Nimeamua sasa kuachana na ualimu na kwenda kusoma

Nimeamua sasa kuachana na ualimu na kwenda kusoma

Mzee nenda kasome. Nitakupa mfano kwenye nyanja mbili nilizoziona napofanyia kazi.
1. Pesa, pesa inaongezeka, sijui huko kwenu. Hapa kwetu ukienda kusoma Master ukaleta cheti unakula Proff. Allowance ya 700k+. Na utaongezwa daraja kila baada ya miaka 2 au 3 ya kutumikia nafasi uliyonayo. Kila daraja la juu na malupulupu yanaongezeka ( hii ni sera ya ofisi)

2. Fursa nje ya ofisi. Kwetu hapa, mwezi uliopita zimekuja fursa kadhaa.
i) Zilikuja nafasi ya UN, mwenye Master ya Sheria apeleke vyeti. Kazini kwetu hakuna tumebaki tunashangaana tu.
ii) Wenye degree ya sheria na experience ya miaka kadhaa (alitaja) wapeleke vyeti wapitishwe kama mawakili wa kujitegemea (wenye certificate na diploma wakakosa).
iii) Alikuja Kiongozi, akataka wenye Masters ya Uongozi awape nafasi kusoma Chuo cha Ulinzi (wale watu wale), baadaye wapewe nafasi serikalini huko. Hakuna mtu, hii nafasi iliwauma watu wengi sana.
Shukrani mkuu, nadhani sio halmashauri hiyo ni taasisi.
 
Nina diploma ya Environmental health science ( Ubwana afya GPA ya 2.7 siwez soma degree Kwa hii GPA) ushauri nirudi chuo nikasome mwaka mmoja Kwa jili ya kubadili GPA niweze kwenda degree miaka 4 or nikasome vector control miaka miwili diploma ambayo wanachukua GPA ya 2+
 
Mkuu, ninavyojua Mimi nikishasoma either uhasibu au IT, napeleka cheti change kwa afsa utumishi kuangalia wapi Kuna uhaba ndani ya halmashauri, kama Kuna uhaba basi kufanyiwa re-categorization ni rahisi, nilipo Mimi uhaba ni mkubwa tu sio kwa IT, hata wahasibu na Sheria pia, ndio maana IT, Pamoja na wanasheria hata wakifanyiwa recategorization hawashushwi daraja hata kama ukiwa E unaendelea hukohuko.
Sasa tofauti ya mshahara wa mwalimu wa degree aliye halmashauri na IT au mhasibu wa halmashauri ni kiasi gani?
 
Watu wana Masters za information technologies wapo kitaa,jichanganye tu utakumbuka Kigoma.Omba uhamisho nenda Mjini ukatimize ndoto zako,kamwe usiache kazi
 
Mtoa mada unataka kuwa kiongozi au mfuasi. Kusoma na biashara yote yana faida zake na hasara zake.Ajira ni maisha ya kuwa mfuasi wa mtu au kikundi cha watu ila biashara yako kwa 15m ni wewe ndio bosi/ kiongozi na waweza kurithisha familia yako.Nakushauri fuata ndoto zako ila pia anza utafiti ni biashara au mradi gani utakaokusaidia kiuchumi.Kwa nchi yetu wasomi ni wengi wasio na kazi hii inakatisha tamaa ya kusoma
 
Watu wana Masters za information technologies wapo kitaa,jichanganye tu utakumbuka Kigoma.Omba uhamisho nenda Mjini ukatimize ndoto zako,kamwe usiache kazi
Acha uongo, IT ni moja ya field chache ambazo ukiwa na ujuzi barabara haukosi kazi.Na kazi za IT zinataka practical knowledge. Kwaiy km unajua kazi zipo ila km unababaisha hupati kazi ata ulie machozi ya damu
 
Hakuna utofauti wowote mkuu, lakini halmashauri Kuna marupurupu kidogo ukilinganisha na ualimu.
Kwa hiyo unataka upoteze pesa na muda kwenda kusoma kwa sababu ya marupurupu

Sasa hauoni pesa zaidi ya hayo marupurupu ungeipata kwenye biashara?

Tumia akili unapofanya maamuzi. Marupurupu wala mshahara havijawahi kutosha

Hapo Kigoma uko halmashauri gani?
 
Back
Top Bottom