SEHEMU YA TANO: SHAMBULIO LA NAFSI
PART 2
Dah, mume sasa naona kashtuka, sijui kashtuka nini, naona anatamani kabisa kunifuatilia siku ya leo, sasa anataka kupata lunch na mimi. Hii sio tatizo.
Muda wa lunch ulifika, Jones alinifuata ofcn peke yake, siku ya leo kila mtu alinisifia sana kwa namna nilivyovalia, Anti kudrati aliniita na kuniambia umevalia vyema sana isipokuwa tu hujapaka marashi yanaoyendana na vazi hilo,, njoo.. Anti kudrati aliniita kisha akanipatia marashi yanayonukia kama udi Fulani hivi,, huwa sipendi sana marashi haya, lakini ilibidi nikubali ili kuleta heshima ya vazi lenyewe.
Nilijipaka manukato yale kisha nikashuka ngazi nikiwa na jones kuelekea kwenye lunch kama alivyohitaji.
Tuliondoka mimi nay eye wawili tu. Tulifika sehemu ambayo walikuwa wakipika vyakula vya kitanzania, vyakula vyenye asili ya kitanzania. Alijua napenda matoke. Hivyo tuliagiza matoke na tukala.
Tukiwa kwenye hotel hiyo kila mmoja alikuwa akiniangalia sana, nafikiri walimfahamu zaidi Jones kuliko mimi, kwani kwa jinsi nilivyovalia sio rahisi ungeweza kugundua mimi ni Charlote. Na ninafikiri walifikiri kwamba pengine Jones kajipatia jidada la pwani na anatoka nalo.
Tulikula chakula na tukamaliza. Baada ya kumaliza, Jones aliniambia, Mke wangu Charlote, tafadhali naomba yaishe , naomba sana tujenge ndoa yetu.
Nilimtazama na kumwambia nini yaishe? Kitu gani? Alniambia nilivyokukosea sana, nilishindwa kuwa muaminifu kwako na kuwa na mahusiano na Husna, naomba unisamehe.
Nilimtazama na nikasema sasa huu ni muda muafaka kumhoji ni kitu gani alikosa kwangu.
Nilimtazama na kumgeukia, kisha kumkazia macho na kumuuliza,
Jones mume wangu,, ninaombe tu unieleza ni kitu gani kilikufanya ukaamua kuwa na mahusiano na Husna.
Jones alinitazama na kuniambia siwezi kusema kitu gani ila ni tamaa tu.
Nilimwambia hapana , haiwezekani, lazima kuna jambo na kitu kilikuvutia kwake. Tafadhali niambie ili nijirekebishe na isije kupelekea tena ukawa na mahusiano nje ya ndoa yako.
Jones aliniambia kwa kweli siwezi kusema kwamba wewe ni sababu ya mimi kuwa na mahusiano na Husna, ila ni mimi peke yangu tu nilishindwa kukuheshimu. Naomba nisamehe.
Nilimwambia nimekusamehe siku nyingi sana,
Aliniambia asante sana, na kisha akatoa mfuko ambao ulikuwa na perfume, viatu na saa.
Akaniambia hizi hapa zawadi zako asante kunisamehe.
Nilimwambia asante sana kwa zawadi, nilichukua zawadi zangu na tukaondoka. Alinielekea ofcn kwake na mimi nilelekea ofcn kwangu.
Aliniandikia msg na kusema,, CHARLOTE MKE WANNGU, MAMA WA WATOTO WANGU, MKE WA UJANA WANGU, MKE WA AHADI NA KIAPO KITAKATIFU, NAOMBA NISAMEHE, NAKUPENDA SANA, SITEGEMEI KUKUKOSEA TENA, NAJUA NIMEKUUMIZA SANA, ISIPOKUWA NISAMEHE, NIPENDE KAMA ZAMANI, NAMISS SANA PENZI LAKO MKE WANGU.”
Niliitazama ile msg, machozi yalinidondoka, ujumbe huu ulinionyesha wazi namna ambavyo Jones amekiri kosa lake. Nililia sana, kisha nikanyamaza, Ujumbe huu niliusave tena, ni ujumbe wa pili kwenye maisha yangu nauserve. Jones, jones, jones, kwa nini umesababisha nikawa na roho ngumu hivi wewe mwanaume? Aghhhhh.. niligonga meza kwa nguvu na kuchukia sana, kwani alipelekea nikawa nimejiingiza kwenye jambo ambalo kuliachia kati siwezi.
Siwezi kuachia jambo hili kati kati, lazima Husna na mama yake kiwaume kama kilivyoniuma.
Haraka nilifuta machozi, na baada ya hapo niliangalia saa yangu ya mkononi ilikuwa ni saa kumi na robo. Tulikubaliana kukutana na Majidi saa kumi na moja na nusu kwenye hotel Fulani.
Nilianza kujiandaa kumalizia kazi zangu za siku ile, kisha baada ya hapo nilienda kwa muajiri wangu ambaye kwa sehemu alijua kuwa siko vizuri kutokana na matatizo ya kindoa.
Muajiri aliniruhusu na nikaondoka. Niliwasha gari yangu, kabla sijaanza kuendesha, niliinama kwenye stsaling, nikitafakari tena maneno ya Jones, ni maneno mazito.
Mungu wangu… si ni msamehe tu jamani Jones… dah,, amejuta kweli, si kawaida yake, Jones anamaanisha kukosea, nimsamehe.
Haraka akili yangu iliniambia….. HUMTOSHELEZI… sauti ya mama Husna ilijirudia kwenye masikio yangu,
Niliwasha gari na moja kwa moja nilielekea kwenye hoteli hiyo.
Majidi namfahamu, ila mimi hanifahamu kabisa.
Nilifika , niliona gari yake ikiwa imepaki, kwani ilkuwa na tyer cover la maandishi ya duka lake la vifaa.
Nilijua kashafika.
Moja kwa moja nilishuka kisha nikaelekea sehemu ambayo amekaa kwani nilimfahamu.
Alikuwa akiniangalia sana kabla hajajua ni mimi ninayemfuata.
Nilifika na kumsalimia. Habari…. Aliitika njema habari yako.
Niliitika nzuri. ..
Mimi ni Charlote,,, tulikubaliana kukutana leo kibiashara..
Ahaa.. karibu karibu sana charlotte, tayari alisimama na kunisogezea kiti. Mezani alikuwa na laptop ya apple, kisha alikuwa na diary na funguo za gari, na simu kama tatu hivi, zote smart phone.
Alisogeza vitu vyake vyema kisha nikakaa.
Alinitazama na kusema dah,,charlotte,,,, why charlotte? Aliniuliza…
Are you musilm or Christian? Nilitabasamu nikasema am Christian.
Aisee,, umependeza sana ulivyovyalia, kama muarabu bwana,, manshalah… alimaliza kusema,
Nilimshukura na kumwambia asante.
Kisha nikamwambia sina mud asana kukaa naye kwani ninahitaji tu kumueleza ninachohitaji. Nilifungua pochi yangu na kutoa karatasi ambayo ilikuwa imendikwa baadhi ya bidhaa, na niliandika mwenyewe as if ni oder kutoka mahali Fulani. Kwa nini asiamini?
Kisha nikamueleza mahitaji yangu, Aliniambia kweli aina za flat screen hizo kwa sasa hana, ila anauwezo wa kuwa nazo kwani hata kwenye mzigo wake hakuna aina hizo. Nilimueleza inachukua muda gani hadi mzigo kufika tangu kuagiza? Aliniabia ni ndani ya siku 21 mpaka 40.
Dah,, nilimjibu ni siku nyingi sana, kwani mwenye anahitaji anazihitaji kwa haraka sana kutokana na kutaka kufungua hotel yake.
ALinihoji kama hotel hiyo iko mjini, nilimwambia hapana iko nje ya mji tena mkoani.
Alifurahi sana kwa mimi kumpa biashara.
Asante sana charlotte, asante sana. Nashukuru kunipatia biashara hii.
Nilimwambia asante sana, huwa watu wengi hukusifia unauza bidhaa zenye ubora hivyo nikaona sio mbaya nikihitaji vifaa kutoka kwako. Aliniambai nisiwe na shaka kwani pia bidhaa zake zina guarantee ya mwaka mzima.
Nilimshukuru, na tukakubaliana kwamba angenipigia simu kunipa feed back ya kinachoendelea.
Dah… Mimi ni mke wa mtu Majid, singependa unipigie simu kabisa, kiusalama zaidi, si unajua wanaume mlivyo na wivu? Ha ha ha, kisha nikacheka.
Na ni kweli, , sasa tutawasilianaje? Alihoji.
Nilimueleza kila nitakapokuwa nahitaji kuwasiliana naye mimi ndiye nitampigia simu, na nitatumia simu ya ofcn kama kawaida.
Alikubali, kisha akaniambia, Ninaharusi mwezi huu hivyo ningependa kujua kabisa oder yako niifanyie kazi mapema kabla sijatoka kwa honeymoon.
Ohooo,, unaoa? Nilionyesha kushangaaa…
Ndio,, ninaoa mwezi huu,, ila dah,, ulivyomrembo natamani kama ungekuwa hujaolewa ningekuoa.
Tulicheka wote kisha nikamuaga na kumueleza kwamba tutawasiliana, anipe saa na siku ya kumpigia simu.
Aliniambia atafanyia kazi hiyo oder na hivyo nimpigie simu baada ya siku mbili tu, kwani anajaribu kuangalia kwa baadhi ya mawakala kuona kama anaweza kupata hizo pc 10 haraka iwezekanavyo ili asikose tender hiyo.
Tulimaliza kuzungumza,, kisha nikamuaga.
Charlote,, wewe ni mrembo sana, umependeza sana, wewe ni mzuri sana,, manshalah,,, dah….
Majid alisema ,, kisha nilitabasamu na kuondoka.
Nilienda moja kwa moja nyumbani, Nilimkuta Jones yuko nyumbani akinisubiri.
Niliingia ndani, nilisalimia na kuangalia watoto wakoje, kisha nikaingia bafuni mara moja kuoga na baadae nikatoka ili kuandaa chakula cha jioni, najua Jones anapenda chapatti. Niliandaa chapatti zake chache na beef stew kwani hupendelea sana. Nilimtengenezea pia na juice ya matunda, kisha nikaanda chakula mezani ili ajipatie mlo wa usiku.
Alikuwa anaonekana kuwa na furaha sana. Alifurahia mlo ule, alikuwa akiongea kwa furaha na kucheka sana huku akinikumbusha baadhi ya mambo mazuri ya zamani.
Tulicheka. … ni kama alianza kunirudisha kwenye mood. Lakini kila nilipokumbuka mission yangu, dah mood ilinipotea ghafla.
Asbh niliamka, nilimuandalia vyema kwa ajili ya kazini, alijiandaa na tukaondoka.
Mzee Zuberi alnipenda sana, kila siku ashb alipofika ofcn kwake alinipigia simu na kunisalimia. Nilideka kwa mzee Zuberi sana, nilikuwa nadeka mno. Na yeye alinidekeza haswa, kila nilichohitaji nilipata kutoka kwake, hakuna nilichokosa.
Asbh alinipigia simu na kunisalimia, kisha akaniambia Mamii mbona huko na furaha?
Nilimueleza kuna kitu nimeona mjini nimekipenda na ningetamani kukipata.
Aliniuliza ni kitu gani, na nilimueleza na viatu ambavyo vinauzwa pamoja na handbag yake ni lether one hundred paceee, na ni made in Italy.
Aliniambia Charlote sijui hivyo vitu mama, wewe sema ni shilingi ngapi nikupatie.
Niliona ni muda wa kumsumbua… nilimueleza vinapopatikana . sikutaka kumwambia ni shilingi ngapi.
Aliniambie angepita hapo muda wa lunch time kucheki, kisha atanijulisha nikavichukue hapo.
Mzee Zuberi ni baba wa miaka kama 58 hivi. Sio mzee sana. Na kwa vile alikuwa na pesa na kujipenda basi alionekana tu ni kijana mzee, alijipenda sana.
Saa saba mchana on dot. Simu yangu iliita, nilitazama, ni Mzee Zuber.
Charlote,, bi mdogo… Abee niliitika.
Haya mama mzigo wako nimeuona sema unataka rangi gani, ziko rangi mbili tu hapa, black an red.
Nilitabasamu na kumwambia nahitaji rangi ya red.
Aliniambia sawa, uje kuchukua basi mzigo wako nimeshalipa sawa mama.
Ndio.. Asante sana.
Hakuna shaka sema kingine.
Alimaliza na kukata simu.
Dah… kweli mzee kajitosha. Viatu na pochi hizo huuzwa dola 400. Ama kweli mzee kapenda.
Nilijichekea mwenye .
Niliendelea na kazi na baadae nilienda dukani kuchukua mizigo yangu.
Nilifika na kumkuta muuzaji wa duka, ni dada ambaye mara nyingi nanunua vitu hapo, ananijua kwa sura tu sio jina.
Na nilipofika niliweka sura ya kazi ili nisimpe nafasi ya kuhoji.
Habari dada… samahani nimeambiwa nikifika hapa nitaje namba hizi ili unipatie mzigo wangu.
Alizitama zile namba kisha akasema ahaa, ni Mr Zuberi sio kakuambia uje uchukue?
Ndio nilijibu kwa mkato. Kisha nikapatiwa mzigo wangu na kuondoka.
Huyooo mpaka nyumbani, I love the shoes,, I love tha handbag… ziko kiwango. Nilicheka kisha nikasema ahaaa… kumbe nimemtosheleza mr Zuberi ee ndo maana ananinunulia vitu vya gharama. Nilikumbuka jambo,,, nilimkumbuka mke wa mzee zuberi, ni mama mwenye miaka kama 50 ama 52 hivi ama 55, hakuzidi hapo. Ila hajipendi hata kidogo, sijui ni umri ama ni nini. Nilijichekea nikasema sasa upele umepata mkunaji.