Nilivyomkomesha tapeli wa viwanja Kivule Dar es Salaam

Nilivyomkomesha tapeli wa viwanja Kivule Dar es Salaam

NILIVYOMKOMESHA TAPELI WA VIWANJA KIVULE

Sehemu ya 3


KAMA NOMA NA IWE NOMA

Siku ya jumatatu asubuhi na mapema nikiwa na akili zangu za usiku nikatoka zangu Magomeni kuelekea pale Staki shari mapema tu moja kasoro kadhaa niko pale nikawakuta maaskari wanajipanga kwa ajili ya lokoo ya kuanza siku mpya na kulikuwa na kiongozi wao yeye akiwa amevaa combat kama za wale field force mtu mzima hivi mfupi na mweupe kiasi nikamngojea awakague wale maaskari na nikamwendea nikidhani ndio mkuu wa kituo nikamsalimu na kumuelezea changamoto zangu na akanambia yeye sio mkuu ila nipite pale kolidoni na nikate kulia nisome vibao juu ya milango na nikae nje ya mlango ulioandikwa MKUU WA KITUO,nikamshukuru na nikaingia ndani kufata maelezo niliyopewa,nilipofika kaunta askari aliyekuwepo akaniuliza ninapoenda na nikamuelezea ninapoenda,nikasoma vibao na nikafika eneo husika uzuri wake kulikuwa na kibenchi nikakaa pale kimya,sasa wakati nimekaa pale kumbuka maaskari wengi si wananifahamu wakawa wananiuliza kulikoni nikawa namngojea mkuu na nadhani katika wale maaskari walionikuta pale wakaenda kumtonya yule mpelelezi mzee Juma akaja pale anajifanya kama anaongea peke yake kuwa najisumbua tu uko ninapotaka kwenda nami wala sikumjibu kwani ilibidi nijiusie mwenyewe moyoni kwani nilikuwa na donge limenibana sana nikifikiria nadai changu naonekana msumbufu? Tena mtuhumiwa nimemkamata amempa dhamana alafu ananambia nikakae nyumbani hadi atakapopatikana eti ndio atanipigia,leo ananiona mimi ndio tatizo,nikajiambia nisifungue mdomo acha alopoke tu.
Mara akafika askari aliyekuwa amevaa kiraia na akatoa ufunguo na kufungua kile chumba na nyuma yake akiwa ameongozana na kundi la watu kama watano hivi na yule kiongozi akanisalimu huku akiwa ameshafungua mlango nami nikajibu salamu yake na akaniuliza tatizo langu maana yeye hakuwa na muda kwani alitakiwa kwenda uwanja wa ndege kusimamia msafara kuna ugeni unakuja kwahiyo lazima awepo eneo la tukio ila kwakuwa ni jumatatu anataka kufanya kikao kidogo na watendaji wake kupata details za yaliyojiri kwa wiki nzima iliyopita,wakati huo ananipa maelezo hayo tukawa yeye na mimi na wale wenzake tumeshaingia ndani ya kile chumba na akanitaka kama sitojali nimngojee hadi atakapotoka uwanja wa ndege ila nikamuomba sana anipe japo dakika 5 tu kwangu zingenitosha kujua hatima ya shauri langu naye akanipa!
Nikajitambulisha na kumueleza suala langu na aliyekuwa na faili na matukio yote toka kumkamata na hadi kuachiwa na kutakiwa nijae nyumbani hadi atakapopatikana mtuhumiwa na nikahitimisha kwa kumuomba kuwa "yeye ndio mtu wa mwisho katika kituo ambacho faili la kesi yangu lipo naomba kauli yako kuwa kituo kimeshindwa kutatua tatizo langu na unanipa ruksa ya kwenda mbele kusaka haki yangu" tena yule mzee Juma aliwa ameitwa na miongoni mwa waliokuwa pale kumbe kulikuwa na mkuu wa upelelezi wa kituo na maofisa wengine,yule mzee Juma anaulizwa hana analosema lenye mashiko na mkuu akawauliza "toka mmeanza kufanya kazi kwenu mmeshakutana na mwananchi mwenye uthubutu wa kudai haki yake katika mfumo huu? Huu ni mtego kwani kama ameweza kuja hadi kwangu je anashindwa kwenda wapi? Mtuhumiwa kamleta mmemtoa,mwendelezo hamtoi je afanyaje?" Yule mzee Juma akajitdmtea kuwa nitoe pesa ya mafuta ya gari ili waende kumsaka na yule mkuu akaniuliza je nipo tayari kutoa pesa ya mafuta? nikamjibu pale pale nishapoteza pesa na mtuhumiwa nishamleta sina hiyo pesa na huyu mpelelezi yeye kama kutoa ndio atoe kwani alijiridhisha akampa dhamana,sina hiyo pesa,yule mkuu akaona huu mziki sasa akanambia sara naomba japo siku 3 nitakupatia jibu nikamwambia poa ntakuja ijumaa na nikatoka zangu huyooo!
Ile ijumaa mimi sikuenda nikakaa kama wiki kadhaa ndipo huo msemo wa MUNGU SI ATHUMAN ukachukua nafasi tena kwani yule bwana Juma Kasangu akawa anaendelea na utapeli wake sijui walimtapeli mama gani uko waliuza nyumba yao ya familia uko Buguruni na yule mama akaenda kununua kiwanja na kwakuwa alikuwa na pesa tayari ujenzi ukaanza mara moja na mama ujenzi umefika kwenye rinta akaja kuelezwa kuwa eneo analojenga sio lake na kule jirani na eneo ambalo mimi nimeuziwa kulikuwa na eneo kubwa sana lilikuwa linamilikiwa na taasisi flani inaitwa UVIKIUTA sijajua wanajihusisha na nini na hawa kina Kasangu wakawa wanaenda kuwauzia watu viwanja kule na wale jamaa uwa wakifanya operesheni inakuwa kama vita wanakwenda kamili na field force na mabomu ya machozi kutokana na historia ya eneo lenyewe na asilimia kubwa ya wakaazi wa maeneo yale walikuwa Wakulya na kama unavyojua hawa ndugu zetu,tatizo kule mpaka wa wale Uvikiuta hakukuwa na mipaka yenye kuonekana wazi sasa unaweza kuwa hapa ukaambiwa upo nje pale ukaambiwa upo ndani yaani wanaweza kuja awamu hii ukaachwa na wakaja awamu nyingine ukatolewa mkukumkuku sasa wale kina Kasangu ndio wakawa wanatumia huo kutokuwepo na mipaka ya wazi kama njia ya kuwapiga wananchi.
Sasa kumbe yule bwana Juma Kasangu akiwa na vijana wake waliuza sijajua eneo gani na nasikia walipata kama milioni 8 hivi yule bwana akawa amewadhulumu wenzake na kati ya aliowashirikiana nao kuna jamaa anaitwa Chacha😂,huyu bwana nadhani alipewa namba yangu na yule Marwa kwani alinipigia siku hiyo sina hili wala lile akataka kuonana nami nikamuelekeza na akaja mara moja Ilala tulikutania pale Ilala mtaa wa Kigoma na Moshi kulikuwa na duka la Mangi,akanieleza mikasa mingi na kueleza waziwazi kuwa amesikia kuhusu ishu yangu na yule wamefanya tukio pamoja na amewazika yeye na wenzake sasa hasira zake anataka kuzihamishia kwa kumkomoa kupitia mimi,ule msemo wa "adui wa adui yako ni rafiki yako" ukachukua nafasi na akanambia jinsi tunatakiwa tufanye na yeye atafanya yake kadri ya uwezo wake na kazi alitaka ifanyike mapema iwezekanavyo nami nikimshirikisha mshkaji wangu mmoja anaitwa Kindamba na Kindamba akampigia Kasangu na kumwambia anataka eneo kwani amepewa namba kupitia rafiki yake,Kasangu akamuuliza kuwa anakaa wapi naye akamjibu kuwa anakaa Mwananyamala A na akamwambia atakuja jioni akitoka kazini ili aje aone maeneo (tulipanga iwe jioni kwa sababu mbalimbali nazo ni kuweza kufika eneo wakati ofisi za serikali ya mtaa kumefungwa,mimi kutoonekana kwakuwa giza litakuwa lishashuka na kuepusha wambea kuwa wengi na kupata kujipanga vyema)


Itaendelea...
"Your enemy's enemy is automatically your best friend"


🙇
 
NILIVYOMKOMESHA TAPELI WA VIWANJA KIVULE


Sehemu ya 6


UTAJUA HUJUI

Yule mshkaji wangu wa Singida dah nilimuonea huruma kwani alijuta kuniunganisha katika lile jambo na akawa amemueleza mshkaji na mshkaji akawa anajitetea kuwa mara nyingi ninapompigia anakuwa kwenye maombi au bize kupitia kesi ambazo yeye akiwa kama mkuu wa mahakama pale aweze kuzitolea ripoti,nikamtumia ule ujumbe wa tigo pesa na yeye nikamwambia sikublack mail ila tambua simamia tulichopatata na najua umekula pesa wewe na wazee wako wa baraza sasa mimi ntakuja kuitoa kesi hapo kuipeleka mbele kwakuwa sina imani na mwenendo mnaoupeleka dah jamaa akaniomba sana msamaha ndio nikawaza inawezekana mtu akisema hana imani na mahakama husika waliopo pale kunawaletea picha chafu basi sasa ule mramaha wake ndio kama ulimponza sasa nikawa hakimu mimi yeye ndio mshtaki😂😂 na nikamwambia nataka siku ya date mshtakiwa awepo sijui utampataje na akubali kosa na alipe changu (hapo nshaclaim gharama zote zimefika M3.3) we bwana pema hapa ninapohadithia siku ya siku nimekaa benchini mtuhumiwa kaja na ndugu zake wawili wakike na wakiume wakaniita nje wakaniomba sana sana nikawambia nyie wekeni m3.3 ubaoni mi nabwaga kesi wakawa wanataka wanipe kwa awamu tena kianzia laki 5 nikawaambia kampeni hakimu hiyo pesa mi ninataka nipoteze tu wakatoka wamelowa! Muda wa kesi tukaitwa na alipoulizwa alipokuwepo akadai alikuwa anaumwa nikanyoosha mkono naomba kupata vielelezo vya hospitali akasema alipelekwa kwa mganga! Dah dunia hii nyie acheni,mheshimiwa akapotezea akaendelea na kesi mara mtuhumiwa akanyoosha tena mkono akamawambia hakimu yeye amekubali kosa na yuko tayari kunilipa ila sio hiyo pesa yote kwani mimi nilimpa yeye M2 tu (alijichanganya wakati mimi nimempa M1.3 na vichenji,sikuwa nimemalizia) na ananiomba twende mimi na yeye kule site kuhesabu gharama zangu za ujenzi kujua gharama halisi nikakubali na kesho yake nikatakiwa kwenda nae kule kwa mama Anna Mkapa.
Asubuhi nampigia kujua tunakutanaje akanambia wala nisiende yeye kaamua atalipa tu hayo madai yangu anaona tutasumbuana,nikaendelea na shughuli zangu kusubiria siku ya kwenda kule mahakamani.Siku ikafika na muda wa kuingia tukaitwa wakati hakimu anatuuliza natoa maelezo akanikana na kusema yeye hajaniona wala sijampigia dah kama mtu ameiona ile sinema ya kihindi ANDHAL KANOON ndio nilikuwa natamani pale Amita Batchan alipomshindilia bisu yule mzee ndio nilitamani nifanye pale yaani nilitoa maneno ambayo wote pale walibutwb nikamwambia "mheshimiwa naona danadana zimekuwa nyingi sasa nasema mbele ya mahakama hii nikijua wazi kama kutamka maneno ya kutishia kudhuru ni kosa kisheria ila hadi muda huu huyu jamaa keshaharibu maisha yangu,utu wangu,muda wangu na anaendelea kuniletea dharau sasa kwakuwa kadhamilia kuharibu maisha yangu basi ingawa sijawahi kuua ila huyu jamaa familia yake haitokaa salama nipo tayari kwa lolote kutoka sasa na wewe nakuachia ukumbi hukumu hii kesi kwa mizani yako unayoona sawa" dah hakimu jasho linamtoka na yule bibi akadakia unatishia mbele ya mahakama,kiujasiri nikamjibu simtishi na hii kesi ndio itakuwa yake ya mwisho kuja hapa wakati huo sio yeye wala mimi tunaojua litakalotokea! Bibi ananitizama huku natetemeka nasema kama mbwai iwe mbwai!
Hakimu akawa ananiplease kaka acha hasira,acha hasira haki yako utaipata ndugu haya yanazungumzika nikamjibt mimi sitaki huruma ya mahakama wewe toa hukumu tu,akawa anamwambia Kasangu ndugu unasikia hayo maneno? We unayaona yanatoka tu mdomoni na unadhani kutakuwa hakuna utekelezaji? Please mpe pesa yake tusije kuingia matatizoni wote,Kasangu akawa kakaa kimya na mheshimiwa akapiga date ndefu kama mwezi kamili!
Sasa wakati tunatoka ukiwa unaelekea pale kituoni kupanda daladala mimi na ndugu yangu yule Juma Kasangu akawa nae anakuja na ndugu zake akawa ananiambia "mtani mtani we mtani wangu bwana usikasirike ebu njoo tuyajenge bwana" haloo ilinitoka ngumi hiyo Juma chini! Nikamtimba kifuani yule ndugu yangu akanipush nikamponyoka nikawa namfata tena kuendelea kumchapa akanyanyuka akawa anakimbia kurudi kule mahakamani yeye mbele mimi nyuma hadi kati viunga vya mahakama akadumbukia ndani mimi nikageuza nikaondoka zangu wale ndugu zake wananitizama tu wanaogopa hata kufunua midomo yao.
Usiku hakimu akanipigia ooh kaka usifanye hivyo punguza hasira nikamwambia kavukavu nyie kuleni pesa ila mtajua tu siku moja uchungu tunaoupitia tunaodhulumiwa, akaniomba sana nikamwambia haki isipotendwa ama zake ama zangu na huyo fala.
Baada ya mwezi tukaenda tena mahakamani Juma hajaja,ikapigwa date hajaja tena,date ya tatu ndio kama alafu sasa anasema atalipa kwa awamu sita nikasema pesa yangu haikuwa mkopo nataka yote kila mtu akaendelee na hamsini zake na hakimu akamsisitizia kama amekubali kulipa alipe yote kikubwa atoe tamko ni muda gani,nikadakia iwe ndani ya mwezi (natamba mie tena hakimu na mtuhumiwa wote wapo kiganjani)wakakubali hivyo nikapewa tarehe kama ile kwa mwezi unaofuata,tukatakiwa twende kwa mhasibu wa mahakama kwenda kuandikishiana kumbe wakati wote huyo mama mhasibu alikuwepo pale mlangoni anafatilia tena ile kesi ikawa ikifika muda wa kusomwa ingawa ilikuwa inasomwa chumbani watu wengi walikuwa wanajaa hadi hakimu anawaomba wapungue pale mlangoni.
Tulipofika pale yule mama mhasibu akawa ananiambia "wewe mjinga badala ya kuchukua hata kidogo kidogo unakataa,utasumbuka" nikamjibu "mama fanya kazi yako kitengo chako cha hesabu pesa hauna shea nayo mama yangu"
Akakaa kimya akatuandikia maelezo nikaondoka zangu.
Mwezi uliofata nikatimba eneo la tukio na mwanangu tukahesabiwa mpunga wetu alafu yule mama mhasibu akawa ananambia "sinywi hata soda" nikamjibu "mama we nisamehe tu mimi sidili na upande wa upinzani" akanipa makaratasi nikasaini nikatia pesa kwenye begi nikaenda na kwa hakimu kuna makaratasi nikasaini nikatoka na mwanangu hao,nikampigia Chacha nikamuukiza nikulindaje akasema wewe usijali nipe 50 kibingwa na yule Marwa nikamtia 50 nae nikasepa zangu

IMEISHA HIYO

NB:Yule hakimu miaka michache mbele alikamatwa kwa kesi ya rushwa na hadi leo hajarejeshwa kazini kwakuwa malakamiko yalikuwa mengi sana juu yake tena ni rafiki yangu fb eti nae anaweka nyimbo za mapambio kujifanya mwema😂😂 kuna siku nikacomment katika moja ya post yake "PRACTICE WHAT YOU PREACH!" Ila kitambo sijamcheki kama bado anapost post na akiendelea kupost kujifanya mwema mtamuweka hadharani NWAMA YULE! MLA RUSHWA NA MPOTEZA HAKI ZA WATU! (nilitaka kuandika za wanyonge nikajipima nikagundua simo kundi hilo)

IMEISHA WANDUGU!
Mtoa mada umeshawahi kusimama mahakamani kweli wewe?, eti Hakimu akakuplease mbona huwa sio taratibu kwa kauli zako hapo mahakamani na utovu wa kutii mahakama ungefungwa japo wiki mbili, sijui kama kweli unaifahamu korti wewe.
Simaanishi napinga kisa chako hapana ispokuwa umeongeza ujasiri ambao haupo hasa kwenye mahakama zetu.
 
Huwa nachukia sana napoona et "itaendelea"
Yaani hovyo kabisa
Watu wengine uwa mnawalazimisha watu kuwatukana na kututaka tuonekane watovu,hivi umesoma hadi kikomo cha post za mbele? Jiheshimu na usinifananishe na hao mie watofauti sana tena ukitaka kujua robo tu ya nilivyo soma hii thread kwa kituo utanijua kiasi,usinilinganishe na wengine ndugu! Jiheshimu kama mimi nilivyowaheshimu wasomaji wangu!
 
NILIVYOMKOMESHA TAPELI WA VIWANJA KIVULE


Sehemu ya 4


USIKU WA DENI ULIPOFIKA


Ilipofika mida ya saa 10 yule bwana Chacha akiwa ameshatangulia kule Kivule na maskani yao hasa ilikuwa pale Kivule njia panda ya shule kuna kipub yule Kasangu alikuwa amekifungua na mara nyingi amekuwa akipatikana hapo ndipo bwana Chacha alipopapanga kama eneo la kufanyia tukio na sisi huku tukawa tunajipanga na nikamfata ndugu yangu flani ambaye alikuwa anafanya shughuli ya ufundi wa magari anaitwa Meddy ambaye alitutaka kuweka mafuta kwenye gari na tungekwenda sote yaani mimi,Kindamba na Meddy kuelekea Kivule,ilipofika muda wa saa 11.30 tukatoka kuelekea uko na katika majadiliano ikaonelewa mimi nishukie eneo linaloitwa Bambucha na wao wangekwenda wenyewe kupitia mwongozo wa Chacha ambaye alishakuwa tayari ameshafika kule Kivule na walipofika pale wakiwa wanawasiliana na hatimaye kukutana naKasangu wakamtaka awapeleke kwenda kutizama maeneo na kuyakagua na ikiwapendeza ndio wakae chini kujadili bei na namna gani ya kufanya malipo sasa yule Kasangu wakati wa kutakiwa hivyo akawa anataka kuwapa vijana wake ndio wawapeleke wale jamaa zangu na akawa anataka kupanda pikipiki ambayo ilikuwa imepaki pale kwenye pub yake ndipo yule Kindamba akamfata na kama aliyepatwa na machale Kasangu akashuka na kuanza kutoka mbio nasikia wakaanza kumkimbiza na akaenda kujikwaa kwenye kisiki na mguu wake mmoja ukawa umejeruhiwa na damu ikawa zinamtoka sasa yule Kindamba akawa anaact kama yeye ni askari akamwambia kimbia nikumwage ubongo na akawa anaomba msamaha na akawa anagugumia na kuka chini,wakambeba msobemsobe na wale kina Chacha wakawa wanawauliza kina Kindamba imekuwaje tena?😂 wakawaambia kuwa huyu ni tapeli na tunaondoka nae na mtaenda kujulia uko Staki shari,sasa yule Kasangu hadi anakamatwa pale hakuwa anajua amekamatwa kwa kosa alilomtendea nani kwakuwa ni mtu wa matukio sana na akawa anaumiza kichwa hawa ni wa nani niliyemtapeli? Wakamtia garini na kuelekea nae Staki shari na wakanipitia pale Bambucha sasa wakati wanasimama na mimi kupanda dah jamaa alichoka sana akajisemea moyoni kweli huu mziki niliouingia safari hii HAPATOSHI!
Nikapanda garini na akawa ananiomba sana awapigie ndugu zake kujua namna gani tunalimaliza lile shauri nje ya polisi,nikamwambia sina njia yoyote zaidi ya kutaka pesa yangu na kama anaendelea kuzingua polisi itamuhusu tena nikamwambia nataka hao matapeli wenzake salama yake walete M3 kamili ndio nimdamp sasa toka saa 1 usiku hadi saa 3.30 tumepaki gari pale ukivuka reli ya njia panda ya Segerea,ilipofika 3.30 wakiwa wenzake wawili wamekuja mmoja akijitambulisha kama mjomba wake😂 kumbe tapeli mwenzake anajifanya kutoa viapo hapo wee nikawa najiambia wewe apa miungu yako yote huyu atafika eneo la tukio kama hamtatoa pesa yangu,baada ya kuona sound zimekuwa nyingi nikamtuta yule bwana hadi Staki shari na kufika kaunta askari anaanza kunifokea mbona umemuumiza bila ya kuhoji imekuwaje (alikuwa anajuana nae akataka kunitingisha) nikamwambia muulize mwenyewe imekuwaje na Juma akamwambia alikuwa anakimbia akajikwaa ndio akaniuliza tatizo nami nikamueleza akanitaka nimpe RB# nikatoa kitochi changu cha Nokia upande wa meseji kwenye draft uwa nasave baadhi ya vitu vyangu muhimu na namba hizi nilizisave huku,nikampatia atamzungusha na kumuweka selo akanitaka nifike kesho yake asubuhi,nami nikatoka pale na nikamjuza kwa simu yule mzee Juma kuwa mtuhumiwa yupo pale na ninaondoka zangu
Asubuhi na mapema nikafika Staki shari nikamkuta yule mzee amenuna hata sikujua kwanini akawa ananambia nenda Madafu uko ukamalizane na jamaa yako (Madafu ni mahakama ya mwanzo Ukonga inayohudumia maeneo yale yote)mi nikatoka zangu nikaelekea kule mahakamani muda kama wa saa 2 hivi gari la kubeba watuhumiwa likawa limefika na nikawa nimekaa pale niko mwenyewe tu,watu wakawa wanaitwa na wenye kuachiwa kwa dhamana wanaachiwa,wenye kushinda wanaondoka na wenye kufungwa wanafungwa hadi mida ya saa 8.30 ndio tunaitwa kumbe pale utaratibu wao flesh case zote wanaziweka mwisho,njaa inaniuma ila hata kwenda kujiibia kwenda kula naogopa isije akaitwa nami sipo eneo la tukio,wakati naelekea mahakamani asubuhi kutoka Staki shari kuna mshkaji wangu mmoja yeye ni hakimu uko eneo flani mkoa wa Singida (naomba nisitaje eneo kumuhifadhi) huyu ni mshkaji wangu sana tumefanya mambo mengi ujanani ya hatari na mazuri sasa nikamvutia uzi kumpa habari kuhusiana na hii ishu akanambia bob we nenda pale hakimu mfawidhi wa pale mwanae sana wamesoma wote intake moja uko Lushoto mambo ya uhakimu nikamwambia poa Imeisha hiyooo!!
Tumekaa pale mara tukaitwa ndani katika kichumba alikuwepo hakimu na wazee wawili wakike na wa kiume ambao ni wazee wa baraza (walaaniwe wale wazee) na mdada aliyekuwa akichukua maelezo tuliyokuwa tunayatoa pale na mheshimiwa akaletewa faili na yule mdada na akatuita majina kuhakiki kama ndio kesi husika na waliopo mbele ndio wahusika wenyewe na alipojiridhisha akamsomea shtaka yule Kasangu na akakana pale na mheshimiwa akaaghilisha kesi kwa muda wa wiki 2 toka siku ile na wakati anaaghilisha palepale nikamuuliza jina lake akanitajia,kumbe ni yule yule mwanae mwanangu nikajua MBUZI KAFIA KWA MUUZA SUPU! nilijidanganya!😂


Itaendelea!
Mwamba Hauna mbambambaa kabisa!
safi sana👍
 
Watu wengine uwa mnawalazimisha watu kuwatukana na kututaka tuonekane watovu,hivi umesoma hadi kikomo cha post za mbele? Jiheshimu na usinifananishe na hao mie watofauti sana tena ukitaka kujua robo tu ya nilivyo soma hii thread kwa kituo utanijua kiasi,usinilinganishe na wengine ndugu! Jiheshimu kama mimi nilivyowaheshimu wasomaji wangu!
Sawa sawa
 
Hahahaaa...mnanitamanisha kujuaaa ya mbelee lol Ngoja niendelee niwafikie
Komaa kwani mie nimekomaa kuiandika leo tu tena kwa kutumia simu nilikuwa naandika napost whatsapp,naandika napost uko hadi nilipopata 4 ndio nikawa napost moja moja
 
Haya mambo ya viwanja nishawahi kutaka kumuua mtu tena ni dalali mmoja fala hivi alikua mshikaji wangu tena mkurya ila nilichomfanya hatokaa asahau hadi siku anazikwa!!
Mwaga thread watu wapate elimu
 
Hakuna ku waste time Mambo ni mengi ausio!! Safiii hio[emoji106]
Jamaa hadi aliwaelezea wadau wake kule kuwa dah sijawahi kuwa na pambano gumu kama la yule jamaa,nimepiga misumari wee wapi kumbe hajui UCHAWI HAUENDI KWA MENTALI! kuna siku mahakamani alitaka kunichota nyayo mchangani nikamwita nikakanyaga,nikamchotea mchanga nikampa,akawa ananitizama tu MAE!
 
Back
Top Bottom