Nimeamua 'kusilimu' je, kisheria na kiimani nitaruhusiwa kuongeza wake nikihitaji?

Nimeamua 'kusilimu' je, kisheria na kiimani nitaruhusiwa kuongeza wake nikihitaji?

1. Sheria ya nchi Itaendelea kumtambua mke wako wa ndoa.

2.kama mkeo Wa awali ukitaka kuishi naye kwakuwa umebadili dini ( kidini) itakupasa ufunge NAYE ndoa ya kiislam , na yeye akibaki na imani yake Kwani uislamu haiitambui ndoa ya awali Mkibaki na ndoa ya kikristu Utakuwa unazini naye. Pia utaruhusiwa kuongeza mke Kwani hata serikali inatambua ndoa ya wake wengi na imani ya dini Yako inaruhusu kuoa mpaka wake wanne na wote wana haki

3. Kama mwanamke naye akiamua kubadili dini, ndoa yenu ya awali itatambulika Kisheria ya nchi, kidini mnapaswa mfunge ndoa ya kiislam .
Kwa hyo namba 1 kumbe yafaa sasa nikibadili dini nitakua na sababu ya kumpa talaka mke wangu wa awali kama hakubadili dili, ili kwamba hata sheria za nchi zisimtambue
 
Kwa hyo namba 1 kumbe yafaa sasa nikibadili dini nitakua na sababu ya kumpa talaka mke wangu wa awali kama hakubadili dili, ili kwamba hata sheria za nchi zisimtambue
Mkuu sheria ya nchi ata kama hamkufunga ndoa ili mradi mmeishi not less of 6months basi huyo ni mkeo achilia mbali kuzaa nae.Kwani Moni na huyo sijui mchepuko wake mbona wanakimbizana mahakamani ili atoe matumizi?ingeu sẻikali haitambui wasio na ndoa unamaana wasingefikishana mahakamani.
 
Katika mchakato wa kujaza fomu ya usajili wa ndoa ambayo ni hati rasmi ya serikali wanandoa watarajiwa hujaza kipengere kinachoainisha muundo wa ndoa itakayofungwa yaani MONOGAMY au POLYGAMY, kipengere hiki ni mkataba baina ya wanandoa mbele ya msajili wa ndoa tarajiwa baada ya hapo wote watatu yaani (Mume, Mke na kasisi, Imam au DC) watasaini makubaliano hayo, sasa ukiachilia mbali huu mtindo wa kufanya mambo kienyeji unaoedelea ktk jamii, kimsingi huwezi kuanzisha mkataba juu ya mwingine bila kwanza kutanzua ule wa awali kisheria, hivyo endapo Mume atabadili dini na kutaka kuingia ktk mfumo wa imani ya ndoa za polygamy ni lazima ajaze fomu ya makubaliano mengine sambamba na Imani yake mpya.
Good. Shida ipo hapa: wakristo hawavunji ndoa (hawatanzui mkataba) je hilo la kusema huezi kuingia mkataba mwingine juu ya mkataba uliopo linawezekanaje? Kwakuwa kanisa hua halivunji ndoa, je ndoa hyo inaweza kuvunjwa na mahakama pekeake ili anagalau kuweka mazingira ya kisheria kwamba mwanandoa aweze kuingia mkataba mwingine (polygamy)? Na utaratibu ukoje
 
Chukulia katika mazingira ambayo ninauhuru (wa kikatiba) kuchagua dini yyte ile ninayoitaka. Na uhuru huu ninayo haki ya kuutekeleza wakati wowote ule. Sifungwi kubaki kwenye dini fulani.

Katika mazingira ya kuwa nimeoa mke kwa ndoa ya kikristo ambayo inaruhusu mke mmoja tu kwa mume mmoja na inatambulika hivyo kisheria. Nikiwa kwenye ndoa hiyo, kesho nikaamua kubadili dini na kuwa muislam na huko ninaruhusiwa kuwa na wake hadi wanne.

MASWALI:
1. Kwakua nitakua nimekana dini yangu ya awali, Je sheria itaendelea kumtambua huyu mke wa ndoa ya kikristo?

2. Hata kama tumeamua kuishi pamoja kama wanandoa (yeye abaki kuwa mkristo), je nitakua na uhuru kisheria kuongeza wake?

3. Hata kama tumeamua kuishi pamoja (na mke wangu naye abadili dini na kuwa muislam), je tutakuwa tumefunga ndoa au tutahitaji kuoana upya?

Nielewesheni kisheria na kwa imani ya kiislam pia.

MAJIBU
1. sheria haitaendelea kumtambua kama mke wako hadi mkafunge ndoa bomani kwani ndo hiyo itakuwa imevunjika baada ya wewe kuwa muislam..(maelezo zaidi ktk jibu la swali # 2)

2. ukishakuwa muislam mkeo akibaki na dini yake ya ukristo ndoa hiyo itakuwa imevunjika..hakuna ndoa ya muislam na mkristo inayokubalika na uislam...labda ujitenge na Mungu uende ukaoe bomani)

3. mkibadili dini wote mkaingia ktk uislam hamna haja ya kufunga ndoa ingine, mtaendela na ndoa yenu na inatambulika kwa Allah (na kwa kuongezea tu dhambi zenu zote zitakuwa zimefutika mnaanza upya na mnafunguliwa vitabu vyenu vya matendo kila mmoja vitabu viwili (cha matendo mema na cha maovu))
 
Kwa hyo namba 1 kumbe yafaa sasa nikibadili dini nitakua na sababu ya kumpa talaka mke wangu wa awali kama hakubadili dili, ili kwamba hata sheria za nchi zisimtambue
Inawezekana Kabisa na hata kwa upande wake wa kikristo ndoa yenu itakuwa batili mwanamke Atakuwa huru.
 
Je lengo la we kuslim ilikua kuonheza mke au kufuata imani yao?
 
Kiimani Hatambuliki.
Kisheria Anatambulika.
Na ili kuyimiza hitaji la yeye kuwa mke. Je akiamua kujitenga na mm, arudi kwao, kwasababu nimebadili dini; je, ninaweza kuchukua hatua gani za kisheria ili aendelee kuishi na mm kama mke wangu. Haitakua na maana sheria imtambue kama mke wangu halafu akimbie nyumba, i should be able to take some legal measures
 
Ndoa za kiislamu zinatoa hati ya ndoa.
Na Uislamu unatambua ndoa iliyofungwa kidini, hata kama hati iliyotolewa ni ya kiserikali, ilimradi imefungwa kidini.
Inapotambua ndoa kikristo Uislamu hautenganishi watu waliooana kidini, bali hakuna hati ya ndoa hapo.

Nakuuliza swali na wewe sasa:
Kwani mtoto aliezaliwa wazee wakiwa wakristo na baadae wazee wakasilimu huyu mtoto anakuwa anaendelea kuwa mkristo au atakuwa muislam?
Atakua muislam
 
Kwanini awe muislam?
Kwasababu alikua mktisto kwasababu ya wazazi wake ni wakristo, na anaendelea kuwa mtoto wakati wazazi wake ni waislam (hyo ni logic, otherwise dini ielekeze vinginevyo)
 
Chukulia katika mazingira ambayo ninauhuru (wa kikatiba) kuchagua dini yyte ile ninayoitaka. Na uhuru huu ninayo haki ya kuutekeleza wakati wowote ule. Sifungwi kubaki kwenye dini fulani.

Katika mazingira ya kuwa nimeoa mke kwa ndoa ya kikristo ambayo inaruhusu mke mmoja tu kwa mume mmoja na inatambulika hivyo kisheria. Nikiwa kwenye ndoa hiyo, kesho nikaamua kubadili dini na kuwa muislam na huko ninaruhusiwa kuwa na wake hadi wanne.

MASWALI:
1. Kwakua nitakua nimekana dini yangu ya awali, Je sheria itaendelea kumtambua huyu mke wa ndoa ya kikristo?

2. Hata kama tumeamua kuishi pamoja kama wanandoa (yeye abaki kuwa mkristo), je nitakua na uhuru kisheria kuongeza wake?

3. Hata kama tumeamua kuishi pamoja (na mke wangu naye abadili dini na kuwa muislam), je tutakuwa tumefunga ndoa au tutahitaji kuoana upya?

Nielewesheni kisheria na kwa imani ya kiislam pia.
Utakuwa umeoa mke mmoja na majini kadhaa
 
Back
Top Bottom