, KAMTOSHELEZE MUMEO… nilijiuliza tena, hivi wanaume wote ambao wanamahusiano nje ya ndoa huwa hawatoshelezwi? Nikajichekea tu nikasema ohooo,, kumbe mama husna hamtoshelezi mzee Zuberi ndo maana akanipenda eee…. Nikacheka na kuingia ofcn na kuanza kazi zangu.
Nikiwa kati kati ya kazi, nilishtuliwa na binti ambaye hutuhudumia chai , akiniambia dada Charlote chai tayari nikuletee..
Niliinua uso wangu kwani nilikuwa busy na kazi, nilimtazama na kumuachia tabasamu kisha nikamwambia asante, nipatie chai, kisha vitumbua viwili.
Aliniambia haya dada. Ni binti mzuri anajipenda ana heshima na hutuhudumia kwa heshima sana, na huwa hunipenda mno. Na mara zote huanza kuniuliza kama nitahitaji chai. Na wengi humtania na kumwambia Ni miss kampuni yetu.
Aliniletea chai, nikiwa nakunywa chai, simu yangu ya mezani iliita, nilipokea.
Mume wangu, alinipigia…. Charlote mke wangu habari….
Mh… niliguna kwanza,, kisha nikamwambia salama.
Akaniambia,, tafadhali naomba tutoke wote kwa lunch leo nina maongezi na wewe.
Nilimwambia sawa haina tatizo.
Kisha nikakata simu.
Baada ya nusu saa alinipigia tena simu akaniambia nichague nataka kula nini.
Nilimjibu na kumwambia, unajua choice zangu naomba nichagulie.
Alicheka kwenye simu kicheko cha furaha, nikajua kapata faraja.

****************************************************************************
 
SEHEMU YA TANO: SHAMBULIO LA NAFSI
PART 2


Dah, mume sasa naona kashtuka, sijui kashtuka nini, naona anatamani kabisa kunifuatilia siku ya leo, sasa anataka kupata lunch na mimi. Hii sio tatizo.
Muda wa lunch ulifika, Jones alinifuata ofcn peke yake, siku ya leo kila mtu alinisifia sana kwa namna nilivyovalia, Anti kudrati aliniita na kuniambia umevalia vyema sana isipokuwa tu hujapaka marashi yanaoyendana na vazi hilo,, njoo.. Anti kudrati aliniita kisha akanipatia marashi yanayonukia kama udi Fulani hivi,, huwa sipendi sana marashi haya, lakini ilibidi nikubali ili kuleta heshima ya vazi lenyewe.
Nilijipaka manukato yale kisha nikashuka ngazi nikiwa na jones kuelekea kwenye lunch kama alivyohitaji.
Tuliondoka mimi nay eye wawili tu. Tulifika sehemu ambayo walikuwa wakipika vyakula vya kitanzania, vyakula vyenye asili ya kitanzania. Alijua napenda matoke. Hivyo tuliagiza matoke na tukala.
Tukiwa kwenye hotel hiyo kila mmoja alikuwa akiniangalia sana, nafikiri walimfahamu zaidi Jones kuliko mimi, kwani kwa jinsi nilivyovalia sio rahisi ungeweza kugundua mimi ni Charlote. Na ninafikiri walifikiri kwamba pengine Jones kajipatia jidada la pwani na anatoka nalo.
Tulikula chakula na tukamaliza. Baada ya kumaliza, Jones aliniambia, Mke wangu Charlote, tafadhali naomba yaishe , naomba sana tujenge ndoa yetu.
Nilimtazama na kumwambia nini yaishe? Kitu gani? Alniambia nilivyokukosea sana, nilishindwa kuwa muaminifu kwako na kuwa na mahusiano na Husna, naomba unisamehe.
Nilimtazama na nikasema sasa huu ni muda muafaka kumhoji ni kitu gani alikosa kwangu.
Nilimtazama na kumgeukia, kisha kumkazia macho na kumuuliza,
Jones mume wangu,, ninaombe tu unieleza ni kitu gani kilikufanya ukaamua kuwa na mahusiano na Husna.
Jones alinitazama na kuniambia siwezi kusema kitu gani ila ni tamaa tu.
Nilimwambia hapana , haiwezekani, lazima kuna jambo na kitu kilikuvutia kwake. Tafadhali niambie ili nijirekebishe na isije kupelekea tena ukawa na mahusiano nje ya ndoa yako.
Jones aliniambia kwa kweli siwezi kusema kwamba wewe ni sababu ya mimi kuwa na mahusiano na Husna, ila ni mimi peke yangu tu nilishindwa kukuheshimu. Naomba nisamehe.
Nilimwambia nimekusamehe siku nyingi sana,
Aliniambia asante sana, na kisha akatoa mfuko ambao ulikuwa na perfume, viatu na saa.
Akaniambia hizi hapa zawadi zako asante kunisamehe.
Nilimwambia asante sana kwa zawadi, nilichukua zawadi zangu na tukaondoka. Alinielekea ofcn kwake na mimi nilelekea ofcn kwangu.
Aliniandikia msg na kusema,, CHARLOTE MKE WANNGU, MAMA WA WATOTO WANGU, MKE WA UJANA WANGU, MKE WA AHADI NA KIAPO KITAKATIFU, NAOMBA NISAMEHE, NAKUPENDA SANA, SITEGEMEI KUKUKOSEA TENA, NAJUA NIMEKUUMIZA SANA, ISIPOKUWA NISAMEHE, NIPENDE KAMA ZAMANI, NAMISS SANA PENZI LAKO MKE WANGU.”
Niliitazama ile msg, machozi yalinidondoka, ujumbe huu ulinionyesha wazi namna ambavyo Jones amekiri kosa lake. Nililia sana, kisha nikanyamaza, Ujumbe huu niliusave tena, ni ujumbe wa pili kwenye maisha yangu nauserve. Jones, jones, jones, kwa nini umesababisha nikawa na roho ngumu hivi wewe mwanaume? Aghhhhh.. niligonga meza kwa nguvu na kuchukia sana, kwani alipelekea nikawa nimejiingiza kwenye jambo ambalo kuliachia kati siwezi.
Siwezi kuachia jambo hili kati kati, lazima Husna na mama yake kiwaume kama kilivyoniuma.
Haraka nilifuta machozi, na baada ya hapo niliangalia saa yangu ya mkononi ilikuwa ni saa kumi na robo. Tulikubaliana kukutana na Majidi saa kumi na moja na nusu kwenye hotel Fulani.
Nilianza kujiandaa kumalizia kazi zangu za siku ile, kisha baada ya hapo nilienda kwa muajiri wangu ambaye kwa sehemu alijua kuwa siko vizuri kutokana na matatizo ya kindoa.
Muajiri aliniruhusu na nikaondoka. Niliwasha gari yangu, kabla sijaanza kuendesha, niliinama kwenye stsaling, nikitafakari tena maneno ya Jones, ni maneno mazito.
Mungu wangu… si ni msamehe tu jamani Jones… dah,, amejuta kweli, si kawaida yake, Jones anamaanisha kukosea, nimsamehe.
Haraka akili yangu iliniambia….. HUMTOSHELEZI… sauti ya mama Husna ilijirudia kwenye masikio yangu,
Niliwasha gari na moja kwa moja nilielekea kwenye hoteli hiyo.
Majidi namfahamu, ila mimi hanifahamu kabisa.
Nilifika , niliona gari yake ikiwa imepaki, kwani ilkuwa na tyer cover la maandishi ya duka lake la vifaa.
Nilijua kashafika.
Moja kwa moja nilishuka kisha nikaelekea sehemu ambayo amekaa kwani nilimfahamu.
Alikuwa akiniangalia sana kabla hajajua ni mimi ninayemfuata.
Nilifika na kumsalimia. Habari…. Aliitika njema habari yako.
Niliitika nzuri. ..
Mimi ni Charlote,,, tulikubaliana kukutana leo kibiashara..
Ahaa.. karibu karibu sana charlotte, tayari alisimama na kunisogezea kiti. Mezani alikuwa na laptop ya apple, kisha alikuwa na diary na funguo za gari, na simu kama tatu hivi, zote smart phone.
Alisogeza vitu vyake vyema kisha nikakaa.
Alinitazama na kusema dah,,charlotte,,,, why charlotte? Aliniuliza…
Are you musilm or Christian? Nilitabasamu nikasema am Christian.
Aisee,, umependeza sana ulivyovyalia, kama muarabu bwana,, manshalah… alimaliza kusema,
Nilimshukura na kumwambia asante.
Kisha nikamwambia sina mud asana kukaa naye kwani ninahitaji tu kumueleza ninachohitaji. Nilifungua pochi yangu na kutoa karatasi ambayo ilikuwa imendikwa baadhi ya bidhaa, na niliandika mwenyewe as if ni oder kutoka mahali Fulani. Kwa nini asiamini?
Kisha nikamueleza mahitaji yangu, Aliniambia kweli aina za flat screen hizo kwa sasa hana, ila anauwezo wa kuwa nazo kwani hata kwenye mzigo wake hakuna aina hizo. Nilimueleza inachukua muda gani hadi mzigo kufika tangu kuagiza? Aliniabia ni ndani ya siku 21 mpaka 40.
Dah,, nilimjibu ni siku nyingi sana, kwani mwenye anahitaji anazihitaji kwa haraka sana kutokana na kutaka kufungua hotel yake.
ALinihoji kama hotel hiyo iko mjini, nilimwambia hapana iko nje ya mji tena mkoani.
Alifurahi sana kwa mimi kumpa biashara.
Asante sana charlotte, asante sana. Nashukuru kunipatia biashara hii.
Nilimwambia asante sana, huwa watu wengi hukusifia unauza bidhaa zenye ubora hivyo nikaona sio mbaya nikihitaji vifaa kutoka kwako. Aliniambai nisiwe na shaka kwani pia bidhaa zake zina guarantee ya mwaka mzima.
Nilimshukuru, na tukakubaliana kwamba angenipigia simu kunipa feed back ya kinachoendelea.
Dah… Mimi ni mke wa mtu Majid, singependa unipigie simu kabisa, kiusalama zaidi, si unajua wanaume mlivyo na wivu? Ha ha ha, kisha nikacheka.
Na ni kweli, , sasa tutawasilianaje? Alihoji.
Nilimueleza kila nitakapokuwa nahitaji kuwasiliana naye mimi ndiye nitampigia simu, na nitatumia simu ya ofcn kama kawaida.
Alikubali, kisha akaniambia, Ninaharusi mwezi huu hivyo ningependa kujua kabisa oder yako niifanyie kazi mapema kabla sijatoka kwa honeymoon.
Ohooo,, unaoa? Nilionyesha kushangaaa…
Ndio,, ninaoa mwezi huu,, ila dah,, ulivyomrembo natamani kama ungekuwa hujaolewa ningekuoa.
Tulicheka wote kisha nikamuaga na kumueleza kwamba tutawasiliana, anipe saa na siku ya kumpigia simu.
Aliniambia atafanyia kazi hiyo oder na hivyo nimpigie simu baada ya siku mbili tu, kwani anajaribu kuangalia kwa baadhi ya mawakala kuona kama anaweza kupata hizo pc 10 haraka iwezekanavyo ili asikose tender hiyo.
Tulimaliza kuzungumza,, kisha nikamuaga.
Charlote,, wewe ni mrembo sana, umependeza sana, wewe ni mzuri sana,, manshalah,,, dah….
Majid alisema ,, kisha nilitabasamu na kuondoka.
Nilienda moja kwa moja nyumbani, Nilimkuta Jones yuko nyumbani akinisubiri.
Niliingia ndani, nilisalimia na kuangalia watoto wakoje, kisha nikaingia bafuni mara moja kuoga na baadae nikatoka ili kuandaa chakula cha jioni, najua Jones anapenda chapatti. Niliandaa chapatti zake chache na beef stew kwani hupendelea sana. Nilimtengenezea pia na juice ya matunda, kisha nikaanda chakula mezani ili ajipatie mlo wa usiku.
Alikuwa anaonekana kuwa na furaha sana. Alifurahia mlo ule, alikuwa akiongea kwa furaha na kucheka sana huku akinikumbusha baadhi ya mambo mazuri ya zamani.
Tulicheka. … ni kama alianza kunirudisha kwenye mood. Lakini kila nilipokumbuka mission yangu, dah mood ilinipotea ghafla.
Asbh niliamka, nilimuandalia vyema kwa ajili ya kazini, alijiandaa na tukaondoka.
Mzee Zuberi alnipenda sana, kila siku ashb alipofika ofcn kwake alinipigia simu na kunisalimia. Nilideka kwa mzee Zuberi sana, nilikuwa nadeka mno. Na yeye alinidekeza haswa, kila nilichohitaji nilipata kutoka kwake, hakuna nilichokosa.
Asbh alinipigia simu na kunisalimia, kisha akaniambia Mamii mbona huko na furaha?
Nilimueleza kuna kitu nimeona mjini nimekipenda na ningetamani kukipata.
Aliniuliza ni kitu gani, na nilimueleza na viatu ambavyo vinauzwa pamoja na handbag yake ni lether one hundred paceee, na ni made in Italy.
Aliniambia Charlote sijui hivyo vitu mama, wewe sema ni shilingi ngapi nikupatie.
Niliona ni muda wa kumsumbua… nilimueleza vinapopatikana . sikutaka kumwambia ni shilingi ngapi.
Aliniambie angepita hapo muda wa lunch time kucheki, kisha atanijulisha nikavichukue hapo.
Mzee Zuberi ni baba wa miaka kama 58 hivi. Sio mzee sana. Na kwa vile alikuwa na pesa na kujipenda basi alionekana tu ni kijana mzee, alijipenda sana.
Saa saba mchana on dot. Simu yangu iliita, nilitazama, ni Mzee Zuber.
Charlote,, bi mdogo… Abee niliitika.
Haya mama mzigo wako nimeuona sema unataka rangi gani, ziko rangi mbili tu hapa, black an red.
Nilitabasamu na kumwambia nahitaji rangi ya red.
Aliniambia sawa, uje kuchukua basi mzigo wako nimeshalipa sawa mama.
Ndio.. Asante sana.
Hakuna shaka sema kingine.
Alimaliza na kukata simu.
Dah… kweli mzee kajitosha. Viatu na pochi hizo huuzwa dola 400. Ama kweli mzee kapenda.
Nilijichekea mwenye .
Niliendelea na kazi na baadae nilienda dukani kuchukua mizigo yangu.
Nilifika na kumkuta muuzaji wa duka, ni dada ambaye mara nyingi nanunua vitu hapo, ananijua kwa sura tu sio jina.
Na nilipofika niliweka sura ya kazi ili nisimpe nafasi ya kuhoji.
Habari dada… samahani nimeambiwa nikifika hapa nitaje namba hizi ili unipatie mzigo wangu.
Alizitama zile namba kisha akasema ahaa, ni Mr Zuberi sio kakuambia uje uchukue?
Ndio nilijibu kwa mkato. Kisha nikapatiwa mzigo wangu na kuondoka.
Huyooo mpaka nyumbani, I love the shoes,, I love tha handbag… ziko kiwango. Nilicheka kisha nikasema ahaaa… kumbe nimemtosheleza mr Zuberi ee ndo maana ananinunulia vitu vya gharama. Nilikumbuka jambo,,, nilimkumbuka mke wa mzee zuberi, ni mama mwenye miaka kama 50 ama 52 hivi ama 55, hakuzidi hapo. Ila hajipendi hata kidogo, sijui ni umri ama ni nini. Nilijichekea nikasema sasa upele umepata mkunaji.
 
SEHEMU YA SITA: NDANI YA MPANGO HASI
PART 1


Majidi hakuweza kuvumilia. Ni saa mbili na robo niko ofcn kwangu nakunywa kikombe cha maji ya moto. Simu yangu ya mezani inaita. Nikiwa naendelea kujiuliza ni nani,, niliipokea.
Habari? Habari,, upande wa pili ulijibu,, ahaaa, niliweza kuitambua Sauti ni ya Majidi.
Habari Charlote…. Nilijibu ni njema sana habari za tangu majuzi?
Ni njema pia. .. enhe jipya? Nilimhoji.
Aliniambia sina jipya, nimekukumbuka tu nikasema nikusalimie, japo bado nafuatilia kazi yako, uwezekano wa kupata oder yako sio mgumu lakini sio mrahisi sana, naweza kupata ila bei itakuwa ghali kidogo kutokana na aina ya mzigo. Aliniambia Majid.
Ohooo, haina shaka,, nilimjibu, kisha nikamwambia wewe hakikisha unafuatilia kisha unirudie na jibu sahihi ili nimueleze anayezihitaji, huenda akaamua kuongeza bei.
Okay , haina shaka…ila pia…. Ila…. Majidi aliongea kwa kuguguma.
Sema. Mboan kigugumizi? Nilimuuliza…
Majidi alicheka,, kisha akasema dah,, ukinikatalia nitajisikia vibaya sana.
Nilishajua lengo lake, kisha nikamwambia wewe bwana kata simu kama huna la kusema.
Sikia, usikate, usikate… alisema Majidi, kisha nikakata simu.
Baada ya sekunde kama 30 hivi simu iliita tena.
Akaniambia,, Charlote unajua nikuambie tu ukweli kama utanikubalia sawa kama utakataa sawa.
Ila ukweli ni kwamba tangu nimekuona nimetokea kuvutiwa sana na wewe na nimekupenda sana, najua wewe ni mke wa mtu na mimi karibuni nitakuwa mume wa mtu, ila nimetokea kukupenda sana Charlote, nimevutiwa na wewe sana sijui una kitu gani chenye nguvu kiasi hicho. Alisema Majidi.
Nilikata simu ,, kana kwamba sitaki kusikia habari hizo.. kumbe ndizo nilizokuwa nikizisubiri. Kisha nikacheka na kutoka kwenye washroom.
Nilimaliza na kurudi tena kukalia kiti cha ofcn na kuanza kupiga kazi. Nilifanya kazi mpaka saa nne na nilikuwa nimeshamaliza kazi zangu.
Mume wangu aliniandikia msg, Hi mamii, hujambo? Unaendeleaje? Pole na kazi.
Niliutazama ujumbe ule, kisha nikamjibu, sijambo naendelea vyema, kazi njema.
Aliniambia Asante sana.
Baada ya kumaliza tu kujibizana kwa msg na mume wangu, mara simu ya mezani iliita tena.
Haloo Charlote… nilitikia haloo… ni majidi.
Naomba unisamehe kama nitakuwa nimekukwaza…. Aliongea Majid kwa mbwembe nilimgndua. Nilimwambia haina shaka, nafurahi kuona kwamba ni mke wa mtu lakini ninavutia.. ila pia nafurahi kuona kwamba naweza kumvutia bwana harusi mtarajiwa.
Alisema dah,,, kweli umenivutia kabisa, najuta kuoa mapema?
Ha ha ha, nilicheka,, akaniambia kwa nini unacheka? Nikamwambia maneno yako,, kwani ni ujute? Hata usingejuta mimi ni mke wa mtu, hungeweza kunioa.
 
SEHEMU YA SITA: NDANI YA MPANGO HASI
PART 2

Kwa nini nisiweze kukuoa? Sina utajiri wala chochote ila nina mapenzi?
Nilicheka nikajua hizo ni gear tu za kiume, ila moyoni tayari nilishakuwa nimenuia kuwa naye, hivyo ni kama nilikuwa nazuga Fulani hivi.
Sikia Majid, kweli mimi ni mke wa mtu, isipokuwa naogopa mume wangu akijua ni hatari sana, ama mkeo akijua ni hatari sana.
Majidi ni kama alishangaa mimi kusema vile, ni kama aliona nimeshamkubali..
Sikia Charlote, nitaiheshimu ndoa yako sana, nakuapia, na mimi pia mchumba wangu hatajua.
Sikia Majid,, naelewa, ila wewe oa kwanza wala usiwe na haraka mimi nipo, wewe oa kwanza.
Majid alniambia, ninasafiri kwenda Zanzibar kufuatamzigo wangu ijumaa, tafadhali kama unaweza nisindikize.
Ni haraka sana, ni haraka sana Majidi, ni haraka sana. Tafadhali wewe nenda tu.
Hapana Charlote kama unaweza nisindikize tafadhali.
Nilimueleza kwamba siwezi kumsindikiza na nikakata simu.
Zilikuwa zimebaki kama wiki tatu za harusi. Nilijiuliza je nilikoroge kabla ya harusi ama?
Niliona intakavyonoga nikisababisha ndoa kutokufungwa, hasara ya sare , ukumbi, na vyakula kwani najua wameshafanya maandalizi.
Lakini nikajiuliza kitu kingine, hapana hii haitauma kama nikilikoroga baada ya kuwa mume, tena sio mume wa siku tatu ama nne, ni masiku mengi haswa, aone raha ya mume na ndoa, kisha ajue nina mahusiano na mumewe. Hii ndiyo niliitaka, niliitamani.
Hivyo sikuwa na haraka kabisa, nikawa nasubiri simu ingine ya Majidi nilijua atapiga tu.
Mara kweli simu ikaita. Majid alipiga,, nilipokea.
Charlote tafadhali tuonane tuzungumze.. nilimueleza kwamba asijali, nitampangia siku ya mimi na yeye kuzungumza, ila ni vizuri kama akisettle kwenye maswala ya harusi yake kkwanza.
Majid, mimi nipo tu, hembu shughulikia harusi kwanza, mimi nipo.
Aliniambia mimi ni mwanaume harusi niachie mimi. Nilicheka,, akaniambiambia mbona unanicheka? Hujui kama uzuri wako umenichanganya?
Nilimwambai nacheka kwa vile najua ninyi wanaume ni waongo sana.Aliniambia kweli huwa wanaume ni waongo, ila sio mimi, nakupenda haswa wewe ni wewe na husna ni husna, huwezi kuwa kama husna na husna hawezi kuwa kama wewe, ila bahati mbaya umeolewa, kama ungekuwa hujaolewa ningekuoa hata mke wa pili, na kama huamini niachie hiyo kazi mimi, na ninakuapia hutateseka, nakupenda charlotte.
Nilimuitikia na kumwambi a basi usijali, ngoja niangalie ratiba zangu zikoje kisha nitakujuza tutasafiri wote kwenda Zanzibar.
Kweli? Ndio,, kweli … ndio, alirudia kama mara tano hivi na mimi nikamhakikishiani ndio.
 
huyo charlote kanifrahisha sana japo alipaswa asamehe na asahau waanze upya na mumewe
 
Back
Top Bottom