Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Kwanza kabla sijakupa jibiu, nikupe elimu ndogo tu. Ngoja nikukate maswali yako niwache swali moja tiulijadili, tukimaliza tutaenda lingine. Hatuna haraka wala "time limit". Uzi upo hapa na posts zipo hapa.

Nilikujibu juu kidogo hapo lakini naona hukuelewa. Maana unachanganya mambo ya uzushi (heresy) mengi mengi kwa pamoja.

Usidhani kuuliza maswali mengi ya kuzusha ndio kuelewa au kujuwa sana. Hiyo kingereza inaitwa "ignorance fallacy" Kiswahili chake ni uongo wa ujinga.

Ili kukuonesha kua huo wako ni "uongo wa ujinga", inatakiwa kwanza utueleze na ijulikane umelitoa wapi hilo swali kielimu; Nani "aliwafuga" na "waliofugwa" ni nani?

Raha ya elimu ya Uislam, ni lazima kipatikane chanzo (source), kama hauna chanzo inabaki kua ni uzushi wako b9nafsi.
Simba.
umepiga juu sana sasa anakata roho.
 
Kisa cha Adam 1.

Salamoun Alaykum!

Leo katika muendelezo wetu wa Kisa cha Adam nitaanza na mada ambayo nilisita sana kuiwasilisha jukwaani kwa sababu mbili kuu.



Sababu ya kwanza; ni kua mada hii ni ndefu na inabidi mnivumilie kwani inabidi tuifanyie tafsil kwa kina bila kuacha kitu kikielea (hangig). Tutaitumia sana mbinu ya kiota, kufata na kuonesha maana kusudiwa katika aya zingine au lilipotumika neno kama tunalolifanyia ‘tafsil”.





Sababu ya pili hii mada itakua na mshtuko (shocker) utaotutikisa kidogo uelewawetu, hususan kwa wale wote ambao hawapendi kuisoma Qur’an kama ilivyo na hupenda kuongezea maneno ya watafsiri hata kama hayamo kwenye Qur’an.



Mtikisoko utakua wa ziadsia kua kwa miaka mingi tumefata na kuamini mambo kwa kufata watu ambao wamefanya makosa kataika tafsser zao au wamefata vitabu vingine ambayo visa au mafundisho yake ni ya kibinadam tu, hayana hata chembe na uhusiano na Qur’an.



Nawaasa wote tustahamili kuisoma hii elimu kidogo kidogo, kwani ina mengi ambayo tutayaleta kidogo kidogo ili yatuingie kwa mitindo (methods) ambayo inatokana na Qur’an yenyewe na wala sio ubunifu wa mtu.



Msiniulize mtayoyasoma hapa kwanini wengi wetu hatujayaona kabla na au kwanini “Maulamaa wetu hawajayaona kabla?”. Tustahamili kuuliza hayo kwani naamini kila tutavyoendelea Qur’an yenyewe itatupa majibu,





Tunakusudia kuanza kuifanyia tafsil aya ya 30 na kuendelea, lakini kabla hatujaingia kwenye aya ya 30 itabidi tupitie aya ya 28 na 29.



Ni muhimu sana tujifunze mbinu mbili tofauti za kutusaidia ufahamu wa Qur’an kutokana na Qur’an yenyewe.



Alhamdulillahi, Mwenyezi Mungu ametujaalia kutupa elimu na mwongozo ulio bora kabisa kuliko wowote ule na usio na shaka ndani yake, Qur’an.



Hatuna budi tufanye hima tujikite kwenye Qur’an kama msingi wetu mkuu wa kuielewa Qur’an yenyewe. Maneno ya watu binafsi tuliofundishwa, haijalishi yanatokea kwa mwenye jina kubwa vipi, kama katumia yake binafsi kuongezea ambayo hayamo kwenye Qur’an au kutumia akili yake, ambayo haiwezi kua na ujuzi wa kumpita Allah kwa lolote li;e, tuyapuuze.



Ikiwa kuna Alim au mwanazuoni yeyote yule, kupunguza kitu au kusema kua hiki hakina maana kilizidi tu, kwa sababu yoyote atakayoitoa, huyo au hao tuwatazame mara mbili mbili, kwani naamini hakuna neno au herufi itokayo kwa Muumba wetu isiyo na kazi yake au maana yake kuwepo kwenye Qur’an.

...2

Kisa cha adam. 2

Je, malaika walimuuliza Mwenyezi Mungu?

Katika sehemu hii tunaanza na swali hilo, la kwenye kichwa cha Habari, ambalo In shaa Allah tutalizungumzia kwa kina.

Je, Maklaika waliuliza kweli?

Wakati tunaendelea. kwanza tujikumbushe kitu ambacho tulikiongelea huko nyuma, kwa kiasi na kijuujuu, nacho ni kua, asilimia kubwa sana ya Qur’an, (nadiriki kusema) zaidi ya asilimia 60 ni visa na hadithi mbali mbali zilizomo ndani ya Qur’an. Kwa usisitiza, ikiwa hakuna visa na hadithi ndani ya Qur’an basi hakuna Qur’an.

Tunapata na istilahi nyingine “dhikr” ambayo kama tutavyojionea, mara nyingi inapotajwa “dhikr” inamaanisha kisa, fumbo au hadith ya Qur’an. Hili tutaliongelea kwa kina na kuonesha Ushahidi uliopo ndani ya Qur’an na tutajionea tunavyoweza kujifunza kutokana na dhikr, ambayo kimaana ya Qur'an ni hadith za Qur’an.

Tutaona pia ndimi “lisan” ya Ibrahim (Abrahamic locution) inavyotolewa kwenye dhikr wakati tunaongelea suala hili la Malaika ambao, eti wamemuuliza maswali Muumba wetu, kama tulivyoaminishwa na watafsiri wengi walioitafsiri aya Q 2:30.

Raha ilioje tunapogundua "bayyinah" mpya na za kipekee ambazo Qur’an yenyewe inatufundisha na kuturekebisha mithili ya “advanced software” ya kompyuta kila tunapoendelea kugundua kuisoma kwa kufata mifumo (methods)yake ya kutuelimisha.

Kwa hakika ni muujiza, wa kushangaza na kustajaabisha. tunapoelewa yote hayo ni kutoka kwenye Qur’an yenyewe. In shaa Allah tutazidi kujionea wenyewe na kuelimika kila tunavyoendelea.

Hii tunaiita moja ya vibainisho “bayyinah” au viashiria vipya tunavyojifundisha kwa pamoja.

In shaa Allah uwe ni ujuzi na elimu yenye manufaa kwetu na kwa wengine wote, pia iwe ni sadaka njema kwetu na kwa Waislam wote, waliopo na waliotutangulia.

Tueleweshane na tuelewe kua, hii ni elimu na sio starehe, raha yake isio na mfano ni pale tunapojitambua kua tunaupata ujuzi wa kina wa kuulewa mwongozo wetu wa Qur’an kwa mbinu za Qur’an yenyewe.

Qur’an ni muujiza ambao huwezi kuufananisha kitabu cha mtu yoyote au chochote au mshairi yoyote duniani. Hakuna mbinu za kujifundishia za mtu yeyote zinayoweza kufanana au hata kuzikaribia mbinu za Qur’an.
...
 
Ni kweli kabisa ... Nipe chanzo au source kutoka kwenya mafunzo ya Mtume ya kuunasibisha uislam na kutumia majini kwenye TIBA au kutaka usaidizi wa majini ..
Ingekua raha sana, ungeanza kwa kujibu maswali unayoulizwa.

Hilo swali lako lipo kwenye (ignorance fallacy) au muongo wa ujinga, kwa kua hujaonesha umelisoma au kujifundisha wapi hilo. sanasana ulisema "umetokea hukohuko mapangoni " nilipoenda mimi kuchukua pete na bakora. Kwa hio na wewe unamaanisha ulijifunza hayo unayoyauliza kutokea "huko mapangoni"? Au umekurupuka tu na kuleta uongo wa ujinga?

In shaa Allah utaelewa tu ni nini maana ya uongo wa ujinga "ignorance fallacy" kwenye mambo ya kielimu. In shaa Allah hatutachoka kuelimishana.
Simba.
 
Ingekua raha sana, ungeanza kwa kujibu maswali unayoulizwa.

Hilo swali lako lipo kwenye (ignorance fallacy) au muongo wa ujinga, kwa kua hujaoneshq umelisoma au kujifundisha wapi hilo. sanasana ulisema "umetokea hukohuko mapangoni " nilipoenda mimi kuchukua pete na bakora. Kwa hio na wwewe unamaanisha ulijifunza hayo unayoyauliza kutokea "huko mapangoni"? Au umekurupuka tu na kuleta uongo wa ujinga?

In shaa Allah utaelewa tu ni nini maana ya uongo wa ujinga "ignorance fallacy" kwenye mambo ya kielimu. Hatutachoka kukuelimisha.
Simba.

Asalaam Alykum Simba , ni jumatatu iliyonjema Alhamdullilah Allah katuepusha na Dhahama ya maandamano kutoka kwa ndugu zetu wa Chadema, kwa hili nampa hongera sana amir jeshi mkuu mama samia suluhu hasani kwa kuimarisha ulinzi ...

Ingekua raha sana, ungeanza kwa kujibu maswali unayoulizwa.
Akhi hakuna swali ambalo sijajibu ... sema majibu yangu hayajakuridhisha and i can do nothing about that .. ndio Allah amekadiria uelewa wako ufikie hapo ..

Hilo swali lako lipo kwenye (ignorance fallacy) au muongo wa ujinga, kwa kua hujaoneshq umelisoma au kujifundisha wapi hilo.
Hamna hoja hapa, zaidi ni manneno tu It seems you're engaging in circumlocution, avoiding a clear and direct response. Let's approach the matter with straightforward clarity, shall we?"
sanasana ulisema "umetokea hukohuko mapangoni " nilipoenda mimi kuchukua pete na bakora. Kwa hio na wwewe unamaanisha ulijifunza hayo unayoyauliza kutokea "huko mapangoni"? Au umekurupuka tu na kuleta uongo wa ujinga?
Alhamdullilah Allah kaniepusha ni shirki za aina hiyo ,, kulala mapangoni, na ulozi ... simply nimesema mimi ni mwenyeji wa Tanga , wilaya ya Mkinga .. kijiji si mbali na mombasa ..na katika story yako hapo juu ilianza ukiwa maeneo ya hukohuko, nashangaa wanizulia mimi elimu yangu nachukulia mapangoni.. ila sishangai uzushi ni kitu cha kawaida kwa ahalul Bidaa..

In shaa Allah utaelewa tu ni nini maana ya uongo wa ujinga "ignorance fallacy" kwenye mambo ya kielimu. Hatutachoka kukuelimisha.
Ittaqullah ewe Mja wa Allah , Toa elimu iliyosahihi kama aliyotoa Rasullah Allah kwa wanafunzi wake, na wanafubnzi wa wanafunzi wake katika zile karne tatu Bora usiopeteze Ummah wa kiislam katika Shirki akhi..
 
Asalaam Alykum Simba , ni jumatatu iliyonjema Alhamdullilah Allah katuepusha na Dhahama ya maandamano kutoka kwa ndugu zetu wa Chadema, kwa hili nampa hongera sana amir jeshi mkuu mama samia suluhu hasani kwa kuimarisha ulinzi ...


Akhi hakuna swali ambalo sijajibu ... sema majibu yangu hayajakuridhisha and i can do nothing about that .. ndio Allah amekadiria uelewa wako ufikie hapo ..


Hamna hoja hapa, zaidi ni manneno tu It seems you're engaging in circumlocution, avoiding a clear and direct response. Let's approach the matter with straightforward clarity, shall we?"

Alhamdullilah Allah kaniepusha ni shirki za aina hiyo ,, kulala mapangoni, na ulozi ... simply nimesema mimi ni mwenyeji wa Tanga , wilaya ya Mkinga .. kijiji si mbali na mombasa ..na katika story yako hapo juu ilianza ukiwa maeneo ya hukohuko, nashangaa wanizulia mimi elimu yangu nachukulia mapangoni.. ila sishangai uzushi ni kitu cha kawaida kwa ahalul Bidaa..


Ittaqullah ewe Mja wa Allah , Toa elimu iliyosahihi kama aliyotoa Rasullah Allah kwa wanafunzi wake, na wanafubnzi wa wanafunzi wake katika zile karne tatu Bora usiopeteze Ummah wa kiislam katika Shirki akhi..
Kuna page huyu bwana aliandika baada ya kurudi Dar, alihitaji kumuita Arsis akakosa pahala.
ikabidi Arsis amwingie kichwani basi wakawa waongea Arsis yuu kichwani akawa hauliza maswali Arsis akasema siwezi kaa sana hapa ntakumiza, Huu ni ushahidi kwamba atumia majini
Malaika siyo waasi.
 
يأيها الذين ءمنو إن جأء كم فاسق بنباء فتبينو أن تصيبو قوما بجهلة فتصبحو عل ما فعلتم ند مين
Habari Suhendra nashauri ukiwa unaweka aya kama hiyo utoe na maelezo kidogo ni aya ya ngapi katika sura gani ili iwe rahisi kwa mtu kufanya rejea kwani kuna watu sio waislamu na wengine ni waislamu wanafatilia ila hawajaifadhi quran yote hivyo inakuwa ngumu kwao kujua what is going on.
Jamani iyo iliyowekwa ni ay ya 6 Katika surat hujurat ni sura ya 49 fafsir yake kwa mujibu wa sahih international iyo apo chini:-
''O you who have believed, if there comes to you a disobedient one with information, investigate, lest you harm a people out of ignorance and become, over what you have done, regretful.''
Kwakifupi ni Aya hii inatufundisha umuhimu wa kuthibitisha habari kabla ya kuziamini ili tusijifanye waandishi wa uongo au kuleta madhara kwa watu wengine.
 
Kuna page huyu bwana aliandika baada ya kurudi Dar, alihitaji kumuita Arsis akakosa pahala.
ikabidi Arsis amwingie kichwani basi wakawa waongea Arsis yuu kichwani akawa hauliza maswali Arsis akasema siwezi kaa sana hapa ntakumiza, Huu ni ushahidi kwamba atumia majini
Malaika siyo waasi.

umeona kama sio uchawi ni nini ??? ..... Imepokelewa na Yaala ibn Morrah, kwamba mwanamke alikuja kwa Mtume S.A.W., akiwa na mtoto wake ambaye alingiwa na majini mwilini mwake, Mtume S.A.W., akamwambia: Toka nje adui wa Mwenyezi Mungu, Mimi ni Mjumbe wa Allah, alisema, mtoto huyo akapona. Hii ni dalili moja ya dalili nyingi RasoolAllah hakuwa na Urafiki na majini mpaka kutoa kauli Adui wa Allah, Iweje hawa wanakuwa na urafiki nayo, kuomba msada kwao .. ni ishara tosha watu wa aina hii kiigizo chao sio Mtume bali ni Shetani ... na watu wa aina hii ndio wanajiita masheikh wakitoa fatwa hazina vichwa wala miguu kuzidi kuupoteza ummah ... Mbaya zaidi hawataki kuambiwa kwamba wamepotea warudi kwenye mstari wa quran na sunna wanakuwa wakali mnoo...
 
Arsis kuna uhusiano gani kati ya ndoto anazoota mtu na uhalisia wa ndoto hizo yani mtu anaota ndoto kuhusu kitu fulani then baadae kuna matukio yanatokea kweli ambayo yanahusu zile ndoto???

Cc Smart911
 
Hujajibu swali la njiwa , swali kwa kifupi ni hili Quran inaruhusu waislamu kushirikiana na majini? Swali fupi tu na rahisi na halijajibiwa bado.
Nimeona comment nyingi kuhusu hili swali ''JE UISLAMU UNARUHUSU KUSHIRIKIANA NA MAJINI ? Na hiki ndio watu wengi wanatamani kujua, Lakini ukiangalia kitaalamu swali hili linaleta swali lingine ambalo ni 'USHIRIKIANO UPI?, WA KHERI AU WA SHARI?
Vyovyote itakavyokuwa swali la msingi linabaki Je uislamu unaruhusu kushirikiana na majini?, Hapa ni pagumu kidogo hasa katika nyakati hizi ambazo elimu imechezewa sana kila mtu atasema lake lakini Binafsi nashauri kwamba embu tuwe na subra, Kwanza tuwafahmu hao majini ni viumbe gani tukishawajua ndio tuje sasa je yafaa kushirikiana nao?.
Hivyo bwana Arsis nakuomba uendelee na kisa cha adamu kwa angalau episode 3 kwa siku maana umesema katika kisa hiko tutawafahamu majini ni viumbe gani. uzuri katika kisa hicho anatembea na aya za quran hivyo natumai tutapata jibu tu.
Ili tusije sema haifai kumbe tunashirikiana nao kila siku ila sisi ndio hatujui kuwa tunashirikiana nao au tuseme yafaa kumbe haifai mwisho tukawa wenye hasara.
Narudia, Tuwe na Subra hasa ukizingatia uzi huu una jumuisha mada nyingi sana tofauti tofauti.
 
Arsis mtu asie na imani sana wala kinga ya mwili kidunia awezaje mtega na kumkamata mchawi anaekuja kumdhuru kwa namna moja ama nyingine ???

Cc Smart911
 
Arsis kuna uhusiano gani kati ya ndoto anazoota mtu na uhalisia wa ndoto hizo yani mtu anaota ndoto kuhusu kitu fulani then baadae kuna matukio yanatokea kweli ambayo yanahusu zile ndoto???

Cc Smart911
Una ufalme wa majini au mizimu mwilini mwako na ufalme huo (Majini /mizimu wanauwezo pia wa kutibia au kuombea watu na kuwaponya matatizo yao .. nime msaidia mtoa mada
 
Una ufalme wa majini au mizimu mwilini mwako na ufalme huo (Majini /mizimu wanauwezo pia wa kutibia au kuombea watu na kuwaponya matatizo yao .. nime msaidia mtoa mada

Heee kumbe!! Ndiomana wachawi wanapotaka kumdhuru mtu huyo huwa anaoteshwa au hadhuriki ama???

Au ndiomana wakimjia kumdhuru huweza kuhisi uwepo wao na anaweza pambana nao??

Hapo kwenye uwezo wa kutibia kivipi???



Cc Smart911
 
Back
Top Bottom