Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Swali langu Arsis
Kwanini nashindwa kupata msaada kwa watu kwenye suala langu la jamaa kutumia vyeti vyangu na anapata mshahara mzuri,posho, na marupurupu mengine?
Nimejaribu kufuatilia mpaka baraza la mitihani (NECTA) Kujua jina langu au vyeti vyangu vinatumika ofisi gani au idara gani iii nipate kuchukua hatua za kisheria?
Ukiwa kama unayeona mpaka mambo yasiyoweza kuonekana kwa macho ya kibinadamu au kwa sisi watu ambao hatuna Mamlaka yoyote kwenye hii nchi. Kinachonisumbua ni kupata upinzani kila mahali, hata watu ambao wana nafasi za kunisaidia lakini bado sifanikishi? Nilienda mpaka NECTA kuhakiki lakini nilikuta upinzani na yule niliyemkuta sehemu ya ukaguzi wa vyeti ikaonesha alijua naenda kufanya nini pale na ananijua. Ninapambana kwa sababu ni haki yangu Chuo ada niliilipa kwa jasho langu mwenyewe hata kuijenga na kuitengeneza CV yangu ni jitihada zangu. Nimeomba msaada kwa ndugu zangu ambao wana nafasi ya kutoa amri mara moja tu lakini nao wanapuuzia. Halafu mtu ambaye hakusoma wala hakupata uzoefu wa kutengeneza wasifu anakula kupitia jina langu. Nikifanya interview kwenye ofisi zingine nafaulu vizuri usaili lakini kuitwa kuanza kazi hakuna. Mpaka nimeamua kufanya mambo yangu binafsi tu na Alhamdulillah nayamudu lakini kwanini nadhurumiwa haki yangu? Na kwanini sipati ushirikiano kutoka kwa Ndugu, marafiki au watu niliosoma nao ? NECTA ni pagumu na UTUMISHI nako ni vikwazo na nimejiapiza sikubali haki yangu ipotee hivi hivi. Ingawa kuna mazingira fulani ya kutishia usalama wangu nayaona au kuhisi hatari ya kufuatiliwa na watu wasiojulikana. Ushauri wako na mwongozo wako nauomba.
Nitafute inbox
 
Inatokea [post namba 672

Vionjo vya Arsis 3 Kumwokoa Msukule 1 C.

Niliporudi nyumbani nikakuta watu wapo macho. Mzee akaanza...
Baba; Vipi simba, kwema baba?
Mama" mwanangu tunaishi nyumba moja kama majirani hatuonani?
Mimi: Niko poa kuna mambo mambo tu yamenishghulisha.
Mama; Usijekua kama babu yako, mie sitaki kujaiwa wateja wa uganga humu ndani. maana babu yako ni hivyo hivyo akijifungia ndani akitoka kuna watu wana matatizo yao.
Baba; Huho karithishwa mikoba na babu yake, huoni bakora yake ile?
Wife: Wasimrithishe mwanangu tu mambi yao, maana kutwa kazi yake kuchewza na hiyoi bakora.
Mama; Nyie mnasema bakora kumbe tunaishi na jini ndani ya nyumba.
Mimi; mama wewe si simba, twambie kweli kama jini lile au sio.
mama: Simba sisi hatuna majini kama ya babu yako huko, majini ya kisimba yanapiga brandy, kazi yao kustarehe tu, hawajui hata kujitibu wenyewe. Hawana kabisa mambo yenu huko.
Wife: Wao watyu wa kujirusha tu.
Mama; Tena wewe hata usiseme, majini ya kwenu huko hawachezi mbali na wewe.
Wigfe' Mie hata sowataki, mie ya upande wako maa, yananitosha kabisa, mimi simba jike.

Naomba ifahamike, mke wangu hata mimi nilikua sijui kama ni mtoto wa shangazi yangu, kalelewa na mama toka mchanga kabisa, ni mtoto wa dada yake baba. Nimekuja kujua kabla ya ndoa. Ni kisa kingine kabisa hakihusiani na Arsis kwa hio kiishia hapo tu.

Baba; Njoo tuongee huku nje simba.

Tukatoka na baba uani, tukaanza kupiga kahawa.
Baba; Simba babu yako kanipigia simu kanambia utakua haupo utakwenda Tanga kwa wiki moja, mbina hujanambia?
Mimi: Ilikua nikwambie, hatujaonana, ndio tunaonana sasa hivi.
Baba: Hakuna tatizo, nilikua nakujulisha tu, wewe nenda tu any time, usijali mambo ya kazi zako, mimi nipo. Maana babu anasema ulimwabia una kazi nyingi.
Mimi; Ndiyo mzee kuna wateja watataka diagnosis ya gari zao.
Baba: Hilo usijali nitamchukua mkeo aje kufamnya diagnosis ikihitajika.
Mimi: Baba wewe unachukulia kila [poa tu, kiwepesi kabisa. Upo kama babu.
baba: Usiwe na wasiwasi simba, kikitushinda kitu tutakupigia simu, ruksa, nenda tu.
Akaondoka, ile naingia ndani nikapata ujumbe niende osisini kwangu kabla sijaingia kulala. Nikaenda.

Nikakamkuta jini mwanamke ananingoja kama kwake. Tukasalimiana akaanzaa...
Jini1: Usistuke simba nimekuja kuweka mambo sawa tu sikucheleweshi. Waambie wageni waende Tanga Jumamosi, wawe pale Jumapili.
Mimi: sawa nitamjulisha mzee Ali kesho.
Jini 1; Mpigie hata sasa hivi ili kesho mapema awaambie wajitayarishe. Na wewe unatakiwa kuanzia kesho uwe Tanga kwa babu yako, huna haja ya kwenda kazini kesho. Mama anakupa salaam. Mpelekee zzawadi Haalima pale Chalinze.

Mimi nikashangaa kidogo.

Jini 1: usishangae mimi hanijui wala simjui lakini si ndio njia yako hio, nakukumbusha tu.
Mimi; Sawa lakini Arsis anasema wewe unajuana na mkewe mzee Ali, sitaki mnifanyiwe mamboya siri zenu za kijini.
Jini1; Mimi namjua Qareen wa mkewe sio mkewe. Arsis kishakueleza kitu. Soisi hatuwezi kua na siri yoyote kuhiusu wewe, tutauliwa. Jambo lingine, hii kazi usimwabie hata mkeo wala mama'ko. ni yako na sisi tu. kwaheri nisikucheleweshe.
Mimi: haya kwaheri.


Nikaenda zangu nikakoga nikalala mpka siku ya pili asubuhi mapema nikaanz kukusanya vitu vyangu vya safari nikamwambia wife nitakua Tanga kwa wiki moja, akanambia ,nikishindwa kukaa peke yangu nakuja hukohuko Tanga, wiki nzima? Kuna nini wewe na babu? Au ushakuwa mwanga kama babu yako? yule mzee anaweza kukuozesha huko mume wangu.

Mimi; Nikacheka, kama mwanga ni wewe na babu yako, mimi simo. Mimi kuna kazi zangu tu zinanipeleka.

Mama alipotoka na yeye nikamuaga, mzee alishakwenda kazini. Nikaondoka, ile nnataka kuondoka nikakumbuka nimesahau bakora yangu nikaifata, nikakumbuka na zawadi ya B Haalima Chalinze, nikamwabia wife kama ana chupa ya perfume haitumii anipe nimpelekee Bi Halimza zawadi. Waife akanitolea chupa mpya ndani ya noz, akanambia hizi ninazo tatu, mtu akijua naipenda hii perfume anailetea zawadi hio hio. akacheka, akasema bora na Halima Msomali anukie kama mimi. Nikajua kijembe cha wanaweke hiko.

nikaanza safari yangu ya Tanga.

Njiani Mzee Ali akanipigia, nikamwabia nipe muda kidogo nitakupigia.

Nilipofika Chalinze kitu cha kwanza nikamueleza kuhusu yule mama na ndgu zake kuja Tanga na lini. Akanambia sasa hivi anaongea nae, yupo kwake pale, Tukakubaliana tuongee juoni kupeana mrajesho. Sikumwambia kama mimi naelekea Tanga.

Nikashuka kwenye gari nikaenda kwa Halima zna zawadi yake. kuniona...

Halima. Mimi nasema boss gani huyu hashuki kwenye gari, kumbe simba mtoto?

Tukasalimiana nikampa zawadi yake, akifungua palepale, akaijaribu akanambia hii perfume mimi naujanja wangu wote siiwezi bei yake, simba umeniroga, umejuaje mimi napenda perfume?
Mimi: Niki[iyta unanukia tu.
Halima: Mie Msomali wewe, wasomali mwanamke kama hanukii huyo feki.
Mimi; Si unukie kwa mumeo tu?
Halima; Harufu ninayomtilia mume wangu wewe huwezi kuielewa wala kuinusa. mwiko kabisa

. Hivi unavyonisikia ni hapa dukani, udi wa kawaida tu huo, sijatia manukato, unataka niwatie wazimu watu?


Nikacheka nikajisemea kimoyomoyo, hivi hawa Watanga mbona hawangoji kusifiwa? Wanajisifu wenyewe.



Itaendelea.
 
Dah! Huyu Arsis 🤣😂 Corazon hana majibu haya
Sio Arsis, hajaja bado. Huyo kijana anatania tu, ni mimi simba. hajaziona chai za za asubuhi kwa kamab huyo.

Hajui kwegtu tanga wanatuikia chai kwa anjari nyeupe ya tangawizi, haitiwi sukari wala viungo qala maji hio.

Anacheza na chai ya Tanga huyo.
 
😂😂😂😂😂😂😂..... Haya mambo huwa yapo hvyo, ukisikia lazima uone ni kamba!!!

Siku nikiamka vizuri ntaleta kisa changu hapa.
(Maana mm nilikabidhiwa kwa mashetwan toka nikiwa mdogo, baadae wakasalitiwa nikanyang'anywa mikononi mwao ilikuwa n vita kali sana..... Wakamgeuka mzee wangu wakamuua kikatili, mzee akaona ni bora yeye afe kuliko mwanae awe mfalme wa mashetwan na wachawi🚶🚶

Siku moja nikiamka vizuri ntaisimamisha jf kwa muda😂

Maana ni visa vya mfululizo kwanzia miaka 4 mpk Sasa hivi nnavyoandika hii comment bado vita inaendelea 🏃
Chai
 
Habari wana jamvi, kama kichwa cha habari kinavyo jieleza ntaomba kuelezea kwa uchache changamoto ninazopitia kwa miaka 3 sasa. Ikibidi nitaandaa treads ya kusimulia mkasa mzima toka ulivyo anza mpaka hali niliyonayo kwa sasa.

Nipende tu kuwaomba wale wenye itikadi za kidini kukaa pembeni kwanza kwani kama hujapitia shida kubwa ktk maisha huwezi kujua kuwa kuna ya walimwengu pia.

Niende kwenye mada, mimi ni kijana wa kiume ambae kazi yangu kubwa ni media producer & fundi wa vifaa vya umeme. Nilihamia wilaya hii iliyoko mkoa x kutoka wilaya nyingine ya mkoa huu huu ili kufata fursa za kibiashara. Mwanzo mambo yalienda vizuri sana na kutokana na kazi yangu iliniwezesha kusafiri mara kwa mara nje na ndani ya mkoa.

Nitafupisha stori, mwanzoni mwa mwaka juzi ndipo nilianza kuona mabadiliko ktk biashara zangu ikawa hata mteja ukimpa bei akaomba punguzo na ukamkubalia ila haitachukua dakika kadhaa kukupigia kuwa ameahirisha kazi hiyo lakini nikifatilia nakuta amefanya kazi sehemu nyingine na haina ubora kama ninavyofanya mimi.

Kifupi niliona ni masuala tu ya kibiashara kufanya au kutokufanya kazi na mteja, lkn hali ikazidi kuwa mbaya kwangu binafsi hata nikienda kazini kwangu ni kulala na hakuna wateja, akienda mwingine kuna nafuu japo hela ya matumizi inapatika. Kiukweli naumia kuona nimewekeza almost vifaa + ofisi zaidi ya 10ml lkn unapata hela ya kula tu hata kodi naelekea kushindwa kilipa.

Kwa muda wote huo mabadiliko yalianza kwangu kuhisi naogopa watu, kujitenga hata sikuwa na ujasili tena ambao nilikuwa nao wa kwenda kwenda kukusanya habari kwenye mikutano, makongamano, sherehe nk kwani watu wamekuwa wakiona kama kitu flani cha ajabu hivi wengine kupelekea kukucheka 😭😭 jambo ambalo limeniathiri sana kisaikolojia, nikiwa na maana kuwa watu wanao cheka ni ambao tunafahamiana nao miaka kadhaa toka nihamie hapa ikiwa kipindi sina tatizo lolote. (Jaribu kuwaza ikiwa wewe ikatokea siku staff wenzo, watu wako wa karibu pengine na familia wanakucheka, kukusengenya na kukudhihaki huku unawaona ni jambo gani utafanya?).

Mpaka sasa nimebaki pekeangu hakuna rafiki wala watu wa dini kuwa karibu tena na mimi, nimebaki na familia yangu hasa mke na watoto ndo wafariji wangu. Na kinachoniumiza zaidi ni mama yangu ambaye kwa sasa anasumbuliwa na pressure iliyotokana na kuniona nikiwa ktk hali hii na jinsi jamii inavyo ni treate kwani mimi ndiye msaada mkubwa kwake.

Kwa muda wote huo nimekuwa nikitafuta suluhiso la tatizo hili, ni nilianzia kwenye maombi miezi kadhaa bila mabadiliko ndipo nikashauriwa kuangalia tiba asili napo nimepita maeneo mengi ya ndani na nje ya mkoa. Kikubwa ambacho nimeambiwa na wengi ni kwamba NIMETUPIWA KIPANDE. Kifupi nimepotea fedha nyingi mpaka sasa na uchumi wangu umeyumba bado sijapata nafuu ya tatizo sababu siwezi kusema kuwa labda wale wataalam wa tiba asili kuwa walikuwa matapeli, hapana sababu kila mtu anao uwezo wake ktk kutatua matatizo ya watu, ndio maana nikaja huku kuomba msaada wa kupata matibabu kwani hali ni mbaya ndugu zangu na familia wananitegemea na sioni nuru mbeleni sababu nimekuwa nikiota ndoto za ajabu ajabu na za kutisha mara nyingi, mara uote unazikwa mara unabeba jeneza nk. 😭.

Japo wengine hufikiria kujiua ili kuondokana na hizi shida za dunia lakini mimi NASEMA KAMA MUNGU ALIRUHUSU MATATIZO HAYA KUNIPATA BASI ASIPORUHUSU KUPATA MSAADA WA KUPONA KABISA BASI NITAISHI HIVIHIVI, SIWEZI KUJIUA.

Naomba nifupishe stori na kuwasilisha kwenu. Kama kuna mtu anaweza nisaidia tiba, namna ya kupona nitashukuru sana.

Mungu awabariki kwa muda wenu.
🙏🏻🙏🏻
Tafadhali Arsis ikikupendeza Anza na maoni yako kuhusu ndugu yetu huyu
 
Nilivyoelewa mimi kuwa Yesu siyo jina lake kabisa. bado naendelea kutafuta wakristo wamelitowa wapi jina Yesu?
Screenshot_20240824-200406.jpg
 
Naam Hoyo wangu alikuwa msomali alikuwa anasema ni matusi kwa mwanamke wa kisomali kunuka wao kununua na nyumba zao nywele wafukiza oud na oud bokhoor ya nyumba sio anayo jifukizia mwilini nywele au kwenye nyumba,asubuhi kisha pika chai ya maziwa somali Xhaa angelo(Angela) maini au nyama (beef sugaar) au sabayad(chapati) nyumba safi yanukia Alkhamis kuamkia ijumaa Mama aliniambia kwao Hergeisa wanawake wanafanya facial na steaming z nywele kwa hinna na qasir (unga wa majani ya mkunazi) sio u Tanga wa Somali wako hivyo ndo maana wanashika waume zao hawafurukuti wana waachia waendeshe mambo wao kula mirungi tu.
Inatokea [post namba 672

Vionjo vya Arsis 3 Kumwokoa Msukule 1 C.

Niliporudi nyumbani nikakuta watu wapo macho. Mzee akaanza...
Baba; Vipi simba, kwema baba?
Mama" mwanangu tunaishi nyumba moja kama majirani hatuonani?
Mimi: Niko poa kuna mambo mambo tu yamenishghulisha.
Mama; Usijekua kama babu yako, mie sitaki kujaiwa wateja wa uganga humu ndani. maana babu yako ni hivyo hivyo akijifungia ndani akitoka kuna watu wana matatizo yao.
Baba; Huho karithishwa mikoba na babu yake, huoni bakora yake ile?
Wife: Wasimrithishe mwanangu tu mambi yao, maana kutwa kazi yake kuchewza na hiyoi bakora.
Mama; Nyie mnasema bakora kumbe tunaishi na jini ndani ya nyumba.
Mimi; mama wewe si simba, twambie kweli kama jini lile au sio.
mama: Simba sisi hatuna majini kama ya babu yako huko, majini ya kisimba yanapiga brandy, kazi yao kustarehe tu, hawajui hata kujitibu wenyewe. Hawana kabisa mambo yenu huko.
Wife: Wao watyu wa kujirusha tu.
Mama; Tena wewe hata usiseme, majini ya kwenu huko hawachezi mbali na wewe.
Wigfe' Mie hata sowataki, mie ya upande wako maa, yananitosha kabisa, mimi simba jike.

Naomba ifahamike, mke wangu hata mimi nilikua sijui kama ni mtoto wa shangazi yangu, kalelewa na mama toka mchanga kabisa, ni mtoto wa dada yake baba. Nimekuja kujua kabla ya ndoa. Ni kisa kingine kabisa hakihusiani na Arsis kwa hio kiishia hapo tu.

Baba; Njoo tuongee huku nje simba.

Tukatoka na baba uani, tukaanza kupiga kahawa.
Baba; Simba babu yako kanipigia simu kanambia utakua haupo utakwenda Tanga kwa wiki moja, mbina hujanambia?
Mimi: Ilikua nikwambie, hatujaonana, ndio tunaonana sasa hivi.
Baba: Hakuna tatizo, nilikua nakujulisha tu, wewe nenda tu any time, usijali mambo ya kazi zako, mimi nipo. Maana babu anasema ulimwabia una kazi nyingi.
Mimi; Ndiyo mzee kuna wateja watataka diagnosis ya gari zao.
Baba: Hilo usijali nitamchukua mkeo aje kufamnya diagnosis ikihitajika.
Mimi: Baba wewe unachukulia kila [poa tu, kiwepesi kabisa. Upo kama babu.
baba: Usiwe na wasiwasi simba, kikitushinda kitu tutakupigia simu, ruksa, nenda tu.
Akaondoka, ile naingia ndani nikapata ujumbe niende osisini kwangu kabla sijaingia kulala. Nikaenda.

Nikakamkuta jini mwanamke ananingoja kama kwake. Tukasalimiana akaanzaa...
Jini1: Usistuke simba nimekuja kuweka mambo sawa tu sikucheleweshi. Waambie wageni waende Tanga Jumamosi, wawe pale Jumapili.
Mimi: sawa nitamjulisha mzee Ali kesho.
Jini 1; Mpigie hata sasa hivi ili kesho mapema awaambie wajitayarishe. Na wewe unatakiwa kuanzia kesho uwe Tanga kwa babu yako, huna haja ya kwenda kazini kesho. Mama anakupa salaam. Mpelekee zzawadi Haalima pale Chalinze.

Mimi nikashangaa kidogo.

Jini 1: usishangae mimi hanijui wala simjui lakini si ndio njia yako hio, nakukumbusha tu.
Mimi; Sawa lakini Arsis anasema wewe unajuana na mkewe mzee Ali, sitaki mnifanyiwe mamboya siri zenu za kijini.
Jini1; Mimi namjua Qareen wa mkewe sio mkewe. Arsis kishakueleza kitu. Soisi hatuwezi kua na siri yoyote kuhiusu wewe, tutauliwa. Jambo lingine, hii kazi usimwabie hata mkeo wala mama'ko. ni yako na sisi tu. kwaheri nisikucheleweshe.
Mimi: haya kwaheri.


Nikaenda zangu nikakoga nikalala mpka siku ya pili asubuhi mapema nikaanz kukusanya vitu vyangu vya safari nikamwambia wife nitakua Tanga kwa wiki moja, akanambia ,nikishindwa kukaa peke yangu nakuja hukohuko Tanga, wiki nzima? Kuna nini wewe na babu? Au ushakuwa mwanga kama babu yako? yule mzee anaweza kukuozesha huko mume wangu.

Mimi; Nikacheka, kama mwanga ni wewe na babu yako, mimi simo. Mimi kuna kazi zangu tu zinanipeleka.

Mama alipotoka na yeye nikamuaga, mzee alishakwenda kazini. Nikaondoka, ile nnataka kuondoka nikakumbuka nimesahau bakora yangu nikaifata, nikakumbuka na zawadi ya B Haalima Chalinze, nikamwabia wife kama ana chupa ya perfume haitumii anipe nimpelekee Bi Halimza zawadi. Waife akanitolea chupa mpya ndani ya noz, akanambia hizi ninazo tatu, mtu akijua naipenda hii perfume anailetea zawadi hio hio. akacheka, akasema bora na Halima Msomali anukie kama mimi. Nikajua kijembe cha wanaweke hiko.

nikaanza safari yangu ya Tanga.

Njiani Mzee Ali akanipigia, nikamwabia nipe muda kidogo nitakupigia.

Nilipofika Chalinze kitu cha kwanza nikamueleza kuhusu yule mama na ndgu zake kuja Tanga na lini. Akanambia sasa hivi anaongea nae, yupo kwake pale, Tukakubaliana tuongee juoni kupeana mrajesho. Sikumwambia kama mimi naelekea Tanga.

Nikashuka kwenye gari nikaenda kwa Halima zna zawadi yake. kuniona...

Halima. Mimi nasema boss gani huyu hashuki kwenye gari, kumbe simba mtoto?

Tukasalimiana nikampa zawadi yake, akifungua palepale, akaijaribu akanambia hii perfume mimi naujanja wangu wote siiwezi bei yake, simba umeniroga, umejuaje mimi napenda perfume?
Mimi: Niki[iyta unanukia tu.
Halima: Mie Msomali wewe, wasomali mwanamke kama hanukii huyo feki.
Mimi; Si unukie kwa mumeo tu?
Halima; Harufu ninayomtilia mume wangu wewe huwezi kuielewa wala kuinusa. mwiko kabisa

. Hivi unavyonisikia ni hapa dukani, udi wa kawaida tu huo, sijatia manukato, unataka niwatie wazimu watu?


Nikacheka nikajisemea kimoyomoyo, hivi hawa Watanga mbona hawangoji kusifiwa? Wanajsifu wenyewe.



Itaendelea.

Sio Arsis, hajaja bado. Huyo kijana anatania tu, ni mimi simba. hajaziona chai za za asubuhi kwa kamab huyo.

Hajui kwegtu tanga wanatuikia chai kwa anjari nyeupe ya tangawizi, haitiwi sukari wala viungo qala maji hio.

Anacheza na chai ya Tanga huyo.
Ukienda Tanga niletee anjari haswa nyeupe naipenda harufu yake ya arki rose usisahau kamba wa Maforoni 😄nawapenda sana haswa ukiwa pika prawns curry au prawns biryani.
 
Back
Top Bottom