Nimeamini safari ya kuitafuta na kuishika ml 100 as cash ni ngumu mno. Najitaidi lakini yataka moyo!

Kuwa na cash ya kutosha sio jambo dogo. Biashara tunazozifanya hazijawahi tosheka na hela... kila siku zinadai kuwekezwa zaidi. Moo alisema alikuta baba yake ana net worth ya 26b akaona bado ni ndogo ikabidi akakope SA mabilioni mengine ili kukuza biashara.
 
Ndugu yangu, unatafuta pesa au maisha mazuri? Omba Mungu akupe maisha mazuri. Utajiri utakusumbua. Ila hamwezi kunielewa.
 
"""Don't ask for a million dollars. Ask for the stuff that'll get you a million dollars - your health, your brain, your sanity, wisdom. Prepare me for when I do get that million. Make sure I don't go crazy, make sure I help my family"""
 
Mbona ni easy sana kwani unapiga Mishe gani?
 
Kama una nia zitafika na zaidi
Ni kuomba afya njema tu na kiwango kizuri cha kuweka na kuingiza pia
Ukifika Mia utasema ngoja nipambane ifike 150 na ukija kufikisha 400m bado utasema ni ndogo kwa sababu unazo
 
Inategemea upo mkoa. Gani hapa Tanzania , kama upo mkoani jaribu biasharavya Nafaka msimu huu Mahindi yameanza na Bei rafiki sana Gunia la KG 110 ni 38000/ Hadi. 40,000/.
Nunua Mahindi Gunia 500 Kwa Thamani ya Tshs 20milioni ,
Then nunua mpunga Gunia 200 za debe kumi kumi Kwa Thamani ya Tshs 10Millioni ,
Alizeti Gunia 300 KG 70 Kwa Thamani ya Tshs 15Milioni.
Hifadhi Kwa muda wa miezi Sita , hapo ni January 2025 Bei zotakuwa. Juu sana Kwani Mazao yanakuwa hamna mashambani.
Mahindi unaweza uza Hadi Tshs 80,000/ mara 500 Gunia = 40milioni.
Mpunga Gunia 200 Mara 140,000/ = 28milioni.
Alizeti Gunia 90000/ mara Gunia 300 = 27milioni
Jumla ya kipato Kwa kuwekeza 45milioni Kwa miezi Sita ni 95milioni.
Option ya pili kama upo Dar es salaam nenda maeneo ya pembeni yanauokuwa Kwa Kasi Nunua ekari tatu za ardhi katika maeneo matatu tofauti then unapima. Viwanja baada ya mwaka Moja Hadi miaka miwili. Ekari Moja inatoa wastani wa Viwanja 10 vya kuanzia 400sq Kila Kiwanja utauza zaidi ya Tshs 4Milioni, hapo mchawi ni kwenye kupoint maeneo Gani yarayokuwa Kwa Kasi.
 
Hizi habari kuhusu nafaka huu ni nzuri kwenye kuandika ila kiuhalisia ni tofauti kabisa ukiingia kwenye gemu lake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…