Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

Nilivyokwenda Afrika Kusini bila kuwa na Ndugu wala Rafiki kule

SEHEMU YA SITA

Ile Asubuhi kabla ya Safari kuanza, Kuna wadogo zetu kama 4 wa umri kama wa Miaka 16/17/18 walipanda ndani ya Bus. Waliomba kwa Konda kuongea na Abiria. Walituambia kuwa na wao wanaelekea South Afrika ila nauli zao ziliishia pale Tunduma. Waliomba tuwachangie Nauli.

Wametokea Dar ila wamekaa pale Tunduma kwa muda wa wiki nzima wakitafuta nauli ya kuendelea na safari. Kwa hiyo walikuwa wanaomba tuwachangie nauli ili waweze kuendelea na safari. Tulianza kuwachangia, Mmoja wao alikuwa na simu akaiuza mle ndani ya Bus. Madogo walikuwa wamechangamka sana. Mpaka wanakwenda South kwa nauli za kuunga unga. Wenyewe kutumia Mwezi mzima njiani ni kawaida tu.

Akiba waliyokuwa nayo, pamoja na Michango yetu waliweza kupata nauli ya kuwafikisha mpaka Harare. Walisema wakifika Harare watakaa tena wiki nzima wakitafuta nauli ya kuendelea na safari. Hivyo tuliendelea nao na safari kwenye bus letu. Kwa kifupi mbele ya safari katika kupiga piga nao story tulikuja kujua kwamba kati ya wale madogo, mmoja wao ndio kiongozi wao, yeye alishawai kuishi sana South Afrika. Ilionekana kila akirudi kwao Manzese Tanzania, wakati wa kuondoka huwa anachukua Vijana wengine anaenda nao South. Yani kwa zile story za Madogo nilijiona kumbe ni mim tu ndo sijafika South Africa, Kwa maelezo yao ni kama vile Vijana wengi wapo huko tayari.

Ni kweli kwa pilikapilika za Vijana niliowaona pale Tunduma niliona ni kama Vijana wengi sana wanaikimbia hii nchi, kila mmoja akilalamika kuwa Bongo Maisha magumu.

Staili ya hawa madogo kusafiri ni ya kuunga unga nauli, hawa madogo walivyofika Tunduma walikaa hapo, sidhani kama Kuna namna nyengine walifanya ili kupata nauli zaidi ya wizi. Na wapo madogo wengine wengi wa staili hii.

Pia pale Tunduma sio Waburundi wote walifanikiwa kupita, kuna baadhi walikosa pesa ya kulipia Visa ya kuingia Zambia. Sisi watanzania tunaingia Zambia bila kulipia Visa. Hivyo waburundi ndani ya Bus walipungua

Kila tulivyokuwa tukiendelea na Safari ndivyo Lugha yetu pendwa ya Kiswahili ilivyokuwa ikipotea. Tulifika Lusaka Mji Mkuu wa Zambia saa tatu usiku. Tulilala hapo. Wengine tulishuka kwenda kupata Huduma za Chooni, Wengine ndo ilikuwa mwisho wa safari yao. Asubuhi kulivyokucha tuliendelea na safari yetu ya kuelekea boda ya Zambia na Zimbabwe inaitwa CHIRUNDU
 
SEHEMU YA SITA

Ile Asubuhi kabla ya Safari kuanza, Kuna wadogo zetu kama 4 wa umri kama wa Miaka 16/17/18 walipanda ndani ya Bus. Waliomba kwa Konda kuongea na Abiria. Walituambia kuwa na wao wanaelekea South Afrika ila nauli zao ziliishia pale Tunduma. Waliomba tuwachangie Nauli.

Wametokea Dar ila wamekaa pale Tunduma kwa muda wa wiki nzima wakitafuta nauli ya kuendelea na safari. Kwa hiyo walikuwa wanaomba tuwachangie nauli ili waweze kuendelea na safari. Tulianza kuwachangia, Mmoja wao alikuwa na simu akaiuza mle ndani ya Bus. Madogo walikuwa wamechangamka sana. Mpaka wanakwenda South kwa nauli za kuunga unga. Wenyewe kutumia Mwezi mzima njiani ni kawaida tu.

Akiba waliyokuwa nayo, pamoja na Michango yetu waliweza kupata nauli ya kuwafikisha mpaka Harare. Walisema wakifika Harare watakaa tena wiki nzima wakitafuta nauli ya kuendelea na safari. Hivyo tuliendelea nao na safari kwenye bus letu. Kwa kifupi mbele ya safari katika kupiga piga nao story tulikuja kujua kwamba kati ya wale madogo, mmoja wao ndio kiongozi wao, yeye alishawai kuishi sana South Afrika. Ilionekana kila akirudi kwao Manzese Tanzania, wakati wa kuondoka huwa anachukua Vijana wengine anaenda nao South. Yani kwa zile story za Madogo nilijiona kumbe ni mim tu ndo sijafika South Africa, Kwa maelezo yao ni kama vile Vijana wengi wapo huko tayari.

Ni kweli kwa pilikapilika za Vijana niliowaona pale Tunduma niliona ni kama Vijana wengi sana wanaikimbia hii nchi, kila mmoja akilalamika kuwa Bongo Maisha magumu.

Staili ya hawa madogo kusafiri ni ya kuunga unga nauli, hawa madogo walivyofika Tunduma walikaa hapo, sidhani kama Kuna namna nyengine walifanya ili kupata nauli zaidi ya wizi. Na wapo madogo wengine wengi wa staili hii.

Pia pale Tunduma sio Waburundi wote walifanikiwa kupita, kuna baadhi walikosa pesa ya kulipia Visa ya kuingia Zambia. Sisi watanzania tunaingia Zambia bila kulipia Visa. Hivyo waburundi ndani ya Bus walipungua

Kila tulivyokuwa tukiendelea na Safari ndivyo Lugha yetu pendwa ya Kiswahili ilivyokuwa ikipotea. Tulifika Lusaka Mji Mkuu wa Zambia saa tatu usiku. Tulilala hapo. Wengine tulishuka kwenda kupata Huduma za Chooni, Wengine ndo ilikuwa mwisho wa safari yao. Asubuhi kulivyokucha tuliendelea na safari yetu ya kuelekea boda ya Zambia na Zimbabwe inaitwa CHIRUNDU
andika story ndefu basi....hivi vipisi vinaboa mkuu


samahani kwa kukuita fala niliju story mbaya....

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom