Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Kuna watu wanasoma kama story halafu kunawengine tupo darasani🤝

Kwahyo ukiwa unaeleza kwenye mafunzo elezea kwa kina, maana kuna watu tunajifunza na kuingiza kwenye utendaji


Mfano juzi.... Baada ya kusoma uzi hapa, na mm nikaenda kuwaita hawa marohani niliorith kwa mzee wangu (nikapanda juu kwenye uwazi sehem ilotulia kwa mbaramwezi, si nikawaita bhana........... Maana nishawazoea kila siku lazima waje karibu muda wote nikiwa pekeangu wanapenda kuja

Sasa juzi nikawaita huku nawapiga beat,,,,, leo staki mje kimyakimya nataka mje muongee hapa au niwaone live😁😁😁😁

Bwama weeeh si upepo ukaanza kuvuma pale,,,,,, nikaanza kuwaza kimoyomoyo "Leo yule jamaa wa Jf kaniponza😂😂😂😂"


Ila walikuja lakini sikuwaona wala hawakusema chochote.... Nikashuka zangu huyooooooo safari🚶🚶🚶
Labda wameona utaogopa. Mimi sijawahi kuona upepo wakija. Au kipupwe tu hicho?
 
Arsis ni kiumbe wa ajabu sana, kuliko tunavyofikiria. Ndio maana ananishikilia sana nimuelezee mafundishpo yake.

Hivi nimeanza tu, intro ya nilipoanzia mimi , sasa nimeingia intro ya Arsis alivyokutana na babu yangu. Tukitoka hapo ndio tutaingia "vionjo vya Arsis". hapo kuna mengi na matamu sana.
Mm nililetewa mwanamke wa kijini ndotoni na babu zangu waliokufa miaka mingi,Mwanamke alijitambulisha kwa jina la Aisha bint Afrit.Alinipa na pete kabisa nikawa naivaa ila baadaye niliitupa nikaachana naye.Ila ajabu sasa siku moja alikuja ndotoni akaniambia kwamba nilimzalisha nikamtelekeza,aliniletea mtoto aje kunisalimia,alikuwa mtoto wa kike mwenye miaka kama sita hivi mzuri kweli.
 
Naona kataa ndoa kaingia😂😂😂.... Kwahyo huyo jinn sahivi ni single mother 🏃🏃🏃

(Natania...
Mm nililetewa mwanamke wa kijini ndotoni na babu zangu waliokufa miaka mingi,Mwanamke alijitambulisha kwa jina la Aisha bint Afrit.Alinipa na pete kabisa nikawa naivaa ila baadaye niliitupa nikaachana naye.Ila ajabu sasa siku moja alikuja ndotoni akaniambia kwamba nilimzalisha nikamtelekeza,aliniletea mtoto aje kunisalimia,alikuwa mtoto wa kike mwenye miaka kama sita hivi mzuri kweli.
 
Naona kataa ndoa kaingia😂😂😂.... Kwahyo huyo jinn sahivi ni single mother 🏃🏃🏃

(Natania...
Hapana kiongozi mm haya mambo siyajui kiundani.Maana walikuja babu zangu wanne ila wameshakufa kitambo,na ndani ya hao mababu niliyemtambua ni mmoja tu ambaye ni wajina wangu yaani aliyenirithisha jina,wakiwa wameshika mwanamke mrembo kama mwarabu hivi,wakanikabidhi wao wakasepa,baada ya hapo ndo tukaanza kufahamiana.Yeye alikuwa anakuja ndotoni tunasex sana tu ila kilichokuja kuniudhi ni yeye kutotimiza ahadi yake ya kunikabidhi hazina ya almasi na dhahabu kama alivyoniambia yy ni sex tu,so nikaamua kuitupa na pete aliyonipa ila akaendelea kunifuatilia ila mm nikampotezea tu
 
Mm nililetewa mwanamke wa kijini ndotoni na babu zangu waliokufa miaka mingi,Mwanamke alijitambulisha kwa jina la Aisha bint Afrit.Alinipa na pete kabisa nikawa naivaa ila baadaye niliitupa nikaachana naye.Ila ajabu sasa siku moja alikuja ndotoni akaniambia kwamba nilimzalisha nikamtelekeza,aliniletea mtoto aje kunisalimia,alikuwa mtoto wa kike mwenye miaka kama sita hivi mzuri kweli.
Hongera sana.

Hao wachawi wanacheza na akili yako.

Nakuahidi, hakuna mwanamke wa kijini mwema atakaefanya hivyo hata siku moja. Usiwajaribu.
 
Itakuwa kweli ni kipupwe 😂😂😂😂😂😂😂

Labda ndo huo uoga....maana pale hata angekatiza panya ningesema ni jinn
(Dah haya mambo yanahitaji roho sana
Endelea kuusoma uzi, utaelewa namna ya kuwaita ili waje kama wapo na kama hawapo watakuja wengine wakueleze ukweli. Ukiwaita hawana sababu ya kujificha.
 
Inatokea post namba 228.

Arsis; Siku ilipofika wakakutana tena, babu yako, Jini bakora na Mzee Mgunya. Baada ya kusalimiana.

Mabruki; Kuna yepi mapya jamani?
Jini Bakora: Mimi nina mapya mengi mazuri tu.

Mzee Mgunya: Anza tu, mimi pia kuna nilioyapata lakini naona ni katika hayohayo yako.
Jini Bakora: Ndio, tulikua tunawasiliana sana na kupanga na majini wako na majini wengine wa Mbruki. Kilichokuwepo sasa ni hiki, kapatikana jini wakuweza kupata chupa aliofungiwa huyo mtu, ni kama tulivyosema sema mwanzo, ipo hapa duniani, inalindwa sana, lakini haimshindi huyo jini kuchukua, kinachomshinda ni kufika tu ilipo, lakini jini wa Mgunya kasema Mzee atatusaidia kwa hilo. Sheikh Mgunya nadhani ni hayo yaliopo kwa sasa.
Mgunya; Na wewe Mabruki sema.
Mabruki; Mimi nimepata habari na mimi katika maongezi ya majini yangu wamesema walikua na nyinyi na kazi yangu itakua ni kuichukua hiyo chupa huku nasoma Qur'an mfululizo, nikisha ichukua niipasue kwa utarartibu wako ili uhai ulio[o ndani usife, kisha vilivyobaki nivivunje na hio chupa na niichome moto. Hakuna jini ataeweza kufanya hivyuo isipokua mimi kama binafdam, kwa kua majini walioiwekea ulinzi na mitego hio chupa hawakulenga binadam walilenga majini wengine wasiwweze kuibeba ilipo.

Jini bakora; Sawa kabisa mabruki, ndio namna hio.
Mgunya; Mimi nimefahamishwa yote na nitakchokifanya nitaivuta ardhi iliopo hio chupa itasogea mpaka tunapopataka, ikionekana tu chupa, iwahiwe haraka sana ndani ya chini ya dakika moja iwe imeshafunguliwa na imeshateketezwa. Lakini jamani, kama kuna binadamu wanahusika watakaputika maana majini waliopewa ulinzi watauliwa wote na majini wenzao na wakubwa hawatakubali, sote tupo mashakani kwa vita kali na majini wa kishetani.
Jini bakora; Hilo nimeongea na wakubwa wengi wa kijini, wamesema watatoa ulinzi kwa kiwangi fulani kwa heshima yetu, lakini kwa bahati nzuri kabisa, kuna jini mmoja mkubwa sana anaejua kisa cha kugfungwa huyo mtu, ni kua akitoka kifungoni ana uwezo wa kuzuia vita na machafuko. Nilipomuuliza kivipi? Akasema atasema mwenye akifunguliwa, mimi siwezi kumsemea, kwa sababu anaweza kua hana tena hizo nguvu.
Jini bakora: umesikia Mabruki, kunamawili tumfungue atoke bila kufahamu uwezo wake aliokua nao kabla ya kufungiwa kama anao tena, na kuomba Mwenyezi Mungu kua atakua sio msaliti. Sababu zake za kufungwa ni wema wake sio usaliti wake. Najua unataka kuuliza kwanini alifungwa, mimi sifahamu, kama hatodhurika ataeleza yeye mwenyewe.

Kwa upande wangu naona kazi ifanyike mapangoni kwetu, mabruki unajua vizuri, lakini wewe Mabruki ukachukue ile sehemu inyozunguka mapango haraka sana ili mapango yawe kwenye himaya yako. Pale hakuna mwenyewe ila kuna wenyeji wawili watatu kwa mbali kidogo, wamehamia tu, sio watu wa asili ya pale, watu wa asili ya pale. pale hakai mtu sisi hatuhusu, binadam wanafanya fujo sana.

Mabruki; Hilo halina tabvu, tena ile sehemu niliipenda, kila navyokuja mapangoni naitamani sana.

Jini: haya fanya hivyo, ukija niiute tukaweke mipaka, halafu fanya karatasi za shamba ziwe zako na wale wote hamisha pale ndani ya mipaka yako, wake nje. Hakuna tabu, wale hawapo pale muda mrefu, hawana makaburi pale, sisi tiuytakuonesha mipaka.
Mgunya: Mikiwa tayari mimi nipo tayari wakati wowote.

mabruki; Mimi nitakuja Jumapili ijayo niangalie mipaka, nigtakuja na mwanangu.
Jini bakora: usije na mtu yoyote, hii vita kubwa, usihatarishe maisha ya mtu mwingine. Ile ile mwenyeji itakusaidia wewe. Chukua chokaa mingi, ile taweka alama, halafu sisi takufahamisha ufunge vipi mipaka.
Mgunya: hta mimi nitakupa ujuzi wa kugfiunhga mipaka niujuao.
Jini bakora: haya, takua na ulinzi aina ya mipaka. fanya bidii sana.


Arsis; basi ikawa kama walivyppanga, Babu yako akaemnda akaweka mipaka, akaambiwa awe anakwenda kupanda migti ya kudumu kwenye mpaka, akapewa na migti mingine anaayoijua Jini Bakora. Yyule ni mataalamu sana wa miti na tiba zake zote ni za miti, majani, mizizi n vitu kama hivyo.


Wakati SArsis anaendelea kuongea tukasikia adhana ya alfajiri kwa mabli, nikamwabia kumbe tumekaa sana.

Arsis; Washa gari yako nenda kasali ukimaliza rudi hapa, leo mpaka tumalize hii habari, maana unasema mimi napiga chenga.

Mimi: Arsis, wacha niende tukutane tena usiku, mimi leo nalala tu, sijategemea kama tutafika mpaka saaa hizi.
Arsis: Siku nyingine usiseme mimi nakupiga chenga. Haya kwa heri usiku ikiniita mimi nitakuja.

Tukaagana nikaondoka zangu.


Itaendelea.
 
1. Mahojiano na Arsis

Yafuatayo ni mahojianao yangu (nitajiita simba kuanzia sasa) ambayo sio ya kwanza kati yangu na Arsis, lakini nimwyaweka namba 1 kwa kua nahisi yataleta mpangilio mzuri wa mahojiano yatakayofatia.

Mimi; Arsis, Arsis, Arsis, upooo?

Baada ya kumwita ikapita kama nusu dakika hivi.

Arsis; Nipo Simba, vipi hali yako?
Mimi; Mimi mzima kabisa na wewe?
Arsis; Mimi nipo salama namshukuru Muumba wetu.
Mimi; Arsis, leo nina swali moja tu, nataka nikuulize utakaponijibu ndio naweza kua na maswali mengine.
Arsis; Uliza Simba.

Mimi; Arsis kuna siku nilikuuliza wewe umejuana vipi na Babu yangu, nikahisi kama kuna vitu umenificha hukunieleza vyote. Ulinielezq umefahamu kupitia Jini wa bakora, nikahisi umenip9ga [piga chenga. Leo nieleze bila chenga, tumeshakua marafiki muda sasa.

Kabla ya kujibu Arsis akacheka kma mtu aliyefurahi. Naomba kusisitiza hapa, Arsis ni kiumbe mmoja ambae ukiongea nae utaona raha sana, hacheki kwa majivuno au kwa kebehi, unamhisi anacheka kwa kua anacheka kweli.

Arsis; Sikiliza, leo umenifutrahisha sana, nilikua nanhgoja siku uwe serious kama leo ili unielewe vizuri. Nilikiua nakuhisi kama ninayokwambia yanakuingia na kutoka. Nisikilize kwa makini.

Simba, mimi nilikua kifungoni kwa miaka zaidi ya 900, mndio ni 925 alaiejitahidi mpaka nikafunguliwa kifungojni ni babu yako kupitia jini wa bakora. Simba nataka uelewe, jini wa bakora ni jini mwenye heshima sana katika majini. Nafahamu kua ukoo wake walikua na uhusiano na ukoo wa babu yako, yaani ukoo wako kwa baba yako kwa muda mrefu sana., karne nyingi sana, vizazi na vizazi, lakini ni wachache sana katika ukoo wenu siku za nyuma wakaweza kukabidhiwa bakora kama uliopewa wewe. Wote wengine waliopewa bakora au wanapewa bakora za ukoo tu, lakini babu yako alipewa bakora kutoka kwa mwenyewe jini bakora, lakini liitengeza, sio ya kurithi. Bakora ya jini bakora ya kurithi kwa wazeewake ni ile uliopewa wewe tu. Ile bakora kuwepo tu kwako ni kinga kubwa na heshima kubwa sana kutoka kwa majini wote watakao kuona nayo. Nakushangaa wewe umeifungia chumbani.

Miimi; Nimeiweka Arsis, siwezi kutoka na kutembea nayo kila mahali.
Arsis; Nafahamu hilo na Jini bakora anafahamu hilo, dunia ya siku hizi hambebi bakora kama zamani, ni watu na makabila machache sana yenye kujua thamni ya mwanamme kubeba bakora. Mimi nakwambia jizoeshe kua nayo katribu zaidi ile bakora. Usiwe na wasi wasi, Jini bakora hasikii haya maongezi yetu wala hawezi kusogea hapa kusikiliza tunachoongea, tunaheshimiana sana.

Mimi; Arsis; Unaanza kunipiga chenga tena? Hujajibu swali langu.
Arsis; Tafadhali tumia lugha nzuri ukiongea na mimi, kqnza mimi ni mtu mazima sana kwako kwa kiwango chochote kile, halafu mimi ni Mwalimu wako. Acha lugha hizo mitaani. Sikupigi chenga, nipo katika kukujibu swali lako lakini nataka uelewe kwa undani zaisi, fanya dsubira.
Mimi; Samahani, unajua lugha zetu za siku hizi, Nitakua mwangalifu.
Arsis; Usijali Simba. Nisikilize kwa makini. Babu yako alikutana na watu kutoka Pemba wakati anaishi Tanga, hao watu walikuja kutafuta mali za Mjetrumani, miaka mingi sana nyuma.
Mimi: Hujui mwaka gani?
Arsis; Najua ilikuwa mwaka gani, ni mwaka wa 1072 kwa miaka ya dunia ya kwanza, hii dunia tuliopo. Hawa watu, alikua ni kijana mmoja ambae alihadithiwa na babu yake kabla hajafa, kua Tanga, nje kidogo ya mji kuna mali ya Wajerumani imefukiwa. Babu yake alimwabia na yeye kahadithiwa na rafiki yake ambae ameshfariki, lakini ameandika jina ya hio sehemu na alama zilizowekwa. Aliambiwa kua asijaribu kwenda boila kutafuta mwenye nguvu za majini na mwenyeji wa Tanga. Bila hivyo itakua ni hatari sana. Ataekwenda tu bila ulinzi wa nguvu za majini anaweza kufa.

Huyo kijana ndio akaanza kutafuta mtu mwenye nguvu hizo kwao Pemba, wapemba kila akiwaambia au wengine wanadhatrau hio habari au wengine wanaogopa. Ukapata mtu mmoja akamwabia kuna mama wa Kipenda yupo Darisalam, anajua kua huyo mama ana majini wakubwa anawatumia kwa kuondoa matatizo ya watu. Ndio kafunga safari akaja Mjini Dar. Akafanikiwa kumuona huyo mama, huyo mama kweli alikua na majini wakubwa sana na anapandisha kichwanikwake. Walipokuja wale majini wakasema sisi hatujui kuhusu hizo mali lakini kuna mganga mmoja yupo Tanga, huyo mganga ni mtu wa Lamu, Mgunya lakini anaishi Tanga, yeye ana majini wakubwa wa kutokea Tanga wanaweza kujua Yule jini wa mama akawapa anuani mpaka mtaa watakapompata huyo mganga wa kigunya, alikua barabara ya tisa, karibusana na sokoni pale Tanga.

Yule mama wa Kipemba hafanyi ile kazi yake peke yake, yeye anapandisha jini lakini mtu anaetafsiri na lazima anakua karibu yake ni mume wake. Yule mume akasikia kisa chote kile akawa na yeye kapata tamaa ya mali.

Mimi; Arsis kumbe ni mtu wa mikasa mingi wewe.
Arsis; Leo umesikia mali ndio unasikiliza kwa makini? Subiri nimalize, usije kusema nakupiga chenga, nyamaza usikilize mpaka nimalize, usitie neno lako.
Mimi; sawa Arsis, mbona leo unakua mkali hivi?
Arsis; Umeuliza kitu ambacho inabidi nikueleze kwa yundani, vipi nimejuana na babu yako, au hutaki tena kujua?Nyamaza. usijibu.

Nikanyamaza kimya.

Arsis; Leo huondoki hapa mpaka nimalize kukufahamisha.

Basi yule mume na ytule kijana wakahangaika kufanya safari ya kuja Tanga kwa mganaga wa Kigunya, alikua hodari sana wa kusoma vitabu huyo mganga, mtu mzima sana, lakini alikua anajulikana sana kwa kutibu watu na alikua anaweza kuita majini wakubw wakubwa sana. Alikua na maarifa mingi sana.

Baada ya muda, wakafanikiwa kuja Tanga, wakakutana na yule Mzee wa Kigunya wakamueleza ile habari. Yule mzee akawasikiliza kawaambia basi nyinyi kaeni hapa kwangu wakati mimi nafanya uchunguzi wa hiyo habari. Watu wengi wanakuja kuuliza habari za mali za Wajerumani, na wanakwenda kuhangaika san, hakuna alierudi kwangu akanambia kama kafanikiwa au hajafanikiwa, lakini inasemekana zipo, wapi mimi sijui, Kwa sababu mmenipa jina ya hio sehemu, wacheni mimi ntauliza nipeni siku mbili tatu, nikipata jibu lolote nitawajulisha.

Basi wale mabwana wakakaa pale siku ya tatu akwaita. Akawaambia nisikilieni kwa umakini sana.

Hapa Tanga Wajerumani wamekaa sana na njia hio mlionambia kuna mtu hapa anfanya kazi serikalini, ni fundi mkubwa sana, huyu amerithi majini wakubwa sana wa ukoo wake, bipi nimejua hii habari msiniulize. Lakini mimi simjui huyo mtu. Nyie tafdoiteni wenyeji wakepelekeni ile sehemu ya serikali wanapotengeza mashine na magari yao, Muulize fundi mkubwa wa pale, mkimpata njooni nae hapa tuongee nae.

Wale wageni hawakupata tabu kuna baraza ya kahwa na hakua pale jirani waklikua wameshizoea na watu wanacheza bao. Wakauliza pale. Kuna mtu akawaambia kuna fundi pale nyumba ile wa hukohuko karakana, ngija tumtume mtoto akamuite kama yupo.

Basi akatumwa mtoto akaenda, kuuliza akaambiwa hajarudi lakini akirudi watampa salaa kua kuna wageni wao kwenye kahawa atakuja, basi akija kama hampo hapa tutawafata hapo kwa Sheikh.


Basi kufika jioni wanarudi kusali alasiri hawjakaa sana wakaja kuitwa wakedna kibaraza cha kahawa, wakampata yule mtu wakamuita pembeni wakamwabia wao wageni kuna mtu wanamtafuta lakinihamwajui jina isipokua ndio fundi mkubwa wa serikali. Yule mtu akawauliza mzungu huyo au mtu wa hapa tanga? maana pale mimi ndipo ninapofanya kazi, kuna Mzungu ndio Worksjop manager. Na kuna funid wetu mkubwa, mtu wa hapa hapa Tanga maarufu sana anaitwa Mabruki. Wakasema itakua huyo wa Tanga. Maana ingekua mzungu wangetuambiwa mzungu. Akawaambia kama ni huyto basi mmeshampata turudi tukanywe kahawa niwape mtoto awapeleke nyumnai kwake, hayupo mali yupo hapo usagrfam barabara ya saba mwisho kule.

Wakarudi kwenye kahawa, akwaambia wale waliokwenda kumwita , hawa wanamtafuta Mabruk sio mimi jamani. Watu wakasheka, walikua hawamjui jina wanaemtafuta, mbona wangeshafika zamani kwa Mabruki.

Wakapewa mtoto akawapeleka kwa babu yako. Wal wakamwabia unaitwa na Sheikh Mgunya katutuma tuje kukita. Huyu Sheikh Mgunya wa barabara ya tisa? Wakamwabia ndio yeye anakuhitaji kwa ajili yetu. Akawaabia haya, tangulieni nikisha sali magharibi nakiuja huko. Mwambieni ikisha magaharib tu mguu wake huu.

Wakaondoka, kweli baada ya kusali magharibi babu yako akaenda, w)alipofika Mzee wa Kigunya kawaambia haya muhadithieni na mwenyeji wa hapa. Mbruki akmwambia mzee Mgunya, wewe ushaoa wake wanne Tanga mimi nakuona wewe kuaniz mdogo hata huko ugunyani kwenu sijui kama unapajua tena, unasema mi mi mwenyeji. Wewre mwenyeji zaidi yangu bwana.

Mzee wa kigunya kawaambia wale wageni wampoishe kidogo aongee faragha na babu yako wakanywe kahawa akiwa tauayari wataenda kuitwa. Mzee Mgunya akamwabia kwanini alimwita yeye, alimwabia mimi nimeongea na majini wakubwa sana, wao wakanmbia wewe una jini mkubwa mwenye hiyo bakora ulioibeba, yeye mwenyeji wa mitaa hiyo walioitaja, si umeisikia bwana wametaja Amboni lkini sio mapangomi upande unaotazama mapango kwa bharini. Nikaambiwa wewe una wenyeji wa huko watatoa mwangza ndio kisa cha kukuita bwana Mabruki.

Babu yako aksema usemayo kweli lakini hio mali sijawahi kusikia, ningeisikia si ningeshakwenda kuichukua? Mzee mgunya akmwabia akmwabia kweli huijui, hata mimi siijui lakini uradi uliopo hapa, ni uwaulize hao wakubwa huko, tutapata fununiu. Babu yako akasema swa atawaita kwa muda wao wampe siku mbili tatu ataleta majibu.

Wakakubalina hivyo. Wakaitwa wlae mbawna waendelee kusubiri, ikwa yule bwana Mihamed hawei kusuniri tena, akrudimDar, yule kijana akasema miminitasubiri. Mzee Mgunya kamwabia wewe subiri na usiwe na shka ni mgeniwa y. Tuombe iwe heri tu. Tumsubiri Mabruki atupe jibi lake na yeye.


Itaendelea.
Ngoja niweke kituo.
 
Inatokea post namba 294.


usiku kama nilivyoahidi kama saa 4 hivi nikaenda viwanja vya kukutana na Arsis, nilipomwita hajachelew akaja.

Arsis; Vipi hali yako Simba?
Mimi; salama, Arsis.
Arsis; Tuendelee. Simab ndio baba yakao akaenda pale mapoangoni akamwita Jini Balra, wakatoka wakaenda kuweka alama ya shamba, wamemaliza siku nzima ya kwanza hawakumaliza, wakafanya ile kazi wiki mzima. Ilikua pori kubwa sana, wanyama wengi, nyoka wengi, tena wewe unapenda pale kwenye mto ule mdogo, pale kuna chatu wakubwa sana, bahati mzuri Jini Bakora ameweka jini inakimbiza ile kila akija. Majani yale ya nyasi ya kule kwenu, manyoezekea yalikua mengi sana, Bahati mzuri walichukua wale wenyeji wanakaa pale karibu karibu wakawasaidia sana, na kundi kubwa ya majini ya Jini Bakora yamesaidia sana kusafisha njia.

Alipomaliza baba yako akaenda kumueleza Mzee Mgunya, wakapanga siku wakaja baba yako na mzee Mgunya mpaka kwenye mapango yale uliolala wewe, wakafanya mkutano wao iakapangwa siku waje pale ndani kugfanya kazi.

Siku ilipofika Mzee Mgunya akasoma vitabu vyake, babu yako amesshapewa njia zote za kufanya, amepewa na kisu cha kukatia lakiri ya ile chupa akaelekezwa akiiona imefika mbele yake, asiogope kitu chochote atachokiona, achukue chupoa akate lakiri, kitu chochote kitakachotoka kwenye chupa asiogope wala asikisemeshe, kikitoka tu ye avunje chupa aikate lakiri na kisu, aifungue akisha ifungua, kuna mawe ya kuvunjia chupa alipewa, alipewa na miti minne aigongelee chini kama mita kila mti kwa pembe nne, kabla ya kuwasha moto. Pale ndani ya miti ndio awashe moto, akiipata chupa akisha ifungua aivunjie chupa pale ndani na atupie pale kwenye moto. Zikaletwa kwanza nyasi nyingi sanaz ikawekwa pembeni zikaletwa kuni nyingi zikawashwa kwanza kuni, ukikolea moto, ndio Mgunya aanze kazi ya kuivuta ardhi kwa elimu yake.

Basi walipowasha moto wa kuni, haikuchukua muda Mgunya akaanza kazi yake, chupa ikaonekana, babu yako akaiona, ilikua imezungukwa na vitu vitu vya kutisha lakini shjaaa yule hakuogopa kabisa na Qur'an aliokua anasoma vile vitu havikuweza kumsogelea, hakupoteza muda akafanya kama alivyoelekezwa huku anaendelea kusoma, akifungua chupa, akaivunjia mule ndani ya moto akaongeza nyasi na juu ya nyasi akaweka magogo ya kuni akjaza nyasi juu yake, Mgunya akamwabia sasa mimi nakwenda zangu, kazi imekwisha. Wewe ondoka hapa, moshi mwingi, kaa nje pale mchangani usiwe na wasi wasi endelea kusoma Qur'an baadae atakuja jini Bakora atakupa maelkezo. Babu akauliza mbona sikuona kitu kilichotoka? Mgunya akacheka akatoka nje. babu yako kutoka nje hamuoni Mgunya, kisha ondoka haonekani hata njia aliopitia. Basi babu yako akakaa pale nje akawa ansoma Qur'an, akasoma pale kama masaa mawili au zaidi kidogo ndio Jini Bakora akaja.


Itaendelea.
 
Inatokea namba 298.


Arsis: Jini bakora akmsalimia babu yako, wakaanza kungea.
Jini Bakora; Mbaruki, wewe mzima heikh?
Mabruki; Mimi mzima sana, mbona hajamtoka mtu?
Jini Bakora: Akacheka akamwambia tumedfanikiwa lakini hayafai kuongelwa sasa hivi. wewe irabidi uendelee kusoma hapa, alfajiri ikiingia ukisha sali uondoke zako, Tutakutana mjini, ukifika salama huko, uniite. Nenda moja kwa moja kwa Mgunya.

Jini Bakora akaondoka bila kuaga, Mabruki akakaa pale hakuwea kulala, hauku[ita ikaingia alfajiri, akasali, akaondoka. Akafika salama mjini Jioni kabisa, zamani gari sio nyingo kam sasa lakini alipta gari.

Arsis: Babu yako akafika kwa Mgunya akamkuta, alipomuona akacheka sana, nbasikia kulikua na hatari huko?
Mabruki: S; tulikua pamoja unaondoka, umefika salama usiku ule?
Mgunya; Mabruki hukua na mimi kule, binadam ulikua peke yako, yule alikua jini kachukua umbo langu, jini mubwa sana yule, kazi yake ilipoishia na kuona kuna usalama akaondoka zake. Lakini habari zote ninazo, nihadithie na wewe kwa muono wako.
Mabruki: Mimi zina ziaidi nilifanya kama nilivyotakiwa kufanya, sikuona mtu akitoka kwenye chupa , lakini nimeivunja vunja nikatia kwenye moto, moto na magogo yale nadhani unawaka mpaka saa hizi.

Mgunya; Ule utawka siku tatu, maana kwanza 8utakua mkaa, mkaa utaungua taratibu mpaka litabaki jivu tu. akwanza ngoja tufuturu, mie nimefunga leo, tukimaliza baada ya Ishaa tutamwita Bakora aje. Wewe mabruki kurudi kwako nyumbani itakua sio leo, mpaka moto uishe kule pangoni. Tutapata habari kwa hio utakua mgani wangu hapa, usiwe na wasi wasi.
Mabruki; Hakuna tabu.


Wakamaliza mambo yao baada ya Ishaa wakamwita Jini bakot)ra akaja.

Mgunya; hanbari zahuko Sheikh?
Jini Bakora; Njema sana, kazi yetu imefanikiwa, tuliemtarajia tunae huko, tumemwekea ulinzi mkali ingawa hauhitaji ni mtu wa elimu kubwa sana, lakini mwenyewe kaamua awe kule anafanya mambo yake kwa muda fulani. Kwa hio nawapa homnngera sna.
Mgunya: Haya; cha mdsingi umemuuliza kuhusu hicho kitabu? maana ndio msingi wa hatari yote hii.
Jini Bakora; Tena ni hatari kweli, bado tupo kwenye harari sote, lakini tuwe na amani mambo yamedhibitiwa vizuri, Mbaruki hapa ndio asoiwache kusoma Qur'an mpaka hili wimbi la hatari liondoke ake. Majini wamekasirika sana, sema tuna bahati kubwa sana.
Mgunya: Ipi hio?
Jini Bakora: Yule bwana kumbe alikua ni mlinza wa lango la kuendea dunia zingine kwa upoande wa huku kwetu duniani, kwa hio kalifunga lango wa kule yupo kule wa huku yupo huku, hakuna jini atakuja kutoka dunia yao akaingia huku bila yule bwana kufungua lango lake. na yeye kasema mpaka aingie nao mkataba ndio atafungua. Lakini hio itachukua muda kutokea, vikao vitafanywa na jaumu nyingoine kavbisa, sio ya kijini wala ya lkkibinadam.
Mgunya: nani tena hao? malaika?
JiniBakota; Tuishie hapo, nimeshayasema memngi ambayo nimeapishwa nisiyaseme, yasinikute mengine tena. Atayasema mwenyewe yule bwana akiwa tayari.
Mgunya; Sawa, nimeelewa.
Mbaruki: kwanini mimi sikumuona?
Jini Bakora; Alifanya vie kwa usalama wake lakini ataongea na wewe, anakushukuru sana tena sana, bila wewe hili zoezi lisingefanyika, hakuna kitu kigumu na cha hatari kama kuifungua ile lakiri ya chupa. Pale ndipo penye kazi kubwa kuliko zote. Kwa hio Mbaruki hgoimgera sana, una rafiki pya na anatoa shukran zake na kasem yeye atakutembelea ataongea na wewee kwa nia mbili lakini hautomuona kwa sasa, mpaka mambo atakapoona yanfaa sasa ajitokeze. hata majini hatumuoni yuke mtu, mimi nimeongea nae tukafanyiana vipimi vua kuhakikisha yupo kweli, yupo kweli na akitaka kuonekana ataonekana, lakini kwa sas tumpe muda ajiweke sawa. Kuhusu vitabu vipo, kasema tusiwe na wasi wasi atamueleza Mbaruki cha kufanya. Anajua jinsi ya kumpta Mbruki, jna usiku kamuona, asiwe na wasi wasi, salaam zake kwa Mabruki ni kua sasa ana rafiki mpya na salaam zako Mzee Mgunya anasema yupo tayari kwa kazi yoyote utakoyitaka kwake lakini hawezi kua na mba)waba waeili, kwa hio utampta kupitia kwa Mbaruki aliekata lakiri.
Mgunya; Nimemuelewa sana, Mabruki akishatulizana na kurudi kwake tutakua na mengi ya kujadilki mimi na yeye.

Bakora; Niliona nije kuwapa huo ujumbe, moto uke tutauacha siku tatu, yaani leo ni moja, kesho ni bili, kesho kutwa tatu, baada yahapo mabruki unawea kurudi kwako nakufanya mabo yako upendavyo. Usifanye ubishi, ni katika kulinda usalama tu.

Mabruki; Sawa, itabidi Mgunya unipe chumba nimuagize mke wangu aje, sijazoea kulala peke yangu.
Mgunya; Tena sasa hivi tumtume mke wangu waende arudi nae. Nilitaka kusema hili, vipi utakaa peke yako siku tatu kwenye mji wako?

Arsis: Wakafanya hivyo na ndio kisa changu cha kuanza kujuana na babu yako. nafahamu una maswali mengi sana ya kuniuliza, utaniuliza taratibu taratibu hautoyamaliza, kila nikukujibu moja liytazaq mengine kumi na moja. Umenielewa Simba?

Mimi; Nimekuelewa Arsis, kweli nina maswali mengi ya jukuuliza lakini yarasubiri, hayana hatraka.


Natumai wasomaji wangu mmeelewa vipi Arsis alionana na babu yangu. Mnaweza kuuliza chochote kinachohusiana na huu mkasa, kwa sababu baada ya hapo nikawa nauliza kidogokidgo kwa Arsis kwa muda mrefu sana, nimengi sana.

Hayo ni kwa mujibu wa Arsis lakini niliongea na babu yangu baada ya kuyajua hayo kwa Arsis, nae alikua na yake alionieleza, nayo nitayaleta kama nilivyoongea na babu yangu.

Itaendelea.
 
Inatokea post namba 7.


Haukupita muda mrefu, tumekaa karibu na mlango wa pango kwa ndani. Mlango wa pango ulikua ni mkubwa sana, na chini ulikua ni mchanga mweupe wa pwani, Kulikua na kivuli kizuri na upepo mzuri sana.

Mwanafunzi wa babu alikua ananieleza lile pango, ni refu sana na huko ndani lina kama vyumba vyumba, vingine ukiingia unakutana na sehemu za kwenda chini zaidi.

Wakati tunaendedlea kuppiga story tukasikia, hodi, mara akaingia yule kijana mwengine waliokuja kunipokea na baiskeli. Kabeba kapu akasema haya, jamani chai ya asubuhi, na mimi mgeni wenu, bibi huko kanitoa mbio, anasema nimwahishie chai mumewe, katoka nyumbani bila kula.

Tukala pale tukamaliza, ilikua samaki wa kuchemsha na vipande vya mihogo. Chai ya rangi imekolea viungo na chupa mbili tatu za maji ya kunyea. Tulipomaliza, jamaa akakusanya vyombo, kulikua na samaki na mihogo imebaki, akasema hii mtakula mkisikia nja. Akaondoka. Nikamuita, nimueagize vitu vyangu juu, akasema, huku ndio hairuhusiwi kuja na chochote ambachoi hujaja nacho kwanza, labda akuletee babu mwenyewe. Akaondoka.

Sisi tuka kaa kaa pale kama kiusingizi kizito killinipipitia, ile nastuka, namuona babu kaja na yule kijana wana kapu lingine. Hiyo kama saa tisa mchana. Akasema haya, chakula chenu. Mmelala sana. Sisi tumekuja kama nusu saa hivi, tukasema tusiwaamshe. Wewe bwana mkubwa nafahamu ukilala, ni zile dawa ulizopakwa, zina nguvu sana. Lakini huyu mwingine, inaonesha kala mihogo mingi. Mihogo inaleta usingizi sana, hasa hii ya mbegu ya bibi yako, mwenyewe aniita dawa ya usingizi. Na kweli, imewasaidia watu wengi weye matatizo ya usingizi.

Babu akasema haya, njoo kuna dawa zingine hapa, sisi tunataka kuondoka. Babu akanipa chupa ya mfuta yenye dawa, kama inachenga inachenga. Akanambia hii utajipaka mwili mzima kikisha ingia kiza kabla hujalala. Na mizizi mingine akanambia hii utatafuna tafuna kila unaposikia mdomo mchungu. Mizizi yenyewe ilikua kama ina sukari fulani hivi kwa mbali unapoitafuna tafuna. Ina harufu nzuri sana.

Babu akatuaga, akasema mshatafuta sehemu ya kulala, pango kubwa sana hili, unaweza kulitenbea mpaka joni hujafika mwisho, linaungana na lile la Amb0ni, mkiingia nia zingine mnaweza kufika Mombasa na njia nyingine mnaweza kufika handeni. Lakini nyie tenbeeni tu ndani msijali. Huyo mwenzako mwenyeji kiasi, sema muoga. Na wewe "bwana mkubwa" muoga? Nikamwambia babu mimi si unajia "komancho" akasema "wewe ndio mroithi wangu", najua wewe uoga huna kabisa, wala sina wasi wasi na wewe simba. Wakaondoka zao.

Tukaamka pale tukaanza kuzunguka ndani pangoni, tukaenda tunaingia vinjia vya vyumba vingine, tunatoka, tunaingia kwengine, mradi tupoteze muda tu, hatujauacha mbali mlango tunayona mwangaza, mwangaza ulipoanza kufifia tukarudi. Tukakuta kiza kimeshaanza kuingia. Hakuna jipya, tukala tukakaa tunapoiga story, jamaaa ananipa story za kijijini na watu wanavyopitisha magendo kutokea Kenya, na jindi wanavyopata pesa kuwavusha wati na mizigo. Wanaingiza poesa nyingi sana, kuliko wangakua mjini. Akanambia kesho nitakuonesha tunapicha mizigo tukija nayo. Kuna oango lingine, hilo lkina kamlango jadogo na kamejaa kichaka, huwezi kujua kama kunapango. ndani pakubw sana. Mie nikajipaja dawa yangu baada ya kula nikakusanya michanga kama mtoi , nikajitupa kulala. Mwenzangu nimemwacha macho anapiga story hata simsikii kwa usingizi, sijui alilala saa ngapi.

Itaendelea.
Stori Nzuri.
 
Back
Top Bottom