mkuu
Arsis mimi naona kisa cha adam ni bora ungeuanzishia uzi wake tu ujitegemee sababu kisa cha adamu kina mambo mengi complex yanachanganya na jinsi ulivyoanza mbali sijui mambo ya tafsili mara lisan na tafsiri za mashkhe haya yanafaa ukiwa umesoma japo vitabu vya dini ndio utaunga doti..ushauri wangu yafungulie uzi mpya uite"UKweli Kuhusu Adam-je, ni binadamu wa kwanza kuumbwa?" maana tulianza vizuri sana kuhusu ww kufunguliwa macho tukaja visa na vionjo vya
Arsis ilikuwa moto sana ila hili darasa la lisan na tafsiri na maandiko ya mashekhe inachosha tena inaboa maana inahitaji uwe na akili pana na kisomi ya kuchanganua vitu hiyo wanayo wachache humu hadi lengo la uzi mama wa visa na vionjo vya arisis linapotea fanya kusitisha hili darasa la adam lipe uzi wake linaonekana refu sana kisha turudi tuendelee kwenye Visa na vionjo vya Arsis..
Kumbuka lengo ni kutoa elimu basi ni bora uwe na nyuzi nyingi tofauti zinazojitegemea zenye elimu tofauti kwa ajili ya marejeo kuliko hii ya kutumia nyuzi moja kurundika mambo kibao yenye maudhui tofauti yasiyohusiana na yaliyotangulia haileti maana zaidi ya kuchoshana.