Nilivyoingiza 17.6M ndani ya mwaka mmoja na nusu, kwa biashara ya Mgahawa kwa mtaji wa kawaida kabisa

Na kwenyewe kule mkuu ungeenda ungetengeneza fedha nimetokako karibuni watu wenye migahawa ikifika saa 3 usiku huwezi kupata chakula na Ni mgodi mkubwa Sana !! Watu Ni nyomi utasema lowasaa kaitisha mkutano wa kuomba kura
Iko mkoa gani na wilaya gani hkk NYAMISHEGA
 
Kwa mtu ambae halijawahi kumkuta atabisha sana swala la kupotea kwa hela. Mimi pia nilikuwa na biashara ya chakula nilikuwa nauza sana na chakula kinaisha ila ikifika muda wa kufumga hesabu huna unachobaki nacho.

Kuna mtu aliniambia nitakuwa nasahau nikinunua vitu, basi nikamkabidhi kitengo cha chips na nyama choma. Siku ya pili kauza hajanunua chochote na asubuhi alikuwa na chenji za mauzo ya jana yake kama 50000 hivi zote zilipotea.

Location ya ile biashara ni nzuri sana ila shida ni kupotea kwa pesa. Kama hajakukuta utabisha mpaka kesho ilifika kipindi nikawa narekodi kwenye daftari kila sahani inayouzwa nione nakosea wapi.
 
Wewe sasa ndo umeelewa nilimaanisha nini.

Biashara haiwezi kwenda kichwakichwa au kwa kutegemea unayoyajua tu, huku mitaani kuna mabingwa wa kuharibu jitihada za watu kwahiyo bila kuwadhibiti hakuna hatuna unaweza kuivuka.

Hili huwezi kulielewa mpaka uingie ulingoni.
 
Biashara haiwezi kwenda kichwakichwa au kwa kutegemea unayoyajua tu, huku mitaani kuna mabingwa wa kuharibu jitihada za watu kwahiyo bila kuwadhibiti hakuna hatuna unaweza kuivuka.
Mimi nilikata tamaa nina miezi kadhaa nimeifunga biashara, maana mwisho wa siku unalipa hadi pango kwa kutoa hela nje na biashara, ila Mungu akijalia nitarudi tena maana ni biashara ninayoipenda.
 
Mimi nilikata tamaa nina miezi kadhaa nimeifunga biashara, maana mwisho wa siku unalipa hadi pango kwa kutoa hela nje na biashara, ila Mungu akijalia nitarudi tena maana ni biashara ninayoipenda.


Moja kati ya biashara nzuri ni hoyo maana haina trend wala misimu, ukipata muda rudi uifanye katika namna nzuri zaidi, naamini kuna vitu tayari umejifunza na hautavirudia tena.

Usirudi kabla haujaimaliza shida iliyokufanya ushindwe mara ya kwanza.
 
Moja kati ya biashara nzuri ni hoyo maana haina trend wala misimu, ukipata muda rudi uifanye katika namna nzuri zaidi, naamini kuna vitu tayari umejifunza na hautavirudia tena.

Usirudi kabla haujaimaliza shida iliyokufanya ushindwe mara ya kwanza.
Naomba nikutafute kama ulivyosema ( kama ilikuwa serious) mkuu nakupataje??
 
Moja kati ya biashara nzuri ni hoyo maana haina trend wala misimu, ukipata muda rudi uifanye katika namna nzuri zaidi, naamini kuna vitu tayari umejifunza na hautavirudia tena.

Usirudi kabla haujaimaliza shida iliyokufanya ushindwe mara ya kwanza.
Mkuu igombe vipi ulifanikiwa kufungua?
 
Naomba nikutafute kama ulivyosema ( kama ilikuwa serious) mkuu nakupataje??

Mawasiliano yanaweza kufanyikia hapa (kama haujali privacy) au PM (kama unajali privacy).

Namba za simu pekee ndio kitu ambacho huwa siwezi kutoa.

KARIBU.
 
Mawasiliano yanaweza kufanyikia hapa (kama haujali privacy) au PM (kama unajali privacy).

Namba za simu pekee ndio kitu ambacho huwa siwezi kutoa.

KARIBU.
Pm yako haiwezi kuanza kupokea meseji, naomba nitumie kwanza if its okay
 
Dah, hapa ulicheza vyema kabisa yani kidogo ukabidhi nyani shamba la mahindi. Biashara ni mtu mwenyewe, yani ukiweka ndugu, halafu ukawa kazi yako ni kupiga simu tu kama telephone operator lazima ulie.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…